Ijue Nyumba Ntobhu - nyumba bila mwanaume kwa jamii ya wanawake wa kijaluo.

Ijue Nyumba Ntobhu - nyumba bila mwanaume kwa jamii ya wanawake wa kijaluo.

Baba Kisarii

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2024
Posts
1,844
Reaction score
3,089
Nyumba Ntobhu maana yake ni "nyumba bila mwanamume" ni aina ya muungano wa jadi usio wa mapenzi ya jinsia moja miongoni mwa wanawake wa kabila la wajaluo Mkoani Mara - ushirikiano huundwa kati ya wanawake wakubwa kiumri na wanaojiweza kiuchumi, ambao kwa kawaida wanawake hao huwa ni wajane au wanawake wa kawaida wasio na uwezo wa kuzaa watoto ambapo hushirikiana na wanawake mabinti wadogo wasio na watoto, wanaojulikana kama mokamööna (mabinti wakwe).

Ni nyumba inayoongozwa na mwanamke kama baba na huwa hakuna mwanaume katika familia hiyo japo kuna watoto wanazaliwa.

Iko hivi....

Mwanamke mwenye uwezo na umri mkubwa anaoa mdada kijana ili ampatie uzao

Mdada akiolewa na huyo mwanamke mwenzie atatafuta mimba kwa mwanaume yeyote... yaani anakuwa anaenda kufanya ngono na mwanaume yeyote hadi apate mimba na kuzaa. Mwanamke aliyemuoa mdada ndiyo anakuwa 'baba' wa kulea mtoto au watoto watakaozaliwa na huyo mdada.

Hapo huyo mwanaume mtia Mimba hatatambuliwa kwa hiyo familia na wala hatajua kama alimtia mimba huyo mdada maana jambo hilo huwa ni siri kwa mdada na mwanamke aliyemuoa.

Kwa kutiwa mimba na wanaume mbalimbali mdada atazaa watoto kadri awezavyo na hao watoto watatumia ubin wa huyo mwanamke.

Hiyo ndiyo Nyumba Ntobhu ujaluoni.

Aliyebuni Nyumba Ntobhu apewe heshima yake kwa ubunifu huo wa kijadi.
 
Nyumba Ntobhu maana yake ni "nyumba bila mwanamume" ni aina ya muungano wa jadi usio wa mapenzi ya jinsia moja miongoni mwa wanawake wa kabila la wajaluo Mkoani Mara - ushirikiano huundwa kati ya wanawake wakubwa kiumri na wanaojiweza kiuchumi, ambao kwa kawaida wanawake hao huwa ni wajane au wanawake wa kawaida wasio na uwezo wa kuzaa watoto ambapo hushirikiana na wanawake mabinti wadogo wasio na watoto, wanaojulikana kama mokamööna (mabinti wakwe).

Ni nyumba inayoongozwa na mwanamke kama baba na huwa hakuna mwanaume katika familia hiyo japo kuna watoto wanazaliwa.

Iko hivi....

Mwanamke mwenye uwezo na umri mkubwa anaoa mdada kijana ili ampatie uzao

Mdada akiolewa na huyo mwanamke mwenzie atatafuta mimba kwa mwanaume yeyote... yaani anakuwa anaenda kufanya ngono na mwanaume yeyote hadi apate mimba na kuzaa. Mwanamke aliyemuoa mdada ndiyo anakuwa 'baba' wa kulea mtoto au watoto watakaozaliwa na huyo mdada.

Hapo huyo mwanaume mtia Mimba hatatambuliwa kwa hiyo familia na wala hatajua kama alimtia mimba huyo mdada maana jambo hilo huwa ni siri kwa mdada na mwanamke aliyemuoa.

Kwa kutiwa mimba na wanaume mbalimbali mdada atazaa watoto kadri awezavyo na hao watoto watatumia ubin wa huyo mwanamke.

Hiyo ndiyo Nyumba Ntobhu ujaluoni.

Aliyebuni Nyumba Ntobhu apewe heshima yake kwa ubunifu huo wa kijadi.
Ahsante kwa uzi. Ila elewa kuwa hakuna Wajaluo bali tuna WALUO
 
Nyumba nthobu SIYO utamaduni wa wajaluo.
Ni utamaduni wa wakurya na vikabila vyenye muelekeo wa wakurya.
Ukikuta mjaluo anafanya nyumba nthobu, jua ni mjaluo anayeishi karibu na maeneo ya wakurya.
 
Nyumba nthobu SIYO utamaduni wa wajaluo.
Ni utamaduni wa wakurya na vikabila vyenye muelekeo wa wakurya.
Ukikuta mjaluo anafanya nyumba nthobu, jua ni mjaluo anayeishi karibu na maeneo ya wakurya.
Wajaluo na wakurya tofauti gani mkuu?
 
Wajaluo na wakurya tofauti gani mkuu?
Wajaluo/waluo ni wanailoti waliosambaa Kenya, Tanzania , Uganda, Sudani kusini na wachache wapo Ethiopia na DRC.

Wakurya ni wabantu wanaopatikana zaidi Tanzania na wachache wapo Kenya.

Wajaluo na wakurya walishare wilaya ya Tarime kwa muda mrefu mpaka ilipogawanywa. Wajaluo wengi wakawa upande wa wilaya mpya ya Rorya, wakurya wakabaki Tarime.

Pia, wajaluo ni wavuvi, wafugaji na wakulima. Wakurya wengi ni wakulima, wafugaji na wafanyabiashara.

Wajaluo ni kama vile wakina Owino, Otieno, Onyango, Odhiambo,n.k

Wakurya ni wakina Marwa, Wambura, Heche, Bhoke, Gati n.k
 
Watoto watamwitaje uyo maza faza? Je uyo maza faza analala na wife wake au? Je anahudumiwa kama faza like kuoelekewa maji ya kuoga nk au wanaishi wanawake wawili ndani? Hii kitu inanipa ukakasi kunamda wanafanya yaliyoangamiza mji ule wa Gomora
 
Back
Top Bottom