I am depressed. Naombeni ushauri

I am depressed. Naombeni ushauri

Miaka 40+, watu wazima wawili hamna hata kipande cha ardhi? Ikitokea mmefumba macho leo huyo mtoto wenu atarithi hiyo flatscreen?

Achana na maneno ya marafiki, achana na magroup ya wamama walioshindikana......watu wanafiki sana, huko kwenye magroup wanajifanya hawachangii chochote kwenye familia, ila kiuhalisia wao ndo wanaendesha familia.

Kaa chini na mumeo, pangeni kwa pamoja, wekeni mshahara mezani muupangie matumizi ya pamoja, kisha muamini, let him lead......mume haelekezwi, mume anashauriwa kwa upole, kisha unamuachia siku kadhaa za kutafakari ulichomshauri........using'ang'anize kila unachotaka au unachoshauri afanye hapo hapo......wenzetu hawapo hivyo.
umemuelewa lakini?
 
Pole Dada,Depression sio kitu chepesi hivyo.Ni shida kubwa inayoweza kupelekea kujitoa Uhai!
Tafakari Hilo shimo unalotaka kujichimbia bila sababu!
Nakusihi ridhika na ulichonacho,usiyatafute makubwa.Kufosi lazima lakini usimpeleke puta sana huyo jamaa,yeye ndio atatangulia kupata depression.
Mwenzako yupo kwa Mama yake Hana wasiwasi,mtoto ni sehemu ya familia Yao.
Mshahara wako ukijipanga unaweza ukajenga Nyumba ya uwezo wako kwa ajili ya mwanao,kama mama mkwe wako alivyofanya kwa mwanaye.
Jamaa akiona umuhimu wa kujenga,atajenga tu!
Uliambiwa shule ya kanisa,zipo pia za bei nafuu sana!
Dada kupanga ni kuchagua,usimpe stress mtoto watu Wala na wewe usijipe stress.
Katoto kamoja tu kanawahangaisha watu mko above 40+!
Kingine kuishi nyumbani sio udhalili,watu wa nje wasiwape presha.

Nawatakia furaha na lastborn wako,huyo hahami hapo!..Tena kama ndio kina sisi wa Magomeni,kkoo na ilala ndo usahau kabisaa!
Furahia Maisha dada,depression kitu kibaya saana.
 
Siku moja nagusa simu nakuta mke wangu kamuhadithia mwenzie asitoe pesa Aache kila kitu afanye Mume wake , wakati kama juzi alitoka kunipa 3M ya issue fulani nilikwama , nikajua kumbe wanawake hua mnapotezana wenyewe maana , familia yoyote mkifanya umoja mnasonga mbele , mkianza ubinafsi na familia inasambaratika na Mnaishia kufa maskini , kama mwenzenu anapata pesa anataka Mume wake aombe kwao wakati wangekaa wakajadili wajichange waanze taratibu , kwanza wanakaa bure hawalipi Kodi ilitakiwa wasave wafanye mambo mengine, lakini pia 40+ kukaa bure kunadumaza akili Sana hawana bills ili akili ziwakae sawa
Yani mimi kila siku nasema ningekuwa mwanaume mke wangu marufuku kujiunga na magroup ya wamama......wanadanganyana sana na kupeana negative energy.
Wakati mwingine mtu anayeshauri hata ndoa hana.

Maisha ya sasa bila kusaidiana hamtoboi......na mara nyingine mke unaweza kukuta anabeba 70% ya majukumu ya familia ila anakausha tu na siku zinaenda.
 
Kuna rafiki yangu Mtanzania anaishi Australia aliniambia yeye hata kuoa alijiuliza sana kwa nini aoe? Mpaka akajiridhisha.

Baadaye akajiuliza sana kama anataka mtoto, kwa nini azalishe mtoto, kuzalisha mtoto katika dunia ya leo ni kitu sahihi ama la, alifikiria saana mambo hayo kabla ya kuamua kuwa na mtoto.

Bongo watu wengi hawafikirii mambo haya, yanatokea by default tu.
Watoto wengi hapa bongo ni wale wa kwa bahati mbaya 😄
 
Habari great thinkers.

Nimekuwa msomaji kwa muda mrefu sana humu, ila imenilazimu nijiunge ili nitoe nilichonacho maana ninahisi kuzidiwa moyoni sipati kulala usiku. Nahitaji ushauri.

Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 6, nimeolewa miaka 8 iliyopita, nyumba tunayoishi tumepewa na mama mkwe kwa hiyo hatujajenga na wala hatulipi kodi. Najua unajiuliza hizi information za nini leta hoja, sawa nakuja na hoja.

