Mbolabilika
JF-Expert Member
- Jul 30, 2019
- 2,128
- 2,867
Nakumbuka kipindi mvua zilipoanza TZ walikua wanatucheka kana kwamba ni uzembe wa serikali leo msiba umetokea kwao je serikali yao nayo haijielewi imeshindwa kuzuia majanga?
=====
Viongozi wa serikali ya Kenya wametangaza habari ya kuongezeka idadi ya wahanga wa mafuriko na maporomoko ya ardhi kuwa imefikia watu 60.
Awali Idara ya Kukabiliana na Majanga Yasiyotarajiwa nchini Kenya ilikuwa imetangaza kwamba idadi ya wahanga hao ni 37 pekee. Ijumaa iliyopita mvua zinazoendelea kunyesha nchini humo, mbali na kusababisha maafa katika eneo la Pokot Magharibi zilisababisha pia hasara kubwa kwenye miundombinu, kuharibu mashamba na makazi. Vyombo vya habari vimetangaza kwamba maporomoko ya ardhi katika eneo hilo yamesababisha kusombwa kwa daraja na kuharibiwa pia barabara na njia zinazounganisha maeneo mengine ya vijijini.
Eneo la Kaunti ya Pokot Magharibi nchini Kenya baada ya kukumbwa na maporomoko ya ardhi
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya, askari wa uokoaji kwa kushirikiana na jeshi la nchi hiyo, wanafanya juhudi za kufungua njia za mawasiliano katika eneo hilo la Pokot Magharibi, sambamba na kuwafikishia misaada ya kibinaadamu wahanga. Naye Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya sambamba na kutoa pole kwa familia za marehemu wa mkasa huo, amewahakikishia wahanga kwamba watapatiwa misaada yote ya lazima haraka iwezekanavyo.
=====
Viongozi wa serikali ya Kenya wametangaza habari ya kuongezeka idadi ya wahanga wa mafuriko na maporomoko ya ardhi kuwa imefikia watu 60.
Awali Idara ya Kukabiliana na Majanga Yasiyotarajiwa nchini Kenya ilikuwa imetangaza kwamba idadi ya wahanga hao ni 37 pekee. Ijumaa iliyopita mvua zinazoendelea kunyesha nchini humo, mbali na kusababisha maafa katika eneo la Pokot Magharibi zilisababisha pia hasara kubwa kwenye miundombinu, kuharibu mashamba na makazi. Vyombo vya habari vimetangaza kwamba maporomoko ya ardhi katika eneo hilo yamesababisha kusombwa kwa daraja na kuharibiwa pia barabara na njia zinazounganisha maeneo mengine ya vijijini.
Eneo la Kaunti ya Pokot Magharibi nchini Kenya baada ya kukumbwa na maporomoko ya ardhi
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya, askari wa uokoaji kwa kushirikiana na jeshi la nchi hiyo, wanafanya juhudi za kufungua njia za mawasiliano katika eneo hilo la Pokot Magharibi, sambamba na kuwafikishia misaada ya kibinaadamu wahanga. Naye Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya sambamba na kutoa pole kwa familia za marehemu wa mkasa huo, amewahakikishia wahanga kwamba watapatiwa misaada yote ya lazima haraka iwezekanavyo.