Hapana,Mbona kuna yule mama muuza mkaa anamsomesha binti yake urubani?Huo ndio uzuri wa kuzaliwa kwenye pesa. OVAAAAA!!!
Mkiwa maskini, hata wazazi waombe vipi, ni kama maombi yao hayafiki vile
Mathematics Mbona unaicha?Urubani hauhitaji akili nyingi.
Ukiwa na mambo 3 tu inatosha.
1. Pesa
2. Utimamu wa akili na mwili
3. Lengo.
Hata ukipata form form D tatu ikiwemo angalau moja ya mathematics au physics inatosha. Ukiwa maskini sahau urubani maishani mwako hata upate A masomo yote, labda utapaisha ndege za jeshi tu
Kweli aseeHuo ndio uzuri wa wwzazi kuombea ndoto za watoto.
Wengi hatujatimiza ndoto zetu sababu shetani na majeshi yake wamezinyakuwa, hatukuwa na wa kutuombea
Sijui kwa kweli, Sipo huko....Capt. Lian naye bado yupo au ameshastaafu?
Ninauliza tu, Ameolewa?Wakuu Habarini
Kuna post zimekuwa zikisambaa mitandaoni zikimuonyesha mmoja wa marubani ambaye ni mtoto wa Mwl Mwakasege, na kila mtu akizumzungumzia lake + kumpongeza kwa ndoto zake.
Huyu ni mmoja wa marubani wawili waliorusha ndege iliyobeba mwili wa Rais Magufuli. Anaitwa Anna Tusajigwe Mwakasege. Ni binti wa pili wa Mwalimu Christopher na mama Diana Mwakasege.
Anna alipata maono ya kuwa rubani akiwa darasa la 3 tu. Baba yake akampeleka uwanja wa ndege angalau kuona ndege "live" badala tu ya kuziona angani tu. Alipofika darasa la 5 baba yake alitembeza uwanja mdogo wa ndege Arusha ambapo alipata nafasi ya kuongea na marubani kuhusu ndoto yake, nao wakampa ushauri masomo ya kusoma ili aweze kuifikia ndoto hiyo.
Alijifunza urubani Afrika kusini, na siku anarusha ndege kwa mara ya kwanza baba yake hakulala usiku huo (hii ni story ya wakati mwingine).
Lakini kwa sasa Anna ni miongoni mwa marubani wa shirika la ndege ATCL. Kabla ya kujiunga na ATCL alifanya kazi mashirika mengine makubwa ya ndwge kama SAA na kupata uzoefu wa kuendesha ndege kubwa kama Boeing 747, Boeing 777 na Airbus A340.
Hongera Anna kwa kuaminiwa kuendesha ndege iliyobeba mwili wa Rais. Umeweka alama kubwa kwa taifa hili, ambayo haitafutika kirahisi. Mara zote tutakapokumbuka kifo cha JPM tutakumbuka kuwa wewe kama Senior First officer na rubani mwenzio (kiongozi) ndio mlipata neema ya kubeba mwili wake.
Najua si kazi rahisi kuendesha ndege ukiwa na majonzi ya kumpoteza Rais wako lakini umeaminiwa na umeweza. Tunawaombea kwa safari ya Zanzibar, Mwanza na Chato. Wewe pamoja na cabin crew yote. Hakika wanawake mnaweza. View attachment 1732239
Mbona kama Unajihami vile Kimtindo?umeanza vizuri tu,
na sijasema kama umemaliza vibaya
Umemuita hapa huyu ili aje afanye nini?
Na mwenzako kauliza eti ameolewa? kwa Mnyakyusa naona tabia na mila hataziacha bado mwanamume atakuwa juu kwake.Tokea Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ameapa nimeanza kuona Kirusi fulani kama cha Kijeuri au Cha Kushindana au cha Kututambia Sisi Wanaume kwamba kwakuwa Mpini wa Ikulu umeshikwa na Mwanamke basi Wanaume tutawakoma na tujiandae Kisaikolojia.
Ndoto yangu kabla sijaujua ukweli wa mambo..nilipokuja kutajiwa kuwa angalau niwe na M150 nikaona si baht yangu acha tu niwe abiria wa kawaida[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Urubani hauhitaji akili nyingi.
Ukiwa na mambo 3 tu inatosha.
1. Pesa
2. Utimamu wa akili na mwili
3. Lengo.
Hata ukipata form form D tatu ikiwemo angalau moja ya mathematics au physics inatosha. Ukiwa maskini sahau urubani maishani mwako hata upate A masomo yote, labda utapaisha ndege za jeshi tu