Huyu ndio firauni

Huyu ndio firauni

Haitoshelezi kwa mujibu wa atavyotaka yeye.

Aya inatosheleza kwa mujibu wa ilivyosema yenyewe.

Mkuu hii aya imesema

"..walio nyuma yako "

Yaani watu ambao tayari wapo katika wakati huo.

Na aya haokusema "watakaokuja baadae"

Makusudio ya aya ni wale ambao waliokuwepo wakati wa firauni na sio mpaka akina sisi wa hivi leo.

Aya haikushindwa kusema ".watakaokuja baada ya firauni..."

Lakini makusudio kama ilivyo aya inavyosema haigusii watu wa baadae.

Hivyo huyo atabaki kuwa firauni feki wa kibiashara mkuu
So huyu sio yule farao aliyekusudiwa hapo?

Probably uko sahihi kwasababu neno pharao ilikua ni cheo cha juu kama raisi ila huyo pichani ana jina anajulikana kama ramisses ii

Pengine quran ingemtaja kwa jina lake na sio kwa cheo tungeweza kujua nani anayekusudiwa
 
Hiyo ni moja ya aya zinazomzungumzia Firauni jinsi alivyogharikishwa na alivyoomba mkiri Allah na Allah alivyo ahidi kile angemtendea, angalia moja ya aya hii ya juu yake inavyosema:-
View attachment 1854125
Mkuu hivi hii habari kwako hauoni kwamba haipo specific kwasababu haijaenda directly kum-point mlengwa kwa kutaja jina lake?

Wewe binafsi unaamini pharao ni cheo au jina la mtu?

Katika historia ya utawala wa misri kuna series ya ma-pharao how do we know for sure kua huyu ramisesees ndio yule aliyekusudiwa kwenye kuran wakati kule alijulikana kwa cheo chake tu?

Ni sawa na hapa tuwe tunasema raisi alikufa bila kutaja jina utaweza kuelewa raisi gani anayekusudiwa?
 
Mkuu hii aya imesema

"..walio nyuma yako "

Yaani watu ambao tayari wapo katika wakati huo.

Na aya haokusema "watakaokuja baadae"

Makusudio ya aya ni wale ambao waliokuwepo wakati wa firauni na sio mpaka akina sisi wa hivi leo.

Aya haikushindwa kusema ".watakaokuja baada ya firauni..."

Lakini makusudio kama ilivyo aya inavyosema haigusii watu wa baadae.

Hivyo huyo atabaki kuwa firauni feki wa kibiashara mkuu.


Mkuu, Safuher, unaposoma Qur'an jaribu kutafakari kila neno, sentensi na maneno ya mwisho wa aya husika, angalia maneno ya mwisho yanavyosema;-

و ان كتيرا من الناس عن اياتن لعافلون

Yaani; Na hakika WATU WENGI wameghafilika na ishara zetu.

Ishara hii ya Mwili wa Firauni watu wengi waliopita na waliopo leo wameghafilika nayo na ndio maana wanatokea watu wanapinga kwamba huo sio ule mwili wa Firauni na mbaya zaidi Waisilamu ndio wanashadidia kupinga ukweli wa Qur'an bila kujua kwamba ni Wasio Waisilamu ndio wanaoeneza huo upinzani ili Qur'an ionekane ni kitabu cha uongo na visa vya kubuni vya Mtume mkukufu (saw) Mungu apishe mbali na hivyo kuzidi kuwaghafilisha watu.

Kwahiyo Maneno ya mwisho wa hiyo aya ndiyo ya kuzingatiwa kwani watu wanaosemwa hapo ni wale waliopita pamoja na sisi, kimsingi aya hiyo ya Qur'an inatuhusu sisi tulio hai leo na hivyo ishara hiyo inatuhusu sisi, mimi ,wewe na yule.
 
So huyu sio yule farao aliyekusudiwa hapo?
Huyu wa pichani hausiani na aliyetajwa kwenye Qurani.

Kwa sbabau Qurani haikusema kwamba atabaki mpaka leo.

Hata mtume muhammad ambaye ndo kashushiwa Qurani hakuwahi kusema pale maka kwamba jamani eeeh huyu firauni mnajua kwamba yupo mpaka leo hivi mimi naongea hapa makka.

