Idara ya uhamiaji yatoa ufafanuzi dhidi ya wachezaji wa kigeni Singida Black Stars, wote ni raia wa Tanzania kwa Tajnisi

Safi kabisa.
 
Mbona hivyo vifungu hawaviweki hapa ili tusome, tujiridhishe na sisi
 
1. Kwa kuwa Sheria hiyo ya Uraia inatamka Wazi kwamba kabla Raia wa Kigeni (Mwombaji wa uraia) hajapatiwa Uraia wa Tanzania, Mwombaji huyo anatakiwa awe ameishi ndani ya nchi hii kwa muda wa angalau minimum miaka saba (7).
Je, hao Wachezaji wa Kigeni waliingia hapa nchini Tanzania lini ili kuishi hapa na ili kutimiza hiyo miaka saba inayotakiwa Kisheria? Lini hasa (tarehe ngapi) ilikuwa siku ya hao Wachezaji waliyotimiza kipindi Cha kuishi hiyo miaka saba wakiwa Wakaazi hapa Tanzania?

Ufafanuzi wa kina kabisa unahitajika kwenye Hoja hizi kwa sababu Uhamiaji ndiyo Taasisi yenye Mamlaka yote kabisa ya kutunza kumbukumbu zote kabisa za Wageni au Wasafiri wote wa Kimataifa ambao wanaoingia na kutoka hapa nchini.

2. Tumekuwa tukiona Matangazo kwenye Magazeti mbalimbali yanayowahusu Raia wa Kigeni ambao wenye nia ya Kuomba Uraia wa Tanzania, Matangazo hayo yamekuwa yakiutaarifu umma wa waTanzania kuwasilisha Mapingamizi yao (endapo kama wanayo) dhidi ya hao Watu wanaoomba Uraia wa Tanzania.
Uhamiaji wanapaswa watueleze, Je, lini hasa hao Wachezaji wa Kigeni waliopatiwa uraia wa Tanzania walitoa Matangazo hayo ili kuutaarifu umma juu ya hilo suala lao la kuomba uraia wa nchi hii? Je, Matangazo hayo yalitolewa lini na yalitolewa kwenye Magazeti gani hasa ya hapa Tanzania?
 
Inawezekana wamepewa kwasababu ya vipaji vyao,acha watusaidie nashno timu maana sisi wenyewe hatujiwezi . Mbumbumbu na wao hawataki kupitwa na huu upepoView attachment 3211254
Hii nchi inaendeshwa kinyumenyume au mandondocha.... Uraia anaomba na raia mwenye uraia wa nchi nyingine yeye binafsi siyo mwajiri wake.
Simba wanaweza tu kuwaombea vibali vya kuishi au exemption lakini sio kuwaombea uraia!.
Huu ni mtihani mwingine kwa jeshi la uhamiaji kama kweli wana weredi.
 
wanachojua ni kubania passport tu
 
Waziri aliyetoa uraia huo amevunja sheria na anatakiwa afunguliwe mashitaka na kuwajibishwa. Sheria ya uraia ya Tanzania sura ya 357 kifungu cha tisa kinasema kuwa Mtu akiomba uraia, atapewa iwapo anatimiza mwatakwa ya Second Schedule.




Halafu Second Schedule inatamka kwamba mwombaji awe ameishi Tanzania mfululizo kwa miezi 12 kabla ya kutuma maombi, na kabla ya miezi hiyo 12 awe ameishi Tanzania mfululizo kwa miaka 7.


 
Nimeona wachezaji wa Singida Sijajua kama ni United au Big Stars. Wamecheza mpira vizuri mpaka wakapewa uraia.

Je hatuwezi mpa uraia Paul Kagame aje agombee Urais Tanzania? Nimewaza tu. Kama nimemuudhi mtu samahani.wala sikuwa na nia mbaya nimewaza tu kwa sauti.

Nimemsikiliza katika hotuba zake na hii ya mwisho hapa... Eeeeeh nikasema hapa kidume yupo ngangari. Nikakumbuka hotuba za Mkapa miaka hiyo... Mi nafikiri kwa maendeleo ya Taifa letu aje Kagame agombee Urais. Halafu Lissu awe Waziri Mkuu.

Sijui kama nimekosea hapo. Wala msichukulie personal.na moderators naamini sijavunja kanuni.kama ipo muandike kabla hamjafuta uzi. Maana kwa sasa JF naona kama inapendekeza sana tuwe tunasifu na kuabudu.

Haya mwisho namalizia salamu kwa watu wawili. Mama Mikumi tena na Mzee (Wasira) mikumi na tano tena. Tutafika lakini...tukiwa hoiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
 
Rwanda ni katika Nchi masikini Africa, hawaja tofauti ana sana na Somalia gdp per capita, Kigali imejaa slums na masikini, kuna Vijumba vya udongo kibao,
 
Hafai ni dikteta mashuhuri huyo Afrika mashariki na kati
 
Mkuu with all due respect huwez kuchanganya watu wanaojua kufikiri kuweka mipango na watu wanaojiendeaendea tu.Kagame is too big sana kwetu.NAPENDEKEZA TUPEWE EVARISTE NDAYISHIMIYE anatufaa sana
 
Pk Siyo cheap kiasi hicho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…