Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

Sie tulieishi Gerezani tunamkumbuka sana Mkama sharp alikuwa anatembea na pistor mbili huku na huku pia Rungu na mikwara kibao. Siku kuna ngumi railways Gerezani kati ya Stanley na Sep wanana au Charles Libondo (Mawe Zambia)au Simba na Yanga Taifa ndo utamjua vizuri mkama sharp kwa mbwembwe. Pale jiran na msimbazi police mtaa wa kibambawe alikuwa mbabe mmoja hatari ambaye mkama sharp alikuwa haongei. Jamaa mbavu nene anaitwa Baba Jua,Huyu jamaa aliwai kuwa Bouncer wa Dar inter ya Marijani Rajabu. Alikuwa mtu hatari sijapata kuona RIP Baba Jua
 
Uko sahihi Mkuu na ukiwa Mtoto wa Mjini kweli hasa wa Dar es Salaam ni lazima tu utamjua Marehemu Nkama Sharp. Nahisi Jeshi la Polisi nchini Tanzania halijamuenzi vile ipasavyo hivyo siwalazimishi na sina huo Uwezo ila Siku Moja nitakuwa ni mwenye Furaha Kubwa pale nikisikia ameenziwa kwa namna yoyote ile au basi hata Mkewe ( kama yupo hai nae ) au Watoto wake wamekumbukwa kwa Heshima Kubwa ya Marehemu Baba yao hapa nchini hasa hasa kwa Mkoa wetu huu wa Dar es Salaam.
Huyo polisi alikuwa Oyster bay pale nakumbuka miaka Ile alisumbua Sana mitaa ya Kinondoni manyanya,aibu,Togo,ufipa na mitaa ya Brazil, Moscow na mkwajuni
 
Alikuwa na mambo mengi na Vituko vingi tu ila binafsi nakumbuka kila alipokuwa akienda katika Vijiwe vya Masela wa enzi hizo wenyewe Masela walikuwa wanapiga Magoti na wanajisalimisha Kwake na ama Bangi walizokuwa nazo na Vitu vya Uwizi walivyoiba na walikuwa wakiongoza wenyewe Kituoni Polisi.

Marehemu Nkama Sharp ndiyo alikuwa Polisi pekee Jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa hata akikukamata humbishii, unamtii na kweli hata Wewe mwenyewe unaamini kuwa ulikosea. Na alikuwa ni Polisi ambaye hana Uonevu na kuna muda alikuwa akiona unataabika au huna Msaada Kituoni basi anaweza Yeye kwa Huruma yake akakusaidia tena bila hata ya Kumpa Rushwa na ukatoka na hata ukitoka ulikuwa hurudii tena Makosa au Uhalifu.

Alikuwa na Uwezo wa Kipekee na Kipaji cha namna yake ambacho leo hii ni Nadra sana kukiona kwa Mapolisi wengi wa miaka hii ya sasa. Na nina uhakika kwa jinsi alivyokuwa Mweledi na ana Msimamo kama angekuwepo hadi miaka hii ya sasa kuna baadhi ya Maandamano ya Kisiasa wala asingekuwa anaiingilia au kuwasumbua Watu tofauti na Polisi wa sasa ambao kila Kukicha wao wanasema kuwa huwa wanatekeleza Maagizo kutoka Juu ( siyo Mbinguni kwa Mungu Baba )

Nashauri kama ikiwezekana Jeshi la Polisi nchini Tanzania litafute namna ya Kumuenzi huyu Marehemu Nkama Sharp ambaye Binafsi pia nakumbuka aliwahi kutufanya Mimi na baadhi ya Wenzangu tugawane Mitaa ile ya Jirani na Shule ya Muhimbili kwa Kumkimbia baada ya Kuambiwa kuwa tulikuwa tunafanya Fujo katika Mechi moja tuliyocheza na Wababe wa miaka hiyo Shule ya Tambaza na nakumbuka katika hali ya Kumkimbia niliweza Kupoteza Kiatu changu cha Mguu wa Kushoto na nilipofika Nyumbani nilipewa Kipigo cha maana ila nikashukuru kuwa ni bora nimepigwa na Wazazi kuliko ningeishia Mikononi mwa Marehemu Nkama Sharp.

Nasisitiza tena Marehemu Nkama Sharp aenziwe tafadhali na Mapolisi wa sasa hebu muigeni huyu Afande ili nanyi tuwapende.
Mmoja kati ya mapolisi walioipenda sana kazi yake na kuwa proud.
Akiingia uwanja wa Taifa kutekeleza majukumu yake , kiatu safi, kiunoni kirungu na pingu zinazo ng'aa, filimbi na kash kash nyingi tu.
Kiujumla Mkama Sharp alikuwa proud na kazi yake na watu walimpenda.
 
Siku hizi kajichokea tu ni ocd huku manyara kituo nimesahau jina,ujanja wote kashindwa kumdhibiti mwanae kawa mdangaji sugu utafikiria sio mtoto wa sabasita
Kwa kweli miaka ya 80s mpaka 90 kulikuwa Askari Polisi waliokuwa na mbinu za kusambaratisha vigenge vya wahalifu yaani kwa kupita tu kwenye mitaa, wale masela wa miaka hiyo waliokuwa wakivuta jani vijiweni walikuwa wakikimbia wenyewe.Nakumbuka pale Arusha kulikuwa na Polisi mmoja alikuwa anafahamika kwa jina la Kimaro maarufu sana kwa jina la "SABA SITA" huyu jamaa hakuwa tofauti na marehemu Mkama Sharp. Pale Arusha miaka hiyo hakuna mtu ambaye alikuwa hamjui "SABA SITA". Kiukweli huyu askari alikuwa very smart katika kazi yake kwanza alikuwa anaipenda. Nakumbuka pale Sheikh Amri Abeid Stadium kulikuwa na mechi ya ligi kuu kati ya Simba SC na Ndovu FC ya Arusha, kwa baadhi ya wapenzi wa soka walikuwa wakiruka ukuta kuingia uwanjani kwa kukosa kiingilio,sehemu nilipokuwa nimekaa wakaja kukaa jamaa watatu walioruka ukuta kumbe Saba Sita alikuwa amewaona akapotezea kama hajawaona, wale washkaji wakajisahau. Kumbe "7 6" alikuwa anawalia timing, Simba ilipata goli la kuongoza lililofungwa na marehemu Edward Chumila uwanja mzima ulizizima kwa kushangilia lile goli, muda huo sasa Saba Sita akiwa amevalia pama lake la FFU, pingu, kirungu na kiunoni akiwa na pistol iliyokuwa kwenye kasha lake alikuja mpaka pale nilipokuwa nimekaa akawachomoa wale jamaa watatu walioruka ukuta sio siri jamaa waliingia hofu kubwa, akaanza kuzunguka nao uwanja mzima akiwa amewafunga mashati yao kwa kuwaunganisha alipofika nao kwenye Defender la Polisi aliwaamuru wapande ndani na walale kifudi fudi, hiyo ndio ilikuwa adhabu yao hawakuwapiga hata kidogo mpira ulipokwisha aliwaachia. Baadae nasikia Saba Sita alihamishiwa Mererani kikazi na kisha alihamishiwa tena CCP kuwa Mkufunzi. Nowadays sijui alipo nadhani atakuwa amestaafu.Lakini niconclude kwa kusema Mkama Sharp na Saba Sita ni Polisi waliokuwa very professional katika kazi yao.
 
Ila nasikia nje ya Kazi yake hiyo ( kama hajavalia Kipolisi ) alikuwa ni Mtu Mmoja Mkarimu na Mwema ile mbaya hadi ungeweza kudhania kuwa hakuwa Askari Polisi. Bado naendelea leo hii Kuwatafuta Maaskari Polisi wenye ama uwezo kama wake Marehemu Nkama Sharp au hata basi Kumkaribia ila bado sijabahatika kuwaona / kuwapata labda kwa nyie Wenzangu.
Nitafute nikuonyeshe
 
Alikuwa na mambo mengi na Vituko vingi tu ila binafsi nakumbuka kila alipokuwa akienda katika Vijiwe vya Masela wa enzi hizo wenyewe Masela walikuwa wanapiga Magoti na wanajisalimisha Kwake na ama Bangi walizokuwa nazo na Vitu vya Uwizi walivyoiba na walikuwa wakiongoza wenyewe Kituoni Polisi.

Marehemu Nkama Sharp ndiyo alikuwa Polisi pekee Jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa hata akikukamata humbishii, unamtii na kweli hata Wewe mwenyewe unaamini kuwa ulikosea. Na alikuwa ni Polisi ambaye hana Uonevu na kuna muda alikuwa akiona unataabika au huna Msaada Kituoni basi anaweza Yeye kwa Huruma yake akakusaidia tena bila hata ya Kumpa Rushwa na ukatoka na hata ukitoka ulikuwa hurudii tena Makosa au Uhalifu.

Alikuwa na Uwezo wa Kipekee na Kipaji cha namna yake ambacho leo hii ni Nadra sana kukiona kwa Mapolisi wengi wa miaka hii ya sasa. Na nina uhakika kwa jinsi alivyokuwa Mweledi na ana Msimamo kama angekuwepo hadi miaka hii ya sasa kuna baadhi ya Maandamano ya Kisiasa wala asingekuwa anaiingilia au kuwasumbua Watu tofauti na Polisi wa sasa ambao kila Kukicha wao wanasema kuwa huwa wanatekeleza Maagizo kutoka Juu ( siyo Mbinguni kwa Mungu Baba )

Nashauri kama ikiwezekana Jeshi la Polisi nchini Tanzania litafute namna ya Kumuenzi huyu Marehemu Nkama Sharp ambaye Binafsi pia nakumbuka aliwahi kutufanya Mimi na baadhi ya Wenzangu tugawane Mitaa ile ya Jirani na Shule ya Muhimbili kwa Kumkimbia baada ya Kuambiwa kuwa tulikuwa tunafanya Fujo katika Mechi moja tuliyocheza na Wababe wa miaka hiyo Shule ya Tambaza na nakumbuka katika hali ya Kumkimbia niliweza Kupoteza Kiatu changu cha Mguu wa Kushoto na nilipofika Nyumbani nilipewa Kipigo cha maana ila nikashukuru kuwa ni bora nimepigwa na Wazazi kuliko ningeishia Mikononi mwa Marehemu Nkama Sharp.

Nasisitiza tena Marehemu Nkama Sharp aenziwe tafadhali na Mapolisi wa sasa hebu muigeni huyu Afande ili nanyi tuwapende.
Alikuwa bondia huyu
 
Alikuwa na mambo mengi na Vituko vingi tu ila binafsi nakumbuka kila alipokuwa akienda katika Vijiwe vya Masela wa enzi hizo wenyewe Masela walikuwa wanapiga Magoti na wanajisalimisha Kwake na ama Bangi walizokuwa nazo na Vitu vya Uwizi walivyoiba na walikuwa wakiongoza wenyewe Kituoni Polisi.

Marehemu Nkama Sharp ndiyo alikuwa Polisi pekee Jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa hata akikukamata humbishii, unamtii na kweli hata Wewe mwenyewe unaamini kuwa ulikosea. Na alikuwa ni Polisi ambaye hana Uonevu na kuna muda alikuwa akiona unataabika au huna Msaada Kituoni basi anaweza Yeye kwa Huruma yake akakusaidia tena bila hata ya Kumpa Rushwa na ukatoka na hata ukitoka ulikuwa hurudii tena Makosa au Uhalifu.

