Huyu trafiki kumkaribia hivi Rais sio hatari?

Huyu trafiki kumkaribia hivi Rais sio hatari?

Mhmhmhmh!

Tuanze mdogo mdogo kwanza!

Kwanza tuelewe mizunguko (guarding circles) inayomlinda Mh Rais. Tukiachana na mzunguko huo ambao umo ndani ambao hatuuoni, kuna mizunguko mitatu iliyo dhahiri katika video.

Mzunguko wa tatu upo huo wa polisi pamoja na wanausalama waliovalia kaunda suti. Unaona kabisa Trafki anaupita na kujitokeza kuukabili mzunguko unaofuata. Hao walijisahau kabisa.

Mzunguko wa pili ni huo wa Wanajeshi walioshikilia mitutu mikubwa mikubwa.
Ukiangalia kwa umakini, kuna mwanajeshi mmoja anamnong'oneza afisa (katika mzunguko wa tatu) kitu. Kumnong'oneza huko kukamfanya kupoteza focus ya kuangalia kwa umakini

Isingelikuwa huyo mwenzake kumuwahi huyo Trafiki na kumuamuru asipite huko bila shaka angelipita karibu kabisa na circle ya kwanza.

Mzunguko wa tatu, unahusisha wanausalama wengine pamoja na huyo mnayemwita Mpambe. Baada ya kuamuriwa kwa kusukumwa trafiki analazimika kupita katikati ya mzunguko wa pili na wa tatu.

Trafiki alifikaje?
Kwanza ametumia advantage ya yeye kuwa sehemu ya usalama. Amevalia kitrafiki.
Akapata upenyo kusogea ndani zaidi.

Lakini tukubali kuwa kuna uzembe ulifanyika wa kumpuuzia.

Hata baada ya kusukumwa anaondoka kwenda kumuagamia mwanausalama kiunoni. Sijui ni makusidi ama kukosa balance.

Huenda ni makusudi kwa kuwa hakusukumwa kwa nguvu sana. Ni kidogo tu. Lakini pia, askari anatakiwa awe mkakamavu, force kidogo kama ile si ya kukuyumbisha kutaka kuanguka.


Huenda si makusidi kwa sababu:
Uoga ulichangia kukosa balance. Nafasi baina ya aliyesukuma na aliyetaka kumuangukia haikuwa ya kutosha.

Je, ni threat?
Hapana, kwa sababu hakusababisha usumbufu wa aina yeyote. Alishindwa kuelewa mipaka yake, mahali anapotakiwa kuishia.

Ila uzembe umefanyika kwa kikosi kushindwa kumzuia kutofika huko.
Iweke tena hiyo clip mkuu
 
Walinzi wa line ya pili na tatu wamefanya kazi yao sahihi.Walikuwa na tahadhari tangu akiwa anatokea kule kuna paka wawili watatu hapo walishanusa harufu yake.
Plus msisahau wale wasiojulikana ambao wanasubiri threat ifikie secondary stage wajitokeze.they observe everything.
Na inaonekana kulikuwa na call mbele maana kuna trafiki mwingine alikuwa anakimbia nyuma ya gari ya Rais.So wanafahamika tayari ingawa alikumbushwa kufuata taratibu😊
Nina hakika yule trafiki hajui wapi anatakiwa apite na wapi hatakiwi apite.

Nilishuhudia tukio moja nilikuwa kwenye hafla fulani hivi sehemu wakaja viongozi,kuna askari wameshika bunduki ati wamekaa wanamtizama yule kiongozi wakati mimi ninachofahamu mlinzi kama mlinzi unatakiwa uwaangalie watu na sio unamuangalia kiongozi.
 
Mfumo wa ulinzi wa mama unatia shaka pakubwa sana kuna picha moja nimeona mlinzi mwanamama kavaa high heels? Hivi wapo serious kweli na uhai wa huyu mama?

Ni kawaida kwa walinzi wa kike kuvaa travolta ila huyu kanishtua kwa kweli leo, mlinzi anavaa kama anaenda ofisini.
Usiongee sana kuna wauza magenge humu wao wanajiaminisha tuko salama watakuja kukupinga. Tangu ile ziara ya kutoka nchini Kenya tulianza kupiga kelele wale wafanyakazi wa airport waliokuwa wanazubaa nyuma ya ndege wakiwa wamevaa reflectors wakati rais anashuka usiku ule. Na ile style ADC wake na delegates wanavyoshuka ovyo bila mpangilio.

Ule uzi uliweka hiyo video siukumbuki waliokuwa wanapinga waje na hapa wapinge. Maeneo mengi anaonekana ulinzi wake ni wa kawaida sijui wasimamizi ndio wale St. Yohana evening class, yani Konde Boy anaweza jichanga akaweka ulinzi wa kuzuga machoni kihunihuni na tukashindwa kuukosoa kuliko hawa wapokea posho.
 
Naona urefu umemsaidia pia
Ndiyo sifa ya walinzi, sasa kwa mama wamejazana walinzi wafupi halafu ni goigoi kweli sijui ni nani anawaruhusu watu wa namna hii kutengeneza safu ya ulinzi wa mama, hawa walinzi wenye kimo kifupi wakafanye kazi nyingine za kulinda mageti na si kuwa katika safu ya ulinzi wa kiongozi mkuu.