Hakuwahi kusema,ni jambo limeibuka miaka kadhaa hapa nyuma muda mrefu baada ya mtume muhammad.
Probably uko sahihi kwasababu neno pharao ilikua ni cheo cha juu kama raisi ila huyo pichani ana jina anajulikana kama ramisses ii
Naskia pia kwamba farao ni cheo ila katika Qurani kama sikosei firauni aliyetajwa maarufu ni huyu jamaa wa nabii mussa aliyejitia uungu,sijui kama kuna firauni mwingine katajwa katika Qurani.
Pengine quran ingemtaja kwa jina lake na sio kwa cheo tungeweza kujua nani anayekusudiwa
Naam pengine lakini huyu wa Qurani ni yule aliyekuwa amemlea nabii mussa,sidhani kama nabii mussa kalelewa na firauni wawili.

Hivyo firauni ambaye kaishi na kusumbuana na nabii mussa kwa mujibu wa Qurani ndiye huyo huyo.

Labda iwe wakati wa nabii mussa walipita firaauni wengi,ikiwa hivyo itakuwa naam ishu ngumu kumjua firauni wa ngapi
 
Huyu wa pichani hausiani na aliyetajwa kwenye Qurani.

Kwa sbabau Qurani haikusema kwamba atabaki mpaka leo.

Hata mtume muhammad ambaye ndo kashushiwa Qurani hakuwahi kusema pale maka kwamba jamani eeeh huyu firauni mnajua kwamba yupo mpaka leo hivi mimi naongea hapa makka.

Hakuwahi kusema,ni jambo limeibuka miaka kadhaa hapa nyuma muda mrefu baada ya mtume muhammad.

Naskia pia kwamba farao ni cheo ila katika Qurani kama sikosei firauni aliyetajwa maarufu ni huyu jamaa wa nabii mussa aliyejitia uungu,sijui kama kuna firauni mwingine katajwa katika Qurani.

Naam pengine lakini huyu wa Qurani ni yule aliyekuwa amemlea nabii mussa,sidhani kama nabii mussa kalelewa na firauni wawili.

Hivyo firauni ambaye kaishi na kusumbuana na nabii mussa kwa mujibu wa Qurani ndiye huyo huyo.

Labda iwe wakati wa nabii mussa walipita firaauni wengi,ikiwa hivyo itakuwa naam ishu ngumu kumjua firauni wa ngapi
Kwani muhammad aliishi wapi?

Sio mekka?
 
Mkuu, Safuher, unaposoma Qur'an jaribu kutafakari kila neno, sentensi na maneno ya mwisho wa aya husika, angalia maneno ya mwisho yanavyosema;-

و ان كتيرا من الناس عن اياتن لعافلون

Yaani; Na hakika WATU WENGI wameghafilika na ishara zetu.

Ishara hii ya Mwili wa Firauni watu wengi waliopita na waliopo leo wameghafilika nayo na ndio maana wanatokea watu wanapinga kwamba huo sio ule mwili wa Firauni na mbaya zaidi Waisilamu ndio wanashadidia kupinga ukweli wa Qur'an bila kujua kwamba ni Wasio Waisilamu ndio wanaoeneza huo upinzani ili Qur'an ionekane ni kitabu cha uongo na visa vya kubuni vya Mtume mkukufu (saw) Mungu apishe mbali na hivyo kuzidi kuwaghafilisha watu.

Kwahiyo Maneno ya mwisho wa hiyo aya ndiyo ya kuzingatiwa kwani watu wanaosemwa hapo ni wale waliopita pamoja na sisi, kimsingi aya hiyo ya Qur'an inatuhusu sisi tulio hai leo na hivyo ishara hiyo inatuhusu sisi, mimi ,wewe na yule.
Mkuu mimi na wewe tunapata mazingatio kumsoma firauni histofia yake.

Wale waliokuwa nae walipata mazingatio kwa kumuona tayari akiwa amekufa.


Kwahiyo Maneno ya mwisho wa hiyo aya ndiyo ya kuzingatiwa
Kama wewe huyazingatii mkuu ninwewe,mimi mpaka haya ya mwanzo nayazingatia kwa sababu ndo yenye habari kamili.

Huwezi kusema nisizingatie habari mku.

Aya inasema "waiopo kabla yake"

Hii ibara haifidishi na watakaokuja hakuna utaalamu huo. Neno waliopo ni sasa sio watakaokuja.
Wasio Waisilamu ndio wanaoeneza huo upinzani ili Qur'an ionekane ni kitabu cha uongo na visa vya kubuni vya Mtume mkukufu (saw) Mungu apishe mbali na hivyo kuzidi kuwaghafilisha watu.
Mimi sioni shida kuwa pamoja kimsimamo na asiyekuwa muislamu pale ambapo tunaendana kimawazo,kwani pengine asiyekuwa muislamu akalielewa jambo la sawa.
 
