IGP Wambura ameshindwa kudhibiti ajali barabarani, asaidiwe!

IGP Wambura ameshindwa kudhibiti ajali barabarani, asaidiwe!

SALOK

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2011
Posts
3,364
Reaction score
2,001
Katika kipindi kifupi cha Uhudumu wa huyu IGP mpya, pengine changamoto kubwa aliyokumbana nayo katika utendaji wake ni kukithiri kwa matukio ya ajali za barabarani.

Matukio haya yamekwenda sambamba na upotevu wa roho za watanzania, nguvu kazi ya Taifa. Inasikitisha sana.

Licha ya ajali kuongezeka kila usiku uchao, bado hatuoni vyombo vinavyohusika vikichukua hatua za makusudi kuhakikisha matukio haya yanapungua kama si kukoma kabisa hususani Jeshi la Polisi tena likiwa na IGP mpya kabisa katika nafasi hiyo baada ya mtangulizi wake kuteuliwa kuwa Balozi Nchini Zambia ambaye katika kipindi cha uhudumu wake alifanikiwa kiasi kikubwa kudhibiti ajali za barabarani.

Matukio ya ajali za barabarani katika siku za hivi karibuni kwa Watanzania imekuwa ni chai ya asubuhi isiyokuwa na vitafunwa ambayo huishilizia kwa kuwaachia Watanzania maumivu na majeraha ya vifo na vilema!

Ni dhahiri kwamba Jeshi la Polisi hasa hasa Idara ya usalama barabarani imefeli katika hili, na hapa tunaanza kuiona dosari kwa Mteule IGP.

Japokuwa mara zote chanzo cha ajali husemwa ni mwendokasi na uzembe wa dereva.

By the way; Sisis tunatekeleza wajibu wetu, kukosoa na kushauri.

#TanzaniaSalamaInawezekana

IMG_20230307_095233.png
 
kuna watu wanaona sifa ku over speed
utakuta unatembea 120kph mtu anakupita kama vile umesimama
Inasikitisha sana, Unasafirisha familia asubuhi, mchana unapokea simu kuhusu ajali mbaya basi alimosafiri wife na watoto... SERIKALI IANGALIE HILI SUALA..!! CORONA HATUKUWA NA NAMNA, HATA HIZI AJALI ZA KIZEMBE??
 
Katika kipindi kifupi cha Uhudumu wa huyu IGP mpya, pengine changamoto kubwa aliyokumbana nayo katika utendaji wake ni kukithiri kwa matukio ya ajali za barabarani...
Hivi madereva wanapata faida gani gari ikipata ajali? Maana naona huwa hawajali kabisa. Jana nimekutana na dereva mashuhuri route ya Mbeya-Sumbawanga pale Uyole amekatwa mguu sijui aliumwa na nyoka?
 
Katika kipindi kifupi cha Uhudumu wa huyu IGP mpya, pengine changamoto kubwa aliyokumbana nayo katika utendaji wake ni kukithiri kwa matukio ya ajali za barabarani....
ww unataka kushindana na "qadar" ya Allah?
 
Hapo utakuja kusikia eti kazi yake mola haina makosa na ukifatilia utakuta Kuna mtu au watu hawakutimiza wajibu wao.
 
IGP hana kosa, wanasiasa wengi ndio wamiliki wa vyombo vya usafiri vya kibiashara.

Polisi wakitaka kufanya kazi yao wao wanakuwa wakali, sasa msilalamikie polisi waulizeni haohao CCM wanaowaambia "tochi zimezidi" na nyie mnafurahia.

Madereva wengi Tanzania hawana hekima wala busara, ni reckless drivers, njia pekee ya kuwaweka kwenye mstari ni tochi za kufa mtu na matuta ya kutosha barabarani.
 
Muda si mrefu yule jamaa ataita udereva wa magari ni laana kama bodaboda kisa vifo na majeruhi.
 
Hivi madereva wanapata faida gani gari ikipata ajali? Maana naona huwa hawajali kabisa. Jana nimekutana na dereva mashuhuri route ya Mbeya-Sumbawanga pale Uyole amekatwa mguu sijui aliumwa na nyoka?
😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom