Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

Kuna siku 90s nimepishana nae sokota temeke pale ana kigroup cha masela kibao kawakusanya vijiweni huko anaenda nao kibla
 
No hiyo 90s kweusi huko

Basi kwa jinsi ulivyoiandika umeikosea kidogo kwani umendika sentensi ambayo kwa haraka haraka Mtu anaweza Kudhani kuwa Mkama Sharp yupo hai. Irekebishe kama hutojali Kiongozi.
 
Si ndio hapo yaani kabinti ni kama kamempiga bao msure wake.
Any way labda Ni mapenzi ya kupitiliza kwa watoto. Au mama yake binti ndio tatizo.
Changamoto Sana sifa zote za mdingi zinaweza kuharibiwa na mtoto
Sahihi, naungana na wewe huenda mama kwa namna moja au nyingine amechangia binti kuwa kama alivyo.
 
Uko sahihi Mkuu na ukiwa Mtoto wa Mjini kweli hasa wa Dar es Salaam ni lazima tu utamjua Marehemu Nkama Sharp. Nahisi Jeshi la Polisi nchini Tanzania halijamuenzi vile ipasavyo hivyo siwalazimishi na sina huo Uwezo ila Siku Moja nitakuwa ni mwenye Furaha Kubwa pale nikisikia ameenziwa kwa namna yoyote ile au basi hata Mkewe ( kama yupo hai nae ) au Watoto wake wamekumbukwa kwa Heshima Kubwa ya Marehemu Baba yao hapa nchini hasa hasa kwa Mkoa wetu huu wa Dar es Salaam.
Hapa nipo ule usemi Wa WANAUME WA DAR unapopata nguvu za kisheria.

Huko mikoani kuna maaskari waliofanya mambo makubwa na ya kutisha kama vile Movie.

Majambazi , Majangili na wahalifu mbalimbali wamekamatwa ,kuhojiwa na kufikishwa Mahakamani na kupata haki zao.

Jambo la Msingi ni kuwaenzi wale wote waliofanya utendaji bora. Na ukifanyika utafiti nani kafanya nn na wapi?

Rip Mkama sharp anaweza potezwa vibaya.


Ila aenziwe katika viunga vyake.
 
76 mndava sana

Siku yupo patrol kitaa chote wahun wanasambaa hata wik nzima hawatokei

Ujambaz ukitokea akipelekwa front kesho yake utasikia majambaz 5 wameuwawa na polisi kwenye mapigano!!!

Ila Tunda watu wanakunja na mzee hana la kusema...
Acha tu, dingi na undava wote lakini kashindwa kudhibiti kale kabinti.
 
Kamanda uko na picha yake utusaidie kwa sie wa mkoani?
Kamanda mkama in action
tapatalk_jpeg_1566344887775.jpeg
 
Ocd kiteto shida yake shule ndogo angeshakua rpc kitambo
Huyu mangi ni proffesional killer

Ndio kazi yake..alikua kituo cha sitakshari nadhan mnajua shughul za hicho kituo

Sijui kwa sasa yupo chimbo gani!!

Kaskazin nadhan aliweka rekod kwa kutoa roho za wahalifu
 
Na hakuishia tu kuwa na Mikwara kama ambavyo unamdhihaki hapa Kiongozi ila Jamaa ( Mrehemu Nkama Sharp ) pia alikuwa ni Mwana Karateka mzuri na mahiri sana tu. Vijana wengi wa miaka hii ya sasa mnajifanya mna Usela ila labda niwaambieni tu kuwa miaka yetu hiyo ambayo tulikuwa na akina Nkama Sharp ndiyo kulikuwa na Wahuni na Masela Wabobezi kabisa ila wote hao walikuwa wakikalishwa na Marehemu Nkama Sharp na wanatulia tuli. Ninaposema huyu Askari alikuwa si Mtu wa kawaida ndiyo namaanisha hivi.

