Ijue sayansi ya chanjo hizi na chimbuko la wasiwasi wake. Hata Ulaya ni 5% tu ndiyo wamechanja katika miezi 3. Je, wanatusubiri sisi?

Ijue sayansi ya chanjo hizi na chimbuko la wasiwasi wake. Hata Ulaya ni 5% tu ndiyo wamechanja katika miezi 3. Je, wanatusubiri sisi?

Uchumi wetu utakapofikia kiwango cha high middle income country mwaka 2025 bila shaka tutakuwa na maabara zetu wenyewe za uhandisi wa vinasaba (genetical engineering laboratories) za kiwango cha kimataifa kama zile za BioNTech ya ujerumani iliyohusika kutengeneza chanjo ya Pfizer au ile ya Oxford University iliyohusika kutengeneza ile chanjo ya AstraZeneca. Ngoja kwanza tumalize bwawa la umeme la Nyerere na SGR ya umeme. Yanayokuja yanafurahisha. Vuta subira. Roma haikujengwa siku moja. Ngosha bado tunaye.

Kwamba?

IMG_20210218_174254_207.jpg


Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Aiseee Mibongo ni mipwenge kabisa umeijaza ujinga, yote inakusujudia
Anzisha kanisa hapa, utakuwa na unatembelea VOGUE kama kina Gwaji


Hizi nchi zote wanakabana koo wenyewe kwa wenyewe kwa upungufu wa chanjo.
Halafu unaleta utopolo ambao uko shallow kuzidi utopolo wenyewe,
Mbona hamna mabingwa wa tiba duniani UK kwenye hii pumba listi yako , unajuwa idadi ya waliochanjwa
Au nikuwekee cheti changu hapa uamini

Hata Israel kwa makusudi haimo kwenye list kwamba hakuiona.

Mijamaa hii ina maslahi makubwa na vifo vya watu.

Yumkini ndiyo hii inayosemekana kuwa ilichanjiwa chattle.
 
Yani hata neno akili hujui linavyoandikwa lakini unamwambia mwenzako atumie akili!! Sasa watu kama wewe ndiyo washauri wa jiwe hapo unategemea nini cha maana?

Hiyo mijamaa bure kabisa. Kila mafanikio ya Chanjo au tiba inapopatikana dhidi ya ugonjwa huu kwao ni msiba mkubwa.

Inajifanya yenyewe kuwa na mamlaka ya uamuzi wa juu ya wengine kufa au kuishi.

Kusikia kwao ni kwa kenge!

Hiiiiii bagosha!
 
Hizi chanjo kwa watanzania waishio huko Ulaya na Marekani na nchi zingine za mashariki ya mbali, hizi chanjo zitakuwa ni lazima.

Sababu kuu ni kwamba ukitaka kusafiri kwa wale wanosafiri mara kwa mara , cheti maalum cha chanjo kinaandaliwa baina ya nchi za Ulaya na kwingine ili kusaidia sekta ya usafri wa anga ambayo ipo ICU.

Mashirika ya ndege yote yatapewa mwongozo na serikali mbalimbali kuhakikisha waangalia hicho cheti na kama huna basi ndege hupandi.

Ushauri wangu kwa serikali ni kwamba kama chanjo zinatolewa ziwe ni kwa ajili ya kuwachanja wale wote wenye matatizo ya kiafya underline conditions kama pumu, na HBP lakini sio wale walo na magonjwa ya kuelekea kaburini.

Pia wale wote wanohitaji kusafiri kwenye Ulaya na kwingine ambako kwahitajika uthibitisho wa kwamba msafiri amedungwa sindano ya chanjo ni lazima wapigwe chanjo.

Hivyo hii michezo ya kutumia akili au "mind games"ipitiwe upya na serikali iangalie ni chanjo ipi yafaa kununuliwa au kupewa bure au kuwa ni sehemu ya mkopo.

