Huzuni/furaha tunazitengeneza sisi katika haya maisha, kila unachodhani kitakupa furaha kipo neutral + SULUHISHO LAKE

Huzuni/furaha tunazitengeneza sisi katika haya maisha, kila unachodhani kitakupa furaha kipo neutral + SULUHISHO LAKE

Hivi kwa mfano mtu alikuwa hataki ndoa akidhani kwamba akiwa single atakuwa na furaha, matokeo yake akaikosa hiyo furaha akaamua kuingia kwenye ndoa sababu anaamini labda huko ndiko ataipata furaha, ila cha ajabu huko nako anakosa furaha huyu mtu anatakiwa afanyaje

Au mtu alikuwa masikini na akawa hana furaha, hivyo akawa anahangaika kutafuta utajiri akidhani kwamba akiwa tajiri ndio atakuwa na furaha, matokeo yake akawa tajiri ila akaikosa hiyo furaha aliyokuwa anaitafuta huyu mtu anatakiwa afanyaje

Mifano ni mingi ila hoja yangu ni, ikiwa kila kitu pamoja na kinyume chake vyote havina furaha, mtu atatakiwa achague kipi
Atafute namna nyingi za kupata furaha, asitegemee moja tu
 
Furaha ni hisia nzuri juu ya Jambo au Hali fulani. Furaha ni huja Kwa muda then utoweka. Hi hisia na vile vichocheo vya mwili vinakufanya ujisikie vizuri.

Kwenye maisha jambo la mhimu ni amani na sio furaha. Amani ni Hali ya akili kuamini Iko sababu njema ya wewe kuwa vile ulivyo. Kutafuta sababu chanya kwenye Hali zote na kubaki na tumaini.

Heshima Sheria za asili ili kuipata amani .
 
Naam enhee..?

Yaani hiyo ni uthibitisho kwamba furaha hapo kwenye vitu ambavyo tunatarajia vitupe furaha.

Kama umepata furaha kwa sababu umeoa,au umenunua gari au nyumba basi tambua kwamba hiyo furaha uliyonayo sio kwa sababu ya hivyo vitu ulivyovipata bali ni kwa sababu ya wewe umeamua kufurahi kupitia hivyo vitu.

Kama ingelikuwa ni kweli kwamba furaha inatokana na vitu basi mtu huyo angekuwa na furaha muda wote ambao yuko na hicho kitu,lakini hali inakuwa tofauti hiyo ina maana ya kwmaba hivyo gitu VIMESHINDWA KULETA FURAHA KWAKE YEYE.

Kwanza anatakiwa afahamu kwamba furaha yake ni jukumu lake,na wala furaha yake sio jukumu la ndoa,au nyumba,au utajiri.

Utajiri,ndoa,mwenza,nyumba,pesa n.k hayo yote usiyabebeshe majukumu ya kukupa furaha,hayo yako neutral wala hayahusiki na furaha yake.

Bali yeye sasa ndio anatakiwa ajifurahishe kwa vitu ambavyo yuko navyo na sio kujifurahisha kwa vitu ambavyo angetamani avipate.

Anajifurahisha vipi ? Tutaona huko chini ila kwa ufupi ni KUSHUKURU au gratitude pamoja na tafakuri ya neema hizo.

Yaani pia hiyo ni uthibitisho kwamba pesa haileti furaha,bali wewe mwenyewe namna ulivyo ndio unaleta furaha.

Kama hauna pesa unaweza kudhani kwamba ukizipata utakuwa na furaha,ila cha ajabu ukishazipata tu baada ya siku kadhaa unaanza kuona ni jambo la kawaida sana,taratibu utaanza kuona ni jambo la kawaida,hiyo itafanya urudi katika system ya zamani na utaanza kuwa bored na maisha.

Mtu atatakiwa achague kuishi katika hali ambayo yuko nayo wakati huo kwa sababu sote tunaishi sasa hivi.

SOte tunaishi sasa hivi ndio maana tunavuta pumzi sasa hivi ili tuendelee kusihi.

HIvyo hata furaha ni makosa kuisubirisha wakati ujao ukipata jambo fulani wakati furaha unatakiwa uiishi sasa hivi na sio baada ya kupata jambo hilo.

Mtu mzima anaweza ku experience furaha.
Mtu mlemavu wa macho anaweza ku experience furaha.
Mtoto mdogo anaweza kuexperience furaha.
kIjana na mzee wanaweza ku experience furaha.
Mwanaume anaweza ku experience furaha
Mwanamke anaweza ku experience furaha.

