Ijue siri na sababu za malalamiko ya Teuzi kwa hoja za Udini katika Awamu hii ya Sita

Ijue siri na sababu za malalamiko ya Teuzi kwa hoja za Udini katika Awamu hii ya Sita

Last...
Mimi si mtu wa kubishana.
Tatizo linafahamika na viongozi wetu.

Zamani watu wakiogopa kusema kweli.
Leo mambo yote yako hadharani.

Agenda iko juu ya meza sasa ni wakati wa kusubiri.
Mzee achana na Mitandao, LEA WAJUKUU.
 
Mzee achana na Mitandao, LEA WAJUKUU.
Mkaruka,
Unapoleta mashambulizi katika maisha binafsi ni dalili kuwa umeghadhibika.

Hii inakuwa bahati mbaya kwetu sote kwako na kwangu.

Kwako kwa kukasirishwa na niliyoandika ambayo naamini sijakushambulia binafsi katika maisha yako lakini bahati mbaya nimekuchoma kwa kile nilichoandika.

Bahati mbaya kwangu kwa kuwa sikutarajia kwanza kukejeliwa kuwa sifai hapa ila nafaa katika ulezi wa wajukuu.

Pili kauli yako imenitia simanzi kwani nimeona umenitukana pasi na sababu.

Tujadiliane kwa heshima na adabu huu ukumbi ni mahali pa elimu si uwanja wa matusi.
 
Hizo ni historia za uislam Kilimanjaro chief sio historia za wachagga. Nilishakuambia ukitaka historia za uchaggan vipo vitabu vingi tu. Shida yako ni kutaka historia ya dini yako ndio iwe historia ya jamii. Hiyo ndio nakuambia wadanganye wavivu wenzio.
Kitali,
Pengine ni namna unavyotafsiri kitabu changu.

Hapa unaweza ukanieleza kipi nilichokosea na hapana sababu ya kuhamaki.

Mimi nimeandika historia ya maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama alivyosilimu na kuwa Muislam.

Akajenga msikiti na shule na ndiyo ikawa madrasa ya kusomesha Qur'an kijijini kwake Machame Nkuu.

Sheikh Rajabu Kirama akaenda Zanzibar akawaleta walimu wanne wawili akawapeleka Upare na wawili wakawa Nkuu.

Kuanzia hapo Uislam ukaanza kuenea Uchaggani.

Kuna mengi katika historia hii kufikia Sheikh Rajabu Kirama kuwa mtu maarufu Upare na Uchaggani kote.

Yote haya yapo kitabuni kwa ushahidi wa nyaraka na picha.

Sijui nini kimekukasirisha kiasi unanita mimi mvivu nk.

Nakuwekea picha ya msikiti mpya unaojengwa mahali Mzee Rajabu Kirama alipojenga msikiti wa kwanza Machame Nkuu zaidi ya miaka 90 iliyopita.

1677876225415.jpeg
 
Kitali,
Pengine ni namna unavyotafsiri kitabu changu.

Hapa unaweza ukanieleza kipi nilichokosea na hapana sababu ya kuhamaki.

Mimi nimeandika historia ya maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama alivyosilimu na kuwa Muislam.

Akajenga msikiti na shule na ndiyo ikawa madrasa ya kusomesha Qur'an kijijini kwake Machame Nkuu.

Sheikh Rajabu Kirama akaenda Zanzibar akawaleta walimu wanne wawili akawapeleka Upare na wawili wakawa Nkuu.

Kuanzia hapo Uislam ukaanza kuenea Uchaggani.

Kuna mengi katika historia hii kufikia Sheikh Rajabu Kirama kuwa mtu maarufu Upare na Uchaggani kote.

Yote haya yapo kitabuni kwa ushahidi wa nyaraka na picha.

Sijui nini kimekukasirisha kiasi unanita mimi mvivu nk.
Na sijawah kuona katika kusoma soma kwangu biographies mbalimbali iwe kwamba mtu anapinga maisha ya muhusika kwa mchango wake katika jamii.mleta hoja anabisha kuwa Rajab Kirama hakuyafanya hayo? Anabishia maisha binafs ya mtu na harakat zake? Nadhan kuna historia nying za watu wa kaskazini na ya Rajabu Kirama nayo mojawapo.sio kwamba mwandish amesema eti hakuna historia ya wachaga isipokuwa ya Rajab Kirama,ila na Ya Kirama katika harakat mbalimbal imo tena kwa ushahid wa nyaraka
 
Na sijawah kuona katika kusoma soma kwangu biographies mbalimbali iwe kwamba mtu anapinga maisha ya muhusika kwa mchango wake katika jamii.mleta hoja anabisha kuwa Rajab Kirama hakuyafanya hayo? Anabishia maisha binafs ya mtu na harakat zake? Nadhan kuna historia nying za watu wa kaskazini na ya Rajabu Kirama nayo mojawapo.sio kwamba mwandish amesema eti hakuna historia ya wachaga isipokuwa ya Rajab Kirama,ila na Ya Kirama katika harakat mbalimbal imo tena kwa ushahid wa nyaraka
Julai...
Historia yoyote nzuri ya Waislam itapingwa.

