Idea yangu kuhusu ufugaji wa mbuzi bila kuchunga (Bandani/Zero grazing)

Idea yangu kuhusu ufugaji wa mbuzi bila kuchunga (Bandani/Zero grazing)

Masamila

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2014
Posts
6,490
Reaction score
7,422
Nimefanya karesearch kangu private kadogo na yafuatayo ni mawazo yangu kuhusu ufugaji wa mbuzi bila kuchungwa.

Nitatumia case ya mbuzi 110 hawa nitawaterm kama "mbuzi wazalishaji" au "parent stock" ambapo miongoni mwao madume ni 10 na majike ni 100.

Nukta ya kwanza; Mbuzi jike (mbegu specific) huzaa watoto wa nne kwa mwaka katika mikupuo miwili, hivyo kwa mwaka hao "Mbuzi wazalishaji" wanazalisha vitoto mia nne(100*4=400) kila mwaka.

Nukta ya pili: naonelea kuwa itafaa kuwachinja/kuuza mbuzi hao mia nne wanaozalishwa kila mwaka punde tu watapo fikisha umri wa miezi nane kwani baada ya umri huo growth rate inapungua kwa kiasi kikubwa. Katika umri huo wa miezi nane wanakuwa na uzito wa kilo 15 na thamani yake huwa ni shilingi elfu sabini( TSH 70,000)

Nukta ya tatu: Ulaji wa mbuzi hao tokea siku ya kwanza yaani kuzaliwa hadi umri wa miezi nane ni kilo sitini (60 KGS) (ulaji utakuwa chini ya hapo, hiyo ni maximum value). Hivyo watakula tani ishirini na nne (24 MT)

Nukta ya nne: 'Mbuzi wazalishaji' kwa idadi hiyo kwa mwaka hula chakula chenye uzito wa tani ishirini (20 MT)

Nukta ya tano: Bei ya chakula kama nikichanganya kwa nguvu zangu mwenyewe inaweza kuwa ni shilingi laki tano kwa tani(NB: sijalifanyia utafiti kuhusiana na bei ya mchaganyiko wa chakula cha mbuzi ila nimerefer chakula cha kuku kama mfugaji atanunua mwenye mchanganyiko halafu akachanganya mwenyewe)

Hitimisho: Faida yake itakokotolewa hivi ; Thamani ya Mauzo ya mbuzi waliozalishwa kutoa (gharama za ulaji wa 'mbuzi wazalishaji' + gharama za ulaji wa 'mbuzi waliozalishwa') ((70,000*400) minus (500,000*44(tons)= 28,000,000-22,000,0000=6,000,000

Faida kwa mwaka ni TSH 6,000,000

Nimalizie kwa kusema kuwa Binadamu tumetofautiana kimawazo hivyo nawe msomaji unao uwezo wa kuchangia mawazo yako kuboresha idea yangu au kujazia idea inapoacha ombwe ili mwisho wa siku tufaidike wote.
 
Kuna uwezekano wa kushusha hizo gharama za ulishaji ili faida iwe na tija.. Kuna kitu wanaita "azolla animal feed".. kuna nyuzi kadhaa humu kuhusu azolla, em jaribu kupitia. Pia inawezekana kuzalisha majani yanayokomaa ndani ya siku chache, kama wiki tu kwa mfumo wa hydroponic, ambayo ni cheap
 
Mkuu mawazo ni mazuri saana, ila kwenye huo mchanganua kuna garama za madawa na utaalam, pia na swala la ulinzi, kunkuwaga na wizi saana hususani kukaribia kipindi cha sikukuu,jamaa wakiona mbuzi mia wakichukua hata 50 tu tayari malengo yao wanakuwa wamesayafikia... ukiwa serious yes unaweza pata faida ila unatakiwa ujipange kisawasawa..
 
Kuna uwezekano wa kushusha hizo gharama za ulishaji ili faida iwe na tija.. Kuna kitu wanaita "azolla animal feed".. kuna nyuzi kadhaa humu kuhusu azolla, em jaribu kupitia. Pia inawezekana kuzalisha majani yanayokomaa ndani ya siku chache, kama wiki tu kwa mfumo wa hydroponic, ambayo ni cheap


Hapo gharama za kuestablish hiyo Hydroponics na azolla systems ni expensive kweli kweli, kwa nini kusiundwe au kubuniwe namna flani ya kuprocess Feed kwa kununua malighafi ambazo ni agricultural produce abundant nchini let say mahindi, maharage e.t.c

Maanake hapo, kulay infrastructure ya kuzalisha hydroponics , mabwawa ya kuzalisha azolla ni ghali kweli kweli ongezea na nguvu kazi itayohitajika hapo. Which means unaongeza ukubwa wa mtaji wa kuanzishia biashara na kumbuka kuna gharama za kujenga warehouse, mabanda makubwa sababu ya idadi ya kutosha ya kuleta significant profit na mambo mengine mengine
 
Mkuu mawazo ni mazuri saana, ila kwenye huo mchanganua kuna garama za madawa na utaalam, pia na swala la ulinzi, kunkuwaga na wizi saana hususani kukaribia kipindi cha sikukuu,jamaa wakiona mbuzi mia wakichukua hata 50 tu tayari malengo yao wanakuwa wamesayafikia... ukiwa serious yes unaweza pata faida ila unatakiwa ujipange kisawasawa..


