Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

Huyu Polisi wa zamani Marehemu Mkama Sharp alikuwa na Kipaji gani ambacho Polisi wengi wa sasa hawana?

Saba Sita
IMG-20190820-WA0022.jpeg
 
Alikuwa na mambo mengi na Vituko vingi tu ila binafsi nakumbuka kila alipokuwa akienda katika Vijiwe vya Masela wa enzi hizo wenyewe Masela walikuwa wanapiga Magoti na wanajisalimisha Kwake na ama Bangi walizokuwa nazo na Vitu vya Uwizi walivyoiba na walikuwa wakiongoza wenyewe Kituoni Polisi.

Marehemu Nkama Sharp ndiyo alikuwa Polisi pekee Jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa hata akikukamata humbishii, unamtii na kweli hata Wewe mwenyewe unaamini kuwa ulikosea. Na alikuwa ni Polisi ambaye hana Uonevu na kuna muda alikuwa akiona unataabika au huna Msaada Kituoni basi anaweza Yeye kwa Huruma yake akakusaidia tena bila hata ya Kumpa Rushwa na ukatoka na hata ukitoka ulikuwa hurudii tena Makosa au Uhalifu.

Alikuwa na Uwezo wa Kipekee na Kipaji cha namna yake ambacho leo hii ni Nadra sana kukiona kwa Mapolisi wengi wa miaka hii ya sasa. Na nina uhakika kwa jinsi alivyokuwa Mweledi na ana Msimamo kama angekuwepo hadi miaka hii ya sasa kuna baadhi ya Maandamano ya Kisiasa wala asingekuwa anaiingilia au kuwasumbua Watu tofauti na Polisi wa sasa ambao kila Kukicha wao wanasema kuwa huwa wanatekeleza Maagizo kutoka Juu ( siyo Mbinguni kwa Mungu Baba )

Nashauri kama ikiwezekana Jeshi la Polisi nchini Tanzania litafute namna ya Kumuenzi huyu Marehemu Nkama Sharp ambaye Binafsi pia nakumbuka aliwahi kutufanya Mimi na baadhi ya Wenzangu tugawane Mitaa ile ya Jirani na Shule ya Muhimbili kwa Kumkimbia baada ya Kuambiwa kuwa tulikuwa tunafanya Fujo katika Mechi moja tuliyocheza na Wababe wa miaka hiyo Shule ya Tambaza na nakumbuka katika hali ya Kumkimbia niliweza Kupoteza Kiatu changu cha Mguu wa Kushoto na nilipofika Nyumbani nilipewa Kipigo cha maana ila nikashukuru kuwa ni bora nimepigwa na Wazazi kuliko ningeishia Mikononi mwa Marehemu Nkama Sharp.

Nasisitiza tena Marehemu Nkama Sharp aenziwe tafadhali na Mapolisi wa sasa hebu muigeni huyu Afande ili nanyi tuwapende.

Huyu ndio alikuwa askari wa "Serve and Protect" sio hawa wa sasa wa "Maim and Kill", askari ambao hata kuwakamata walevi wa gongo wanahitaji msaada wa mabomu ya machozi!
 
Alikuwa na mambo mengi na Vituko vingi tu ila binafsi nakumbuka kila alipokuwa akienda katika Vijiwe vya Masela wa enzi hizo wenyewe Masela walikuwa wanapiga Magoti na wanajisalimisha Kwake na ama Bangi walizokuwa nazo na Vitu vya Uwizi walivyoiba na walikuwa wakiongoza wenyewe Kituoni Polisi.

Marehemu Nkama Sharp ndiyo alikuwa Polisi pekee Jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa hata akikukamata humbishii, unamtii na kweli hata Wewe mwenyewe unaamini kuwa ulikosea. Na alikuwa ni Polisi ambaye hana Uonevu na kuna muda alikuwa akiona unataabika au huna Msaada Kituoni basi anaweza Yeye kwa Huruma yake akakusaidia tena bila hata ya Kumpa Rushwa na ukatoka na hata ukitoka ulikuwa hurudii tena Makosa au Uhalifu.