NINI MAANA YANGU ?

maana yangu ni kwamba kila mtu hapo juu ni tofauti na mwingine na utakuta alichonacho huyu mwingine hana lakini je KWA NINI WOTE WANAWEZA KU EXPERIENCE FURAHA LICHA YA TOFAUTI ZAO ?
jawabu ni kwamba wataexperience furaha pale ambapo wataanza ksuhukuru na kuona umuhimu wa vile vitu au hali ambazo WAKO NAZO KWA WAKATI HUO,na sio kwa vitu au hali ambazo wanazitamani za baadae.

Ya kuandika ni mengi sana ila tuanze hapo tu mkuu kama kuna swali sehemu naomba uulize mkuu..
Mkuu uko sahihi ila mimi huwa naona hakuna haja ya kupima furaha ya mtu fulani kwa kutumia mtu mwingine, yani mfano mtu anasema yeye atakuwa na furaha akiwa na ndoa au mali nyingi hakuna haja ya kumuambia eti kuna mtu anavyo hivyo vyote na hana furaha, na hapo ndipo inapokuja ile kauli ya happiness is subjective sababu tunatofautiana jambo linalomletea au linalomnyima furaha fulani si lazima limletee au limnyime furaha mwingine
 
Furaha ni hisia nzuri juu ya Jambo au Hali fulani. Furaha ni huja Kwa muda then utoweka. Hi hisia na vile vichocheo vya mwili vinakufanya ujisikie vizuri.

Kwenye maisha jambo la mhimu ni amani na sio furaha. Amani ni Hali ya akili kuamini Iko sababu njema ya wewe kuwa vile ulivyo. Kutafuta sababu chanya kwenye Hali zote na kubaki na tumaini.

Heshima Sheria za asili ili kuipata amani .
Umegusia kitu cha msingi sana ambacho ilitakiwa nikizungumze.

ILitakiwa tuweke mjadala wa ni nini furaha,furaha ni nini,hiyo furaha tunayoizungumzia ni nini ?

Binafsi naungana na wewe kwamba ile furaha tunayoexperience katika matukio mazuri ile mimi siiiti furaha naweza kuiita kama stress nzuri.

Furaha kwangu mimi ni ile amani,utulivu wa nafsi na akili inakuwa imetulia kabisa kila kitu unaona kinaenda powa katika ulimwengu.
 
Hivi kwa mfano mtu alikuwa hataki ndoa akidhani kwamba akiwa single atakuwa na furaha, matokeo yake akaikosa hiyo furaha akaamua kuingia kwenye ndoa sababu anaamini labda huko ndiko ataipata furaha, ila cha ajabu huko nako anakosa furaha huyu mtu anatakiwa afanyaje

Au mtu alikuwa masikini na akawa hana furaha, hivyo akawa anahangaika kutafuta utajiri akidhani kwamba akiwa tajiri ndio atakuwa na furaha, matokeo yake akawa tajiri ila akaikosa hiyo furaha aliyokuwa anaitafuta huyu mtu anatakiwa afanyaje

Mifano ni mingi ila hoja yangu ni, ikiwa kila kitu pamoja na kinyume chake vyote havina furaha, mtu atatakiwa achague kipi
Uchaguzi ni mmoja tu mkuu!

Acha nihuzunike ndani ya DISCOVERY 3 kuliko kuhuzunika kwenye daladala!!
 
Ndio hapo Sasa ukiwa na malengo ya basic life hizo billions utazisikia tu.

Hapo hapo Kwa kipato unachokipata wewe Kuna mtu anasema akiwa na Hali kama Yako amemaliza biashara, anaacha dhambi zote, kazi yake inakua ibada tu.
Atakuwa amelogwa basi 🤣 maana mie mwenyewe kipato hicho hakintoshi. Ukitamani maisha ya juu sana ndio unarisk marinda yako ama maisha kabisa toka kwa mawakala wa kuzimu walioko maeneo mbali mbali nchini.
 
Hiki ndicho kitu ambacho wadau wengi hawajakinote katika point zako.

Wao wanadhani utabadilisha maisha na kuishi maisha flani classic.

Yaani ni life simple tu,huku hakuna ambaye anajua kwamba unamiliki utajiri mkubwa namna hiyo.

Ishu inakuja vijana wa sasa hivi sisi wengi tunataka kutumbua maisha ili tuonekane kwamba tunazo,hatuna ile roho ya kuficha mafanikio yetu,tunataka tukioata kila mtu atuheshimu na ajue kwamba pesa ipo ili wasituchukulie poa.

Kumbe kuna watu ambao wakizipata wataejdelea kumaintain their normal life na wakaendeleza uhusiano na watu ambao walikuwa nao mwanzo
Yeah tunaendelea ku keep it low key. Afterall ku flash maisha huwa sipendagi hizo tabia.
 
Atakuwa amelogwa basi 🤣 maana mie mwenyewe kipato hicho hakintoshi. Ukitamani maisha ya juu sana ndio unarisk marinda yako ama maisha kabisa toka kwa mawakala wa kuzimu walioko maeneo mbali mbali nchini.


