IDF Jeshi bora kabisa duniani na MOSSAD idara bora zaidi ya ujasusi duniani!

Nelson...
Kitu gani kimekufanya wewe uhisi mimi nitafurahia kuuliwa kwa Wayahudi?

Nilikuwa na rafiki yangu tunasoma darasa moja St. Joseph's Canvent School.
Siku alipokuja kujiunga na darasa letu mwalimu alimleta ninapokaa mimi akamweka pembeni yangu na tukawa marafiki sana.

Jina lake akiitwa Israel na baba yake ndiye alikuwa Balozi wa Israel Tanzania.
Bahati mbaya sana sikumbuki jina la pili la Israel.

Six Day War 1967 ilipokuwa inaanza kila siku asubuhi Israel akinipa taarifa za jinsi majeshi ya Israel yalivyokuwa yanasonga mbele na kuyasambaratisha majeshi ya Misri, Syria, Iraq na Jordan.

Nilikuwa naumia sana.
Israel alinieleza mengi na kuwa yeye akirudi kwao ataingia jeshini nk. nk.

Nakuwekea picha hapo chini tuliyopiga tukiwa shule:



Kulia waliochutama: Edward Anthony Makwaia, Salma Bhatia, Asya Kharusi, Razia Bhatia, Iddi Mvule, David Gabba, Waliosimama kulia: Mwandishi, Shayo, Maximillian Mafuru. Kulia waliosimama: Gulamabbas Jivraj, Israel, Charles Mesquita​
 
Ungefika pia Eliat na ungefika pia Sham al Sheikh iliyokua chini y IDF na ungetembelea kumbukumbu za vita vya yomm kippur katika maktaba za Tel aviv na Jerusalem.Hapo ungekua na simulizi ya kitaaluma zaidi na ungesoma vitabu zaidi ya Road to Ramadan.Vipo vitabu vingi tu kama Valley af tears na vinginevyo sawa mzee wangu
 
Jinsi unavyodadafua hiyo vita kwa kuegemea pande flani na sio mchambuzi huru mzee wangu.
 
Nelson...
Kweli lakini bahati mbaya sijafika Israel.
Kusoma wala usipate tabu.

Mimi nimeandika vitabu vinafika 10.

Kitabu changu cha mwisho 2023 hicho hapo chini kitabu changu cha kwanza kuchapwa na Amazon.

2021 nilikuwa na kingine angalia hapo chini.
Naamini hata wewe nimekustaajabisha maisha yangu ni vitabu.

Sawa kaka.


 
Nelson...
Kuhusu Vietnam.
Tuache habari za vitabu.

Unajuaje kuwa sijakisoma?
Vitabu ni maisha yangu.

Nimesoma mauaji ya Mai Lai nina umri wa miaka 15.
Nimekuwa mwanachama wa Library ya Congress Washington katika 1980s.

Tanzania nzima tulikuwa watu wawili tu tulipewa heshima hii na Mkuregenzi wa USIS.

Tuache habari za vitabu.


Library of Congress Washington DC​
 
Jinsi unavyodadafua hiyo vita kwa kuegemea pande flani na sio mchambuzi huru mzee wangu.
Nelson,
Nimekujibu kuwa ikiwa unaniona mimi siko huru au naegemea upande fulani sawa siwezi kuingilia fikra zako.

Lakini mimi nimekuweka ushahidi wa hali ilivyokuwa na Nuclear Alert waliyotoa Marekani.

Wewe unasema Nuclear Alert walitoa Warusi.
Si kweli.

Unaandika bila ya ithibati.
Unatakiwa uwe na ushahidi wa kile unachoeleza.

Msomi haandika bila utafiti.
Umeshindwa kunipa source ya maandishi yako.

''The conflict soon became a proxy war between Egypt’s principal backer, the Soviet Union, and Israel’s patron, the United States. Things became so dire that U.S. global forces went to a Defcon 3 alert, the highest state of peacetime readiness, reflecting the risk of nuclear confrontation with the Soviets.''

(The Arab-Israeli war 50 years ago brought us close to nuclear Armageddon)​


By Gordon F. Sander
October 10, 2023 at 2:28 p.m. EDT
Washington Post


Zawadi ya vitabu kutoka kwa rafiki yangu anaetambua mapenzi yangu katika kusoma​
 
Hujanistaabisha na kitabu chako hicho mzee wangu mpendwa ila nimeona umeweka picha ya mbantu au chotara wa kibantu aliyeathiriwa na Arab-nazation colonialism.Mm nadhani ungeelezea pia mashujaa wa kibantu waliotetea tamaduni na imani zetu za kibantu.Na sio kutukuza imani za wageni kutoka mbali.
 