Mwisho wa siku ni lazima kutakuwa na watanzania wanotaka kusafiri kwenda nje (wakiwemo viongozi wa serikali) na ni lazima wawe wamechanjwa na pia wananchi ambao wa matatizo ya kupumua ambao pengine wangepatiwa chanjo basi wangeepushwa na vifo.
 
Germany's vaccine commission has approved the use of the Oxford-AstraZeneca jab in people aged over 65.
 
Bro hizo statistics za vaccination umotoa wapi? Israel ndio inaongoza kwa vaccination 92% ya ppn inamaana hao wote wameathirika. Instead of criticizing others come up with a practical solution for Africans. Source of african problems is the african themselves. We are damn enough to accept vaccination from the rest world instead of us developing our own Rate of COVID-19 vaccination by country 2021 | Statista
Takwimu za kweli na zinazoeleweka kuhusu masuala ya afya zinapatikana WHO. Hizo za akina John Efflein na wengineo zitakupoteza, hasa kama hujui kuzitafisiri kitaluma.

Chanjo zinatolewa kwa utaratibu maalum wa doses zake. Dose ya kwanza ni ya kusituwa tu (activate or prime) hizo seli za askari wa kinga (T memory & B memory cells). Dose ya kwanza haikupi kinga yo yote. Unahitaji doses zingine baada ya kipindi fulani (booster doses). Kwa hizi chanjo za covid-19 unahitaji dose ya pili baada ya wiki 4 kwa Moderna na AstraZeneca na wiki 3 kwa zile chanjo za aina nyingine. Hapo ndipo tunasema umepata chanjo (fully vaccinated) itakayoweza kukukinga usipate ugonjwa huo kwa kipindi fulani - kipindi hiki kwa kawaida ni miezi 6 ambapo utalazimika kupata booster dose nyingine etc

Hivyo takwimu tunazo ongelea hapa ni za wale waliopata full vaccination hasa huko ulaya, kwa wazungu na amerika ambao ni miezi 3 sasa tangia waanze kuchanjana. Hatuongelei takwimu za idadi ya doses zilizotolewa kwani hilo ni la wahasibu, sisi halituhusu. Tunaongelea ni watu wangapi wamepata dose ya kwanza na wangapi wamekamilisha chanjo:

1. Israel: Hii si nchi ya ulaya wala watu wake si wazungu bali ni waarabu. Halafu ni kainchi kadogo sana kenye watu million 9 tu kanpitwa na Burundi yenye watu million 12. Hivyo takwimu zake haziwezi kubadili cha maana huo wastani wa uchanjaji. Takwimu za sahihi za Israel toka WHO hadi tarehe 5 March 2021 ni:
- At least 1 dose 4,901,162 people sawa na 54.14%
-Full vaccinated 3,654,820 peopĺe sawa na 40,3%

2. United Kingdom:
Huyu ndiye alikuwa wa kwanza huko ulaya kuanza kuchanja watu wake tarehe 8 December 2020. Tena alianza kwa mbwembwe nyingi akifurahia uhuru wa kujitoa kwenye Umoja wa ulaya. Kwamba halazimiki kusubiri maamuzi ya EU kuanza uchanjaji. Hadi tarehe 5 March takwimu zake ziko hivi:
  • At least 1 dose 21,358,815 =32%
  • Fully vaccinated 3,660,333 = 1.5%

Yaani watu wake wengi baada ya kudungwa hiyo sindano ya kwanza waliingia mitini. Walikataa kurudi kukamilisha chanjo baada ya wiki 3 kama masharti ya chanjo ya AstraZeneca yanavyotaka. Yaani ni aibu. Full vaccination rate yake ni 1.5% tu. Halafu katuletea machanjo yake hayo bure sisi waafrika. Wewe unataka tumweleweje huyu mzungu tajiri na ugonjwa huu unatesa sana wananchi wake?