Naelewa unachokisema lakini ndio Kuna watu ni maombi Yao Kila siku wawe na maisha kama Yako.
 
hahahahah kweli sikatai ila kwa mtu mwenye familia hawezi ombea kipato kidogo.

Kwa uzoefu wangu, uhalisia wa mambo uko tofauti sana na vitu vinavyoonekana Kwa nje.

Ndio maana mleta uzi kasema itengeneze furaha Yako mwenyewe, ikiwezekana isitegemee vitu au hali.

Unapokuwa shule, furaha Yako ni kufaulu, ukisha faulu unaona si chochote.

Ukiwa kwenye masomo, unatamani upate kazi, ukisha pata kazi unafurahia siku za mwanzo Kisha inakua kawaida.

Hapo unatamani upate usafiri, nyumba, familia n.k

Vyote hivyo vinakupa furaha ya muda mfupi sana Kisha unaona kawaida huku ukiwa na kitu ya kitu kingine unachofikiri kirakupa furaha.

Hapo wale ambao hawana kazi, wanatamani hata ipatikane sehem ya kujitolea tu.

Kuna watu hawana wenza, wanafikiri walipata italeta furaha lakini walio na wenza wengine wanatamani wabaki bila wenza.

Ukiweza kuridhika na kufurahia Kila hatua unayopiga, unawezakuwa mtu mwenye furaha zaidi hata kama hauna vitu vingi.

Haya maisha Hadi unaingia kaburini unakua Bado Kuna vitu unafukuzia vikupe furaha.
 
Yan haya maisha bhana,ukioa mwanamke mweusi utahisi labda ungeoa mweupe ungeinjoy zaidi yan unatamani kujua mweupe ana ladha gani
 
Kwa uzoefu wangu, uhalisia wa mambo uko tofauti sana na vitu vinavyoonekana Kwa nje.

Ndio maana mleta uzi kasema itengeneze furaha Yako mwenyewe, ikiwezekana isitegemee vitu au hali.

Unapokuwa shule, furaha Yako ni kufaulu, ukisha faulu unaona si chochote.

Ukiwa kwenye masomo, unatamani upate kazi, ukisha pata kazi unafurahia siku za mwanzo Kisha inakua kawaida.

Hapo unatamani upate usafiri, nyumba, familia n.k

Vyote hivyo vinakupa furaha ya muda mfupi sana Kisha unaona kawaida huku ukiwa na kitu ya kitu kingine unachofikiri kirakupa furaha.

Hapo wale ambao hawana kazi, wanatamani hata ipatikane sehem ya kujitolea tu.

Kuna watu hawana wenza, wanafikiri walipata italeta furaha lakini walio na wenza wengine wanatamani wabaki bila wenza.

Ukiweza kuridhika na kufurahia Kila hatua unayopiga, unawezakuwa mtu mwenye furaha zaidi hata kama hauna vitu vingi.

Haya maisha Hadi unaingia kaburini unakua Bado Kuna vitu unafukuzia vikupe furaha.
Mkuu umefafanua vizuri sana.

Kuna mama yangu mmoja yeye alikuw a akiona toleo la simu nzuri huwa anatamani aipate na hujisemea kabisa "yaani nikiipata simu ile nitafurahi sana"

Matokeo yake akishaimiliki ile simu baada ya mwezi anatangaza kuiuza keshaichoka,so nilikuwa najiuliza nini shida tena..

Nikaja kugundua hicho kitu kwamba uhalisia wa furaha ni tofauti na vile tunavyofikiria.

Binafsi nimekuwa mtu ambaye ninaweza kujishift pale ninapopitia katika changamoto.

Naweza kuamka asubuhi nikaa nikaanza tu kushukuru Mungu kwa kuwa na ulimi ambao hauna vidonda na naanza kuwaza tabu zinazopatikana mtu akiwa na ulimi wa vidonda,baada ya hapo najisemea asante sana Allah,kisha nahamia kwenye kitu kingine kushukuru na kutafakari,nikipata vitu vuangu 10 tu vinanitisha basi najikuta nina amani na maisha.
 
Yan haya maisha bhana,ukioa mwanamke mweusi utahisi labda ungeoa mweupe ungeinjoy zaidi yan unatamani kujua mweupe ana ladha gani
😄😄.

Yani mkuu ni kuridhika na kile ulichonacho tu.

Na ili uridhike inabidi uone umuhimu wa kile ambacho uko nacho.

Na unaonaje umuhimu ? Utaona umuhimu kwa kushukuru.

Na unashukuru vipi ? Unashukuru kwa kutafakari umuhimu wa kitu hicho.
 
