Ibara ya 100 ya Katiba ya JMT imewapa wabunge Uhuru wa kujadili Hoja na Mijadala mbalimbali bila kuingiliwa na Mhimili wala Mtu yeyote. Tusiwaingilie

Hayo unayasema wewe. Katiba ni sheria kuu ya nchi. Hakuna aliye juu ya katiba.
Hili suala Pascal Mayalla aliwahi kumuuliza mwendazake.
Akajibiwa kuwa kuna muhimili umejichimbia chini zaidi ndio unakusanya kodi na kusimamia matumizi yake.
Haiwezekani kodi ikusanywe,wabunge walipwe mamilioni ya wananchi halafu waende bungeni kuzungumza umbeya wa mitandaoni usiokuwa na uthibitisho wowote na kuacha kujadili bajeti ya nchi!Never!
Uhuru wanao "but not to that extent!(in magufuli's voice!)😊
 
Duh.
 
Ruksa kujadili hoja iliyoko bungeni sio iliyo nje ya bunge huo.ni umbeya io.kujadili hoja

Hoja iliyopo ni bajeti halafu mtu anaanza kujadili ooh kati ya Samia na Magufuli nani mrembo mwenye sura nzuri zaidi huo ujinga unapaswa ukemewe

Katiba inataka wajadili hoja sio vituko
 
Mwendazake alivyokuwa anaingilia bunge kinyume...milkuwa kimya!! FA ,Babu Tale,msukuma,kibajaji.. ..wachambue tipoti ys CAG,wasimlinganishe Madame na JPM
 
Hawajaingiliwa,wamekumbushwa na wameshauriwa.
Kumbuka Hayati Magufuli alisha tuambia hata kama Luna mihimili lakini tujue kwamba upo mhimili mmoja ambao umejichimbia zaidi na ndio unaowezesha mingine
 
Sasa si Bora wangekuwa wanajadili hizo hoja tatizo wanademka tu.
 
Kuna mawili, hujasoma shule au huna akili.
 
Hawajaingiliwa,wamekumbushwa na wameshauriwa.
Kumbuka Hayati Magufuli alisha tuambia hata kama Luna mihimili lakini tujue kwamba upo mhimili mmoja ambao umejichimbia zaidi na ndio unaowezesha mingine
Lack of education.
 

Rais ni sehemu ya Bunge.
 
Wanatakiwa kujadili hoja zilizowakilishw bungeni sio kujitungia hoja .Wajinga sana

Spika naye anawaangalia tu badala ya kuwashinikiza warudi kwenye hoja iliyo mbele yao.Sema tatizo na yeye mara nyingi anatoka nje ya hoja.Mama Samia yuko sahihi.Kwenye devate yeyote hata zetu zile za sekondari za kata ukiongelea unatakiwa kujikita kwenye Motion au topic husika tu.Mibunge mizima mijinga inatoka nje ya topic halafu mtu anasema ohh inaingiliwa inatakiwa iwe huru kuongea chochote!!! Lile ni bunge

Spika awaambie wenzie wajikite kwenye mada au hoja iliyowakilishwa tu.Tusije siku ingine tukazingira bunge tukawazomea na kuwaambia watoke wote
 
Unaelewa maana ya uhuru wa kujadili?
 
Ni kweli hatuna haki ya kuwaingilia, ila tunayo haki Kikatiba ya kuwashauri au kutoa maoni yetu kwa ajili ya wao kuyafanyia kazi kama wataona kuwa yanafaa. Wapo Bungeni kwa ajili yetu, ni sisi tuliowatuma. Kwa hali hiyo, Rais naye pia bado anaendelea kuwa mwananchi wa kawaida wa JMT na mwenye haki hiyo hiyo ya kutoa maoni yake kama wewe na mimi tunavyoweza kufanya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…