Uchaguzi 2020 Huyu mtu anaweza kuchukua hii nchi au anaweza kusababisha mambo yatakayosababisha mageuzi kutokea katika hii nchi

Kuna watu hutokea duniani kazi Yao siyo kuwa Viongozi wakubwa, mf Ndg Malema wa SA, ndug Prof Lumumba Kenya, Ndg Wine Uganda n.k

kazi Yao ni uanaharakati ndio inawafaa, na hata wa kwetu Yuko kwenye kundi hilohilo, kuchangamsha watawala, Uraisi ni kuwaonea. Watavurunda Asubuhi na mapema
 
Kila mtu na mbabe wake! hakuna cha tingatinga wala nini. Airforce one iko angani sasa ni wakati wa kuyaambia hayo mauaji na mijizi ya kura yafanye fyoko yaone. Muwahi kwenda kurecharge pace maker mapema sababu hana ubavu hata wa mita mbili kwe huyo mnyama aliyeangani tayari kupiga!
 
Maybe ni mgeni kwenye siasa
Mrema alikuwa amepandikizwa tu so ccm walikuwa wanajua nn kinafanyika

Lowassa still alikuwa ni Mwanaccm Tena ambae 80% ya maisha yake katumikia Chama

Lisu hajawahi kabisa kuwa ccm
kila siku mambo yanabadilika ndugu,Kuna nyakati vijana hawakujishughilsha na kupiga kura lakini sasa wanapiga,Kuna nyakati hata kura zenyewe hazikuonekani lakini nyakati zinakuja kura zitaonekana,Vyombo vya ulinzi na usalama vilijitanabaisha kua sehemu ya chama tawala lakini nyakati zinakuja vitajitenga nao kwa kua wananchi wa wanaounga mkono chama tawala watakua sawa na wa vyama pinzani.Nyakati zinabadilika hakuna aliyetegemea Lissu kupata haya mapokezi kwa kua matusi kejeli na maaminisho kua ni msaliliti vilimwagwa lakini watu hawasikilizi tena Propaganda zisizo wasaidia.Nyakati zimefika watu hawatazami tena umaarufu wa chama wanatazama watu.Nyakati zimebadilika usikalili.
 
Mwenyekiti wao jana kasema atafanya zaidi ya alivyofanya katika miaka yake mitano aliyomaliza,hiyo tafsiri yake ni moja tu ambapo kila mbinyo tulioshuhudiautaongezeka.Kama ni mbinyo kwa watumishi utaongezeka,kodi na kesi za uhujumu uchumi zitaongezeka,wakulima mbalimbali walioporwa mazao yao kutaongezeka,wafugaji walioteseka kwa miaka mitano ndiyo hivyo hivyo,wavuvi na nyavu zenu zilizoitwa haramu mtaendelea kupiga mbizi kupata samaki bila nyavu nk.
Hali inatisha,mkuu akisema atajenga sgr kwenda kusini ama kaskazini,akinunua bombadia mara 2 ya alizonunua,bado ugumu huu wa maisha tulioushuhudia utakuwa maradufu huku tukiendelea kukopa na kukuza deni la Taifa kwa kisingizio cha kukopesheka.
Fikiria utakuwa na hali gani wewe mnyonge?Tuepuke ushabiki bila kufikiria yajayo.
 

Mkuu nimesoma points zako, nani naomba kuweka neno.
kwanza kabisaaa toka mfumo wa vyama vingi uanze Lisu ndiye mgombea mpinzani pekee (asiye na asili ya ccm kabisaa), mwenye uwezo wa kujenga hoja, uelewa mkubwa wa mambo , anaejua kukera bila kuvunja sheria ili ujaesumu.

Unaposema lowasa na mrema hawa hakuwa wapinzani kwa mujibu wa fikra zangu kwa sababu baada ya kukosa nafasi ccm wakaenda kujaribu kutimiza ndoto zao upande wa pili...but kifikra & itikadi walikuwa wana ccm.
Pili unasema ccm imejaa vijana, ebu angalia hao vijana ni wale ambao baba au mama zao ni mazao ya ccm au wana historia ndefu ndani ya ccm. kurithishana.
Kwachadema imewekeza vyuoni na ina pic direct na kuwapa vijana fursa ya kuwa wawakilishi. eg. silinde, lijualikali, wenje, pambalu, nasari. Hata kama baadae wanajifanya kununulika lakini historia inabaki palepale.
 
kwa kweli huyu jamaa ni jasiri kupita maelezo.
 