Alikuwa na Uwezo wa Kipekee na Kipaji cha namna yake ambacho leo hii ni Nadra sana kukiona kwa Mapolisi wengi wa miaka hii ya sasa. Na nina uhakika kwa jinsi alivyokuwa Mweledi na ana Msimamo kama angekuwepo hadi miaka hii ya sasa kuna baadhi ya Maandamano ya Kisiasa wala asingekuwa anaiingilia au kuwasumbua Watu tofauti na Polisi wa sasa ambao kila Kukicha wao wanasema kuwa huwa wanatekeleza Maagizo kutoka Juu ( siyo Mbinguni kwa Mungu Baba )

Nashauri kama ikiwezekana Jeshi la Polisi nchini Tanzania litafute namna ya Kumuenzi huyu Marehemu Nkama Sharp ambaye Binafsi pia nakumbuka aliwahi kutufanya Mimi na baadhi ya Wenzangu tugawane Mitaa ile ya Jirani na Shule ya Muhimbili kwa Kumkimbia baada ya Kuambiwa kuwa tulikuwa tunafanya Fujo katika Mechi moja tuliyocheza na Wababe wa miaka hiyo Shule ya Tambaza na nakumbuka katika hali ya Kumkimbia niliweza Kupoteza Kiatu changu cha Mguu wa Kushoto na nilipofika Nyumbani nilipewa Kipigo cha maana ila nikashukuru kuwa ni bora nimepigwa na Wazazi kuliko ningeishia Mikononi mwa Marehemu Nkama Sharp.

Nasisitiza tena Marehemu Nkama Sharp aenziwe tafadhali na Mapolisi wa sasa hebu muigeni huyu Afande ili nanyi tuwapende.
Kwa kweli miaka ya 80s mpaka 90 kulikuwa Askari Polisi waliokuwa na mbinu za kusambaratisha vigenge vya wahalifu yaani kwa kupita tu kwenye mitaa, wale masela wa miaka hiyo waliokuwa wakivuta jani vijiweni walikuwa wakikimbia wenyewe.Nakumbuka pale Arusha kulikuwa na Polisi mmoja alikuwa anafahamika kwa jina la Kimaro maarufu sana kwa jina la "SABA SITA" huyu jamaa hakuwa tofauti na marehemu Mkama Sharp. Pale Arusha miaka hiyo hakuna mtu ambaye alikuwa hamjui "SABA SITA". Kiukweli huyu askari alikuwa very smart katika kazi yake kwanza alikuwa anaipenda. Nakumbuka pale Sheikh Amri Abeid Stadium kulikuwa na mechi ya ligi kuu kati ya Simba SC na Ndovu FC ya Arusha, kwa baadhi ya wapenzi wa soka walikuwa wakiruka ukuta kuingia uwanjani kwa kukosa kiingilio,sehemu nilipokuwa nimekaa wakaja kukaa jamaa watatu walioruka ukuta kumbe Saba Sita alikuwa amewaona akapotezea kama hajawaona, wale washkaji wakajisahau. Kumbe "7 6" alikuwa anawalia timing, Simba ilipata goli la kuongoza lililofungwa na marehemu Edward Chumila uwanja mzima ulizizima kwa kushangilia lile goli, muda huo sasa Saba Sita akiwa amevalia pama lake la FFU, pingu, kirungu na kiunoni akiwa na pistol iliyokuwa kwenye kasha lake alikuja mpaka pale nilipokuwa nimekaa akawachomoa wale jamaa watatu walioruka ukuta sio siri jamaa waliingia hofu kubwa, akaanza kuzunguka nao uwanja mzima akiwa amewafunga mashati yao kwa kuwaunganisha alipofika nao kwenye Defender la Polisi aliwaamuru wapande ndani na walale kifudi fudi, hiyo ndio ilikuwa adhabu yao hawakuwapiga hata kidogo mpira ulipokwisha aliwaachia. Baadae nasikia Saba Sita alihamishiwa Mererani kikazi na kisha alihamishiwa tena CCP kuwa Mkufunzi. Nowadays sijui alipo nadhani atakuwa amestaafu.Lakini niconclude kwa kusema Mkama Sharp na Saba Sita ni Polisi waliokuwa very professional katika kazi yao.
Huyu mangi ni proffesional killer

