If you can't beat them, join them: Naziona dalili za CCM kuja na wazo la Serikali ya mseto huko mbeleni

If you can't beat them, join them: Naziona dalili za CCM kuja na wazo la Serikali ya mseto huko mbeleni

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Upinzani nchi hii umekomaa na kuota mizizi kiasi kwamba ni vigumu kufuta upinzani hapa nchini na ndio maana Mwendazake alifeli vibaya katika adhma yake ya kutaka kuua upinzani(kafa yeye kaacha upinzani ukiwa imara kuliko jana).

Kwasababu CCM hawako tayari na pia hawawezi kushindana na upinzani (CHADEMA) katika uchaguzi ulio huru na wa haki, option pekee waliyobaki nayo ni kuwashirikisha wapinzani (hasa CHADEMA) katika kuunda serikali huko mbeleni .

Kinachoitwa maridhiano leo hii kesho kinaweza kuwa ni mwanzo wa kufikia makubaliaona ya kuwa na serikali ya mseto kupitia katiba mpya au mabadiliko madogo ya katiba tuliyonayo leo hii.

CCM kukaa na wapinzani sio kama wanapenda, bali wanatambua nguvu waliyonayo wapinzani na hapo ndipo ule msemo wa "if you can't beat them, join them" unapopata nafasi.

Hata kama kutakuwa au kuna shinikizo la Wahisani, shinikizo hilo ni matokeo ya nguvu waliyonayo wapinzani na si vinginevyo kwani huwezi weka shinikizo kama hilo pasipo kuwa na upinzani wenye nguvu.

All in all, pamoja na kutoaminiani kuliopa saaa katika mazungumzo yanayoendelea baina ya CHADEMA, CCM na serikali, naiona serikali ya mseto ikizaliwa huko mbeleni huku Mbowe na Mama Samia wakiingia katika historia ya Taifa letu.

Muda utahibitisha.
 
Bado CCM ni chama bora kabisa Tanzania ukilinganisha na vyama mbadala vilivyopo. Hakuna hata chenye dalili ya kuikaribia kwa sasa. Kinachofanyika ni kufanya reconciliation kwa sababu hii nchi ni ya watanzania wote, na raha ya mechi kuwe na uwanja sawa, CCM inataka ipige goli zake safiiii bila malalamiko kuwa wanacheza rafu.

Kuhusu CCM kuua vyama vya upinzani, CCM haina sababu ya kuua vyama vya upinzani, iviue halafu icheze na nani sasa ? Simba inakuwa ni Simba kwa sababu kuna yanga, mwanaume ni mwanaume kwa kuwa kuna mwanamke, na mwanga ni mwanga kwa kuwa kuna giza n.k. dhana ya chama A kuua chama B ni dhana fulani ya kitoto.
 
Kwa kiburi walichonacho viongozi wa CCM na hasa ukizingatia wanacomand dola (polisi na usalama wa Taifa) kamwe haiji kutokea labda tukipata katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi!
 
Bado CCM ni chama bora kabisa Tanzania ukilinganisha na vyama mbadala vilivyopo. Hakuna hata chenye dalili ya kuikaribia kwa sasa. Kinachofanyika ni kufanya reconciliation kwa sababu hii nchi ni ya watanzania wote, na raha ya mechi kuwe na uwanja sawa, CCM inataka ipige goli zake safiiii bila malalamiko kuwa wanacheza rafu.

Kuhusu CCM kuua vyama vya upinzani, CCM haina sababu ya kuua vyama vya upinzani, iviua halafu icheze na nani sasa ? Simba nakuwa na Simba kwa sababu kuna yanga, mwanaume ni mwanaume kwa kuwa kuna mwanamke, na mwanga ni mwanga kwa kuwa kuna giza n.k. dhana ya chama A kuua chama B ni dhana fulani ya kitoto.
Hizo porojo bila ya msaada wa polisi kuiba uchaguzi usingezitoa hapo

ccm hawashindi kwa sababu ya sera,no, ila kwa sababu ya kuiba uchaguzi
 
Mwendazake alifanikiwa kuua upinzani na angeendelea kuwa hai kwa miaka 10 mingine upinzani ungekuwa umekufa kabisa..

Kufa huwa ni mipango ya Mungu na sio kweli eti Kufa kwa JPM ulikuwa ushindi wa upinzani kana kwamba upinzani ndio ulipambana naye na kumdhidi nguvu mpaka kufa....HAPANA tuache uongo huu...

Upinzani wa Tanzania huwa unategemea huruma ya watawala ndio uweze kusurvive, sikuona strategy yeyote ya upinzani kupambana na JPM zaidi ya kutegemea msaada wa mabeberu ambao nawao hupima maslahi yao kwanza...
 
Bado CCM ni chama bora kabisa Tanzania ukilinganisha na vyama mbadala vilivyopo. Hakuna hata chenye dalili ya kuikaribia kwa sasa. Kinachofanyika ni kufanya reconciliation kwa sababu hii nchi ni ya watanzania wote, na raha ya mechi kuwe na uwanja sawa, CCM inataka ipige goli zake safiiii bila malalamiko kuwa wanacheza rafu.