3. Haya takwimu za full vaccination coverage za WHO za nchi za wazungu na waarabu hadi tarehe 5 March hizi hapa:

One dose Full vaccination
Russia 3.4% 1.2%
France 5.1% 2.7%
Italy 5.9% 2.6%
Germany 5.7% 2.8%
Belgium 4.9% 2.9%
Greece 6.5% 3.4%
Spain 6.7% 2.8%
Turkey 9.1% 2.8%
Bulgaria 3.3% 0.7%
Hungary 9.7% 3.1%
United Kingdom 32%. 1.5%
Israel 54.1% 40.4%
Morocco 10.6% 1.4%
USA 16.9% 8.7%

World 2.2% 0.8%


Hizo ndizo takwimu za kweli zizoko WHO. Efficacy inayooneshwa kwenye hizo chanjo ni ya baada ya kupata full vaccination. Hiyo dose moja ya kwanza haikupi kinga yo yote bali ni ya maandalizi tu ya immune system yako. Unahitaji dose ya pili (booster) baada ya wiki nne au tatu kutegemea na aina ya chanjo. Hapo ndipo tunasema umepata full vaccination. Na badoinawezekana ukahitaji booster dose nyngine baada ya miezi sita na kila mwaka baada ya hapo.

Tukisema Efficacy ya chanjo ya AstraZeneca ni 62% maana yake ni kuwa katika watu 100 waliopata full vaccination, watu 62 kati yao watakuwa miili yao imepata kinga (immunity) ya ugonjwa huo, hao 38 waliobaki hawatapata kinga yo yote dhidi ya ugonjwa huo yaani wako sawa tu na wale ambao hawakuchanja kabisa. Hakuna cha kinga kidogo. Tatizo huwezi ukawatambua au kwa vipimo kujua katika hao 100 nani kafanikiwa mwili wake kupata kinga. Kipimo pekee ni kukutana na kirusi hicho - kama hakitakugalagaza basi wewe utajua uko kwenye kundi hilo la watu 62. Full vaccination haimaanishi full immunization. Yaani kati ya watu 100 wanaopata full vaccination ya Astrazeneca vaccine ni 62 tu ndiyo wanapata full immunization against CoV-2.

Lengo kuu la chanjo dhidi ya magonjwa ya kuambukiza ni kupata angalao 60% ya watu wawe na kinga (fully immunized) ili kupata herd immunity to cut off transmission. Kwa mwendo huu wa matokeo ya chanjo kama hii ya AstraZeneca tusahau kufikia hiyo 60% herd immunity.
 
Huna lolote jombi.

Hivi vi propaganda uchwara kwao chattle vijijini. Hata pale mjini vitaboomer.

Kwani marekani wasiotaka chanjo hawapo?

Chanjo ni suala binafsi.

Tusilazimishane kuchanjwa au kutochanjwa. Ndiyo ustaarabu au vipi?

Kwanini kutuzungumzia tulioko hatarini wakati nyie haiwahusu?

Mambo ya ngoswe yanawahusu nini nyie?
Nenda kenya au rwanda ukachanjwe
 
Nenda kenya au rwanda ukachanjwe

Hata huko chanjo zilizopo haziwatoshi wananchi wao tu. Si leo na labda wala mwaka huu kuwa watakuwa wamepokea zakuwatosheleza, sembuse na za kuchanja makapuku toke usengeremani?

Kila chanjo iliyopo katika nchi iko tagged kwa namba yake ya NIDA.

Ila huyu hapa:

IMG_20210218_173848_589.jpg



Kwa anayotufanyia sisi tunaoihitaji mno hii chanjo, ana kesi ya kujibu angalau kwa kila kifo tangia pale alipogoma kuzipokea tu chanjo za ugonjwa huu.

Si umewasikia japo Padre wa Kilimanjaro na yule msomi wa Dar achilia mbali huku mitaani. Hao ni leo tu.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
All mass medias will propagate biological war for certain states survival as super powers, in this war the majority will die both the ignorant and innocents,, and they will come with solution under the so called problem-reaction-solution plan(prs), in the name of humanity the ignorant wll be forced to receive their achieved solutions, and in that way a world will be controlled very simple by the builders.
666



Sijuii huyu mtu asiye julikana alisema kisichojulikana na kikapotelea kusiko julikana!!!!!?
 
