Huyu ndio Dr. Emmanuel Nchimbi ninayemfahamu

Huyu ndio Dr. Emmanuel Nchimbi ninayemfahamu

Peter Dafi

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
392
Reaction score
272
Anaitwa Dr Emmanuel John Nchimbi, Moja Kati Ya Masenior Comredi Ndani Ya Chama Cha Mapinduzi Ni Mtu Mahiri Katika Kile Anachokiamini Na Hafundishwi Punda Kumwita Farasi.

Ni Mwanasiasa Mwenye Nguvu Ndani Na Nje Ya ccm katika Ushawishi na Ukubalikaji wake.

Wasifu wake kiuongozi ni mpana sana Ameanza Kuwa Raisi Wa Chuo Kikuu Mzumbe Akaja kuwa Mwenyekiti Wa uvccm Taifa Akagombea Ubunge jimbo La songea mjini akirisi mikoba ya Laurensi gama.

Amekuwa mbunge kwa miaka kumi na amekuwa waziri kamili katia wizara mbili tofauti Wizara Ya Nyumba Na Makazi Na Wizara Ya mambo ya ndani pia Amekuwa naibu waziri katika wizara mbili tofauti wizara ya habari tamaduni na michezo pamoja na wizara ya mambo ya ndani.

Anasifika kwa uwelewa mpana wa mambo ya kitaifa katika nyanja mbali mbali kijamii kisiasa na kiuchumi.

Ameweza kuwatenegeza wanasiasa wengi mashughuli wakiwemo madc na wabunge wabunge lijalo katika baraza la vijana taifa la mwaka 2008

Makatibu wa uvccm na wa wilaya na mikao ni product yake pia ni mjumbe kamati kuu kwa miaka isopungua 17 anajua ajenda za chama na kitaifa

Kijana na msomi mwenye uwezo wa kulimudu Bunge lijalo la 11

#Twende na Nchimbi Uspika

* AKICHAGULIWA, NCHI KUPATA SPIKA BORA KAMA "JOHN BERCOW" WA UINGEREZA

Uongozi ni mchakato wa ushawishi ndani ya jamii, kwamba mtu moja anapopata madaraka uwasaidia wengine kukamilisha malengo ya pamoja.

Uongozi ni kuvuka mipaka ya mazoea na kuanzisha mchakato wa mabadiliko inayowasaidia watu kufikiri, kushiriki na kufikia malengo kwa tija na ufanisi mkubwa. Katika mbio hizi za kumtafuta Spika wa bunge la JMT lazima tukiri wengi waliojitokeza wana sifa ila ni vyema pia tukakiri ya kwamba Dr. E. Nchimbi ana sifa za ziada dhidi ya wengine...

1. Anawaza Mafanikio Makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake au eneo lolote alilofanyia/analofanyia kazi inapata mafanikio makubwa. Tumeshuhudia hilo kwa Dr. Nchimbi alipokuwa UVCCM, serikalini katika wizara mbalimbali na idara mbalimbali..

2. Ana Nia
Haitoshi tu kwa kiongozi kuwa na mawazo bali kiongozi mzuri lazima awe na nia ya kutimiza. Kiongozi mzuri na bora atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo atakuwa na uwezo wa kuratibu na kutekeleza alichowaza, ajue njia anayopita na kuwatangulia anaowaongoza kwa vitendo. Dr. Nchimbi ana sifa hii

3. Kujitambua
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na mapungufu yake na awe tayari kujiongeza maarifa kila siku, ili aweze kupokea changamoto na mabadiliko. Dr. Emmanuel Nchimbi ana sifa hii

4. Msimamizi wa Maamuzi
Katika maisha ya siasa, mara nyingi malengo hukumbana na vikwazo. Hivyo ni wajibu kwa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kwa wakati. Dr. Emmanuel Nchimbi ana sifa hii

5. Kukubali Kukosolewa
Viongozi wengi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hivyo ndio njia ya kuthibitisha usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa. Dr. Nchimbi ni kiongozi anayekubali kukosolewa...

6. Kuwa Msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasikiliza walio chini yake, wakubwa, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Dr. Nchimbi kalionyesha hili alipokuwa UVCCM, wizara mbalimbali alizopita, ndani ya NEC na CC. Huyu ndio tunamhitaji katika nafasi ya spika wa bunge la JMT

7. Kufata Haki
Kiongozi imara anatakiwa kufata haki. Asijione au kuona kundi fulani ina haki zaidi ya wengine katika sheria. Ni muhimu kwake kuonyesha jamii wako huru katika mawazo na matendo. Dr. Nchimbi marazote amekuwa mfano wa kuubiri HAKI na Amekuwa muumini wa haki.