Kiukweli Project hii kwa kuonekana tu inahitaji mtaji mkubwa, and let say mtu akaplan kuzalisha mbuzi kama 5000 hivi basi gharama za ulinzi,madawa na utaalamu hazina athari. Ila kwa mradi wa kuzalisha mbuzi 500 hivi, shida kweli ipo
 
Kiukweli Project hii kwa kuonekana tu inahitaji mtaji mkubwa, and let say mtu akaplan kuzalisha mbuzi kama 5000 hivi basi gharama za ulinzi,madawa na utaalamu hazina athari. Ila kwa mradi wa kuzalisha mbuzi 500 hivi, shida kweli ipo
Kwa uzoefu sio kubwa kihivyo, itakuwa kubwa kama hujajiandaa,,tambua eneo la kufugia/kuotesha malisho/miundombinu/maji/na Mbuzi wenyewe/kwa njia rahisi..kama unaeneo kubwa kipindi cha masika unaweza otesha majani (hii inategemea na eneo)kabla ya masika kuisha unaweza vuna majani mara mbili na kuyahifadhi...azola ni njia rahisi kwani ukichanganya azola na pumba hususani kwa mbuzi wazazi na wenye mimba itakupa matokeo mazuri......
 
Kwa uzoefu sio kubwa kihivyo, itakuwa kubwa kama hujajiandaa,,tambua eneo la kufugia/kuotesha malisho/miundombinu/maji/na Mbuzi wenyewe/kwa njia rahisi..kama unaeneo kubwa kipindi cha masika unaweza otesha majani (hii inategemea na eneo)kabla ya masika kuisha unaweza vuna majani mara mbili na kuyahifadhi...azola ni njia rahisi kwani ukichanganya azola na pumba hususani kwa mbuzi wazazi na wenye mimba itakupa matokeo mazuri......


Ni ghali mkuu, cheaper ndio labda tuseme mahali pa kuwaweka hao mbuzi ujengee mabanzi.
 
Idea nzuri mkuu,me pia mfugaji ila yuko mchungaji anayechunga,sijajua hiko chakula unachozungumzia ni kipi


Hapo sijafukua, ila nimeassume kama Chakula hicho cha mbuzi mchanganyiko wake utakuwa na thamani sawa na thamani ya chakula cha kuku wa kisasa.
 
Kuna uwezekano wa kushusha hizo gharama za ulishaji ili faida iwe na tija.. Kuna kitu wanaita "azolla animal feed".. kuna nyuzi kadhaa humu kuhusu azolla, em jaribu kupitia. Pia inawezekana kuzalisha majani yanayokomaa ndani ya siku chache, kama wiki tu kwa mfumo wa hydroponic, ambayo ni cheap
kaka naomba nisaidie kama unajua gharama za aluminium tray kwa ajili ya hydroponics,pia bei ya mbegu za azolla!
 
Project nzuri ya Mbuzi ni Mbuzi wa maziwa Utauza sana watoto na pia maziwa utauza au unaweza anza kuprocess Yogurt. Maziwa ya mbuzi ni mazuri kwa Yogurt.


Heshima yako mkuu,

Kiukweli mkuu sinaga imani sana na maziwa sababu ni kama naonaga ni comodity ya watu wa kipato cha juu hivi, maana hata watumishi wa umma ambao ndio tuseme ndio middle class hapa nchini consumption yao ya maziwa unakuta familia nzima kwa siku inanunua lita moja au wakijitahidi lita mbili. Maziwa kiukweli nimeona kama yalikuwa yana soko kubwa kipindi cha JK na si hivi sasa. Ila kumuuza mbuzi kama mbuzi ndio naona inamatter sana, sababu wako traded sana na kuna minada, machinjio, mabucha n.k
 
kwanza nikupongeze maana unawazo ambalo lipo kwenye orodha ya mawazo yangu sikunyingi na linatija kubwa sana ila kibiashara lazima ujue wahitaji ni nani na soko ni la uhakika katika mazingira yako au nje ya hapo .