Watu wa bavicha ndo tuwafanyie majaribio kwa kuwa wana hamu nayo sana.
Sasa kama wenye umri mkubwa huku na wenye magonjwa hawatakiwi bali wanatakiwa watu wenye afya njema huoni kuna shida?

Maana wanaokufa huku ni wenye afya mgogoro,
Sasa wenye chanjo wanataka watu wenye afya, na kundi la nyumbu wanaililia chanjo,

Mimi nadhani wangejiorozesha kisha serikari iwachanje tu hao nyumbu ili iwakoroge wenyewe.
Mkuu hizo huwa ni kelele za mitandaoni tu,unaweza ukaleta chanjo na kuwaita huko mitaani na asitokee hata mmoja.
 
Nitajaribu kuieleza sayansi hii kwa njia na lugha nyepesi ili jamii ipate mwanga suala hili ambalo kisayansi ni complex. Lengo ni kuelimishana ili kupunguza mihemuko na mivurugano tunayoishuhudia kwa sasa hasa kwa baadhi ya wanasiasa na viongozi mbali mbali wa kijamii na wenye taaluma ya habari.

Atakayeweza kusoma nakala hii ndefu anakaribishwa.

1. Nitaanza na vinasaba (genes):
Miili ya viumbe hai ina undwa na chembe chembe ndogo sana zinazoitwa seli (cells). Binadamu ana matrillion ya seli. Seli hizi zinafanya kazi mbali mbali za kuwesha kuishi (metabolism). Kila seli ina nukleasi iliyozungukwa na saitoplasm. Kwenye nukleas kuna molecules za Deoxyriboncleic acid - kifupi chake DNA. Kila seli ya binadamu ina DNA zipatazo billion 3 zilizobebwa kwenye mikufu (chromosomes) 46 ndani ya nukleas.

Taarifa zote za jinsi miili yetu inavyojengeka na kufanya kazi inabebwa kwenye hizo DNA. Kazi zote za miili yetu inafanyika kwenye saitoplasm ya seli zetu. Yaani kwenye saitoplasm ndiko kwenye viwanda mbali mbali vya kuiwezesha miili yetu iishi na kufanya kazi zote vizuri.

Kazi zote zinazofanyika kwenye kwenye saitoplasm zinafanyika kwa maelekezo na usimamizi wa DNA. Ili DNA iweze kusimamia kazi inayofanyika kwenye saitoplasm huwa inatengeneza molecule ya Ribonucleic acid - kwa kifupi RNA na kuituma huko kwenye saitoplasm kwenda kusimamia kazi husika. Hivyo inaitwa messenger RNA - kwa ufupi mRNA.

DNA ilivyumbuliwa mwaka 1953. Huu ulikuwa ni uvumbuzi wa siri ya maisha kwani siri zote za uhai na jinsi kila seli ya mwili inavyofanya kazi zimebebwa kwenye DNA. Baada ya sayansi mpya ya uhandisi wa vinasaba (genetical engineering) kuendelea (advance), kwa kipindi cha miaka 13 kuanzia mwaka 1990 hadi 2003 wanasayansi toka sehemu mbali mbali duniani walifanikiwa kuzing'amua (decode) siri zote za DNA zote billion tatu zilizoko kwenye seli za mwili wa binadamu. The entire human genetic code was decoded/ revealed. Ziko kwenye ving'amuzi vya maabara mbali mbali za uhandisi wa vinasaba.

Kuanzia hapo wanasayansi wameendelea kucheza na hizo vinasaba vya DNA ili kuweza kuangamiza baadhi ya magonjwa kwenye seli za binadamu hususani ya saratani kama ya kongosho (pancreas cancer) na ya baadhi ya virusi kama virusi vya Zika vilivyogundulika huko Uganda mwaka 1947 kwenye msitu wa Zita vikienezwa na mbu Aedes.