Inamchoma moyo anatamani kama Rajabu Ibrahim Kirama asingekuwapo na historia ya maisha yake isingeandikwa.

Baba yake Rajabu Kirama Muro Mboyo alimpa mmeshionari Bruno Gutman ardhi ajenge kanisa lake.

Watu hawa walikuwa marafiki wakubwa Kidia, Old Moshi na Gutman aliwabatiza Wachagga wengi ila Mboyo alimshinda hakutaka kutoka katika Upagani.

Ili kumfurahisha rafiki yake ndiyo akampa kipande cha ardhi ajenge kanisa.

Kanisa hili lipo hadi leo.
 
Mpeni salamu mama yenu kwamba 2025 tutampa salamu kwa vitendo kutoka baraza ka maaskofu Tanzania. Hapo akili itamkaa sawa...
Walisema waswahili "mkamia maji hayanywi", ulipaswa kutoa salam kwa jamaa zako mtaani kabla ya huyo ambae hata babu yako hatafikia hadhi yake "The Commander in chief", tuwe na ustaarabu wa kujizuia na hasadi za kitoto waafrika
 
Last...
Mimi si mtu wa kubishana.
Tatizo linafahamika na viongozi wetu.

Zamani watu wakiogopa kusema kweli.
Leo mambo yote yako hadharani.

Agenda iko juu ya meza sasa ni wakati wa kusubiri.

..lakini Waislamu mmezidi kuiunga mkono Ccm pamoja na kwamba haiwathamini.
 
Luz...
Fanya utafiti ndani ya Bunge la Tanzania uangalie udadi ya Wakatoliki dhidi ya madhehebu nyingine.

Kisha idadi ya Waislam.

Nakuhakikishia utapata mshtuko mkubwa sana.

Utajiuliza hii ni bahati mbaya au ni mikakati maalum?

Ukishajua ukweli utaona kichekesho kilichopo ati Waislam kulalamika kuhusu uchaguzi wa Suni katika serikali.

Kwa taarifa ni kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika inazunguka katika imani hizi mbili: Uislam na Ukristo.

Umuhimu wa Waislam na Wakristo umejikita kwanza katika ujumla wa wingi wao kuwa dini mbili kubwa.

Pili katika dini hizi mbili Waislam ndiyo wenye historia ya pekee katika kujikusanya kupambana na ukoloni.

Kanisa na viongozi wake hawakujitokeza kuunga harakati za uhuru.

Hii ni tofauti kubwa na Waislam.
Hili nishalieleza sana hapa kwa ushahidi.

Uhuru ulipopatikana uendeshaji wa serikali kwa sehemu kubwa ukawa mikononi mwa Wakristo kwa sababu ndiyo walioelimishwa na kanisa.

Kanisa halina tatizo wafuasi wake ndiyo wanaoendesha nchi hadi hivi sasa kwa mgao wa 80:20.

Kuna watu Waislam wanapodai haki ya kuwemo katika madaraka ya uongozi wa nchi kuna watu huja na hoja ya kuwasemea Wapagani.

Ukiwauliza Wapagani hao wametoka wapi?

Kulikuwa na chama cha siasa kilichokuwa na Wapagani wapigania uhuru?

Jibu ni kuwa hapakuwepo na kamwe hawatakuwapo.

Lakini hoja hii inapendwq sana ikidhaniwa inaweza kuwazuia Waislam jamii ambayo ikiongoza harakati za uhuru katika TANU kudai haki yao.
Kwa jinsi nilivyokusoma na kukuelewa ndugu Mohamed, inaonekana harakati za kupigania uhuru wa tanganyika kwa mujibu wa waisilamu ilikuwa ni uhuru kwa ajili ya uisilamu, bahati mbaya iliyotokea ni kwamba Nyerere aliushtukia huu mchezo hivyo akautengenezea dawa ila akaifucha akasubiri uhuru upatikane ndipo akaiachia.

Nashukuru kwa elimu hii sikuwahi KUFIKIRIA hivyo.
Na kwa hali ilivyo nadhani mna haja ya kukubali yaishe kwamba Nyerere aliwadhibiti sana kwa namna ambavyo ni ngumu sana kunasuka kama jamii ya kiisilamu.

Ukifanya sensa ya vyuo vikuu vinavyomilikiwa na kanisa hapa nchini ukalinganisha na idadi ya vyuo vikuu vinavyomilikiwa na waisilamu utagundua kuna pengo kubwa sana, maana hadi sasa chuo kikuu cha waisilamu kinachofahamika sana ni mum.

Kwa mantiki hiyo ningeomba acheni kufikiri wakristo wanapendelewa fikirini kwamba waisilamu hawajaandaliwa. Waombeni wafadhili wenu wajenge vyuo vikuu Kila mkoa pia waweke hela ya kufadhili watoto wa kiisilamu wasome bure ikibidi wapewe na ruzuku juu. Ili kuwapiku wakristo Kwa idadi ya wasomi.

Jambo lingine ni namna unavyomuongelea nyerere, yaani unamzungumzia kana kwamba ni kamtu tu ambako waisilamu walikaokota wakakaweka pale Kwa huruma zao. Ukweli ni kwamba waongoza harakati za kupigania uhuru walipokutana na Nyerere waliona hawana sifa hata nusu za kumkaribia hivyo ikabidi wasalimishe harakati zote kwake.
Na kuonyesha kwamba aliwazidi parefu ni namna alivyowageuka na kuwabana vilivyo, na ndiyo maana nakumbuka miaka ya nyuma kulikuwa na makongamano ya kupinga mfumo kristo Tanzania yakiratibiwa na mum redio na tv Iman na wanazuoni wa kiisilamu walikuwa wakifikia kumtaja Nyerere basi utasikia wanasoma dua ya kumlaani.
 
Mtaje sheikh walau mmoja aliyekula zile hela za Tegeta Escrow tukutajie wachunga kondoo wenye heshima kubwa walipewa ule mgao

Au ulikuwa bado uko primary
Mkuu hongera sana kwa kuwabana hawa mashoga, waambie mwaka huu mpaka wasilimu wote au wahame inchi waende kwa mashoga wenzao
 
Ozark,
Nilifanya mhadhara University of Iowa, Iowa City mwaka wa 2011 na nilipewa takwimu za CIA kuhusu ''Tanzania Religious Distribution.''

Takwimu hizi zinaonyesha kuwa Waislam ni ''minority'' Tanzania.
Jibu langu nililotoa mfano wake ni kama huo hapo chini:

"Mtu akikuwekea mbele ya macho yako fimbo iliyopinda na akaitangaza kote kuwa fimbo hiyo imenyooka jibu lake ili lieleweke vyema ni kuweka fimbo iliyonyooka pembeni ya fimbo iliyopinda.

Macho hayadanganyiki.
Clip imeonyesha kuwa Tanganyika ni nchi ya Kikristo.

Zanzibar haina ubishi kuwa ni nchi ya Kiislam lakini ili kunogesha kilichokusudiwa imewekwa picha ya kanisa.

Wamishionari wamefika Tanganyika miaka ya 1800 na kufuatiwa na wakoloni na wamewakuta Waislam na Uislam uko zaidi ya miaka 1000.

Hapa tunacheza na picha na sauti ya fimbo iliyonyooka dhidi ya fimbo iliyopinda.

Mmishionari Johann Krapf kafika Vuga kwa Chief Kimweri mwaka wa 1848 kamkuta anatawala raia Waislam na wanajua kuandika, kusoma na kuhesabu.

Tunaweka picha ya Kimweri kavaa kanzu, juba na kapiga kilemba yuko katika baraza lake anaamua kesi akiandika kwa herufi za Kiarabu.

Krapf kaukuta Uislam Zanzibar na kaukuta Uislam Milima ya Usambaa.

Wajerumani wamefika Kilwa wamewakuta wenyeji wake wote Waislam na kukutana na upinzani mkali kutoka kwa Waislam wakiongozwa na Hassan Omari Makunganya.

Tunaweka picha ya Msikiti Mkuu wa Kilwa na picha ya Makunganya aliyenyongwa na Wajerumani mwaka wa 1895.

Tunaweka pia picha ya mnara wa kumbukumbu ya Waislam wa Kilwa walionyongwa na Wajerumani kwa kunyanyua silaha kuipigania nchi yao.