Ww ni binadamu muongo. Mtu yoyote asiyetaka Tl ashinde hawezi kuwa muongo wa kiwango chako Bali yule tu anayetaka kuhadaa ili ashinde.
 
Mungu alipanga mwisho wa CCM kwa namna ambayo akili ya mwanadamu haiwezi kuelewa kirahisi. Aliamua aje mtu mgeni kwenye chama (Magufuli) ambaye atawanyang'anya chama wakongwe (Makamba, Kinana, Kikwete, Membe nk) na kuingiza watu wake wapya (Bashiru, Makonda, Polepole).

Hawa wapya kwa namna yake watakivuruga chama na misingi yake kwa maagizo yake Mafufuli. Wataleta chuki na maovu kama utekaji (Mo Dewji, Roma ) na uuaaji (Ben Sanane, Azory Gwanda nk).

Halafu watamshambulia mmoja wa viongozi wa upinzani (Lissu) kwa risasi za bunduki ya vita lakini mtu huyo hatokufa. Nchi nzima itashangaa namna mtu huyo alivyoshambuliwa, kunyimwa matibabu, kunyang'anywa mshahara kisha kufukuzwa ubunge.

Wanaposhangaa hayo na kumhurumia ndiyo watataka awe Rais wao wa 2020-25. Mungu ana sababu kwa kila jambo. Mwisho wa CCM ni mwaka huu. Alilopanga Mungu Binadamu hawezi kubadilisha. Hata kama NEC itaiba kura na kumtangaza Maguduli, nguvu ya umma itamtoa tu Ikulu. Wananchi wamechoka maonezi, dhuluma, ukandamizaji, na ubaguzi wa maendeleo.

Enzi ya CCM imekwisha
 
Ww ni binadamu muongo. Mtu yoyote asiyetaka Tl ashinde hawezi kuwa muongo wa kiwango chako Bali yule tu anayetaka kuhadaa ili ashinde.
Asante sana huo ni muono kipofu wako. Umekataa ukweli na ukweli unauona ni uwongo. Tusubiri matokeo.
 
Hilo liko wazi
 
Ila kile nimeshuhudia leo Kyela baada ya kutajwa mgombea. Nderemo vifijo bodaboda kelele mji kushangilia.
 
Nimeshasema huko nyuma ashinde asishinde siasa za Tanzania hazitakuwa kama tulivyo zoea. Likizo yao ya miaka mitatu imekwisha. Na kwa sababu CCM ni sauti moja tunahitaji mtu wa kumwambia mfalme yuko uchi ikibidi na hilo CCM hawaliwezi.
Jana nilimsikia mjumbe wa NEC ya CCM akimsifia JPM kuwa "alimuweka kando mtoto wa dada yake baada ya kumuona hatoshi". Kwake hiyo ni sifa ya kiongozi wake, kwangu mmi huo ni ushahidi kuwa kule kuna sauti moja tu.
 
Both ways,Nyerere alifunga multiparty system pia akafunga au akapiga marufu kuibiwa mali zetu na makampuni ya kigeni.
Kaja Ben Mkapa tukiwa na multiparty akidhani kuruhusu makampuni ya kigeni yawekeze kwetu itakuwa jambo zuri sana.Hakujua kati yao wamo ruthless investors wasiotaka tubaki na chochote na ndio wengi walikuja kwetu.
Lakini kuja kwa mjomba Magufuli kapinduwa meza kawafungisha virago au wakubali tugawane kwa usawa.
Bila kuwa mkaidi utavuna mabuwa.
 
Ona mawazo ya think tank wa lumumba , mataga mwaka mtaongea yote , mtatapika ndoano.
 
Hakuna mgombea anayeweza kufikisha 70% uchaguzi wa mwaka huu. Itakuwa ni close tie, 50/50; 52/48; 54/46!
CCM vs Upinzani kiujumla.
Serikali ya Umoja wa kitaifa loading...
Umoja wa kitaifa kwa mgombea yopi wa urais? Kwa wabunge wapi? Nipe idadi ya wabunge wa CDM watakao shinda .
 
Asante sana huo ni muono kipofu wako. Umekataa ukweli na ukweli unauona ni uwongo. Tusubiri matokeo.
Matokeo yoyote hayatahalalisha uongo wako, Jpm atakuwa raisi uwezekano ni mkubwa sana ndio. 97% ni raisi ila haitamaanisha kuwa ulisema kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…