Ni hivi mume wangu ana kipato cha kawaida tu kwa mwezi labda laki 8 take home. Binafsi nina kipato kwa mwezi kama 2.3m take home. baada tu ya kufunga ndo mume wangu alipoteza kazi kwahiyo alikaa nyumbani kuanzia 2017 akaja kupata kazi 2021 lakini tuliiishi bila shida.

Yeye kwao ni last born ana kaka na dada. Mimi kwetu ni wa pili kuzaliwa ila nahudumia wazazi pia. Kipindi yupo nyumbani ni kamwambia aongee na kaka yake amuazime mtaji wa kufanya biashara lakini mwenzangu alikuwa akikaa kimya, so miaka ikaenda mpaka alivyokuja kupata kazi.

Mwaka jana mwishoni nikagusia tena na kumpa idea ya biashara na alionekana kuipenda sana akasema sawa, na hiyo mwaka jana nilimwambia kwa kuwa mtoto anaingia darasa la kwanza hatuwezi kutegemea mshahara pekee. Ingawa mimi nimefungua biashara ila bado changa na pia ninafanyaga tender za kuprint, kufunga zawadi na kadhalika.

Mtoto tumemtafutia shule kwa pamoja na ada alikuwa anaijua tangu Novemba, nikamwmabia ngoja nikupunguzie mzigo nitalipia usafiri na uniform akasema sawa.

Nikawa namkumbusha kulipa ada anasema anakumbuka. juzi jumapili anasema hiyo ada kubwa sana hatoweza hiyo shule, imagine bado wiki shule zifunguliwe.

Baadae nikamuuliza kuhusu ile idea ya biashara vipi? mana haijalishi mtoto anasoma wapi jinsi anavyozidi kukua madarasa ndivyo gharama zinazidi, akasema mi mambo ya biashara siyawezi wala sijawahi kuyawaza, duuh nikabaki nimetoa macho, nikamuuliza mbona ile idea uliipenda na ukasema utaifanya utamuazima kaka yako mtaji akasema mi siwezi hayo mambo.

Haa, moyo wangu uliinama sana tangu hiyo siku nina mawazo sipati usingizi. Najiuliza niongee na kaka yake au dada yake wamshauri kama hawezi kutegemea kukua kimaendeleo kwa mshahara tu au nibaki nalo? na nikibaki nalo nifanyeje?

Hawazi kujenga, hawazi kununua kiwanja, 2024 january nilimwambia tuweke kiasi cha fedha kwa ajili ya kununua kiwanja akaweka mwezi wa kwanza nadhani kwa kuwa nilimkalia kooni.

Baada ya hapo akawa hawezi kuna siku nikamuuliza akasema mi niache tu na hayo mambo. Nikaacha nikaendelea mwenyewe, ila peke yangu nguvu ni ndogo.

Naombeni ushauri jamani mimi ni mtu mzima nina 40+ nashindwa kuomba ushauri wa rafiki zangu mana ndo yataenezwa.

Nadhani ninaweza pata depression kama ningebaki navyo moyoni kichwa kinauma kwa kuwaza.

Naombeni ushauri tafadhali.

Ushauri ni mgumu sana, sidhani kama Mme wako ana shida kubwa, mwanaume ukiwa huna hela ya kueleweka na mke ana kipato kikubwa ni changamoto sana!

Tatizo lako sio kubwa kama unavyofikiri, tatizo lako lipo kwenye misingi ya kiuanawake na kiuanaume, Hakuna mwenye kosa hapo!

Kwa umri ulio nao upo matured enough na unaweza work around hayo mazingira, 2.5m ongeza laki 8 na Kodi hamlipi; Hakuna sababu ya kumsukuma huyo jamaa kwenye biashara, ni kwamba unataka uhuru na fedha zako.
 
umemuelewa lakini?
Nimemuelewa sana, uzuri anajua mume hana passion ya biashara kuanzia mwanzo, hawezi kumlazimisha.....dawa ni kutumia vipato walivyonavyo kufanya maendeleo ya kiwango chao.....from there mume anaweza kubadilika.
Sasa hivi mume hawezi kutafuta pesa kwa nguvu kwa sababu hana project ya kumuumiza kichwa inayohitaji pesa.....so mshahara unamtosha.