Ndio kazi yake..alikua kituo cha sitakshari nadhan mnajua shughul za hicho kituo

Sijui kwa sasa yupo chimbo gani!!

Kaskazin nadhan aliweka rekod kwa kutoa roho za wahalifu
 
Aiseee nilikuwa nadhani ni mimi tu ndo namkumbuka yule Pot kwa members wote wa Jf, kumbe tupo wengi tunaomkumbuka!

Kiukweli, kwa mtu ambaye hakuwahi kumuona au kuingia kwenye 18 za huyu njagu anaweza akadhani jamaa tunampamba bure au tunazungumzia story ya abunuasi.

Nilikuwa namuona sana pale Uwanja wa Taifa wa zamani (shamba la bibi). Na mimi kama mrukaji ukuta maarufu enzi hizo nilishanusurika mara kadhaa kuingia mikononi mwake. Nakumbuka sometimes jamaa alikuwa na mbwa, na mbwa huyu alikuwa anafata maelekezo ya afande Sharp kwa namna ya kushangaza sana.
 
Aiseee nilikuwa nadhani ni mimi tu ndo namkumbuka yule Pot kwa members wote wa Jf, kumbe tupo wengi tunaomkumbuka!

Kiukweli, kwa mtu ambaye hakuwahi kumuona au kuingia kwenye 18 za huyu njagu anaweza akadhani jamaa tunampamba bure au tunazungumzia story ya abunuasi.

Nilikuwa namuona sana pale Uwanja wa Taifa wa zamani (shamba la bibi). Na mimi kama mrukaji ukuta maarufu enzi hizo nilishanusurika mara kadhaa kuingia mikononi mwake. Nakumbuka sometimes jamaa alikuwa na mbwa, na mbwa huyu alikuwa anafata maelekezo ya afande Sharp kwa namna ya kushangaza sana.

Kuna Siku moja nikiwa pale pale Shamba la Bibi ( Taifa ) huku nikiwa bado ni Mdogo kabisa Kipindi kile Katibu Mkuu wa Simba SC alikuwa Mzee Mmoja Mbabe sana ( sasa Marehemu ) Priva Mtema niliwahi Kuona Mbwa wa Mkama Sharp akiondoka na Kipande cha Nyama cha Tako la Kushoto la Mhalifu na sina uhakika kama alipona ile Siku au alikufa baadae.
 