8. Kuwa Egemeo la Watu
Kiongozi lazima awe egemeo la watu katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza au kufurahi pamoja na watu anaowaongoza bila kujitenga nao. Na kubwa zaidi ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali. Dr. Nchimbi katika hili ni mfano wa kuigwa. Amefanya hayo UVCCM, serikalini na wizara mbalimbali..

9. Kukubali Lawama
Kiongozi mzuri ni yule anayediriki kukubali lawama, awe amefanya au la. Anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Dr. Nchimbi ni mfano wa kuigwa katika hili, amewahi kubeba lawaza zisizo zake kwa sababu anaelewa dhana ya dhamana na ni kiongozi aliyeiva.

10. Utatuzi wa Matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo bora katika hili ni kusimama katika mawasiliano bora na watu unaofanya nao kazi. Hakuna shaka kwamba Dr. Nchimbi ni wa kuigwa katika hili. Amefanya hili akiwa ndani ya UVCCM, wizara mbalimbali na katika vikao vikubwa vya kimaamuzi..

11. Uaminifu/Ukweli
Kiongozi mzuri na bora ni yule aliyemwaminifu na mkweli. Ni yule atakayekuwa tayari kuonyesha ubora wa matendo na kauli zake. Dr. Nchimbi amekuwa mfano katika hili..

12. Mbunifu
Kiongozi mzuri ni yule anayejua au kubashiri nini kitatokea kesho kulingana na mienendo ya jamii. Baada ya kugundua hilo ni wajibu wake kuwa mbunifu na kuzuia madhara kutokea. Dr. Nchimbi ni kiongozi aliyembunifu, ndio maana katika kipindi chake UVCCM tulishuhudia jumuiya iliyoimara na kulinganishwa na jumuiya zenye nguvu kama ANC Youth League au iliyokuwa KANU Youth 1992...

13. Mfuatiliaji wa Katiba, Taratibu, Sheria na Kanuni za kiutendaji na kiuongozi...
Lazima tukubaliane kuwa uongozi ni utaratibu na sio maamuzi ya watu fulani. Ni taratibu, sheria na kanuni zinazowekwa kufikia malengo. Dr. Nchimbi marazote amekuwa muumini wa kufanya kazi zake kwa kufata utaratibu, sheria, na kanuni husika..

NB: Ni jambo la wazi kwamba kumchagua Dr. Nchimbi kuwa spika wa bunge la 11 la JMT nchi itakuwa imepata spika bora, mahiri na shupavu kama "John Bercow" wa House of Commons. Dr. Nchimbi ana uwezo, ana sifa, na kubwa zaidi anatosha..

Note: Haya ni mawazo huru, hayana muingiliano na kundi lolote!.....
 
Twende na Nchimbi
Ni msomi
Ni kijana
Ana uwezo
Ana uzoefu mkubwa
Anaweza kuunganisha watu wa mitizamo tofauti
Ni mwanadiplomasia
Ana kipaji cha uongozi
Ni rika la wabunge waliowengi ktk kipindi hiki
Anaijua ccm ndani nje
Anaijua nchi yetu
Anaweza tumsaidie atalisaidia bunge.
 
Tatizo kwenye u-doctorate wake wa P.hD thesis yake hakui-disseminate kama inavyotakiwa kwa watu wenye kufanya maandiko kama hayo. Kufanya research ngazi ya andiko hilo bila kufanya dissemination ni sawa na kuandika report ya mradi na kuiweka kabatini bila kuwapa watu wasome.Je! alikuwa anaficha nini? Hivyo hivyo na Mery Nagu;

Halafu muda wa masomo ya Bachelor then Master halafu PhD haushabihiani, hakuna andiko la PhD thesis yake ukaandia kwa mwaka mmoja.
 
mnasafishana eee!!!!

Magufuli anachagua majembe kama yeye kuunda Serikali, longolongo no chance!!
 
Hujasema sifa zote, hujasema ukanjanja na unafiki.
Ni hawa ndio Magu alizungumza atawatimua Lumumba.
Bond yake na Lowasa haileti Afya kwa Taifa.
 
hakugombea ubunge kwa sababu ya uspika .


atakatwa tu kama rafiki yake alivyokatwa kwenye urais.
 
hakugombea ubunge kwa sababu ya uspika .


atakatwa tu kama rafiki yake alivyokatwa kwenye urais.

Ubunge alikatwa na kitengo, baada ya kulalamika kukatwa Lowassa!
 