Mi ningemshauri yeye atake a lead indirectly.....like amshauri mume wangu unaonaje tukisave kila mtu laki na nusu kwa mwezi halafu mwisho wa mwaka tununue kiwanja.....akikubali yeye mke anaongeza kiasi cha kusave baada ya miezi lets say 6 anamwambia mume wangu pesa hii, tukatafute kiwanja.....(Muda huo ana options za maeneo anayoyataka)
Kuanzia hapo mume anaweza kuanza kuchangamsha kichwa....

Ila sio anamwambia ooh wanaume wenzio wananunua viwanja wanajenga wee upo tu🤣🤣🤣🤣 atajua hajui.
 
Nimesema machache tu mkuu. Mshahara wangu ndo unalisha wazazi wangu , kulipa bills zao na ninakatwa bima yao na ya mkwe pia kwahiyo kinabaki kiasi kidogo cha fedha ambacho ndo tunatumia kwa pamoja na yake kwa familia.

Acha ndoa kakae na wazazi wako, wewe una Matatizo makubwa sana, na unakatisha tamaa watu kuoa, jamaa wa watu anateseka kuliko wewe!
 
Pole.
naona hamna haja yeye kuanza kuzunguka kwa kaka yake kuomba mtaji. Nyie wawili kama mke na mume ndio mlitakiwa msaidiane kwa kila hali. Mngetafuta namna ya kutumia mshahara wako na wake mpate ya biashara na msiwe na biashara ya mke au ya mume kuweni na biashara ya familia.
Ila wanawake wanajitoa sana kwenye majukumu aisee.

Sasa anamkomalia mwamba ndo afungue biashara yake na sio waongeze nguvu kwenye hiyo yake kama yeye ana idea hizo za biashara basi watumie akili ya mke.

Kuna familia mume hayupo kabisa kwenye mambo ya biashara yeye ni kilimo tu, mambo ya kuzurula kwenye biashara kamuachia mkewe.
 
Duuuuh. Pole Mama.

Usipate presha wala stress.

Kama wewe unaweza kufanya biashara, wewe fanya. Kama anaweza kukusapoti na hakuzuii.
Muhimu zingatia upendo kutoka kwake na wewe Muheshimu hivyo hivyo alivyo. Hayo ndio mapungufu yake.

Mfano.
Kuna familia moja Baba mwenye nyumba hafanyi Kazi yoyote na sio kwamba hana nguvu hapana yupo vyema Kabisa. Yeye ni mitungi muda wote. Mama ndio anapambana, ila huwezi amini ukiwakuta wanavyoishi, Mama humwambii kitu kuhusu Mzee na Mzee humwambii kitu kuhusu Mke wake.

Na familia yao imebarikiwa.

Asante
Ni mapungufu tu mkuu, sio kila mwanaume anawaza kua kama Bakhresa. Akizidi kumlazimisha ndo mwanzo wa malumbano ilhali mke anaweza kufanya yake, taratibu tu jamaa akiona progress atatia mkono wake.

Wanaume hasa wenye mapungufu fulani hawapendi ukweli na hawapendi kuambiwa fanya hivi. Japo ni ushauri ila yeye ataona kama dharau na amri.
 
Nimesema machache tu mkuu. Mshahara wangu ndo unalisha wazazi wangu , kulipa bills zao na ninakatwa bima yao na ya mkwe pia kwahiyo kinabaki kiasi kidogo cha fedha ambacho ndo tunatumia kwa pamoja na yake kwa familia.
Si umesema kipato chako yaani take home ni 2.3m? Kwa hiyo pesa ni ndogo sana?
Mmeo laki 8 + 2.3 m = 3.1 m
Halafu unaleta gazeti? Relax
 
Yani mimi kila siku nasema ningekuwa mwanaume mke wangu marufuku kujiunga na magroup ya wamama......wanadanganyana sana na kupeana negative energy.
Wakati mwingine mtu anayeshauri hata ndoa hana.

Maisha ya sasa bila kusaidiana hamtoboi......na mara nyingine mke unaweza kukuta anabeba 70% ya majukumu ya familia ila anakausha tu na siku zinaenda.
Tena mkipatana watu mnaoweka mipango pamoja kutoboa ni chapchap , lakini mkianza ubinafsi na uchoyo shida huanzia hapo,
 
Habari great thinkers.

Nimekuwa msomaji kwa muda mrefu sana humu, ila imenilazimu nijiunge ili nitoe nilichonacho maana ninahisi kuzidiwa moyoni sipati kulala usiku. Nahitaji ushauri.

Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 6, nimeolewa miaka 8 iliyopita, nyumba tunayoishi tumepewa na mama mkwe kwa hiyo hatujajenga na wala hatulipi kodi. Najua unajiuliza hizi information za nini leta hoja, sawa nakuja na hoja.

