IGP Sirro, Tafadhali usiligeuze jeshi la polisi kama mob

IGP Sirro, Tafadhali usiligeuze jeshi la polisi kama mob

Km hawakuomba kibali unamlaumu vipi IGP?
Ndg yangu, nadhani Katiba na sheria za vyama vya siasa zinasema Chama cha siasa kilichosajiliwa rasmi kinatakiwa kutoa taarifa kwa Polisi si chini ya masaa 48 kama kinataka kufanya mkutano wa hadhara. Lengo kulingana na sheria hiyo ni kutoa fursa kwa jeshi letu la Polisi kujipanga ili kutoa huduma nzuri ya ulinzi. Siyo kwamba jeshi la polisi linatakiwa kutoa kibali kwa Chama cha siasa kufanya Kazi zake. Na kwa vikao vya ndani sidhani kama kunatakiwa kutoa taarifa hiyo polisi kwani hakutakiwi kuwa na ulinzi wa polisi. Lakini polisi wanaweza kuingilia kama wataona kunaweza kuwa na tishio la uvunjifu wa amani sehemu yoyote.Lakini ni busara Kama hali hiyo ikitokea washauriane na na Chama husika na siyo kutumia tu ubabe.
 
Kamanda Sirro, kuna clip inatrend kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha jeshi lako la polisi likivamia mkutano halali kabisa wa chama cha ACT wazalendo.
Mkutano wao huo wa amani na wa ndani ulikuwa ungali ukiendelea huku wananchi wakiwa wanaimba nyimbo kumkaribisha kiongozi wao wa chama, ghafla polisi wakajitokeza na kuvamia mkutano huo huku mmoja akotoa maelekezo yakionyesha Zitto aondolewe kwa nguvu.

Wakati huohuo Polisi ikiendelea kuwasumbua wapinzani kufanya shughuli zao halali zilizoko kwa mujibu wa katiba, Chama cha mapinduzi chenyewe kimeonekana kuendelea kufanya shughuli zao za kisiasa bila kusumbuliwa na yeyote.

Tunalaani matendo haya ya polisi, ningependa kumueleza IGP Sirro, Si vizuri jeshi la polisi kufanya mambo kama Mob, tunapojaribu kujenga Taifa letu.

Vyama vya upinzani vipo kwa mujibu wa sheria za nchi na katiba, na vina haki ya kufanya siasa kwa uwazi kabisa bila kubughudhiwa na Yeyote.

Kitendo cha polisi mara kwa mara kusumbuasumbua wapinzani, au kutoa matamko ya kuashiria kuwa linatumika kisiasa, ni mambo ya kihuni, aibu na hayafai hata kidogo. Hayo mambo hayawezi kuleta heshima kwa jeshi la polisi nchini.

Tunalitaka jeshi la polisi kuacha mara moja matendo haya aibu na yasiyokuwa ya kiungwana hata kidogo.

Hayo mambo hayalifai jeshi la polisi, hayo mambo hufanywa na mobs lakini si kwa jeshi la polisi linalopaswa kuheshimiwa

IGP Sirro unafeli sana kwenye angle hii, usikubali kutumika kisiasa!

Hii video ya uvamizi wa mkutano wa ACT huko Kilwa inasikitisha sana

View attachment 1488202
Haya yataisha siku tutakaposhikishana adabu.
 
Polisi wasiwajengee watu tabia ya kutoogopa kukamatwa tukifika huko ni hatari watu awatoogopa tena,wataona ni sawa na kwenda chumbani tu
 
Kamanda Sirro, kuna clip inatrend kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha jeshi lako la polisi likivamia mkutano halali kabisa wa chama cha ACT wazalendo.

Mkutano wao huo wa amani na wa ndani ulikuwa ungali ukiendelea huku wananchi wakiwa wanaimba nyimbo kumkaribisha kiongozi wao wa chama, ghafla polisi wakajitokeza na kuvamia mkutano huo huku mmoja akotoa maelekezo yakionyesha Zitto aondolewe kwa nguvu.

Wakati huohuo Polisi ikiendelea kuwasumbua wapinzani kufanya shughuli zao halali zilizoko kwa mujibu wa katiba, Chama cha mapinduzi chenyewe kimeonekana kuendelea kufanya shughuli zao za kisiasa bila kusumbuliwa na yeyote.

Tunalaani matendo haya ya polisi, ningependa kumueleza IGP Sirro, Si vizuri jeshi la polisi kufanya mambo kama Mob, tunapojaribu kujenga Taifa letu.

Vyama vya upinzani vipo kwa mujibu wa sheria za nchi na katiba, na vina haki ya kufanya siasa kwa uwazi kabisa bila kubughudhiwa na Yeyote.

Kitendo cha polisi mara kwa mara kusumbuasumbua wapinzani, au kutoa matamko ya kuashiria kuwa linatumika kisiasa, ni mambo ya kihuni, aibu na hayafai hata kidogo. Hayo mambo hayawezi kuleta heshima kwa jeshi la polisi nchini.

Tunalitaka jeshi la polisi kuacha mara moja matendo haya aibu na yasiyokuwa ya kiungwana hata kidogo.

Hayo mambo hayalifai jeshi la polisi, hayo mambo hufanywa na mobs lakini si kwa jeshi la polisi linalopaswa kuheshimiwa

IGP Sirro unafeli sana kwenye angle hii, usikubali kutumika kisiasa!

Hii video ya uvamizi wa mkutano wa ACT huko Kilwa inasikitisha sana

View attachment 1488202
Chonde polisi. Musielekeze nchi kwenye visasi na machafuko. Tendeni haki kuifanya nchi ibaki salama. Ni "USHAURI" tu.
 
Vyeo hivi ni mzigo sana.

Sirro wa 2010 pale Nyamagana sio Sirro wa 2020.

Legacy zao zitawahukumu.
Sirro anafuata maelekezo tu mkuu isitoshe RC na DC huku mikoani ndio wenyeviti wa kamati za ulinzi hivyo wanaweza kumuamrisha RPC au OCD kuzuia mikutano kama hiyo ya wapinzani.

Tatizo kubwa lipo kwa wanasiasa japo kuna baadhi ya polisi wamejigeuza wanasiasa kama njia ya kujipendekeza (Jonathan Shana).
 
Back
Top Bottom