IGP Simon Sirro, kwanini askari polisi wanatumwa field na silaha nzito wamevaa kiraia? Kwanini unatuma askari na silaha nyingi tukio dogo la kiraia?

IGP Simon Sirro, kwanini askari polisi wanatumwa field na silaha nzito wamevaa kiraia? Kwanini unatuma askari na silaha nyingi tukio dogo la kiraia?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Ni jambo ambalo linazidi kuenea Tanzania. Mara nyingi unakuta askari polisi wanatumwa kwenye tukio linalohitaji silaha (japo ni machache Tanzania) huku wakiwa wamesheheni silaha na bado wamevaa kiraia. Kwa nini wanafanya hivyo? Je inaruhusiwa kwa askari polisi aliye kwenye response unit kwenda akiwa na silaha kamili za kuingia filed lakini akawa amevaa kiraia?

Nimeangalia askari walioenda kumkamata huyu mama wa Iringa alietoroka kambi ya Corona, na karibu askari wote walioenda walikuwa wamesheheni silaha lakini wamevaa kiraia.

Halafu, hili tukio si la ujambazi. Kwa nini Polisi wapeleke kikosi chenye uzito wa silaha kiasi hiki kumkamata mwanamke mmoja aliekimbia kambi ya Corona? Hivi polisi wetu wanawashwa kubeba silaha na kuzitumia?

Nchi haiko vitani, unapeleka kikosi cha polisi kumkamata mwanamke mmoja aliyetoroka kambi ya Corona utafikiri unaenda kumkamata kiongozi wa Al-Qaeda, Unataka kumtisha nani na askari wako na silaha zao, wananchi wa Tanzania?

Unapeleka askari na silaha kwenye tukio dogo kama hili utafikiri huyo mwanamke ndio Corona yenyewe unaenda kuikamata! Mkitukanwa mnatumia nguvu badala ya busara mnalalamika. Hii display ya force kwenye tukio kama hili inawasaidia nini hasa? Polisi badilikeni. Mnatuaibisha.

Siku moja askari wako wenye silaha na wamevaa kiraia watakuja kuuwawa wakidhaniwa ni majambazi.

1585926705909.png


1585926771918.png
 
Unataka watumwe na silaha ndogo ili uwafanye nini askari wetu?

Au ndiyo nyie wauaji wa Kibiti ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo lenu nyie askari ubabe wenu wote mnaufanyia uraiani. Siku mkikutana na wanaume wenyye kujibu mapigo mnatimua mbio! Mnapigiwa simu eneo limevamiwa na majambazi mnaenda mkijua majambazi wameshaondoka. Kumkamata mwanamke aliyetoroka kambi ya Corona mnaenda na silaha hata wanajeshi wakiwa vitani hawabebi silaha namna hiyo!
 
Tatizo labda iwe hizo silaha ila sio nguo.
Hao askari wa idara ya upepelezi, ambao kimajukumu hawavai uniform.
Sasa huko wameenda kupeleza kitu gani? Uliona askari anaenda kupeleleza kajivalisha mibomu ya machozi kama hana akili sawa?

Askari wawili wenye SMG walitosha kabisa, na hata bila kuwa na silaha isingekuwa tatizo. Hata mmoja, kwa sababu hili sio tukio ambalo lingeweza kuleta vurugu.

Au labda huyo mwanamke ni mwanachama wa Chadema!
 
Synthesizer wako na mwenyekiti wa kamati ya usalama ya wilaya. Lengo la nguvu ni ili mimi na wewe tukitakiwa kuwepo kwenye karantii tusitoroke
Mkuu kwa hiyo wako hapo kwa ajili ya kumlinda Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Wilaya?
 
Mkuu hujawazoea tu? Wao ubabe wao kwa raia wakawaida. Penye mtiti wa kweli hawaonekanwi. Jaribu kwapigia simu usiku halafu uwambie kama nyumba imezungukwa na majambazi kama watatokeza.
 
Mkuu hujawazoea tu? Wao ubabe wao kwa raia wakawaida. Penye mtiti wa kweli hawaonekanwi. Jaribu kwapigia simu usiku halafu uwambie kama nyumba imezungukwa na majambazi kama watatokeza.
Wanasema hawana gari, au gari haina mafuta!
 
Sasa huko wameenda kupeleza kitu gani? Uliona askari anaenda kupeleleza kajivalisha mibomu ya machozi kama hana akili sawa?

Askari wawili wenye SMG walitosha kabisa, na hata bila kuwa na silaha isingekuwa tatizo. Hata mmoja, kwa sababu hili sio tukio ambalo lingeweza kuleta vurugu.

Au labda huyo mwanamke ni mwanachama wa Chadema!
Unafahamu P.G.O zinaongoza jeshi la polisi? Kama ndio wamevunja P.G.0 ipi/zipi?
Maana hapa naona tunabishana kitoto.
 
Unafahamu P.G.O zinaongoza jeshi la polisi? Kama ndio wamevunja P.G.0 ipi/zipi?
Maana hapa naona tunabishana kitoto.
Mtoto ni wewe. Mie natumia busara ya kawaida katika mazingira ya Tanzania. Sasa ukiniletea term zenu za polisi na mimi sio polisi unategemea nini? Na mimi nikikuletea terms za kazi yangu nitegemee utanielewa? Ndio maana mnaambiwa jaribu kutumia akili kidogo.Sihitaji kujua P.G.O sijui kuelewa upumbavu na ujinga unaojionyesha hapa. Hizo P.G.O mbona mkiitwa kwenye tukio la ujambazi mnazisahau?
 
Mtoto ni wewe. Mie natumia busara ya kawaida katika mazingira ya Tanzania. Sasa ukiniletea term zenu za polisi na mimi sio polisi unategemea nini? Na mimi nikikuletea terms za kazi yangu nitegemee utanielewa? Ndio maana mnaambiwa jaribu kutumia akili kidogo.Sihitaji kujua P.G.O sijui kuelewa upumbavu na ujinga unaojionyesha hapa. Hizo P.G.O mbona mkiitwa kwenye tukio la ujambazi mnazisahau?
Acha povu bwanamdogo PGO ni Police General Orders. Hivyo ulikuja na hamaki kwa kulaumu ufavaaji huo, kana kwamba kwenye PGO wamevunja kifungu.
Ndio kusema nakutaka kukufunda kabla hujalalamika suala ambalo hulifahamu jitahidi ufahamu nalo kabla ya kutoa lalamiko.

Lalamiko ni hitimisho kwamba walikosea kwa mujibu wako, by theway nisamehe hapo juu kama nilitumia lugha mbaya.
 
Back
Top Bottom