Wewe kama tu Wavuta Bangi wa zamani Vijiweni wakipewa tu Signal kuwa Marehemu Nkama Sharp ameamka Kitini Kwake Ofisini na anaenda Kuvitembelea hivyo Vijiwe Kukamata Watu ndani ya Sekunde 7 au dakika 1 tu ulikuwa huoni Mtu Kijiweni bali unaona tu Vumbi huku kila Msela akilitafuta Boda la kwenda Kwao.

Nakumbuka kuna Siku moja Marehemu akiwa Full Mkoko kapigilia Kiaskari kabisa alitoka Baru / Mita ( alikimbizana ) na Mhalifu kutoka Kariakoo hadi maeneo ya Msasani jirani na ulipokuwa Uwanja wa Mpira wa Magunia na Yule Mhalifu kwa Kuchoka ilibidi asalimu Amri kwani alikuwa kila akikata Kona anamuona Mwanamume Nkama Sharp yuko Matakoni mwake.

Jamaa ( Mhalifu ) alipochoka na Kukaa chini Marehemu alikuja na kumuinua na Kumwambia waendelee na Marathon yao ambayo haikuwa rasmi na kilichotokea Yule Mhalifu sijajua kama alikuwa amechoka kweli au alikuwa anatafuta tu Huruma ambapo alijinyea / alikunya pale pale ndipo Afande Nkama Sharp nae akaamua Kuachana nae ili asije Kunuka Mimavi bure.
afande alikuwa mtu hatari anakimbiza mhalifu mpaka anakunya? kweli watu wema hawadumu
 
76 mndava sana

Siku yupo patrol kitaa chote wahun wanasambaa hata wik nzima hawatokei

Ujambaz ukitokea akipelekwa front kesho yake utasikia majambaz 5 wameuwawa na polisi kwenye mapigano!!!

Ila Tunda watu wanakunja na mzee hana la kusema...
sie wababa kwa watoto wa kike huwa hatuchomoi mara nyingi,chunguza familia nyingi.

mama na watoto wa kiume
baba na watoto wa kike.
 
NASHAURI NECT MSISUBIRI MTU AFE
MPONGEZENI AKIWA HAI MAUTI IKIMFIKA ASIKII HAYA MNAYOMPONGEZA WAKATI ANASTAHILI HILII

ROJAROJA
 
Watakao changia hapa wengi wa mjini Kkoo na vitingoji vyake. Wengine mtasoma comments tuu!
Nakumbuka siku ile Nelson Mandela ametoka jela na kuja Tanzania tulikatiza Barabara mitaa ya Uhuru Gerezani alitusumbua sana na ule msafara wa Mzee Mandela hata kutua nchini ulikuwa bado..
R. I. P Mkama alimuliki kikundi cha Mchiliku enzi za Hisani gari kubwa..
Mtaa wa posta pia lazima wamkumbuke mkuu. Alikuwa anatusaidia foleni ya uda mtaa wa posta enzi hizo.
 
JAMANI HATA AMAWONGELEI MICHANGO SIFA ZA MANENOO AZINA MAANA SANA ALIEKOO MSIBANI EMBU TUPE TAARIFA PLS NA NAMBA ZA SIMU TUNAFANYAJEEE....
ROGER ROGER
 
Weweeeee hao waliokuleta Duniani walitokea hukuhuku mikoani na halafu huku mna kutamani sana sema kutafuta hela ndio inawafanya mjazane huko mnapopaita town wakati hata kutafuna miwa hamuwezi mnataka juice

Kiongozi mbona unakuwa na Hasira hivi na Mimi wa Mjini? Hata Mimi sikuomba nizaliwe na nikulie hivi Mjini na nashukuru sijawa na Maisha ya huko Vijijini. Wewe ulivyo Pimbi hapo ulipo sasa unashinda zako Majarubani huko na Mashambani unalima hadi Vigimbi vimekushupaa ili uitafute tu Nauli ya kukuwezesha kuja Makonda City ( Dar es Salaam ) nawe angalau uweze Kuosha Macho.
 
Back
Top Bottom