Huyu mnyama anaitwaje kwa kiswahili? Analiwa?

Unapofungua kamusi ya kiingereza neno la kwanza kukutana nalo ni "Aardvark." Mnyama huyo ni huyu hapa chini na anapatikana Afrika yote kusini mwa jangwa la Sahara. Kwa kiswahili anaitwaje? Analiwa?

Huyu mnyama anaitwa Mhanga chakula chake ni wadudu na anapenda sana kula mchwa, ni mnyama mwenye makucha marefu na ulimi mrefu sana anapenyeza hata kwenye kichuguu, wanapatika sehemu nyingi ila huwezi kumuona mchana ila usiku tu, hana madhara kwa binaadamu zaidi ya kumkimbia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…