Kwa kweli miaka ya 80s mpaka 90 kulikuwa Askari Polisi waliokuwa na mbinu za kusambaratisha vigenge vya wahalifu yaani kwa kupita tu kwenye mitaa, wale masela wa miaka hiyo waliokuwa wakivuta jani vijiweni walikuwa wakikimbia wenyewe.Nakumbuka pale Arusha kulikuwa na Polisi mmoja alikuwa anafahamika kwa jina la Kimaro maarufu sana kwa jina la "SABA SITA" huyu jamaa hakuwa tofauti na marehemu Mkama Sharp. Pale Arusha miaka hiyo hakuna mtu ambaye alikuwa hamjui "SABA SITA". Kiukweli huyu askari alikuwa very smart katika kazi yake kwanza alikuwa anaipenda. Nakumbuka pale Sheikh Amri Abeid Stadium kulikuwa na mechi ya ligi kuu kati ya Simba SC na Ndovu FC ya Arusha, kwa baadhi ya wapenzi wa soka walikuwa wakiruka ukuta kuingia uwanjani kwa kukosa kiingilio,sehemu nilipokuwa nimekaa wakaja kukaa jamaa watatu walioruka ukuta kumbe Saba Sita alikuwa amewaona akapotezea kama hajawaona, wale washkaji wakajisahau. Kumbe "7 6" alikuwa anawalia timing, Simba ilipata goli la kuongoza lililofungwa na marehemu Edward Chumila uwanja mzima ulizizima kwa kushangilia lile goli, muda huo sasa Saba Sita akiwa amevalia pama lake la FFU, pingu, kirungu na kiunoni akiwa na pistol iliyokuwa kwenye kasha lake alikuja mpaka pale nilipokuwa nimekaa akawachomoa wale jamaa watatu walioruka ukuta sio siri jamaa waliingia hofu kubwa, akaanza kuzunguka nao uwanja mzima akiwa amewafunga mashati yao kwa kuwaunganisha alipofika nao kwenye Defender la Polisi aliwaamuru wapande ndani na walale kifudi fudi, hiyo ndio ilikuwa adhabu yao hawakuwapiga hata kidogo mpira ulipokwisha aliwaachia. Baadae nasikia Saba Sita alihamishiwa Mererani kikazi na kisha alihamishiwa tena CCP kuwa Mkufunzi. Nowadays sijui alipo nadhani atakuwa amestaafu.Lakini niconclude kwa kusema Mkama Sharp na Saba Sita ni Polisi waliokuwa very professional katika kazi yao.
Huyu 7 6 ana mtoto wake wa kike anajiita tunda [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sharp na mbwa wake (mbwa wa polisi).

Si mara 1 au mara 2 niliwahi kumwona Sharp akiwa na mbwa. Kuna wakati angemwacha mbwa karibu na geti la kuingia kwenye Uwanja wa Taifa wa zamani (shamba la bibi) bila kumfunga popote.Angemwamrisha "tulia hapa hadi nikukute, usiondoke!" na mbwa angatulia hapo. Hata akikuona unajipenyeza getini kiwizi wizi au unajaribu kuruka ukuta mbwa huyo asingekuwa na time na wewe.

Ila ole wako aamrishwe kukukamata ndo utaisoma namba.Afande Sharp angemwelekeza mbwa wake " unamwona yule jamaa aliyevaa kofia ya blue, t-shirt nyeupe na jeans ya blue?nenda kamkamate!" Ni hivi mbwa angekusonga wewe tu aliyeelekezwa akukamate (hata kama uko kwenye kundi la watu wengi, na angekukamata).

Iliwahi kutokea afande Sharp alimsakizia mbwa msela mmoja aliyekuwa anajaribu kupita chini ya geti, jamaa alivyoona atadakwa ikabidi akimbilie kwenye kambi ya jeshi ya Abdallah Twalipo (almaarufu 'Ngome') iliyo jirani kabisa na Uwanja wa Taifa na kituo cha mafuta. Jamaa alivyoingia kambini, wazee wa JWTZ waliokuwa zamu walimlinda na kumwambia asiwe na hofu, walichofanya ni kumsubiri mbwa aingie kambini kisha wamfanyie mambo ya Samson na Simba wa Wafilisti. Ila yule mbwa alikuwa na akili bhana, alifunga breki getini na kurudi kwa boss. Wajeda wakamwambia Sharp "huyo mbwa wako na wewe mwenyewe leo tulitaka tuwafundishe adabu.Rudia tena uone". Sharp hakujibu neno.

Ila huyu Pot alikuwa tishio kwa wahuni kwakweli.Kuna mtoto yupi wa mjini ambaye hakumfahamu?
 
