CAPPACITOR
Member
- Nov 2, 2013
- 17
- 5
Habarii wana jamvi..Leo nimeona tujalibu kufunguana mawazo juu ya dalaja C vyuo vikuu Tz. Hili suala tunaliona dogo lakini linamghalimu mtu mmoja mjoja huko mtaani, Wakati tukipitapita na bahasha zetu huko maofisini hatutakuwa tukiulizwa kuwa umesoma chuo gani, shida itafika wakati wa kuangalia certificate za watu tokea vyuo tofauti vyenye madalaja ya ufaulu tofauti,kuna baadhi ya vyuo dalaja C linaanza na 40 na vingine linaanza na 50% cjajua kama kuna vyuo dalaja C linaanza chini ya 40%, kwa vyuo ambavyo C ni 40% au chini ya hapo mwenye 41% atakuwa na dalaja C wakati huohuo kwa ambao C inaanza na 50% mwenye 49.9% atakuwa na D hivyo lazima awe alifaya mtihani wa supplimentary nakupewa C*(suppl..).Hawa watu wawili wakiingia kwenye kinyan'ganyilo ataonekana mwenye C alifanya vizuri kuliko mwenye C* na huenda mwenye C* akakosa nafasi kwasababu hiyo. Hili mnalionaje wasomi wenzangu na mnamaoni gani????.