Mambo ya kukumbuka ni
  1. banda zuri ambalo litakuwa na uwezo wa kupokea mbuzi 110 then ambalo litakuwa na uwezo wa kupokea ongezeko la watoto hao maana 100 mara nne si mbuzi wadogo kabisa ni idadi kubwa
  2. pia lazima ujifunze kuhusu mbuzi kwa kina na utumie muda wako mwingi ukiwa na mbuzi ili kulinda wale wanaozaliwa wasife maana watoto wengi 100 usipokuwa nao makini watakufa taratibu mpaka utakuta wamebaki 60
  3. weka gharama za watunzaji, gharama za madawa na chanjo kwa mbuzi wote pamoja na watoto itakapo bidi, gharama za ujenzi wa banda, gharama za mtaalamu wa mifugo.
  4. malisho jitahidi kupata eneo lililopo nje kidogo na makazi ya watu ambalo utanunua kwa bei nzuri na utajipatia malisho ya bure ya nyasi, ziada utanunua kutoka sehemu mbali mbali na itakuwa ni pumba, mashudu, na madini mbali mbali hasa ya calcium (hela yake kumbuka pia na gharama ya kusafirisha)
  5. Hitimisho usipende kuwafugia kwenye makazi ya watu maana dharama ya kuwaendesha itakuwa kubwa zaidi wakati sie ni money oriented
 
kwanza nikupongeze maana unawazo ambalo lipo kwenye orodha ya mawazo yangu sikunyingi na linatija kubwa sana ila kibiashara lazima ujue wahitaji ni nani na soko ni la uhakika katika mazingira yako au nje ya hapo .

Mambo ya kukumbuka ni
  1. banda zuri ambalo litakuwa na uwezo wa kupokea mbuzi 110 then ambalo litakuwa na uwezo wa kupokea ongezeko la watoto hao maana 100 mara nne si mbuzi wadogo kabisa ni idadi kubwa
  2. pia lazima ujifunze kuhusu mbuzi kwa kina na utumie muda wako mwingi ukiwa na mbuzi ili kulinda wale wanaozaliwa wasife maana watoto wengi 100 usipokuwa nao makini watakufa taratibu mpaka utakuta wamebaki 60
  3. weka gharama za watunzaji, gharama za madawa na chanjo kwa mbuzi wote pamoja na watoto itakapo bidi, gharama za ujenzi wa banda, gharama za mtaalamu wa mifugo.
  4. malisho jitahidi kupata eneo lililopo nje kidogo na makazi ya watu ambalo utanunua kwa bei nzuri na utajipatia malisho ya bure ya nyasi, ziada utanunua kutoka sehemu mbali mbali na itakuwa ni pumba, mashudu, na madini mbali mbali hasa ya calcium (hela yake kumbuka pia na gharama ya kusafirisha)
  5. Hitimisho usipende kuwafugia kwenye makazi ya watu maana dharama ya kuwaendesha itakuwa kubwa zaidi wakati sie ni money oriented


Namba 2 hapo, ni kweli magonjwa yanayoshambulia mbuzi na mbuzi wenyewe, sijajua kwa nini mbuzi huwa wako vulnerable vile kwenye magonjwa.

Malisho hasa nyasi ni changamoto kwa idadi kubwa kama hiyo, na ina maana kuwa katika ufugaji kama huu inahitajika eneo kubwa la mabanda na eneo kubwa zaidi vile vile kwa ajili ya malisho ya nyasi.
 
Namba 2 hapo, ni kweli magonjwa yanayoshambulia mbuzi na mbuzi wenyewe, sijajua kwa nini mbuzi huwa wako vulnerable vile kwenye magonjwa.

Malisho hasa nyasi ni changamoto kwa idadi kubwa kama hiyo, na ina maana kuwa katika ufugaji kama huu inahitajika eneo kubwa la mabanda na eneo kubwa zaidi vile vile kwa ajili ya malisho ya nyasi.
kweli ila kwa malisho ya nje itakuwa nafuu sana
 
Kuna magonjwa matatu ya virusi ambayo huwashambulia mbuzi sana na hivyo Kupunguza uzalishaji na wewe kama mfugaji utahitaji kuwakinga mbuzi wako kwa kuwapa chanjo dhidi ya magonjwa hayo ambayo ni;

1. Pesti des petis ruminants (PPR)

Mbuzi hupewa akiwa na miezi 6+ na chanjo hii huwa ni ya maisha hakuna haja ya kurudia kuchanja tena

2. Caprine pox

Hupewa chanjo hii wakiwa na umri na miezi 6+ na chanjo hii hudumu kwa miaka 2 tu baada ya hapo utatakiwa kurudia tena

3. Contagious caprine pleuro pneumonia

Huchanjwa wakiwa na miezi 6+ na chanjo hii hurudiwa baada ya mwaka mmoja....

Hitimisho:

Kila baada ya miezi mitatu ni muhimu kuwapa dawa ya minyoo (Albendazole) hapa mbuzi watakuwa na afya na mwonekano mzuri

Kwa huduma hizi za chanjo tusisite kutafutana kwa wakazi wanaokaa dar na pwani tu. Karibuni sana
 
Back
Top Bottom