Pamoja na kuonesha matokeo mazuri sana katika tiba za maradhi haya, hadi sasa kwa kipindi cha mwongo mmoja mamlaka za FDAs zilishindwa kuzipa kibali tafiti hizi kuendelea na phase 2 ya clinical trials za watu wengi zaidi. Wasi wasi ukiwa ni athari ya muda mrefu ambayo inaweza kutokea kwenye vinasaba (DNA) ya seli ya binadamu.

2. Virusi ni vitu gani:
Virusi ni vimifuko ya vipande vidogo sana ya vinasaba (genes). Kuna virusi ambavyo genetic material yake ni DNA tupu na zingine ambazo ni za RNA tupu. Kirusi cha ukimwi ni cha RNA chenye genetic code 9 tu. Kirusi cha coronavirus nacho ni cha RNA na kina genetic codes 56.

Seli ya kirusi haina saitoplasm. Yaani hizo RNA au DNA zake zimehifadhiwa kwenye gamba (envelope) la protein. Kwa coronavirus gamba hili la protein ni la duara lenye miiba midogo midogo mingi (spike protein). Maji ya sabuni (soapy water) huweza kulisambaratisha (denature) gamba hili kwa urahisi na kukiua kirusi hiki. Ndiyo sababu ya kuwashauri watu kunawa mikono yao kwa sabuni mara kwa mara. Pia joto la nyuzi 45 hadi 56 C kwenye mazingira ya unyevunyevu huweza kulisarambaratisha gamba hili. Hii nayo ndiyo sababu ya tafiti mbali mbali duniani ambazo zimeweza kuonesha faida ya steam inhalation therapy ambao kwetu tunaita kujifukuzia.

Kwa kuwa virusi havina saitoplasm ili viweze kuzaliana zinahitaji kuingia kwenye seli za kiumbe kingine chenye saitoplasm. Hivyo zinaingia kwenye seli ya binadamu kwa lengo la kwenda kuzaliana. Kikishaingia kwenye seli ya binadamu genes ya virusi hivi huchukua kamandi ya maelekezo na usimamizi wa viwanda vya saitoplasm. Vinaamurishwa kufanya kazi ya kuzalisha virusi tu. Kazi zingine zinasitishwa. Hivyo seli zizovamiwa na virusi hivi zinageuzwa kuwa viwanda vya kufyatua virusi tu na vikishafyatuliwa vinavyamia seli zingine. Seli za askari wa mwili (immune cells - B lymhocytes, T lymphocytes, macrophages, Killer cells, cd4 cells etc) zinaingia vitani ambayo matokeo yake ni kifo au kupona.

3. Chimbuko la chanjo za SARS-CoV-2
Baada ya mlipuko mkubwa wa SARS (kiswahili chake Changamoto la Upumuaji) wa kirusi cha CoV-2 au coronavirus wa pili huko Wuhen, China mwezi Nov 2019 wahandisi mahiri wa vinasaba waliingia kazini kumchakata huyu kirusi. Hadi March 2020 wakawa wameweza ku decode the entire genetic code ya kiumbe hiki kidogo ambacho hadi wakati huo hakuna aliyekuwa anazijua hapa duniani. Mchina angeweza kukaa na king'amuzi hicho kwa siri peke yake maana ilikuwa ni uvumbuzi mkubwa wa siri ya maisha ya kirusi hiki. Lakini kwa upendo wa kipekee aliamua kuwasambazia bure maabara zote kubwa za genetic engineering ulimwenguni. Maabara hizi zilipokea kwa furaha ving'amuzi hivi na mara moja kuanza kucheza na vinasaba za kirusi hiki ili kupata dawa au chanjo ya kumwangamiza.