Ni hivi mume wangu ana kipato cha kawaida tu kwa mwezi labda laki 8 take home. Binafsi nina kipato kwa mwezi kama 2.3m take home. baada tu ya kufunga ndo mume wangu alipoteza kazi kwahiyo alikaa nyumbani kuanzia 2017 akaja kupata kazi 2021 lakini tuliiishi bila shida.

Yeye kwao ni last born ana kaka na dada. Mimi kwetu ni wa pili kuzaliwa ila nahudumia wazazi pia. Kipindi yupo nyumbani ni kamwambia aongee na kaka yake amuazime mtaji wa kufanya biashara lakini mwenzangu alikuwa akikaa kimya, so miaka ikaenda mpaka alivyokuja kupata kazi.

Mwaka jana mwishoni nikagusia tena na kumpa idea ya biashara na alionekana kuipenda sana akasema sawa, na hiyo mwaka jana nilimwambia kwa kuwa mtoto anaingia darasa la kwanza hatuwezi kutegemea mshahara pekee. Ingawa mimi nimefungua biashara ila bado changa na pia ninafanyaga tender za kuprint, kufunga zawadi na kadhalika.

Mtoto tumemtafutia shule kwa pamoja na ada alikuwa anaijua tangu Novemba, nikamwmabia ngoja nikupunguzie mzigo nitalipia usafiri na uniform akasema sawa.

Nikawa namkumbusha kulipa ada anasema anakumbuka. juzi jumapili anasema hiyo ada kubwa sana hatoweza hiyo shule, imagine bado wiki shule zifunguliwe.

Baadae nikamuuliza kuhusu ile idea ya biashara vipi? mana haijalishi mtoto anasoma wapi jinsi anavyozidi kukua madarasa ndivyo gharama zinazidi, akasema mi mambo ya biashara siyawezi wala sijawahi kuyawaza, duuh nikabaki nimetoa macho, nikamuuliza mbona ile idea uliipenda na ukasema utaifanya utamuazima kaka yako mtaji akasema mi siwezi hayo mambo.

Haa, moyo wangu uliinama sana tangu hiyo siku nina mawazo sipati usingizi. Najiuliza niongee na kaka yake au dada yake wamshauri kama hawezi kutegemea kukua kimaendeleo kwa mshahara tu au nibaki nalo? na nikibaki nalo nifanyeje?

Hawazi kujenga, hawazi kununua kiwanja, 2024 january nilimwambia tuweke kiasi cha fedha kwa ajili ya kununua kiwanja akaweka mwezi wa kwanza nadhani kwa kuwa nilimkalia kooni.

Baada ya hapo akawa hawezi kuna siku nikamuuliza akasema mi niache tu na hayo mambo. Nikaacha nikaendelea mwenyewe, ila peke yangu nguvu ni ndogo.

Naombeni ushauri jamani mimi ni mtu mzima nina 40+ nashindwa kuomba ushauri wa rafiki zangu mana ndo yataenezwa.

Nadhani ninaweza pata depression kama ningebaki navyo moyoni kichwa kinauma kwa kuwaza.

Naombeni ushauri tafadhali.
Depression? Mishahara laki8+m ara m 2.3? Mtaji wa biashara mnataka utoke nje ya familia,Tena kwa kuazima...wanawake mnakuwaga wabinafsi sana,sasa usiombe huyo mumeo awe kashagundua huo ubinafsi na kuukatia tamaa kuwa kwa ubinafsi huu hatutofika popote...anasubiri tu useme tuachane,akujibu kwa kifupi tu 'sawa'...halafu baadaye uje kugundua kuwa mwamba alishatega mitego yake vizuri tu, na alijiandaa vizuri kuishi bill wewe.
 
Habari great thinkers.

Nimekuwa msomaji kwa muda mrefu sana humu, ila imenilazimu nijiunge ili nitoe nilichonacho maana ninahisi kuzidiwa moyoni sipati kulala usiku. Nahitaji ushauri.

Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 6, nimeolewa miaka 8 iliyopita, nyumba tunayoishi tumepewa na mama mkwe kwa hiyo hatujajenga na wala hatulipi kodi. Najua unajiuliza hizi information za nini leta hoja, sawa nakuja na hoja.

Ni hivi mume wangu ana kipato cha kawaida tu kwa mwezi labda laki 8 take home. Binafsi nina kipato kwa mwezi kama 2.3m take home. baada tu ya kufunga ndo mume wangu alipoteza kazi kwahiyo alikaa nyumbani kuanzia 2017 akaja kupata kazi 2021 lakini tuliiishi bila shida.