Ulinzi wa mama unapaswa kuwa na watu wenye miraba minne na wakakamavu hivi huyu kiongozi wa hiki kikosi cha ulinzi hajifunzi kwenye mataifa yaliyo endelea? Aone ni sifa zipi zinahitajika kwa walinzi hasa hao escort team ambao wako na mama muda wote ameshindwa kufanya copy and paste kutoka kwa wale walinzi waliokuwa wanatembea na Hayati John Magufuli.
 
Mbona anaonekana kama amepiga TUNGI? Na lengo lake lilikuwa nini na kwanini asipite nyuma ya gari badala ya mbele?
 
Nina hakika yule trafiki hajui wapi anatakiwa apite na wapi hatakiwi apite.

Nilishuhudia tukio moja nilikuwa kwenye hafla fulani hivi sehemu wakaja viongozi,kuna askari wameshika bunduki ati wamekaa wanamtizama yule kiongozi wakati mimi ninachofahamu mlinzi kama mlinzi unatakiwa uwaangalie watu na sio unamuangalia kiongozi.
Polisi inahitaji reform kuanzia recruitment hadi mental drills.
You can see kisaikolojia huyo trafiki hapo anaonekana ni mpenda sifa haswa.Na alipokumbushwa limits zake na walinzi wa Rais you can see the way he reacted bila utulivu mpaka alipomwona kamanda wake mbele ndio akili ikamtulia.Kakumbuka kumpigia saluti polisi mwenzie lakini yule kanali aliyemfurusha pale alimkimbia tuu na cde anayelindwa kampita tuu.Huyu akarushwe kichura kidogo aisee!
 
Rais nae n binadam Tu Kama Sisi
Kiufupi hawajiamin ndo maana
Walikua na walinz mda wote
 
Kweli kuna yeyote duniani anaweza kumdhuru mama yetu? Kuna yeyote ana uthubutu wa kunyanyua mkono na kumdhuru mama? Hamna kabisa
Wewe diaspora nakuuliza wakati John F. Kennedy anapigwa risasi kuna kenge yeyote alikuwa anapendwa pale States kuliko yeye?
Wakati Ronald Reagan anapigwa risasi pale Hilton Hotel kuna mtu alikuwa anakubalika hata kumkaribia?
 
Ndiyo sifa ya walinzi, sasa kwa mama wamejazana walinzi wafupi halafu ni goigoi kweli sijui ni nani anawaruhusu watu wa namna hii kutengeneza safu ya ulinzi wa mama, hawa walinzi wenye kimo kifupi wakafanye kazi nyingine za kulinda mageti na si kuwa katika safu ya ulinzi wa kiongozi mkuu.

Ulinzi wa mama unapaswa kuwa na watu wenye miraba minne na wakakamavu hivi huyu kiongozi wa hiki kikosi cha ulinzi hajifunzi kwenye mataifa yaliyo endelea? Aone ni sifa zipi zinahitajika kwa walinzi hasa hao escort team ambao wako na mama muda wote ameshindwa kufanya copy and paste kutoka kwa wale walinzi waliokuwa wanatembea na Hayati John Magufuli.
Naona wale kina mama walikuwa wanashangaa tu na barakoa zao no reaction kabisa labda kidogo yule npambe wa raisi nimeona akishusha mikono kuelejea kiunoni labda kujiandaaa kutoa silaha yoyote (kama kweli alikuwa nayo)
 
Huyo trafiki ni kama amefanya kusudi kumsukuma mwanausalama baada ya kuelekezwa kwa kupita. Kimsingi, hapo kulikuwa na makosa na huyo trafiki hakufanya vyema kumsukuma mwanausalama na kumtwangia saluti mkuu wake tu.

Lipo jambo la kuchunguzwa na kurekebishwa hapo. Binafsi, sikupenda namna huyo trafiki alivyomsukuma kwa makusudi( tazama mkono wake wa kushoto) mwanausalama.
alikua ana mkwepa mwanaume mwenyewe silaha
 
Mfumo wa hiyo video. Wengine kwetu haifunguki.. tuambieni ni katika mkutano upi ikibidi tuingie you tube
 
Naona wale kina mama walikuwa wanashangaa tu na barakoa zao no reaction kabisa
Wapo kuuza sura kuna mmoja ni mlinzi naona kavaa kiofisi na katupia kabisa high heels utafikiri yupo kwenye maonesho ya u- miss, mkuu wao ajaribu kuliangalia hili kwa upana zaidi aweke watu walio makini na kazi yao maana wengi wao wanakula posho za bure na kazi hawataki kufanya.
 
Wapo kuuza sura kuna mmoja ni mlinzi naona kavaa kiofisi utafikiri yupo kwenye maonesho ya u- miss mkuu wao ajaribu kuliangalia hili kwa upana zaidi.
Mkuu naomba uniambia tofauti ya huyo mama namna alivyovyaa na hao wengine waliovaa suti kuna tofauti gani mkuu
 
Back
Top Bottom