Hata mimi namkumbuka. Ila kwangu naona ni kama chongo kwenye kundi la vipofu. Nadhani ushamba wetu hasa enzi zile za zamani ndizo zilimkuza zaidi. Naomba nieleweke kuwa sisemi kuwa alikuwa ''mzuri'' wa kazi yake lakini nasema tu ''uzuri'' wake ulipaishwa na ushamba na woga wetu.
wamekupa rangi zake zote mkuu.nyeupe na nyeusi yake.

hivi unajisikiaje ukiambiwa huyu mtu hapendi tabia fulani,lakini ni muelewa sana kama umefanya kwa kutokukusudia!!!!!

halafu unasikia wanaume na mbavu zao wanaufyata akikatiza,kwanini yeye tu na si manjagu wengine???maana yake hakuwa wa kawaida anapoamua kukutolea betri.
 
Aiseee nilikuwa nadhani ni mimi tu ndo namkumbuka yule Pot kwa members wote wa Jf, kumbe tupo wengi tunaomkumbuka!
Kiukweli, kwa mtu ambaye hakuwahi kumuona au kuingia kwenye 18 za huyu njagu anaweza akadhani jamaa tunampamba bure au tunazungumzia story ya abunuasi.
Nilikuwa namuona sana pale Uwanja wa Taifa wa zamani (shamba la bibi). Na mimi kama mrukaji ukuta maarufu enzi hizo nilishanusurika mara kadhaa kuingia mikononi mwake. Nakumbuka sometimes jamaa alikuwa na mbwa, na mbwa huyu alikuwa anafata maelekezo ya afande Sharp kwa namna ya kushangaza sana.
 
Sharp na mbwa wake (mbwa wa polisi).

Si mara 1 au mara 2 niliwahi kumwona Sharp akiwa na mbwa. Kuna wakati angemwacha mbwa karibu na geti la kuingia kwenye Uwanja wa Taifa wa zamani (shamba la bibi) bila kumfunga popote.Angemwamrisha "tulia hapa hadi nikukute, usiondoke!" na mbwa angatulia hapo. Hata akikuona unajipenyeza getini kiwizi wizi au unajaribu kuruka ukuta mbwa huyo asingekuwa na time na wewe.

Ila ole wako aamrishwe kukukamata ndo utaisoma namba.Afande Sharp angemwelekeza mbwa wake " unamwona yule jamaa aliyevaa kofia ya blue, t-shirt nyeupe na jeans ya blue?nenda kamkamate!" Ni hivi mbwa angekusonga wewe tu aliyeelekezwa akukamate (hata kama uko kwenye kundi la watu wengi, na angekukamata).

Iliwahi kutokea afande Sharp alimsakizia mbwa msela mmoja aliyekuwa anajaribu kupita chini ya geti, jamaa alivyoona atadakwa ikabidi akimbilie kwenye kambi ya jeshi ya Abdallah Twalipo (almaarufu 'Ngome') iliyo jirani kabisa na Uwanja wa Taifa na kituo cha mafuta. Jamaa alivyoingia kambini, wazee wa JWTZ waliokuwa zamu walimlinda na kumwambia asiwe na hofu, walichofanya ni kumsubiri mbwa aingie kambini kisha wamfanyie mambo ya Samson na Simba wa Wafilisti. Ila yule mbwa alikuwa na akili bhana, alifunga breki getini na kurudi kwa boss. Wajeda wakamwambia Sharp "huyo mbwa wako na wewe mwenyewe leo tulitaka tuwafundishe adabu.Rudia tena uone". Sharp hakujibu neno.

Ila huyu Pot alikuwa tishio kwa wahuni kwakweli.Kuna mtoto yupi wa mjini ambaye hakumfahamu?
mbwa alijua atapigwa risasi.

mbwa yule wa polisi ni sawa na farasi,ana uwezo wa kujua dhamira iliyoko usoni kwa mtu.
 
Huyu afande Nkama Sharp alikuwa anamiliki kikundi cha Mchiriku kilichoitwa Night star musical club ambacho makao yake yalikuwa mtaa wa Kibambawe Kariakoo.
 
hIVI MAYENU WA UBUNGO BADOO YUKOO OFISINII MJI ULIKUWA NA FURAHAAA ACHA SIOO WA SASA WANAKOMAA NA BAULA MPAKA WANA.....
 
Back
Top Bottom