Huyu ndiye msanii mwenye mafanikio makubwa kuliko yeyote Tanzania nzima

🙂 🙂 punguza kidogo mkuu, weka hata Kenyan shillings kidogo tuamini
hah hah hah hah mkuu unaomba kama umepungukiwa tsh100 ya nauli daaah.
 
Hapana ajavurungwa hesabu za makum na mamia zilimpita.

Mo IBrahim (Mohamed ) huyu aliyetajwa na jarida la fobes kama tajiri namba moja TZ kwa mwaka 2016 ana utajiri wa
$ 1.1 b, mwanamuziki JAY Z ana $ 648 millioni, sasa hao kina AY, cjui WIZKID, Diamond na wengine jiulize wana utajiri wa kiasi gani kama Jay Z ndiyo yuko hapo.
 
Hakuna utafiti hapo tabia zingine zinakuja automatically ndio maana watoto wa kike wanapenda chips na watoto wa kiume wanapenda mihogo hapo hakuna utafiti ukiwa kidume lazima uwe na tabia za tofauti.

Sasa wewe inavyoonekana ipo wazi kabisa wewe ni MWANAMKE...Ukibisha kama sio MWANAMKE uweke evidence ya picha maana WANAUME hatuna tabia za kuchukiana tena bila sababu yoyote eti "mimi simpendi tu" ebooo
 
Mkuu ingia Google tafuta top ten richest musician in East Africa, huyo jamaa yako hata top ten hayupo,cheki hii top four.
Jose chameleon
Diamond
Akothe
Jaguar
Wacha kukariri, tambua kuwa kuna search engine zaidi ya hiyo google. Na kibaya zaidi hata mtu akiingia hapo google hawezi kutoka na data kamili za kudhibitisha hayo maelezo yako..
 
Hahhaahaaaa hiyo ipo kabisa na una haki ya kuyasema ya moyoni, jamaa namkubali ila FA anavijitabia vya malingo flani vinaboa sana ila mi kuna mtu anaitwa Tunda Man nilimchukia toka siku nimesikia nyimbo yake ya kwanza toka enzi hizo nimejeribu kubalisha jinsi ninavyomchukulia ila nikisikia tuu sauti yake kuna kitu ndani kwa ndani nakasirika ghafla, Mungu anisaidie tuu kuniondolea hii chuki isiyo a sababu.
 
Mkuu ingia Google tafuta top ten richest musician in East Africa, huyo jamaa yako hata top ten hayupo,cheki hii top four.
Jose chameleon
Diamond
Akothe
Jaguar
Akhothee???
Kweli Mungu hamtupi mja wake
Nikilinganisha interview yake AYO TV na millard ayo
 
SIO KWELI, UMEONGEZA CHUMVI NYINGI SANA

Hebu tutajie hizo biashara nyingi zaidi ya lile duka la nguo pale sinza.

Ulipima hizo ekari zake zikafika 100? Hilo shamba liko kweli? Ukiambiwa ukalioneshe unaweza mkuu?

Hivyo vipindi vya EATV vinamuingizia shilingi ngapi?
 
Haupo peke yako mkuu
 
Nakuunga mkono katika swala la mtu kuchukia mtu lakini kiungwana hua tunachukia mtu huku tukiappreciate mchango wa mtu husika katika swala fulani.
Mfano mimi kuna wasanii siwapendi na showbiz zao lakini naappreciate walipoufikisha muziki wetu, sikumpenda marehemu as a person lakini nilimheshimu kwa mchango wake katika ubondia.
 
hata masanja alivyosema utajiri wake unatokana na kilimo raia mlibisha sana kwhyo sikushangai
 
Ni kweli kabisa usemacho, na utajiri wake kwasasa ni 5.6b$.
Mwenzie kwa mujibu wa jarada la Forbes domo la mond utajiri wake ni $4.5 million ambayo ni zaidi ya TZS 10bil na ndo anaongoza East Africa akifatiwa na Chameleone anayemiliki vitu vya thamani ya $3.9million ndo wanafata Akothee na Jaguar wa Kenya! AY yuko vizuri lakini tukubaliane huyu bwana mdogo na domo lake yuko vizuri zaidi. Mchawi mpe sifa yake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…