Jephta2003
JF-Expert Member
- Feb 27, 2008
- 6,590
- 6,355
Sahihi ni MKAMA ni watu wa MaraKwa nini wewe kila unapomtaja jina unaandika Nkama Sharp ila wengine wanaandika Mkama Sharp? Usahihi ni upi?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sahihi ni MKAMA ni watu wa MaraKwa nini wewe kila unapomtaja jina unaandika Nkama Sharp ila wengine wanaandika Mkama Sharp? Usahihi ni upi?
Nadhani pia utakuwa na usuhuba naye...nkama!Huyu uliyemtaja hapa ni Mweupe ( Mchovu ) sana Kiongozi ukimlinganisha na Marehemu Nkama Sharp.
Aisee! kumbe Tunda ni mtoto wa Kimaro a.k.a "SABA SITA" mbona sasa binti machepele sana mzee ameshindwa kum-discipline ?Huyu 7 6 ana mtoto wake wa kike anajiita tunda [emoji23][emoji23][emoji23]
Daaah nimecheka utafikiria mazuriKuna Siku moja nikiwa pale pale Shamba la Bibi ( Taifa ) huku nikiwa bado ni Mdogo kabisa Kipindi kile Katibu Mkuu wa Simba SC alikuwa Mzee Mmoja Mbabe sana ( sasa Marehemu ) Priva Mtema niliwahi Kuona Mbwa wa Mkama Sharp akiondoka na Kipande cha Nyama cha Tako la Kushoto la Mhalifu na sina uhakika kama alipona ile Siku au alikufa baadae.
Si ndio hapo yaani kabinti ni kama kamempiga bao msure wake.Aisee! kumbe Tunda ni mtoto wa Kimaro a.k.a "SABA SITA" mbona sasa binti machepele sana mzee ameshindwa kum-discipline ?
Acha tu, dingi na undava wote lakini kashindwa kudhibiti kale kabinti.Si ndio hapo yaani kabinti ni kama kamempiga bao msure wake.
Any way labda Ni mapenzi ya kupitiliza kwa watoto. Au mama yake binti ndio tatizo.
Changamoto Sana sifa zote za mdingi zinaweza kuharibiwa na mtoto
Huyu nae ni mtoto wa mkama auasilimia kubwa ya watoto WA maafande wamepinda,kuna mwingine anajiita Gigy money.
Acha tu, dingi na undava wote lakini kashindwa kudhibiti kale kabinti.
Hee kumbe tunda mtoto wa polisi??[emoji1787]
Mmmeanza kutaja na wakwe zenuuu huku dooooh .......endeleaAisee! kumbe Tunda ni mtoto wa Kimaro a.k.a "SABA SITA" mbona sasa binti machepele sana mzee ameshindwa kum-discipline ?
Wengi wachomoaaa betri mkuuuasilimia kubwa ya watoto WA maafande wamepinda,kuna mwingine anajiita Gigy money.
nilishawahi kumuona moro huyu mshkajihuyu nasikia aliwakimbiza sana waarifu mjini moro,sijui yuwapi sasa
kwaiyo dog akajua nikiingia hum wazee wa kaz watanifanya ndivyo sivyo dah ejikuta nacheka sanaSharp na mbwa wake (mbwa wa polisi).
Si mara 1 au mara 2 niliwahi kumwona Sharp akiwa na mbwa. Kuna wakati angemwacha mbwa karibu na geti la kuingia kwenye Uwanja wa Taifa wa zamani (shamba la bibi) bila kumfunga popote.Angemwamrisha "tulia hapa hadi nikukute, usiondoke!" na mbwa angatulia hapo. Hata akikuona unajipenyeza getini kiwizi wizi au unajaribu kuruka ukuta mbwa huyo asingekuwa na time na wewe.
Ila ole wako aamrishwe kukukamata ndo utaisoma namba.Afande Sharp angemwelekeza mbwa wake " unamwona yule jamaa aliyevaa kofia ya blue, t-shirt nyeupe na jeans ya blue?nenda kamkamate!" Ni hivi mbwa angekusonga wewe tu aliyeelekezwa akukamate (hata kama uko kwenye kundi la watu wengi, na angekukamata).
Iliwahi kutokea afande Sharp alimsakizia mbwa msela mmoja aliyekuwa anajaribu kupita chini ya geti, jamaa alivyoona atadakwa ikabidi akimbilie kwenye kambi ya jeshi ya Abdallah Twalipo (almaarufu 'Ngome') iliyo jirani kabisa na Uwanja wa Taifa na kituo cha mafuta. Jamaa alivyoingia kambini, wazee wa JWTZ waliokuwa zamu walimlinda na kumwambia asiwe na hofu, walichofanya ni kumsubiri mbwa aingie kambini kisha wamfanyie mambo ya Samson na Simba wa Wafilisti. Ila yule mbwa alikuwa na akili bhana, alifunga breki getini na kurudi kwa boss. Wajeda wakamwambia Sharp "huyo mbwa wako na wewe mwenyewe leo tulitaka tuwafundishe adabu.Rudia tena uone". Sharp hakujibu neno.
Ila huyu Pot alikuwa tishio kwa wahuni kwakweli.Kuna mtoto yupi wa mjini ambaye hakumfahamu?
Nilifanya nae kazi Oysterbay Police kabla ya umauti,huku mwishoni baada ya kutoka FFU na kuhamia CID hakuwa na makeke mengi,Apumzike kwa Amani
aaaaah wa mkoani mnaanchwa sana na hii dunia[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Kamanda uko na picha yake utusaidie kwa sie wa mkoani?
Kamanda uko na picha yake utusaidie kwa sie wa mkoani?