Kuhusu CCM kuua vyama vya upinzani, CCM haina sababu ya kuua vyama vya upinzani, iviue halafu icheze na nani sasa ? Simba inakuwa ni Simba kwa sababu kuna yanga, mwanaume ni mwanaume kwa kuwa kuna mwanamke, na mwanga ni mwanga kwa kuwa kuna giza n.k. dhana ya chama A kuua chama B ni dhana fulani ya kitoto.
Utakua unawasema mkuu na wana awamu ya 5, kwamba walikua na hiyo dhana ya kitoto!
 
Unajua, itikadi za kisiasa hazina tofauti sana na za kidini.
Tofauti ni kwamba, kwenye siasa huwezi kuanzisha serikali nyngine ndani ya nchi moja.
Na kinachowaponza watu wengi ni tamaa ya madaraka na uchu wa mali za umma.

Ila, kama mtu una nafasi ya kuishauri serikali na ikafanyia kazi ushauri wako, hakuna haja ya kupambana hadi uwe kiongozi wa serikali. Kuna watu sio wanasiasa ila inapotokea machafuko au migogoro, wanaitwa kuwa wasuluhishi.
Si lazima kila mtu awe kiongozi wa serikali.

Kwenye dini tunashuhudia utitiri wa madhehebu mbalmbali kwasababu ndogondogo ambazo wakati mwingine zingetatuliwa kwa kujishusha tu; lakini mtu anatoka na kuanzisha dhehebu lake.

Laiti kama kungekuwa na serikali ndani ya serikali, basi hayo yangejitokeza hata kwenye siasa. Tungekuwa na serikali zisizo na idadi ndani ya nchi moja!
 
Serikali za mseto sio jambo geni Tanzania hii au Afrika..Kule zenji mpaka wakt huu ipo ndoa ya CCM na ACT iliyozaa serikali ya mseto..Issue ni kwamba je itatuvusha zaidi ya hapa tulipo? Je nani ktk ndoa hiyo atakuwa ME/KE? au ishu ni 'hata wale nao wale'
 
Bado yaan hata diwani yenyewe kupata ni ngumu sembuse serikali ya Mseto? Upinzani upi huo ambao mwisho wa siku woote wanakuwa ccm, wengine ccm B. Wengine wanaenda kuchukua ela ikulu yenyewe alafu wanakuja kupiga bit wafuasi wao wasitukane serikali,

1.Zito= ccm B
2.Mrema= ccm
3. Dr. Silaa ccm
4. Mdee and co. Covid 19= mamluki es ccm
5. Kitila= ccm
6. Mbowe =( mtu wa michongo) anapiga deal ccm e.g reffer uchauzi wa 2015 na lowassa. Juzi tuu hapa kaenda ikulu kala pesa ya karne.
 
Upinzani nchi hii umekomaa na kuota mizizi kiasi kwamba ni vigumu kufuta upinzani hapa nchini na ndio maana Mwendazake alifeli vibaya katika adhima yake ya kutaka kuua upinzani(kafa yeye kaacha upinzani ukiwa imara kuliko jana)

Kwasababu CCM hawako tayari na pia hawawezi kushindana na upinzani (CHADEMA) katika uchaguzi ulio huru na wa haki, option pekee waliyobaki nayo ni kuwashirikisha wapinzani (hasa CHADEMA) katika kuunda serikali huko mbeleni .

Kinachoitwa maridhiano leo hii kesho kinaweza kuwa ni mwanzo wa kufikia makubaliaona ya kuwa na serikali ya mseto kupitia katiba mpya au mabadiliko madogo ya katiba tuliyonayo leo hii.

CCM kukaa na wapinzani sio kama wanapenda, bali wanatambua nguvu waliyonayo wapinzani na hapo ndipo ule msemo wa "if you can't beat them, join them" unapopata nafasi.


Hata kama kutakuwa au kuna shinikizo la wahisani, shinikizo hilo ni matokeo ya nguvu waliyonayo wapinzani na si vinginevyo kwani huwezi weka shinikizo kama hilo pasipo kuwa na upinzani wenye nguvu.

All in all, pamoja na kutoaminiani kuliopa saaa katika mazungumzo yanayoendelea baina ya CHADEMA, CCM na serikali, naiona serikali ya mseto ikizaliwa huko mbeleni huku Mbowe na Mama Samia wakiingia katika historia ya Taifa letu.

Muda utahibitisha.
Upinzani ni CHADEMA pekeee ? Mie nadhani kama hii imekalia kitoto kidogo, hizi levels ambazo wapinzani Tanganyika wanapitia kule visiwani tulikuwa na mijadala ya maridhiano na mseto kitambo kidogo!

Tena nadhani watanganyika wengi wakicheka jitihada zile na mawazo yale. Kiufupi nchi nyingi zilizokomaa kidemokrasia hakuna cha chama kimoja kuchukua kila kitu. Hii haina afya.
 
Mkuu
Hayo yatatokea
Lakini ni Baada ya KATIBA MPYA kupatikana
Wakati HUO hayo yakitokea mama hatokuwa Rais wa nchi HII
Na uchaguzi wa 2025 hautokuwepo Hadi KATIBA MPYA ipatikane KWANZA!!
TUSUBIRI
 
Back
Top Bottom