Kuwa na pesa, gari, nyumba sio chanzo Cha FURAHA!
Hata ujekuwa na mabilions of money bado hutaweza kywa na FURAHA ya kudumu!
FURAHA pekee ni Ile inayoletwa na Mungu katika shida na raha bado inakaa nawewe!
Wafilipi 4:4 “Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.”

Warumi 12:12 “kwa tumaini, mkifurahi katika dhiki, mkisubiri; katika kusali, mkidumu;
 
Kama kweli furaha inatokana na kitu fulani ambacho unakihitaji jee kwa nini baada ya kupata kitu hiko bado kuna vitu vingine vitakukosesha furaha na kukutia stress ?

Yaani utajikuta umepata mtoto tayari,lakini kodi ya nyumba inakunyima raha

,je ni ipi faida ya furaha ya mtoto kama furaha hiyo haiwezi kuondoa hata huzuni ya kudaiwa kodi ya nyumba ?

Ni ipi faida ya furaha ya kuwa na gari kama furaha hiyo haiwezi kuondoa huzuni ya kazi nyingi ofisini ?

Ni ipi faida ya kuwa na furaha ya kupata nyumba kama furaha hiyo haiwezi kuondoa huzuni ya kipato kidogo ?

katika haya maisha hicho unachodhani ukikipata kitakupa furaha sio kweli.

FURAHA YA KWELI NI ILE AMBAYO INAKUONDOLEA HUZUNI UNAYOIPATA KATIKA VITU VINGINE.

furaha unayo mwenyewe na wala haipo kwenye vitu unavyovihitaji Kama vile watoto,pesa,nyumba n.k.

Unaweza kutamani gari,ukalinunua na siku za mwanzo ukawa na furaha sana na upya wake.

lakini masiku yakikatika unaliona gari la kawaida hivyo halikupi tena furaha kama ile ya mwanzo,imeenda wapi furaha ile ?

vitu ambavyo tunategemea vitatupa furaha tukishavimiliki tu baada ya masiku kadhaa tunaviona vya kawaida na havitupi tena furaha.

Nilitamani sana kuoa na siku ya kuoa nilikuwa na furaha sana,lakini leo hii sijui furaha ile imeenda wapi na ndoa bado ninayo.

Nilitamani kuwa na mtoto,nilipopata mtoto nilikuwa na furaha sana.

leo mtoto ninaye lakini sijui ile furaha ya mwanzo ya kuwa na mtoto siioni tena na mtoto bado yupo.

Hakuna kitu chochote ambacho ni chanzo cha furaha kwenye maisha yetu isipokuwa sisi wenyewe.

SULUHISHO.

FURAHA TUNATAKIWA KUZITENGENEZA KAMA AMBAVYO TUNATENGENEZA CHAKULA,MAGARI AU NYUMBA.

KUITENGENEZA FURAHA.

furaha tunaitengeneza kwa KUSHUKURU na kutafakari faida ya kitu hicho.

Utakapotafakari faida unazopata kwa kitu fulani na kushukuru basi hapo ndipo furaha utaiona.

Ukiamka asubuhi unaenda kazini kwa daladala sawa hauna gari jee umeshawahi kutafakari kwa uchache umuhimu wa daladala kwako na ukasema asante Mungu..?

Umeshawahi kutafakari kwa uchache umuhimu wa macho yako kwa namna unavyotumia na ukasema asante ?

Je miguu,masikio,pua,mdomo umeshawahi kutakarai kwa ucahche umuhimu wa hivyo vitu kwako kwa namna unavyovitumia ?

Bila kuwa na utaratibu huo utajikuta unaamka kila siku uko bored,hauna mood,hauoni kitu kipya katika dunia na utaanza kudhani kwamba furaha yako kuna sehemu imejificha.

Ukweli mchungu ni kwamba hapa duniani kila kitu sisi ndio tuntengeneza,hata furaha tunatakiwa tuitengeneze wenyewe.
Utajuwaje kupata bila kukosa?
 
Angalau umenitia moyo kidogo mkuu.

Nilitamani kupata kazi nzuri thanks God kwa kiwangochangu nimeipata.

Pesa ya mboga na mambo mengine ya kimaendeleo vyote sio tatizo tena kwa kipindi chote nitakacho kuwa hapa.

Lakini silali nawaza familia, leave rotation yangu ni kila baada ya miezi minne then na rudi kwa uyo mamaenu mwezi mmoja.

Hapa ninamastres zakutosha hasa inapofika usiku.

Ninamke mzuri lakini simfaidi hukuniliko mawazo chungu kizima hahaa Duuh.
 
Haha si ndio kuna watu wanasema hivyo kwamba kuwa tajiri siyo kuwa na furaha, unaweza ukawa na hivyo yote na bado ukawa na huzuni, sasa ndio watuambie huyu mtu anatakiwa afanyaje
Huo Msemo kujifariji tu pesa inaleta furaha mno
 
Back
Top Bottom