Bado nakuona kama mchambuzi unaegemea upande mmoja na sio mchambuzi huru mzee wangu mpendwa
 
Kuna aina ya vitabu unavikwepa kuvisoma mzee wangu.Nadhani hiyo ni kwa sababu umekua brain washed na Arab-nazation.Rejea tu makala zako za maisha binafsi,mitazamo yako na imani yako binafsi utadhibitisha maneno yangu mzee wangu mpendwa
 
Jonathan alikuwa anaenda frontline sababu alikuwa mwanajeshi na kamanda ila mpika mipango alikuwa Benjamini na wenzie pale head quater Jerusalem ya wizara ya ulinzi ya Israel!!
Kuna watu wanaongea utafikiri washafilka na kuishi huko

Wewe umesema
 
Wewe itaendelea kuwa ya mchezo kwa sababu ya ma ccm
 
Nelson...
Hujasoma kitabu unaeleza dhana zako.

Hupendi kusoma Waarabu.
Unapenda kusoma Wabantu.

Unazungumza mashujaa wa Kibantu na imani za Kibantu.

Mashujaa Wabantu nimewaandika wengi ndani ya kitabu cha Abdul Sykes.

Tatizo litakuja kwenye imani za Kibantu.

Nifahamishe imani za Kibantu ni zipi?

Kwa makusudi nimekwepa kuzungumzia kuhusu ubaguzi.

Jina lako Nelson na wewe si Muingereza.
 
Kuna aina ya vitabu unavikwepa kuvisoma mzee wangu.Nadhani hiyo ni kwa sababu umekua brain washed na Arab-nazation.Rejea tu makala zako za maisha binafsi,mitazamo yako na imani yako binafsi utadhibitisha maneno yangu mzee wangu mpendwa
Nelson...
Unajuaje nakwepa vitabu?

Hii Arab-nazation ni nini naona imekukaa.

Au ni tatizo la Kiingereza?
Unakusudia "ization?"

Mimi Muislam na Uislam ndiyo maisha yangu haya hayaitaji uthibitisho.

Halikadhalika nimeathirika na utamaduni wa Pwani na Magharibi kama wengine wengi tulivyo.

Naamini wewe ni Mkristo na ni mtu kutoka Bara na una utamaduni wako kutoka kwenu.

Sioni tatizo liko wapi.

Ila "brain wash," sielewi umekusudia nini khasa?
 
Kuna watu wanaongea utafikiri washafilka na kuishi huko

Wewe umesema
Oga...
Alitakiwa aeleze source ya hayo anayoandika.

Hivyo afanyavyo ni makosa kwa kuwa anatoa picha kuwa alikuwapo wakati hayo yanatokea.
 
Hili jina alinipa babu yangu mpendwa ambae nae ni muhanga kama wewe alifanyiwa brain washed na wakoloni wa kizungu ambao ni wajerumani na akaacha ubantu.Kama ambavyo wewe mzee wangu mpendwa ulivyofanyiwa brain washed na wakoloni wa kiarabu.
NB: Hakuna shujaa wa kibantu mwenye jina la kiarabu au kizungu.
Hakuna shujaa wa kibantu mwenye kufuatisha dini za wazungu na waarabu.
Hao sio mashujaa bali vibaraka waliokua brain washed ili kueneza tamaduni za kigeni na wakoloni kwa wabantu ili tupoteze alama zetu
 
Oga...
Alitakiwa aeleze source ya hayo anayoandika.

Hivyo afanyavyo ni makosa kwa kuwa anatoa picha kuwa alikuwapo wakati hayo yanatokea.
Mzee wangu mpendwa kwahiyo nikutajie majina ya sources zangu ndani ya IDF za wanajeshi waastaafu???
 
Mimi natokea himaya za wanyoro,wanyambo,waganda,wahima ,wahangaza,waha,warundi na wanyarwanda sijaathirika na tamaduni za kigeni kama mlivyokua watu wa pwani mpaka mkaukimbia ubantu na kujinasibisha na uarabu mzee wangu.
Hakuna mbantu mkristo au mbantu muislamu.Ukiona mbantu anajiita hivyo ni kwamba huyo ajitambui sababu amekataa dini zake za asili na tamaduni zake na kuingia ulimbukeni wa dini na tamaduni za kigeni.
NB: Yale ni makosa ya kiuandishi,nilikua namaanisha wewe mzee wangu mpendwa ni muathirika wa ukoloni wa wageni na umeshaupoteza ubantu wako kupitia arabs influence iliyowakumba babu zako wa kingoni hapo kariakoo.
Kwahiyo wewe ni mtumwa wa tamaduni za kigeni.
Kwa kua upo brain washed na tamaduni za kigeni basi ni sahii unaposema huoni tatizo liko wapi!!
 
Nelson,
Ahsante.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…