Alikuwa na Uwezo wa Kipekee na Kipaji cha namna yake ambacho leo hii ni Nadra sana kukiona kwa Mapolisi wengi wa miaka hii ya sasa. Na nina uhakika kwa jinsi alivyokuwa Mweledi na ana Msimamo kama angekuwepo hadi miaka hii ya sasa kuna baadhi ya Maandamano ya Kisiasa wala asingekuwa anaiingilia au kuwasumbua Watu tofauti na Polisi wa sasa ambao kila Kukicha wao wanasema kuwa huwa wanatekeleza Maagizo kutoka Juu ( siyo Mbinguni kwa Mungu Baba )

Nashauri kama ikiwezekana Jeshi la Polisi nchini Tanzania litafute namna ya Kumuenzi huyu Marehemu Nkama Sharp ambaye Binafsi pia nakumbuka aliwahi kutufanya Mimi na baadhi ya Wenzangu tugawane Mitaa ile ya Jirani na Shule ya Muhimbili kwa Kumkimbia baada ya Kuambiwa kuwa tulikuwa tunafanya Fujo katika Mechi moja tuliyocheza na Wababe wa miaka hiyo Shule ya Tambaza na nakumbuka katika hali ya Kumkimbia niliweza Kupoteza Kiatu changu cha Mguu wa Kushoto na nilipofika Nyumbani nilipewa Kipigo cha maana ila nikashukuru kuwa ni bora nimepigwa na Wazazi kuliko ningeishia Mikononi mwa Marehemu Nkama Sharp.

Nasisitiza tena Marehemu Nkama Sharp aenziwe tafadhali na Mapolisi wa sasa hebu muigeni huyu Afande ili nanyi tuwapende.
Siku hizi kila sehemu ilikuwa kimbilio la ajira ma fursa
 
Ila nasikia nje ya Kazi yake hiyo ( kama hajavalia Kipolisi ) alikuwa ni Mtu Mmoja Mkarimu na Mwema ile mbaya hadi ungeweza kudhania kuwa hakuwa Askari Polisi. Bado naendelea leo hii Kuwatafuta Maaskari Polisi wenye ama uwezo kama wake Marehemu Nkama Sharp au hata basi Kumkaribia ila bado sijabahatika kuwaona / kuwapata labda kwa nyie Wenzangu.
Unamkumbuka kitonsa, alikuwa bonge la mtu ndio walikuwa wa mwanzo kuendesha gari la polisi la kupeleka wahabusu mahakamani (karandinga)
 
Saba Sita
 

Attachments

  • IMG-20190820-WA0022.jpeg
    IMG-20190820-WA0022.jpeg
    54.4 KB · Views: 41
Alikuwa na mambo mengi na Vituko vingi tu ila binafsi nakumbuka kila alipokuwa akienda katika Vijiwe vya Masela wa enzi hizo wenyewe Masela walikuwa wanapiga Magoti na wanajisalimisha Kwake na ama Bangi walizokuwa nazo na Vitu vya Uwizi walivyoiba na walikuwa wakiongoza wenyewe Kituoni Polisi.

Marehemu Nkama Sharp ndiyo alikuwa Polisi pekee Jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa hata akikukamata humbishii, unamtii na kweli hata Wewe mwenyewe unaamini kuwa ulikosea. Na alikuwa ni Polisi ambaye hana Uonevu na kuna muda alikuwa akiona unataabika au huna Msaada Kituoni basi anaweza Yeye kwa Huruma yake akakusaidia tena bila hata ya Kumpa Rushwa na ukatoka na hata ukitoka ulikuwa hurudii tena Makosa au Uhalifu.

Alikuwa na Uwezo wa Kipekee na Kipaji cha namna yake ambacho leo hii ni Nadra sana kukiona kwa Mapolisi wengi wa miaka hii ya sasa. Na nina uhakika kwa jinsi alivyokuwa Mweledi na ana Msimamo kama angekuwepo hadi miaka hii ya sasa kuna baadhi ya Maandamano ya Kisiasa wala asingekuwa anaiingilia au kuwasumbua Watu tofauti na Polisi wa sasa ambao kila Kukicha wao wanasema kuwa huwa wanatekeleza Maagizo kutoka Juu ( siyo Mbinguni kwa Mungu Baba )

Nashauri kama ikiwezekana Jeshi la Polisi nchini Tanzania litafute namna ya Kumuenzi huyu Marehemu Nkama Sharp ambaye Binafsi pia nakumbuka aliwahi kutufanya Mimi na baadhi ya Wenzangu tugawane Mitaa ile ya Jirani na Shule ya Muhimbili kwa Kumkimbia baada ya Kuambiwa kuwa tulikuwa tunafanya Fujo katika Mechi moja tuliyocheza na Wababe wa miaka hiyo Shule ya Tambaza na nakumbuka katika hali ya Kumkimbia niliweza Kupoteza Kiatu changu cha Mguu wa Kushoto na nilipofika Nyumbani nilipewa Kipigo cha maana ila nikashukuru kuwa ni bora nimepigwa na Wazazi kuliko ningeishia Mikononi mwa Marehemu Nkama Sharp.

