Huyu ndio gwiji, jabali na Mfalme wa muziki nchini Tanzania

Hili bonge la tungo. Unapaswa kupongezwa.
 
Umenikuna sana kwa post hii. Yani umenifanya nikumbuke mbali sana aloo.
 
Juma Kilaza (Qubqn Malimba), Peter Kinyonga,Malanga Thom (Jamhuri Jazz baadaye Simba wa Nyika)
 
Sasa hapa huyu gwiji WA zilipemdwa kila zama na kitabu chake
 
Sasa hapa huyu gwiji WA zilipemdwa kila zama na kitabu chake
Ni kweli kila zama na kitabu chake, lakini huyu ameacha alama ambayo inaenziwa kwa namna fulani.

Hata wimbo wa zuwena wa Diamond ume copy kutoka katika wimbo wa zuwena wa Marijani Rajabu. Hapo bado sijazungumzia wakongwe wengi walio copy nyimbo zake zikawatoa.

Hata Bob Marley ni zilipendwa, lakini kazi yake iliacha alama inayokumbukwa mpaka leo.
 
Ahh! Mashairi ya Mzee Marijani Rajabu..... sio mchezo. Mwenyezimungu amlaze mahali pema peponi. Bahati kazaliwa ndani ya nchi isiyothamini vipaji vya watu wake.
Kweli mkuu, wenzetu wa Congo mwaka jana walizindua sanamu la kumuenzi Francoo, na kuliweka katikati ya jiji la Kinshasa. Ila sisi hatuna wazo la kuwaenzi wanamuziki wetu hata mmoja.
 
Dah nimezaliwa miaka ya katikati ya 90 na 2000 na nimetoka kapa kabisa!

Au nami mtaniita kizazi cha akina mondi?
 
Kweli mkuu, wenzetu wa Congo mwaka jana walizindua sanamu la kumuenzi Francoo, na kuliweka katikati ya jiji la Kinshasa. Ila sisi hatuna wazo la kuwaenzi wanamuziki wetu hata mmoja.
Nakubaliana na wewe kabisa. Tanzania ni nchi ya ajabu sana. Mzee Marijani alikuwa mtu wa msimamo na mwenye kujiheshimu. Wakati wanamuziki wenzake wanakimbila bendi za siasa kama Juwata, Vijana Jazz na Mlimani Park, yeye hakufuata huo mkumbo. Alijiamini sana. Uchawa ilikuwa mwiko kwake.

Alipenda kua mowanamuziki huru na anaejitegemea. Bahati mbaya, finali haikuwa njema kwake. Utu uzima, ufukara na mabadiliko ya muziki wa dansi vileta mitihani mikubwa sana kwa wanamuziki wa dizaini yake.

Mwenyezimungu amlaze mahali pema peponi.
 
Kwa TZ unaweza kuwa na elimu na bado usiwe msaada kwa taifa zaidi ya kuwa fisadi wa kalamu, pia nae akute angekufa kifo cha kuacha maswali kama Sokoine tu
 
1. Marijani Radjab
2. Bitchuka
3. Maneti
4. Shaban Dede
5. Muhidin Gulumo
6. Tx Moshi
7. Mbaraka Mwinshehe
2: Hassan Rehani Bichuka
3: Hemed Maneti
5: Muhidin Ngurumo


Kuna

Nico Zengekala
Cosmas Chidumule


Ama kweli mziki wa zamani kwa sisi vijana wa 90s unatumbusha mbali sana. Baba yangu alikua na kanda za kaseti nyingi sana za Juwatta Jazz Band, hadi ilipokua Ottu Jazz Band na mwisho Msondo Ngoma Music Band. Pia kaseti za DDC Mlimani Park ambayo nadhani ilikua rival band na hii Ottu Jazz Band. Ahhhh i miss the old days.​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…