Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Mkama Sharp.PNG

Alikuwa na mambo mengi na Vituko vingi tu ila binafsi nakumbuka kila alipokuwa akienda katika Vijiwe vya Masela wa enzi hizo wenyewe Masela walikuwa wanapiga Magoti na wanajisalimisha Kwake na ama Bangi walizokuwa nazo na Vitu vya Uwizi walivyoiba na walikuwa wakiongoza wenyewe Kituoni Polisi.

Marehemu Nkama Sharp ndiyo alikuwa Polisi pekee Jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa hata akikukamata humbishii, unamtii na kweli hata Wewe mwenyewe unaamini kuwa ulikosea. Na alikuwa ni Polisi ambaye hana Uonevu na kuna muda alikuwa akiona unataabika au huna Msaada Kituoni basi anaweza Yeye kwa Huruma yake akakusaidia tena bila hata ya Kumpa Rushwa na ukatoka na hata ukitoka ulikuwa hurudii tena Makosa au Uhalifu.

Alikuwa na Uwezo wa Kipekee na Kipaji cha namna yake ambacho leo hii ni Nadra sana kukiona kwa Mapolisi wengi wa miaka hii ya sasa. Na nina uhakika kwa jinsi alivyokuwa Mweledi na ana Msimamo kama angekuwepo hadi miaka hii ya sasa kuna baadhi ya Maandamano ya Kisiasa wala asingekuwa anaiingilia au kuwasumbua Watu tofauti na Polisi wa sasa ambao kila Kukicha wao wanasema kuwa huwa wanatekeleza Maagizo kutoka Juu ( siyo Mbinguni kwa Mungu Baba )

Nashauri kama ikiwezekana Jeshi la Polisi nchini Tanzania litafute namna ya Kumuenzi huyu Marehemu Nkama Sharp ambaye Binafsi pia nakumbuka aliwahi kutufanya Mimi na baadhi ya Wenzangu tugawane Mitaa ile ya Jirani na Shule ya Muhimbili kwa Kumkimbia baada ya Kuambiwa kuwa tulikuwa tunafanya Fujo katika Mechi moja tuliyocheza na Wababe wa miaka hiyo Shule ya Tambaza na nakumbuka katika hali ya Kumkimbia niliweza Kupoteza Kiatu changu cha Mguu wa Kushoto na nilipofika Nyumbani nilipewa Kipigo cha maana ila nikashukuru kuwa ni bora nimepigwa na Wazazi kuliko ningeishia Mikononi mwa Marehemu Nkama Sharp.

Nasisitiza tena Marehemu Nkama Sharp aenziwe tafadhali na Mapolisi wa sasa hebu muigeni huyu Afande ili nanyi tuwapende.
 
Sijui nmuelezaje???

Ova

Muelezee tu unavyomjua Wewe Kiongozi. Kila nikiikumbuka tu ile Mikogo yake hasa ya Kiutembeaji pamoja na ile Miwani yake, Ubabe wake huku akiwa na Mwili wake ule Mdogo nabaki Kucheka tu lakini nikijiuliza alikuwa na Kipaji gani au Uwezo gani kiasi kwamba kuna wakati alikuwa anamudu Kulikamata Kundi Kubwa tu la Masela na akaongozana nalo peke yake hadi Kituoni lakini hamna hata Mtu Mmoja anayekimbia.
 
Mkakamavu,anayejiamini...daah long time,tumekimbizana sana kwenye michiriku mission quarters enzi hizo....R.I.P Kamanda.

Uko sahihi Mkuu na ukiwa Mtoto wa Mjini kweli hasa wa Dar es Salaam ni lazima tu utamjua Marehemu Nkama Sharp. Nahisi Jeshi la Polisi nchini Tanzania halijamuenzi vile ipasavyo hivyo siwalazimishi na sina huo Uwezo ila Siku Moja nitakuwa ni mwenye Furaha Kubwa pale nikisikia ameenziwa kwa namna yoyote ile au basi hata Mkewe ( kama yupo hai nae ) au Watoto wake wamekumbukwa kwa Heshima Kubwa ya Marehemu Baba yao hapa nchini hasa hasa kwa Mkoa wetu huu wa Dar es Salaam.
 