Nasisitiza tena Marehemu Nkama Sharp aenziwe tafadhali na Mapolisi wa sasa hebu muigeni huyu Afande ili nanyi tuwapende.
Wa hivyo wapo wengi...sema unamjua huyu tu
 
Na hakuishia tu kuwa na Mikwara kama ambavyo unamdhihaki hapa Kiongozi ila Jamaa ( Mrehemu Nkama Sharp ) pia alikuwa ni Mwana Karateka mzuri na mahiri sana tu. Vijana wengi wa miaka hii ya sasa mnajifanya mna Usela ila labda niwaambieni tu kuwa miaka yetu hiyo ambayo tulikuwa na akina Nkama Sharp ndiyo kulikuwa na Wahuni na Masela Wabobezi kabisa ila wote hao walikuwa wakikalishwa na Marehemu Nkama Sharp na wanatulia tuli. Ninaposema huyu Askari alikuwa si Mtu wa kawaida ndiyo namaanisha hivi.

Wewe kama tu Wavuta Bangi wa zamani Vijiweni wakipewa tu Signal kuwa Marehemu Nkama Sharp ameamka Kitini Kwake Ofisini na anaenda Kuvitembelea hivyo Vijiwe Kukamata Watu ndani ya Sekunde 7 au dakika 1 tu ulikuwa huoni Mtu Kijiweni bali unaona tu Vumbi huku kila Msela akilitafuta Boda la kwenda Kwao.

Nakumbuka kuna Siku moja Marehemu akiwa Full Mkoko kapigilia Kiaskari kabisa alitoka Baru / Mita ( alikimbizana ) na Mhalifu kutoka Kariakoo hadi maeneo ya Msasani jirani na ulipokuwa Uwanja wa Mpira wa Magunia na Yule Mhalifu kwa Kuchoka ilibidi asalimu Amri kwani alikuwa kila akikata Kona anamuona Mwanamume Nkama Sharp yuko Matakoni mwake.

Jamaa ( Mhalifu ) alipochoka na Kukaa chini Marehemu alikuja na kumuinua na Kumwambia waendelee na Marathon yao ambayo haikuwa rasmi na kilichotokea Yule Mhalifu sijajua kama alikuwa amechoka kweli au alikuwa anatafuta tu Huruma ambapo alijinyea / alikunya pale pale ndipo Afande Nkama Sharp nae akaamua Kuachana nae ili asije Kunuka Mimavi bure.
Kwa nini wewe kila unapomtaja jina unaandika Nkama Sharp ila wengine wanaandika Mkama Sharp? Usahihi ni upi?
 
Muelezee tu unavyomjua Wewe Kiongozi. Kila nikiikumbuka tu ile Mikogo yake hasa ya Kiutembeaji pamoja na ile Miwani yake, Ubabe wake huku akiwa na Mwili wake ule Mdogo nabaki Kucheka tu lakini nikijiuliza alikuwa na Kipaji gani au Uwezo gani kiasi kwamba kuna wakati alikuwa anamudu Kulikamata Kundi Kubwa tu la Masela na akaongozana nalo peke yake hadi Kituoni lakini hamna hata Mtu Mmoja anayekimbia.
Hata mimi namkumbuka. Ila kwangu naona ni kama chongo kwenye kundi la vipofu. Nadhani ushamba wetu hasa enzi zile za zamani ndizo zilimkuza zaidi. Naomba nieleweke kuwa sisemi kuwa alikuwa ''mzuri'' wa kazi yake lakini nasema tu ''uzuri'' wake ulipaishwa na ushamba na woga wetu.
 
Back
Top Bottom