Idara za Uokoaji zinalenga nini kutangaza Ajali za Uongo kwa kisingizio cha Mazoezi?

Idara za Uokoaji zinalenga nini kutangaza Ajali za Uongo kwa kisingizio cha Mazoezi?

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Ndugu zangu, binfasi natambua na kuheshimu kabisa hili suala la kufanya Mazoezi ya Utayari kwa sababu lina manufaa lakini bado napata shida sababu za kutangaza matukio hayo kwenye Vyombo vya Habari tena kwa kutaja idadi ya waathirika, aina ya Chombo kilichopata ajali na eneo.

Hivi hawa watu hawaoni kuwa taarifa hizo zimekuwa zikizua taharuki bila sababu za msingi kwa wananchi hasa wenye ndugu na jamaa wanaokuwa safarini? pamoja licha ya lengo zuri la mazoezi hayo lakini sioni sababu ya kutangazia umma kuwa kuna ajali.

Hizi idara za Uokoaji na Mamlaka husika zifanye Mazoezi yao kama zinavyotakiwa na Sheria lakini watoe Taarifa zinazohusu Zoezi hilo mapema na sio Kutangaza Ajali na kisha kukanusha baada ya muda wakati wanakuwa wameshasababisha usumbufu kwa Wananchi.

Ni hayo.
1677156569592.png
 
Kwenye ajali za uhalisia yanashika viuno na kushangaa wavuvi wakiokoa
 
Za ukweli hawaoki Ila za mchongo ndo balaa
 
Wwnachokitafuta Watakipata Tu, Huu Uchuro Umeshika Kasi Mno Sasa Hivi
 
Unaambiwa ajali haina kinga, operesheni hizo zinalenga kuwaweka kuwa tayari wakati wowote kuokoa ikitokea janga la ghafla. Kama wakiambiwa kuna ndege imeanguka sehemu halafu wakaanza kujivutavuta na kuchelewa kufika eneo la tukio watakuta kuna madhara makubwa yametokea, kumbe wangewahi fasta wangepunguza au kuzuwia maafa makubwa. Lengo kubwa ni kuwa tayari muda wowote.
 
Maigizo wanayamudu vizuri tu. Litokee tukio halisi sasa!! Unakutana na madudu mwanzo mwisho.
 
Back
Top Bottom