Ifahamu Biashara ya supu ya pweza

Ifahamu Biashara ya supu ya pweza

Habari zenu kama kichwa cha habari kinavosema naomba mnisaidie natamani sana kufanya hii biashara, Ila sielewi ni mtaji kiasi gani utatosha na pia ni vitu gani niweke ili biashara iwe nzuri
 
Habari zenu kama kichwa cha habari kinavosema naomba mnisaidie natamani sana kufanya hii biashara, Ila sielewi ni mtaji kiasi gani utatosha na pia ni vitu gani niweke ili biashara iwe nzuri
Upishi mzuri ndio kitu cha kwanza ,cha pili usafi
Pia usisahau kuweka kachori, kababu nk.

Ndimu na vitunguu maji pia lazima viwepo kuongeza ladha ya mchuzi.
 
images (11).jpeg
 
Naomba nijibu kadri mungu atakavyonijalia......mtaji ukitoa meza,jiko, karai, sahani ,vikombe , na vifaa vingine,basi mtaji ni mdogo tu, pweza wanauzwa kwa kilo ,kilo moja haizid buku kumi,inategemea na siku hiyo, so inategemea na kilo unayoitaka, kachori mtaji wake hauzid 10000, hapo toa mafuta na mkaa.

Kuhusu pilipili,kule kule zinauzwa uliza pilipili ya pweza,kuna babu anauza hiyo pilipili,na ndio maana unakuta maeneo mengi pilipili zinafanana kwa utamu. location nzuri has a ni sokoni au stend ya basi au kwenye mkusanyiko wa watu wengi. kuhusu mchuzi,unaponunua pweza kule feri,vuka upande wa pili wakati unatoka nje,utaona kunasehemu wanachemsha na kukaanga hao pweza,so wanachemsha kwanza kisha unapata mchuzi unaweka kwenye kidumu chako,kisha unamkaanga kwa gharama ndogo tu........pia kuna wengine wanaweka na samaki hapo hapo kwenye meza so integemea na maamuzi yako........

NB sijawahi kufanya hii baishara ila nilitaka kufanya ,hivyo nikafanya research kwanza kujua ABC zake.,......... ila kwa wenyewe wanasema inafaidaa, so Mimi hii biashara niaifahamu kwenye makaratasi,so ukichukua ushauli wangu,usije kunihumu huko baadaye..........tuendelee kuombea ndege yetu waiyachieeeee.
 
Habari JF,

Leo nimekutana na dogo mmoja nikaanza kupiga naye stori anitafutie mfanyakazi wa kutembeza biashara.Ila katika mazungumzo ya biashara ambayo niliplan dogo akanikatisha tamaa akanishauri nifungue biashara ya kuuza supu ya pweza na pweza akaanza kunipa na darasa la kunishawishi, ila mimi naona kama anataka aniingize cha kike vile?

Hebu wataalamu wa hizi biashara za pweza na supu ya pweza hebu kaeni humu mara moja mtupe uzoefu wenu maana nasikia watu wanapiga sana supu mjini hapa.
 
Back
Top Bottom