IDF Jeshi bora kabisa duniani na MOSSAD idara bora zaidi ya ujasusi duniani!

Nelson...
Katika kanuni za uandishi dots zinakuwa tatu tu...

Uandishi mfano wa huu epuka exclamation marks !!!.
 
Sawa mzee wangu mwandishi mbobefu nitalifanyia kazi na nitakuja kwako kuchukua vitabu vya kutosha.
Nelson...
Kwa nini uje kuchukua vitabu kwangu?
Jaribu Maktaba Kuu ya Taifa na British Council Library.

Nakuwekea hapo chini moja ya kipande kuhusu IDF na Hizbullah katika mhadhara niliotoa University of Zanzibar mwaka wa 2017.

Nimekichagua kipande hiki kwani kilipendeza sana hadhira yangu.
Hili nilielezwa mwisho wa mhadhara:

''Vita iliyokuja kumaliza kile kilichokuwa kimeaaminika na dunia kuwa Wayahudi hawawezi kushindwa katika vita, ni vita vya mwaka wa 2006 kati ya Hizbullah na Wayahudi.

Vita vilipoanza fikra za wengi katika nchi za Kiarabu zilirejea katika Vita Vya Siku Sita vya mwaka wa 1967 na wengi waliamini kuwa Hizbullah watamalizwa kwa muda mfupi kwa kusagwasagwa na Israel.

Hili halikutokea.

Vita vilipiganwa kwa siku 34 katika mwezi wa Julai na Agosti hadi pale Umoja wa Mataifa ilipoingia kati na kuweka makubaliano ya kuweka silaha chini na kumaliza vita.

Wayahudi kwa mara ya kwanza katika historia ya mapambano yao na Waarabu walionekana katika stesheni nyingi kubwa za televisheni duniani wakirudi Israel kutoka uwanja wa mapambano wameinamisha chini vichwa vyao.

Israel ilikuwa kwa mara ya kwanza imeonja kipigo katika vita. Hapakuwa na shamrashamra ziliyozoeleka za ushindi dhidi ya majeshi ya Kiarabu.

Hizbullah ilikuwa imevunja, ‘’myth,’’ ile fikra ya kuwa Wayahudi hawawezekani. Hassan Nasrallah kiongozi wa Hizbullah alikuwa akiuliza wakati wa vita, ‘’Wako wapi askari wa Kiyahudi mbona hatuwaoni katika uwanja wa vita?

Tunachoshuhudia ni ndege za Kiyahudi wakipiga mabomu nyumba za raia.’’

Baada ya vita, ilipofika wakati wa kubadilishana mateka Wayahudi walipata fadhaa zaidi pale walipokuwa wao wanapokea majeneza ya askari wao waliouliwa vitani na Hizbullah na wao wakiwaachia huru askari hai wa Hizbullah.''


Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Zanzibar katika mhadhara​
 
Mm Sizungumzii dini bali nazungumzia madhara ya ukoloni wa waarabu na wazungu mzee wangu.
Upo sahii mzee wangu
Nelson...
Una mapenzi na usomi.
Hili ni jambo jema sana.

Lakini umechagua kitu kinachotaka ujitolee kwa damu na jasho.
Unatakiwa usome sana na uwe msikivu kutafuta elimu kwa kusoma na kusikiliza.

Mimi najitolea kuwa mwalimu wako ukiwa utapenda.
Ukizungumza kuhusu imani hiyo ni dini.

Wala usitishike na kuzungumza kuhusu dini yako.
Ieleze ili ifahamike.

Mimi huwaeleza Wakristo kuwa endapo Muislam kakudhulumu kutokana na cheo chake huyo kenda kinyume na Qur'an.

Allah anawaeleza Waislam kuwa wasidhulumu wala wasikubali kudhulumiwa.

Hakuna ubaya kueleza mafunzo ya imani yako.
Wewe ni Mkristo na hakuna kosa kuwa Mkristo.

Wala hakuna Muislam ataekufanyia uadui kwa kuwa wewe ni Mkristo.
Nyerere Mkatoliki kapokelewa na Waislam na wakampa uongozi wa Tangnayika.

Historia hii ninaieleza hapa kila siku.
Ukijikataa utapata shida.

Mimi Muislam na kote ninakoalikwa kuzungumza wananijua hivyo.
 
Na lakwetu ni namba 6
 
Ona ng'ombe hii.
 
Huyu nelson ni amekaririshwa na hapendagi kusoma yeye ana ubishi wa vijiweni ukimpa hata authority akasome ,anakuuliza kwani imesemaje? Sasa mtu kama huyo huwezi kumuelimisha maana hakuna anachojua
 
Nata Mimi sio mkristo bali mimi ni muafrika mbantu nataka nisome na akili za wabantu waliokataa ubantu wao na kuukumbatia uarabuni nijue kiini cha fikra zao kipoje.
Na pia nataka nisome ule mpango wa waarabu na waislamu wa kuwafanya wayahudi kua watumwa wao umefikia wapi kwa sasa.
NB: Wewe ni msomi wa elimu ya wakoloni wa kizungu na kiarabu uliyeukataa ubantu na kuukumbatia uarabu nataka nisome vitabu vyako.
 
Huyu nelson ni amekaririshwa na hapendagi kusoma yeye ana ubishi wa vijiweni ukimpa hata authority akasome ,anakuuliza kwani imesemaje? Sasa mtu kama huyo huwezi kumuelimisha maana hakuna anachojua
Mkuu nimekuuliza maswali umeniletea story za wazungu wamarekani.
Nilikua najua umeenda Beirut na Jerusalem na ukawahoji wahusika,kumbe ripoti za wazungu ndio unazitegemea.
 
Nelson...
Hukupata kuwa Mkristo?
 
Huyu nelson ni amekaririshwa na hapendagi kusoma yeye ana ubishi wa vijiweni ukimpa hata authority akasome ,anakuuliza kwani imesemaje? Sasa mtu kama huyo huwezi kumuelimisha maana hakuna anachojua
Elimu ya kuwafanya Wayahudi na Wakurdi na Wayazidi kua watumwa wa waarabu hiyo mimi siafikiani nayo.
 
Nelson...
Hukupata kuwa Mkristo?
Dini ya wagiriki na walatini na waitaliano na jamii nyingine duniani zinazoamini katika msalaba.Dini hiyo sikubahatika kupata nafasi ya kua mfuasi.Ila nipo kwenye utafiti kuhusu Mungu wa wakrsto na nikimaliza hapo nitafanya utafiti pia kuhusu Mungu wa waislam.
 
Hii historia ni ya kuwabagua watu wa bara waliokataa ushawishi wa wakoloni wa kiarabu bara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…