Watakao changia hapa wengi wa mjini Kkoo na vitingoji vyake. Wengine mtasoma comments tuu!
Nakumbuka siku ile Nelson Mandela ametoka jela na kuja Tanzania tulikatiza Barabara mitaa ya Uhuru Gerezani alitusumbua sana na ule msafara wa Mzee Mandela hata kutua nchini ulikuwa bado..
R. I. P Mkama alimuliki kikundi cha Mchiliku enzi za Hisani gari kubwa..
 
Alikuwa na mbwembe hasa kwenye mechi na shughuli za kitaifa uwanja wa taifa, akipita lazima watu wamshangilie

Ila nasikia nje ya Kazi yake hiyo ( kama hajavalia Kipolisi ) alikuwa ni Mtu Mmoja Mkarimu na Mwema ile mbaya hadi ungeweza kudhania kuwa hakuwa Askari Polisi. Bado naendelea leo hii Kuwatafuta Maaskari Polisi wenye ama uwezo kama wake Marehemu Nkama Sharp au hata basi Kumkaribia ila bado sijabahatika kuwaona / kuwapata labda kwa nyie Wenzangu.
 
Watakao changia hapa wengi wa mjini Kkoo na vitingoji vyake. Wengine mtasoma comments tuu!
Nakumbuka siku ile Nelson Mandela ametoka jela na kuja Tanzania tulikatiza Barabara mitaa ya Uhuru Gerezani alitusumbua sana na ule msafara wa Mzee Mandela hata kutua nchini ulikuwa bado..
R. I. P Mkama alimuliki kikundi cha Mchiliku enzi za Hisani gari kubwa..
hivi hilo kundi la mchiriku lipo
 
Ila nasikia nje ya Kazi yake hiyo ( kama hajavalia Kipolisi ) alikuwa ni Mtu Mmoja Mkarimu na Mwema ile mbaya hadi ungeweza kudhania kuwa hakuwa Askari Polisi. Bado naendelea leo hii Kuwatafuta Maaskari Polisi wenye ama uwezo kama wake Marehemu Nkama Sharp au hata basi Kumkaribia ila bado sijabahatika kuwaona / kuwapata labda kwa nyie Wenzangu.
Mambosasa mkuu lol
 
Umenikumbusha Sharp mwembamba ana rangi na mikwara kibao

Na hakuishia tu kuwa na Mikwara kama ambavyo unamdhihaki hapa Kiongozi ila Jamaa ( Mrehemu Nkama Sharp ) pia alikuwa ni Mwana Karateka mzuri na mahiri sana tu. Vijana wengi wa miaka hii ya sasa mnajifanya mna Usela ila labda niwaambieni tu kuwa miaka yetu hiyo ambayo tulikuwa na akina Nkama Sharp ndiyo kulikuwa na Wahuni na Masela Wabobezi kabisa ila wote hao walikuwa wakikalishwa na Marehemu Nkama Sharp na wanatulia tuli. Ninaposema huyu Askari alikuwa si Mtu wa kawaida ndiyo namaanisha hivi.

Wewe kama tu Wavuta Bangi wa zamani Vijiweni wakipewa tu Signal kuwa Marehemu Nkama Sharp ameamka Kitini Kwake Ofisini na anaenda Kuvitembelea hivyo Vijiwe Kukamata Watu ndani ya Sekunde 7 au dakika 1 tu ulikuwa huoni Mtu Kijiweni bali unaona tu Vumbi huku kila Msela akilitafuta Boda la kwenda Kwao.

Nakumbuka kuna Siku moja Marehemu akiwa Full Mkoko kapigilia Kiaskari kabisa alitoka Baru / Mita ( alikimbizana ) na Mhalifu kutoka Kariakoo hadi maeneo ya Msasani jirani na ulipokuwa Uwanja wa Mpira wa Magunia na Yule Mhalifu kwa Kuchoka ilibidi asalimu Amri kwani alikuwa kila akikata Kona anamuona Mwanamume Nkama Sharp yuko Matakoni mwake.

Jamaa ( Mhalifu ) alipochoka na Kukaa chini Marehemu alikuja na kumuinua na Kumwambia waendelee na Marathon yao ambayo haikuwa rasmi na kilichotokea Yule Mhalifu sijajua kama alikuwa amechoka kweli au alikuwa anatafuta tu Huruma ambapo alijinyea / alikunya pale pale ndipo Afande Nkama Sharp nae akaamua Kuachana nae ili asije Kunuka Mimavi bure.
 
Back
Top Bottom