Yeye kwao ni last born ana kaka na dada. Mimi kwetu ni wa pili kuzaliwa ila nahudumia wazazi pia. Kipindi yupo nyumbani ni kamwambia aongee na kaka yake amuazime mtaji wa kufanya biashara lakini mwenzangu alikuwa akikaa kimya, so miaka ikaenda mpaka alivyokuja kupata kazi.

Mwaka jana mwishoni nikagusia tena na kumpa idea ya biashara na alionekana kuipenda sana akasema sawa, na hiyo mwaka jana nilimwambia kwa kuwa mtoto anaingia darasa la kwanza hatuwezi kutegemea mshahara pekee. Ingawa mimi nimefungua biashara ila bado changa na pia ninafanyaga tender za kuprint, kufunga zawadi na kadhalika.

Mtoto tumemtafutia shule kwa pamoja na ada alikuwa anaijua tangu Novemba, nikamwmabia ngoja nikupunguzie mzigo nitalipia usafiri na uniform akasema sawa.

Nikawa namkumbusha kulipa ada anasema anakumbuka. juzi jumapili anasema hiyo ada kubwa sana hatoweza hiyo shule, imagine bado wiki shule zifunguliwe.

Baadae nikamuuliza kuhusu ile idea ya biashara vipi? mana haijalishi mtoto anasoma wapi jinsi anavyozidi kukua madarasa ndivyo gharama zinazidi, akasema mi mambo ya biashara siyawezi wala sijawahi kuyawaza, duuh nikabaki nimetoa macho, nikamuuliza mbona ile idea uliipenda na ukasema utaifanya utamuazima kaka yako mtaji akasema mi siwezi hayo mambo.

Haa, moyo wangu uliinama sana tangu hiyo siku nina mawazo sipati usingizi. Najiuliza niongee na kaka yake au dada yake wamshauri kama hawezi kutegemea kukua kimaendeleo kwa mshahara tu au nibaki nalo? na nikibaki nalo nifanyeje?

Hawazi kujenga, hawazi kununua kiwanja, 2024 january nilimwambia tuweke kiasi cha fedha kwa ajili ya kununua kiwanja akaweka mwezi wa kwanza nadhani kwa kuwa nilimkalia kooni.

Baada ya hapo akawa hawezi kuna siku nikamuuliza akasema mi niache tu na hayo mambo. Nikaacha nikaendelea mwenyewe, ila peke yangu nguvu ni ndogo.

Naombeni ushauri jamani mimi ni mtu mzima nina 40+ nashindwa kuomba ushauri wa rafiki zangu mana ndo yataenezwa.

Nadhani ninaweza pata depression kama ningebaki navyo moyoni kichwa kinauma kwa kuwaza.

Naombeni ushauri tafadhali.
ajira za connection hizo 😂😂 mimi sina ajira rasmi lakini huenda nikawa nawazidi maendeleo
 
Depression? Mishahara laki8+m ara m 2.3? Mtaji wa biashara mnataka utoke nje ya familia,Tena kwa kuazima...wanawake mnakuwaga wabinafsi sana,sasa usiombe huyo mumeo awe kashagundua huo ubinafsi na kuukatia tamaa kuwa kwa ubinafsi huu hatutofika popote...anasubiri tu useme tuachane,akujibu kwa kifupi tu 'sawa'...halafu baadaye uje kugundua kuwa mwamba alishatega mitego yake vizuri tu, na alijiandaa vizuri kuishi bill wewe.
Nimehisi hivo maana mwanaume akishagundua mke ni mbinafsi , basi hajitumi kwa lolote ana relax kabisa , na angegundua wapo pamoja basi jamaa angechacharika hata kidogo , Mamy K amelielezea vizuri , kwanza kashangaa bibie anatoa mawazo halafu anashauri mwenzake akakope kwao , mtoto wanae mmoja kipato 2.3M +800k wanashindwa kujipanga na kiwanja hawana,
 
unanikandamiza kwa kuwa nimesema kipato changu mkuu? nimejibu hapo juu shule ni ya kanisa na alishauri yeye mtoto aende shule ya kanisa. hapo tatizo ni mimi kivipi?
Mkuu sema tu ukweli,
2.3+0.8=3.1 mnaiweka mezani na kuipanglia?
 
Umesema ni last born!! Aah dada pole tu kwakweli. Hapo huna namna zaidi ya kushikilia tu usukani.
 
Back
Top Bottom