Bahati mbaya au nzuri zilijielekeza zaidi kwenye genetic code ya gamba la mdudu huyu - the spike protein genome. Ziliona hapo ndipo rahisi kummaliza mdudu huyu. Clinical trials zikafanyika haraka haraka. Ilikuwa ni fursa kwa tafiti zao za tiba kwa njia ya vinasaba zilizokuwa zimekwamishwa na FDAs zao kwa miaka mingi sasa kupewa ruhusa angalao ya dharura. Hadi kufikia December 2020 zikawa zimepata hiyo emergency approval na kuanza mass vaccination ya watu wote duniani kama phase IV clinical trial.

Cha kushangaza Mchina ambaye ugunduzi wake wa vinasaba ndiyo ulipelekea utengenezaji wa hizo chanjo, yeye chanjo yake haikutumia teknolojia hiyo. Yeye chanjo yake inatumia kirusi chote (the whole virus with its entire structure including the entire genome intact) kilichopunguzwa makali kama ambavyo zilivyo chanjo za magonjwa mengine tulizozizoea.

Chanjo hizi za wengine ni kama ifuatavyo:

- Pfizer na Modern: Hizi saitoplasma ya seli za binadamu inaingiziwa mRNA kuiamuru izalishe magamba (spike proteins) ya virus vya corona. Unapata kinga dhidi ya magamba yake na hivyo hataweza kuingia tena mwilini mwako kama ataendelea kubaki na gamba lile lile. Ndani ya muda mfupi imeonekana kwamba gamba la kirusi hiki ni kama la kinyonga. Hujibadilisha mara kwa mara kutegemea na mazingira. Kwa muda mfupi zaidi ya aina 7 ya magamba haya yamegundulika - kuna South Africa variant, UK variant, Brazil variant, na majuzi Kenya variant na kadhalika.

Chanjo hizi za mRNA ni ngumu kuzitunza kwani zinahitaji ubaridi wa -20 C kwa Moderna na -70 C kwa Pfizer.

- Johnson & Johson, AstraZeneca na Gamaleya (Spunik V from Russia):
Ili kutatua tatizo la uhifadhi, chanjo hizi zinatumia DNA adenoviruses zilizofanyiwa engineering kubeba ndani yake gene ya spike protein ya CoV-2. Tofauti kati yake ni aina za hizo adenovirus zilizotumika kama kibebeo. Ile ya Astra Zeneca inatumia kirusi cha mafua ya sokwe (chimpanzee flue virus). Ile ya Urusi ina viral vector mbili (Ad26 na Ad5). Ile ya J & J ina viral vector Ad26.

- Efficacy ya chanjo hizi kwa matokeo ya phase III clinical trials: Moderna 94%, Pfizer 95%, Gamaleya 91.4%, AstraZeneca 62%, Johnson & Johnson 62%.

4. Coverage ya chanjo huko ughaibuni:
Zoezi la chanjo huko ughaibuni na america lilianza mwanzoni mwa mwezi December 2020. Lilienga kuanza kwa wale waliokwenye hatari zaidi ya kupoteza maisha kwa gonjwa hili ambao ni wanaohudumia wagonjwa hawa mahospitalini, wazee wenye umri zaidi ya miaka 70 na wenye magonjwa hatarishi km kisukari, magonjwa ya moyo au figo au maini, saratani na ukimwi.

Hadi kufikia tarehe 4 March ni wastani wa asilimia 5 tu ndiyo walioweza kuchanjwa ndani ya muda huo wote wa miezi mitatu pamoja na hamasa kubwa iliyofanyika na inayoendelea kufanyika. Sababu kubwa ni wasi wasi walionao wananchi pamoja na baadhi ya wanasayansi wao kuhusu chanjo hizo zinazocheza na vinasaba za genes zao. Bado kuna vitu vingi havijajulikana kisayansi. Kwa mfano unaambiwa hata ukichanja lockdown, kuvaa barakoa na mambo mengine unaendelea nayo kama awali. Yaani hata hiyo efficacy yake hawaiamini.

