Huyu mwanamke Pasua kichwa nakabiliana naye vipi?

Huyu mwanamke Pasua kichwa nakabiliana naye vipi?

Waungwana habari!

Direct to the topic.
Kuna mtu nilimlipia deni polisi akanipa simu yake 'smart' nishike ili nimrudishie siku alinilipa pesa niliyomlipia.

Sasa hapa mtaani kuna mwanamke nimekuwa natembea naye, wiki mbili zilizopita huyu mwanamke aliniambia ana mimba lakini akawa anasisitiza nimpe hela akaitoe, basi mimi nikaona dalili za kupigwa tu na mimba hana.

Sasa juzi Jumapili asubuhi alikuja geto tukawa na mazungumzo halafu akasepa, aliposepa nikawa simu ya watu siioni, ikabidi nimtafute huyu mwanamke lakini alikataa katakata kwamba haujachukua na hakuiona.

Usiku huu nimetumia mbinu ya kujishusha kwamba nipo tayari nimpe hela anirudishie simu. Amekubali kwamba alichukua simu lakini bila laki harudishi.

Sasa wakuu naomba busara zenu ili nitatue changamoto hii.
Mwizi huyo Nenda Police
 
Ulikua unamtiq bure mtoto wa watu ety..?

mzee pambana na hali yako, malaya hapelekwi geto mzee, geto unapeleka mwanamke anae jiheshimu.
 
Back
Top Bottom