Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
- Thread starter
-
- #21
Hawa viumbe wanapenda kutumia udhaifu tulionao kwao katika kufanikisha malengo yao.Usikubali kua daraja.
Nukuu ya baba wa taifa.
""UTII UKIZIDI SANAA HUZAA UOGA, UOGA UKIZIDI SANA HUZAA UNAFIKI NA KUJIPENDEKEZA NA MWISHO WAKE NI MAUTI""
Utalii uliposhuka arusha ndoa nyingi zilishake. Nilikuwa arusha by then. Wanawake waliwaacha wanaume zao live live bila haya meana maisha yalibadilika gaflaNapata ugumu kuamini mtu ambaye ana watoto wake na wapo chuo, maana yake hiyo ni ndoa ya labda miaka 18+ au hata 20+ kwamba mume kuyumba kidogo imsumbue hivi. Washapitia vingi huyu mmama menopausal anahangaika na nini bado? Ungekuwa kijana mdogo kwa hali ya hewa ya dunia ya sasa kidoooogo ningeelewa. Ila hapa, duh! Hata mie chujio sina la kuchuja
Mpatie mwenzio rejeshooInaweza kuwa ndio chanzo
Nami nitanufaika na nini? kwa sababu akishafanikiwa nitakuwa blockedMpatie mwenzio rejeshoo
Life management is toughthibitisha ....
Umeishasema alikueleza hali halisi ya Maisha yake, kinachotakiwa ni wewe kumsaidia kibinadamu na sio lazima umkule.Habari wakuu
Kuna dada mmoja nilisoma naye zamani, miaka mingi kidogo iliyopita. Katika mazingira ya shule tulikuwa tukionyeshana hisia kwa mbali ingawa mpaka tunamaliza hatujawahi kuwa wapenzi.
Baada ya kuhitimu kila mmoja aliendelea na maisha yake, yeye aliolewa na bwana x, aliyekuwa akimiliki kampuni y ya kupeleka watu mbugani. Maisha kwao yalikuwa mazuri sana na walifanikiwa kupata watoto wawili ambao kwa sasa wako chuo kikuu.
Maisha hayatabiriki, kile kipindi cha majanga, wageni wakapungua na kupelekea kampuni kufilisika, na kujikuta jamaa anaanza sifuri. Ilibidi jamaa aame mkoa na kwenda kujaribu shughuli zingine, ambazo kwa sasa zinampa hela tu ya kula.
Kutokana na mwanamke kupenda maisha ya juu, kwake ikawa ni mtihani, kwa sababu yale maisha alioyazoea hayapo tena. Ndipo siku moja, nikapokea simu yake kwa mara ya kwanza, na kunijulisha amenitafuta sana muda mrefu, anataka niwe mshauri wake afanye biashara ipi.
Nikamwambia hakuna shida tutakuwa tunashauriana abc pale panapo wezekana; ndipo akanieleza mkasa wake na kutaka kujua mimi niko na familia au vipi.
Basi tukawa tunawasiliana hapa na pale, ila yeye akawa ananipigia simu ata usiku, nikimuuliza humuogopi mzee wako? anasema yeye ni mtu mzima afuatilii haya mambo.
Baada ya kuumiza kichwa na kutafakari sana, nikagundua huyu anataka anitumie kama daraja ili afanikishe lengo lake kisha anibwage.
Nikaona kabla sijafika mbali, inabidi tubadilishane joto kwanza; tukaweka mikakati ikawa imepangilika vizuri.
Kuna siku nilikuwa nimeenda nchi jirani, wakati wakurudi nikafikia kwenye mkoa aliopo, nikampa taarifa tuonane, akasema haina shida; baada ya dakika 20 ananitumia meseji ametembelewa na mama mkwe kwa hiyo atutaweza kuonana.
Nilipiga mahesabu kiutu uzima, nikagundua nimepigwa chenga; nami nikamjibu sawa. Nikaendelea na shughuli zangu na hatimaye nikarudi mkoani kwangu.
Baada ya kufika mkoani sasa amekuwa akinisumbua sana, mara mwezi ujao nimtumie nauli aje anitembelee, mara ninachangamoto kidogo ya salio naomba unitumie; kwa huruma nilimtumia kiasi kidogo kama 50 hivi.
Kibaya zaidi kwa sasa, amezidisha hali ya kuomba omba; sasa najiuliza haya ni mapenzi au anatafuta mteremko wa maisha?
Sasa hivi kuna 'missed call' zake tatu, na sitaki kupokea; kwa sababu nimeshagundua anataka kunitumia kama daraja.
Equation x mzee wa michepuko nimeshastaafu.
Karibuni kwa ushauri.
mahesabu
Sio kila msaada unatoa unafaidika. Mbona sie tunawapa vipochi bila kujali mnatupatia niniNami nitanufaika na nini? kwa sababu akishafanikiwa nitakuwa blocked
Angekuwa ni mzee wake hapo sawa, sasa mwanaume kuwa na ukaribu na mke wa mtu, unategemea nini? Unaweza ukawa unatenda wema, je mmewe atajua huo wema?Umeishasema alikueleza hali halisi ya Maisha yake, kinachotakiwa ni wewe kumsaidia kibinadamu na sio lazima umkule.
Msaidie tu kwa moyo mmoja bila kuwaza vibaya.😜
Mume hapo hahusiki msaidie rafiki yako hayo mengine yaache.Angekuwa ni mzee wake hapo sawa, sasa mwanaume kuwa na ukaribu na mke wa mtu, unategemea nini? Unaweza ukawa unatenda wema, je mmewe atajua huo wema?
Wanaume wengi huwa tuna huruma, ndio maana tunaongoza kwa kuhonga vitu vikubwa, mwisho wa siku tunaangukia pua; tujifunze kwa walitutangulia, Tyrese amefilisiwa na mwanamke aliyekuwa mke wake.Sio kila msaada unatoa unafaidika. Mbona sie tunawapa vipochi bila kujali mnatupatia nini
Wakati mambo yakiwa safi, kwa nini asinikumbuke kama rafiki 😀Mume hapo hahusiki msaidie rafiki yako hayo mengine yaache.
Kweli mkuu, maongezi yake mengi anajiongelea yeye kufanikiwa tu.Pesa inatoa mtu thamani.aisee Mungu atujalie mwisho mwema
Huyo mama kakosa heshima kabisa
Mkuu Achana nae.
Mpige block anataka kukutumia TuKweli mkuu, maongezi yake mengi anajiongelea yeye kufanikiwa tu.
Nipe ushauri wenye akili sasaSamahani ila huna akili
Uko sahihi kabisa, ngoja nipambane na uzao wangu usije ukanilaumu huko mbeleniMpige block anataka kukutumia Tu