Huyu ndiye binti wa Mwl Mwakasege ambaye ni mmoja wa marubani aliyerusha ndege iliyobeba mwili wa Rais Magufuli

Huyu ndiye binti wa Mwl Mwakasege ambaye ni mmoja wa marubani aliyerusha ndege iliyobeba mwili wa Rais Magufuli

Urubani hauhitaji akili nyingi.
Ukiwa na mambo 3 tu inatosha.
1. Pesa
2. Utimamu wa akili na mwili
3. Lengo.
Hata ukipata form form D tatu ikiwemo angalau moja ya mathematics au physics inatosha. Ukiwa maskini sahau urubani maishani mwako hata upate A masomo yote, labda utapaisha ndege za jeshi tu
Mathematics Mbona unaicha?
 
Natambua sana Umahiri na Uweledi wa Mwanadada Ana T. Mwakasege (Mtoto wa Mwalimu wa Kiroho Mwakasege ) hasa katika Suala zima la Kurusha Ndege (kuwa Rubani) tena sasa akiwa ni wa Shirika letu la ATCL.

Kinachonishangaza sasa tu ni kuona katika Mitandao mbalimbali Picha inayotamalaki (trend) sasa ni ya Kumuonyesha huyu Dada Ana Mwakasege ambaye bado ni Co - Pilot ( Rubani Msaidizi ambaye katika Cockpit hukaa upande wa Kulia) akisifiwa kuwa ndiyo amerusha Ndege iliyobeba Mwili wa Hayati Rais Dkt. Magufuli kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma huku Rubani Mwandamizi (Mkuu) ambaye Kicheo ndiyo huwa Captain (ambaye katika Ndege huwa anakaa upande wa Kushoto) kule katika Cockpit yao.

Tokea Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ameapa nimeanza kuona Kirusi fulani kama cha Kijeuri au Cha Kushindana au cha Kututambia Sisi Wanaume kwamba kwakuwa Mpini wa Ikulu umeshikwa na Mwanamke basi Wanaume tutawakoma na tujiandae Kisaikolojia.

Mheshimiwa Rais wangu Mama Samia Suluhu Hassan na Wewe ukijiroga tu ukaingia katika Mfumo huu wa Kijeuri ambao Wanawake Wenzako wanataka Kukuingiza watakuponza na huenda hata ukakosa Ushirikiano wa kutosha kutoka Kwao (Kwetu) Wanaume ma hatimaye Uongozi ukakushinda na ukapigwa Zengwe la maana na ukapakimbia Mwenyewe hapo Ikulu.

Wewe ni Rais wa Tanzania na siyo Rais wa Wanawake wote nchini Tanzania. Ni Kakirusi ka Kipuuzi kama siyo ka Kipumbavu naona kanaanza tu Kujizolea Umaarufu na kuwavimbisha Vichwa Wanawake. Pamoja na Samia ndiyo Rais na ni Mwenzenu Kijinsia, ila mkiwa na Sisi Wanaume mkizingua au mkituzingua tu hata Kuachika mtaachika vile vile.

Imeisha hiyo!
 
Wakuu Habarini

Kuna post zimekuwa zikisambaa mitandaoni zikimuonyesha mmoja wa marubani ambaye ni mtoto wa Mwl Mwakasege, na kila mtu akizumzungumzia lake + kumpongeza kwa ndoto zake.

Huyu ni mmoja wa marubani wawili waliorusha ndege iliyobeba mwili wa Rais Magufuli. Anaitwa Anna Tusajigwe Mwakasege. Ni binti wa pili wa Mwalimu Christopher na mama Diana Mwakasege.

Anna alipata maono ya kuwa rubani akiwa darasa la 3 tu. Baba yake akampeleka uwanja wa ndege angalau kuona ndege "live" badala tu ya kuziona angani tu. Alipofika darasa la 5 baba yake alitembeza uwanja mdogo wa ndege Arusha ambapo alipata nafasi ya kuongea na marubani kuhusu ndoto yake, nao wakampa ushauri masomo ya kusoma ili aweze kuifikia ndoto hiyo.

Alijifunza urubani Afrika kusini, na siku anarusha ndege kwa mara ya kwanza baba yake hakulala usiku huo (hii ni story ya wakati mwingine).

Lakini kwa sasa Anna ni miongoni mwa marubani wa shirika la ndege ATCL. Kabla ya kujiunga na ATCL alifanya kazi mashirika mengine makubwa ya ndwge kama SAA na kupata uzoefu wa kuendesha ndege kubwa kama Boeing 747, Boeing 777 na Airbus A340.

Hongera Anna kwa kuaminiwa kuendesha ndege iliyobeba mwili wa Rais. Umeweka alama kubwa kwa taifa hili, ambayo haitafutika kirahisi. Mara zote tutakapokumbuka kifo cha JPM tutakumbuka kuwa wewe kama Senior First officer na rubani mwenzio (kiongozi) ndio mlipata neema ya kubeba mwili wake.

Najua si kazi rahisi kuendesha ndege ukiwa na majonzi ya kumpoteza Rais wako lakini umeaminiwa na umeweza. Tunawaombea kwa safari ya Zanzibar, Mwanza na Chato. Wewe pamoja na cabin crew yote. Hakika wanawake mnaweza. View attachment 1732239
Ninauliza tu, Ameolewa?
 
umezungumzia tishio la kupanda juu
Tokea Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ameapa nimeanza kuona Kirusi fulani kama cha Kijeuri au Cha Kushindana au cha Kututambia Sisi Wanaume kwamba kwakuwa Mpini wa Ikulu umeshikwa na Mwanamke basi Wanaume tutawakoma na tujiandae Kisaikolojia.
Na mwenzako kauliza eti ameolewa? kwa Mnyakyusa naona tabia na mila hataziacha bado mwanamume atakuwa juu kwake.

Kuna jamaa yangu kaoa mwaka jana, lakini miezi hiyo alikuwa akimfuatilia (Kumchumbia si kirasmi) kwa hiyo naona hajaolewa
 
Urubani hauhitaji akili nyingi.
Ukiwa na mambo 3 tu inatosha.
1. Pesa
2. Utimamu wa akili na mwili
3. Lengo.
Hata ukipata form form D tatu ikiwemo angalau moja ya mathematics au physics inatosha. Ukiwa maskini sahau urubani maishani mwako hata upate A masomo yote, labda utapaisha ndege za jeshi tu
Ndoto yangu kabla sijaujua ukweli wa mambo..nilipokuja kutajiwa kuwa angalau niwe na M150 nikaona si baht yangu acha tu niwe abiria wa kawaida[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom