Idara ya Usalama wa Taifa ipewe Mamlaka zaidi ili kuinusuru Nchi

Mimi siko huko mkuu, ila nilichokiandika ndicho.
 
Mimi siko huko mkuu, ila nilichokiandika ndicho.

Hivi unaweza kuwajua Wachawi kama na siyo mmoja au miongoni mwao? Mkuu nimeshaanza kukuogopa sasa na utanifanya nikae mbali na Wewe humu JF kwani nasikia nyie ( wana TISS au Eaglewing House ) ndiyo wenye nchi halafu hamshindwi jambo kama mkikivalia ' njuga '. Hongera kwa kuwa huko na bila shaka huwa unaonana sana na hawa wenzako ' Kimajukumu ' akina Mussolin5 na Evelyn Salt. Nawatakieni tu majukumu mema katika kutusaidia kutulindia usalama wa ndani na wa nje ili nchi yetu ibaki kuwa salama.
 
Safi sana ni uchambuz makin na wenye kujitosheleza kabisa
 
Ipewe meno zaidi ya sasa?Mbona sikuelewi mkuu?Hao ndio wanakuamulia Leo uishi vipi,wewe unasema wapewe meno?
 
Ukisikia yallalah fahamu jiwe limemgusa mwenyewe.nafuatilia tu huu uzi kwa miaka 4 kuna mengi nayapata.
Endeleeni kutujuza mnaojua.

Tueleze Ofisa vip Mkuu naona umekuja kivingine, jambo
 
Acha kumtisha Jamaa yeye ni Mlipa Kodi Hao TISS wanalipwa Kupitia kodi zetu kwanini asihoji? Mpaka imetungiwa Act 1996 ina maana Ni Taasisi inayotambulika kisheria sasa kwanini mtu asihoji?
 
TISS ina uzoefu wa zaidi ya miaka 50 katika shughuli zake wewe kijana wa juzi umetoka kuangalia series za "kijasusi" unakuja hapa unatema pumba unazoita ushauri

Pathetic
Mkuu mbona una mshambulia Mleta mata hata kama TISS iwe na miaka 100 je Tangu inaanza mpaka leo DG ni yule Yule kwanini Hubadilishwa? Jamaa ameshauri poa Sana kwa Uzi kwa kwanza apo.
 
Hivi si tuliambiwa waliovamia clouds ni kikosi maalum toka tiss? Aliyemtolea Nape bastola so walisema sio police? Kama sio polisi ni nani basi maana angekua RAIA Wa kawaida police wangeondoka nae...
 
Jamani TISS bado inafanya kazi hata ambazo hukuzitarajia, serikali hii ni kubwa. TISS nawapongeza, sana ila wajipange vyema kuwakamata hao wa ESCROW NA ACACIA BULYANG'HULU NA BARRICK COOPORATION.

Otherwise nawapa a GO AHEAD makanda hawa watiifu wa idara hii kwa kuitetea nchi na serikali, jamani wanafanya kazi kwa kiapo kikali kuliko hata cha Rais mwenyewe. I salute.

TISS, ur hero kiintelijensia.
 
tiss ingependeza kuwa taasisi huru yenye mamlaka ya kuchunguza na kufikisha mahakamani bila kuingiliwa..
lakini suala la kuingiliwa kisisasa na kuundwa kwake...imeinyima uwanja mpana wa kudeal na matishio ya kiusalama ktk nyanja zote za kitaifa...
ndio maana unakuta makashfa ya upigaji deal kubwa kubwa zenye kuyumbisha uchumi wa kitaifa imekuwa kawaida tuu kutokea.... kiasi masuala hayo yanaibuliwa na wapinzani kisha serikali ndio inayabeba kitu ambacho ni fedhea kwa tiss...
ila sijajua wao tiss wanawajibika wapi na kwa nani wanapokosea ktk uwajibikaji wao dhidi ya masuala ya kitaifa...??...
 
 
.jpg[/IMG]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…