Halafu wanaona kabisa licha ya kuchanja gonjwa hili badala ya kupungua huko kwao limekuwa likiongezeka. Kwa nini?
Vaccination coverage kwa baadhi ya nchi zao ni kama ifuatavyo:

USA 7.7%, Belgium 7.2%, Italy 7.8%, France 7.1%, Netherland 5.9%, Russia 3.7%, Bulgaria 3.5%, Sweden 8.1%, Germany 8.1%, Spain 8.6%, Portugal 8.8%, Greece 9.5%,

5. Huu upendo kwa nchi za Afrika umetokea wapi?:
Wakati kasi ya coverage ya chanjo kwenye nchi zao zimekuwa za kusuasua, sisi wametuandama tuchanjane haraka. Wametupa au kutuahidi kutupa chanjo bure zinazotosheleza kuchanja watu laki 5 kila nchi ya Afrika. Masharti ya chanjo hizi za bure ni kwamba zichanje watu wenye afya nzuri walio na umri wa miaka 18 hadi 45. Wasiwe na magonjwa mengine ye yote including morbid obesity. Wamediliki hata kutuamuru kuwa watu hawa wawe ni walimu na polisi wetu.

Kwa nini wanataka watu wa aina hii ndiyo tuwachanje wakati watu wa aina hii miili yao iko imara kukabili virusi vya corona kwa asilimia 99.9%?
Kwa mjanja atagundua kuwa wanataka kuwafanyia a phase IV clinical trial watu hawa ambayo matokeo yake yanaweza kuondoa wasi wasi walionao watu wao huko ughaibuni kuhusu hizi chanjo.

Wanatusubiri sisi tuchanjane. Hadi sasa nchi 10 za Afrika zimekubali 'msaada' huu na faster faster zimepelekewa hizo chanjo na wameanza kuchanjana.

Nchi inayokataa au kusuasua kupokea 'msaada' huu inaandamwa kinoma na inachukuliwa kama adui. Sisi hatujaukataa bali tumewaambia watupe muda wa wanasayansi wetu kufanya uchambuzi na utafiti. Loo ona mashinikizo tunayoyapata hadi kutoka kwa watu tunaowaheshimu sana. Tupeni muda kidogo. Uamuzi tutatoa bila kushinikizwa tuzitoe wapi na tumchanje nani.

6. Ushauri wangu: Tuangalie zaidi chanjo ya Sinopharm ambayo imeiwezesha China kuudhibiti vizuri sana ugonjwa huu.
Tunaomba version za wanasayansi wetu. Kama hakuna chanjo kutoka Afrika basi huakuna haja ya kupinga hizo chanjo.Miaka yote tumekuwa tukichanjwa chanjo ila ya corona tumejifanya tunajua huku hatuna ugunduzi wa dawa yoyote ya maana.
 
Yaani mnasema as if mtu anaenda tu kupata chanjo akiamua, kama vile mtu anaenda sokoni, mnashindwa kuelewa zinatolewa chanjo kwa prioritization, wazee na wale at risk ndio walianza kuwa vaccinated, sasa uhesabu hesabu yao hao wazee ni wangapi in total UK population?
 
Umezungumza kiutaalam Sana, shida ni hawa watu wa bavicha. Subiri uone
Kama bavicha ndiyo walileta corona na chanjo kaa hivyo hivyo,,
Ndiyo maana kwa baadhi ya nchi za Africa kuendelea ni ndoto,,toka uhuru mpaka sasa mnaongoza wenyewe mmeshindwa hata kutengeneza chanjo,, mtaendelea kulamba miguu ya watu weupe mpaka mtoke madarakani, maana hamjui hata kuongoza wananchi zaidi ya misafi tu na ubinafsi
 
Hili ndiyo tatizo. Yaani watu wanadhani elimu inapatikana kwenye kampuni ya wamarekani inayoitwa google badala ya shuleni na vyuoni. Wao ni ku google tu na cho chote watakachokipata huko google wanaamini ndiyo ukweli.
Hata walimu wa vyuo huwa wanampenda sana MR.GOOGLE.Vitabu vyote vipo google, yani chuo kikaizidi google we! umesomea wapi ndugu mbona unatia mashaka?
 
Back
Top Bottom