Mimi ukiniambia anasimamia anachokiamini sikuelewi maana tumeshuhudia hapa majuzi katoka nje ya kikao cha kamati kuu akisema CCM hawajatenda haki, halafu baada ya mwezi mmoja anapanda jukwaani kumnadi huyo mtu aliyesema hakupitishwa kwa haki, huu msimamo wa kinafiki umenifanya nimshushe vyeo
 
Jamani Sita hafai kabisa.Tungekuwa na katiba mpya sasa hivi na hii matatizo ingekuwa hakuna.afadhali ya polepole kuliko sita.huku Jusa haingii...Polex2 ajaribu.
 
fisadi wa elimu,hii ni kwa mujibu wa kaenerugaba
 
Spika wa bunge lijalo hatakiwi kabisa kuwa mtu wa mhemuko kama Ndugai, hebu tulieni kutafuta spika anayefaa ndani ya bunge au nje ya bunge. Daktari fake Emmanuel Mchimbi anamheko sana na aliunyesha wazi wakati wa kifo cha Mwangosi akiwa waziri wa mambo ya ndani , pia alivyolipokea suala la kukatwa Lowassa.

Katiba inawaruhusu Kikwete na Lowassa kuomba U-Spika
 
Twende na Nchimbi
Ni msomi
Ni kijana
Ana uwezo
Ana uzoefu mkubwa
Anaweza kuunganisha watu wa mitizamo tofauti
Ni mwanadiplomasia
Ana kipaji cha uongozi
Ni rika la wabunge waliowengi ktk kipindi hiki
Anaijua ccm ndani nje
Anaijua nchi yetu
Anaweza tumsaidie atalisaidia bunge.

Pia ni TEAM LOWASA!
 
Dr. Emmanuel Mchimbi akiwa spika wa bunge lijalo litamshinda saa 4 asubuhi tu, bunge litakuwa na mavuvuzela kama Nape, si mnakumbuka walivyokuwa wanapalulana wakati wa kugombea uenyekiti wa vijana. Bunge lijalo Emmuel Mchimbi uspika hatoshi.
 
Spika wa bunge lijalo hatakiwi kabisa kuwa mtu wa mhemuko kama Ndugai, hebu tulieni kutafuta spika anayefaa ndani ya bunge au nje ya bunge. Daktari fake Emmanuel Mchimbi anamheko sana na aliunyesha wazi wakati wa kifo cha Mwangosi akiwa waziri wa mambo ya ndani , pia alivyolipokea suala la kukatwa Lowassa.

Katiba inawaruhusu Kikwete na Lowassa kuomba U-Spika

Ungeongeza pia kuwa hatakiwi kuwa mtu wa mabavu kama Zungu. Tunataka mtu wa kanuni na logic
 
Huyu sina imani naye hata kidogo kwanza alikuwepo katika ile list ya mafisadi wa elimu sijui kwanini hakumpeleka mahakamani mtunzi wa kile kitabu.
 
Hivi watanzania mtaacha lini tabia ya kuabudu watu na hatimaye kuanza kuwauza au kwa swahili cha mtaani kuwapigia debe.Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu kuwa kinga yake na huku amemwaacha Mungu.
Anaitwa Dr Emmanuel John Nchimbi, Moja Kati Ya Masenior Comredi Ndani Ya Chama Cha Mapinduzi Ni Mtu Mahiri Katika Kile Anachokiamini Na Hafundishwi Punda Kumwita Falasi .......

Ni Mwanasiasa Mwenye Nguvu Ndani Na Nje Ya ccm katika Ushawishi na Ukubalikaji wake ........
Wasifu wake kiuongozi ni mpana sana Ameanza Kuwa Raisi Wa Chuo Kikuu Mzumbe Akaja kuwa Mwenyekiti Wa uvccm Taifa Akagombea Ubunge jimbo La songea mjini akirisi mikoba ya Laurensi gama

Amekuwa mbunge kwa miaka kumi na amekuwa waziri kamili katia wizara mbili tofauti Wizara Ya Nyumba Na Makazi Na Wizara Ya mambo ya ndani pia Amekuwa naibu waziri katika wizara mbili tofauti wizara ya habari tamaduni na michezo pamoja na wizara ya mambo ya ndani....

Anasifika kwa uwelewa mpana wa mambo ya kitaifa katika nyanja mbali mbali kijamii kisiasa na kiuchumi.....

Ameweza kuwatenegeza wanasiasa wengi mashughuli wakiwemo madc na wabunge wabunge lijalo katika baraza la vijana taifa la mwaka 2008

Makatibu wa uvccm na wa wilaya na mikao ni product yake pia ni mjumbe kamati kuu kwa miaka isopungua 17 anajua ajenda za chama na kitaifa

Kijana na msomi mwenye uwezo wa kulimudu Bunge lijalo la 11

#Twende na Nchimbi Uspika
 
Back
Top Bottom