Ijue Kirumba jijini Mwanza kwa maandishi

Ijue Kirumba jijini Mwanza kwa maandishi

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,030
Reaction score
20,391
IJUE KIRUMBA YA JIJINI MWANZA PIA PIGA MISELE NAMI KWA NJIA YA MAANDISHI

KIRUMBA Ni eneo kongwe tangia wareno, waarabu, wajerumani , na waingereza wamewahi kuishi kirumba, ni mojawapo ya maeneo ya mwanzo kabla ya uhuru kuwa na miundo mbinu ya bara bara ya lami na changarawe.

Umeme, simu na mfumo wa maji ya bomba, kirumba ndilo eneo la mwanzo mwanza kuwa na ginerys, bandari kabla ya mwanza south kule igogo

Kabla ya kugawanya eneo la sasa la Kitangili na bwiru na eneo baadhi la nyamanoro ilikuwa ni kirumba yote.

KIRUMBA YA SASA inapakana na nyamagana mpaka ni mto mirongo upande wa chini ya bara bara ya lami ,ukivuka jengo la CCM Mkoa chini ya kliniki ,eneo lote hilo ambalo kuna bustani unakuja marine police hadi furahisha chini ya s/msing Mwenge.

,kirumba ni yenye uwanda na ufukwe wa ziwa mkubwa zaidi ukianzia mto mirongo, Mwaloni kirumba(soko la kimataifa), kigotto, ibanda, busisi eneo hili ni lenye ufukwe mzuri wa ziwa na hewa safi kabisa mwanana wa ziwa victoria.

kirumba inapakana na eneo la katikati ya jiji na kupakana na isamilo, mirongo, nyamagana na maeneo ya nyamanoro, Kitangili
pia kirumba kwa eneo la ziwani (majini)ziwa victoria kupitia eneo la kigotto inapakana na eneo la maji na wilayani Sengerema.

Ijue kirumba ndio maeneo kabla ya uhuru kuwa na shule kama s/msing kirumba, zahanati kituo kikuu cha police na kambi mbili kubwa za police kirumba na kambi ya police kigotto iliyo ufukweni mwa ziwa victoria.

Kirumba ina vilima vya uoto wa asili kama vilima vya kigotto vyenye mandhari nzuri na ya kuvutia na wanyama wadogo wadogo kama pimbi ,tumbili(ngedele), kenge.

Ukiwa Kirumba karibu eneo zima utaweza kuliona eneo lote la katkati ya jiji la mwanza vizur na bandari ya mwanza ,hospital ya rufaa ya bugando ,capripoint na ikulu ya Mwanza.

Eneo la Kirumba pia lina muuingiliano la watu mbali mbali ki mkoa ,kanda ya ziwa ,kitaifa afrika mashariki na eneo lote la maziwa makuu. Kirumba licha ya shughuli za uvuvi pia ni eneo la kibiashara.

licha ya haya kirumba ni eneo la ukanda duniani lenye kuwa kitovu cha utoaji wachezaji mahiri wa soka katika ukanda huu wa nchi za maziwa makuu. Karibu nchi zote za ukanda huu zina hama kwa wakati tofauti zimewahi kuwa na wanasoka wa kirumba ..na igogo/ mkunguni

Kirumba kumbi za burudani ziko karibu pia mahotel ya hadhi ya fedha yako Kirumba ni yenye mitaa 8 ,kigotto iliyo ufukweni na vilima vya uoto wa asili pia kuna ibanda (A) na (B) na busisi,mamlaka ,mlimani /kiyungi, kabuhoro, na eneo la centre la kirumba kati lenye maeneo mengi ya kibiashara na maofisi ya kiserekali , binafsi ,umma ,na kijamii yakiwemo mahotel makubwa,masoko yote mawili makuu na huduma muhimu za kijamii.

KARIBU KIRUMBA NA UIJUE KIRUMBA
Usafiri kirumba upo wa majini kwa safari za ziwani visiwani na bukoba pia daladala usafiri upo wa njia mbili ibanda mzunguko zianziazo safari kemondo kupitia mwaloni ,kigotto , Kiyungi, kabuhoro hadi ibanda na za bwiru zipitiazo kirumba police ,kirumba sokoni ,mjini
pikipiki pia unaweza zungushwa popote kirumba.

Hii ni safari ya maandishi nimeamua kukutembeza kirumba ewe mdau wa JF

Mandhari ya jiji la Mwanza
 
Nilikua nasubiria uielezee na profeshen kongwe pande hizo ila naona umegoma ,kwa sisi ambao hatujafika huko tukisikia tu kirumba kitu cha kwanza kinstujia ccm kirumba au wauza UCCI
 
Nilikua nasubiria uielezee na profeshen kongwe pande hizo ila naona umegoma ,kwa sisi ambao hatujafika huko tukisikia tu kirumba kitu cha kwanza kinstujia ccm kirumba au wauza UCCI
🤣🤣🤣 watu bhana
 
Bila picha ni unafki mkuu...Sina nia mbaya ya kkupinga ila umeielezea kirumba kwa kifupi sanaa na bila ata picha??ungeenda ata kwenye ule Uzi wa ( Mwanza vs Kisumu) kuna picha za mall,CCM kirumba n.o nmk
 
Bila picha ni unafki mkuu...Sina nia mbaya ya kkupinga ila umeielezea kirumba kwa kifupi sanaa na bila ata picha??ungeenda ata kwenye ule Uzi wa ( Mwanza vs Kisumu) kuna picha za mall,CCM kirumba n.o nmk
Sawa mkuu ngoja nikazisake.
Ila si vibaya hata wewe ukaongezea
 
Asante mkuu, umetufumbua macho wengi. Wengi tulijuwa Kirumba ni uwanja wa mpira, na sio mtaa! Kwa hiyo picha tuliyokuwa tunapata mtu akisema nipo Kirumba basi tunajuwa yupo uwanja wa mpira, sawa na mtu akisema nipo taifa, tunajuwa yupo uwanja wa mpira wa taifa (Mkapa au Uhuru). Kumbe uwanja wa mpira wa Kirumba (CCM) uliukuta mtaa wa Kirumba upo tayari, na wala sio mtaa ulipewa jina la uwanja. Asante kwa ufafanuzi.
 
La kairo ilifungwa kwa Sasa naona wameikalabati na kupaka rangi lakini haijaanza kufunya kazi,
Pia Villa Park imefungwa kabisa,Kilumba imepooza kabisa.
Kweli Hali ilikua ngumu,nikikumbuka la kairo miaka Ile ilikua poa Sana.

Villa nasikia CCM wamempiga figisu hapo kwny eneo lao Ila Sina uhakika,nilisikia huyo jamaa wa Villa kuna sehemu anajenga club hapo Mwz Ila sikumbuki Ni sehemu gani.
 
Back
Top Bottom