Unachosema ni kweli kwamba Mafarao wote miili yao ilikuwa mumified (kukaushwa) na hii ilikuwa ni jadi au mila yenye fahari kubwa sana kwao, lakini katika hao Mafarao aliyekuwa Jeuri na Katili na kibri ni huyo Farao wa Musa (the pharaoh of oppression/Marenpth), huyu alikulia nyumba moja ya kifalme pamoja na Musa, kipindi hicho Baba yake ndiye alikuwa Farao, hivyo Nabii Musa alikuwa anamjua vizuri sana tabia za huyo Firauni of oppression.

Musa alipokimbia nchi pale alipoua mtu kwa ngumi baada ya miaka kupita yule Firauni aliyewalea Musa na huyo Marenptha akafariki ndipo Marenptha akawatawazwa kuwa Farao na Musa akapata hizo habari akiwa ukimbizini kwamba Marenptha kawa Farao, na kama utasoma Qur'an utaona jinsi Musa alivyomjibu Mungu akiwa na khofu kwamba atawezaje kumpelekea ujumbe wa Mungu kwamba kuna Mungu mwingine na sio yeye Firauni na pia huyo Mungu anataka kuwachukua wana wa Israeli na aindoke nao, Musa alikuwa anamjua toka walipokuwa watoto
jinsi Pharao Marenptha alivyokuwa Jeuri na kibri.

Kifupi ni kwamba, ni Farao marenptha ndiye aliyekuwa katili na jeuri na ndiye huyo aliyejiita Mungu na akataka aabudiwe na Mungu akamuadhibu kwa kumzamisha majini huku akitubu na kumkiri Mungu wa Musa--- ndipo Mungu akasema atauhifadhi mwili wake ili iwe ishara kwa watu wajao, mwili unapokuwa majini unaweza kuharibika au kuliwa na samaki nk, lakini Mungu alitaka Mwili wa huyo Firauni upatikane na ufanyiwe Mumification ili iwe ishara kwetu kwamba alipita mtu mmoja mwembamba, jeuri, katili, kibri aliyejifanya Mungu na alipingana na Nabii wa Mungu.
Hadithi za kusadikika.
 
Kwani muhammad aliishi wapi?

Sio mekka?
Naam maka na madina.

Kama unataka kuuliza "atajuaje habari za misri kama firauni yupo au hayupo "

Basi najibu hivi

"Habari za firauni na mussa zimetokea huko huko lakini yeye kajua akiwa huko huko makka"

Hivyo na habari hii ilikuwa jambo jepesi kujua kwamba jamaa yupo mpaka sasa.

Labda kama umekusudia ksema vingine.
 
Mkuu hivi hii habari kwako hauoni kwamba haipo specific kwasababu haijaenda directly kum-point mlengwa kwa kutaja jina lake?

Wewe binafsi unaamini pharao ni cheo au jina la mtu?

Katika historia ya utawala wa misri kuna series ya ma-pharao how do we know for sure kua huyu ramisesees ndio yule aliyekusudiwa kwenye kuran wakati kule alijulikana kwa cheo chake tu?

Ni sawa na hapa tuwe tunasema raisi alikufa bila kutaja jina utaweza kuelewa raisi gani anayekusudiwa?


Huyo anajulikana kama Farao wa Musa, ni Farao aliyepambana na Musa , ni Farao aliyekufa kwa kuzama baharini ni Farao aliyekuwa exceptional brute, hivyo pamoja kwamba cheo cha Farao ni common among the Ancient Egyptian rulers lakini kuna sifa unique za huyo Farao tunayemzungumzia.
 
Aya inasema "waiopo kabla yake"

Hii ibara haifidishi na watakaokuja hakuna utaalamu huo. Neno waliopo ni sasa sio watakaokuja.


Ngoja niandike transilliteration ya maneno ya kiarabu ya hiyo aya ikiambatana na tarjama zake za neno kwa neno.

Fa alyaum= Basi leo hii
nunajjyka=tutauokoa
bibadanika=(kwa) mwili wako
liyakuuna=kwa ajili (ili uwe)
liman KHALFAKA ayat= kwa ajili ya wanaokuja, ishara (iwe ni ishara kwa wanaokuja baada yako).

Khalfaka= wanaokuja baada yako, baada ya wewe kuondoka, kufa, kustaafu nk.
 
Watu wa zamani walikuwa wembamba sana!!?
hana nyama kabisa huyu Pharao....
cheki mkono!!?


Huyo alikuwa mtu mwembamba, mfano ni kama Rais fulani wa nchi jirani, sio kwamba watu wa zamani walikuwa wembamba laa bali walikuwepo watu wa aina zote.
 
Wanazuoni wetu wakubwa wanakataa ya kuwa huyu si yule aliye zungumziwa katika Qur'aan na kwamba ayahifadhiwa,sababu walio kusudiwa ili wuone ni wale wale Waisraeli wa zama hizo na wali muona na ikawa ushahidi kwao.

Hakuna anaye weza kuthibitisha ya kuwa huyu ni yeye na kumnasibisha na aya ya Qur'aan ni uchachefu wa maarifa. Shaykh Ibn 'Uthaymiin (Allah amrehemu) ameliezea hili kwa upana.

Ziada ya maneno kuhusu mwili wa Firaun,ni baada ya wana wa Israeli walikuwa wana shaka juu ya kifo cha Firaun,ndiyo maana Allah akaimrisha bahari imteme,na kweli walikuja kumuona na kusadiki,haya ameuasema swahaba Ibn Abbas,rejea Tafsir Ibn Kathir. Kadhalika maelezo ya Imamu Mujaahidi.

Kadhalika rejea Tafsir ya Ibn Ashuuri iitwayo "Tahriri wa Tanwiir".
Hizo ni hadithi kama hadithi za bweha na sungura
 
Unachosema ni kweli kwamba Mafarao wote miili yao ilikuwa mumified (kukaushwa) na hii ilikuwa ni jadi au mila yenye fahari kubwa sana kwao, lakini katika hao Mafarao aliyekuwa Jeuri na Katili na kibri ni huyo Farao wa Musa (the pharaoh of oppression/Marenpth), huyu alikulia nyumba moja ya kifalme pamoja na Musa, kipindi hicho Baba yake ndiye alikuwa Farao, hivyo Nabii Musa alikuwa anamjua vizuri sana tabia za huyo Firauni of oppression.

Musa alipokimbia nchi pale alipoua mtu kwa ngumi baada ya miaka kupita yule Firauni aliyewalea Musa na huyo Marenptha akafariki ndipo Marenptha akawatawazwa kuwa Farao na Musa akapata hizo habari akiwa ukimbizini kwamba Marenptha kawa Farao, na kama utasoma Qur'an utaona jinsi Musa alivyomjibu Mungu akiwa na khofu kwamba atawezaje kumpelekea ujumbe wa Mungu kwamba kuna Mungu mwingine na sio yeye Firauni na pia huyo Mungu anataka kuwachukua wana wa Israeli na aindoke nao, Musa alikuwa anamjua toka walipokuwa watoto
jinsi Pharao Marenptha alivyokuwa Jeuri na kibri.

Kifupi ni kwamba, ni Farao marenptha ndiye aliyekuwa katili na jeuri na ndiye huyo aliyejiita Mungu na akataka aabudiwe na Mungu akamuadhibu kwa kumzamisha majini huku akitubu na kumkiri Mungu wa Musa--- ndipo Mungu akasema atauhifadhi mwili wake ili iwe ishara kwa watu wajao, mwili unapokuwa majini unaweza kuharibika au kuliwa na samaki nk, lakini Mungu alitaka Mwili wa huyo Firauni upatikane na ufanyiwe Mumification ili iwe ishara kwetu kwamba alipita mtu mmoja mwembamba, jeuri, katili, kibri aliyejifanya Mungu na alipingana na Nabii wa Mungu.
Hakuna record zozote za wa misri wa kale wanasema Israel iliwahi kuwa utumwani Misri.. Hii ilikua janja ya Wayahudi kujihusisha na utamaduni mkubwa wa enzi hizo
 
Hizo ni hadithi kama hadithi za bweha na sungura
Mpaka una kufa huwezi kuthibitisha hili.

Kuna watu kama nyinyi huwa tuna wapuuza. Sababu huna ukijuacho zaidi ya kuandika kama hivi. Unakuta hapo hata maana ya Hadithi hujui. Hili tatizo kubwa mno.
 
Hakuna record zozote za wa misri wa kale wanasema Israel iliwahi kuwa utumwani Misri.. Hii ilikua janja ya Wayahudi kujihusisha na utamaduni mkubwa wa enzi hizo
Thibitisha hili.
 
Hakuna record zozote za wa misri wa kale wanasema Israel iliwahi kuwa utumwani Misri.. Hii ilikua janja ya Wayahudi kujihusisha na utamaduni mkubwa wa enzi hizo


Siyo Israeli bali wana wa Israeli ndio walikuwa utumwani na nabii Musa as aliondoka nao, kipindi hicho nchi hiyo the Ancient Egypt ilikuwa chini ya Wamisri (sio hawa waarabu walioingia hivi karibuni na ku dominate nchi nzima leo).

Soma historia ya wana wa Israeli jinsi walivyoingia huko Misri, anzia na Nabii Yusuf (Joseph mwana wa Yakobo).
 
Back
Top Bottom