Vita vya Abushiri na Wajerumani viliitikisa utawala wa Wajerumani.

Abushiri alinyongwa Pangani mwaka wa 1889.

Abushiri kabla ya kifo chake alifika Kalenga kwa Mtwa Mkwawa na kumsilimisha Mkwawa.

Mkwawa akachagua jina la Abdallah na akamfunza kusoma na kuandika.

Viongozi hawa wawili walikuwa maadui wakubwa wa Wajerumani.

Barua alizoandika Mtwa Mkwawa kwa herufi za Kiarabu zipo Mkwawa Museum, Kalenga.

Leo Manispaa ya Iringa ina misikiti 25 yote inasaliwa Ijumaa na Mkoa mzima una misikiti 80.

Zinawekwa picha ya Mtwa Mkwawa na kizazi chake katika utawala wa Wahehe hadi leo pamoja na picha za misikiti iliyoko Iringa.

Huu ndiyo urithi alioacha Mtwa Mkwawa aliyesilimishwa na Abushiri bin Salim.

Mwaka wa 1905 Vita Vya Maji Maji vikaanza dhidi ya Wajerumani hadi mwaka 1907.

Hapa kuna historia kubwa ya majemadari 67 wa vita hivi walionyongwa na kuzikwa katika kaburi moja la halaiki isipokuwa Nduna Abdulrauf Songea Mbano.

Inawekwa picha yake Nduna Abdulrauf Songea Mbano.

Historia yake inaelezwa kuwa huyu ndiye Songea Mbano ambae waandishi wa historia ya Tanganyika wanakwepa kuandika jina lake la Kiislam "Abdulrauf," kwa hofu ya kuidumisha historia ya Uislam Tanganyika.

Halikadhalika wanakwepa kuandika jina la mwanamke pekee aliyenyongwa na Wajerumani kwa kuwa mmoja kati ya majemadari wa vita ile Bi. Khadija bint Mkomanile.

Waandishi wa historia ya Tanganyika wanamtaja kwa jina moja tu "Mkomanile."

Wanataka kufifilisha historia ya vita hivi na Waislam.

Ikiwa tutakaa kimya bila kujibu clip kama hizi hakika dunia itaamini kuwa Tanzania ni nchi ya Kikristo.

Historia ya uhuru wa Tanganyika iligeuzwa ikawa historia ya Julius Kambarage Nyerere.

Historia ya TANU ikawa historia ya mtu mmoja.

Hili lilifanikiwa kwa kuwa tulikaa kimya lau kama walikuwapo wazalendo wenyewe walioupigania uhuru kwa hali na mali zao.

Sasa tueleze harakati za uhuru wapi zilianzia.
Tunaweka picha ya Dictionary of African Biography (DAB).

Kinawekwa kipande kifupi kinachomweleza Dr. Kwegyir Aggrey (1875 - 1927) kisha ndani ya Kamusi hilo hilo tunatoa na kumwekea mtazamaji wa clip yetu kipande kifupi cha Kleist Abdallah Sykes (1894 - 1949).

Wazalendo hawa waliotajwa ndani ya Kamusi hilo tunaeleza hawamo katika historia rasmi ya Tanganyika.

Mazungumzo kati ya Waafrika hawa wawili Dar-es-Salaam mwaka wa 1924 ndiyo yalisababisha Kleist kuunda African Association mwaka wa 1929 kisha kuunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) mwaka wa 1933.

Vyama vyote hivi viwili vilitawaliwa na Waislam.
Kwa nini ilikuwa hivi?

Swali hili atajibu mtazamaji.

Vyama hivi viwili ndivyo vilivyowasha moto wa utaifa kwa kuunda TANU mwaka wa 1954 kupigania uhuru wa Tanganyika Waislam wakiwa mstari wa mbele.

Tunaweka picha ya wanawake Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Tunaweka picha za masheikh walioongoza kupigania uhuru umoja Watanganyika.

Hawa wakaja na kauli mbiu: "Uhuru na Amani."
Kwa kuhitimisha tutauliza.

Huu wingi wa Wakristo Tanganyika umeanza lini?

Kwa nini madai haya hayakuwapo miaka yote na katika historia ya nchi hii wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika?

Iweje wingi huu uzuke ghafla miaka hii tena bila kufanya sensa na kuweka kipengele cha dini?

Huu Ukristo unaopigiwa chapuo leo nini sababu yake?

Hakuna nchi duniani iliyokombolewa kwa amani au kwa kupigana vita ikawa wapigania uhuru wake ni kutoka jamii ndogo yenye watu wachache.

Halikadhalika hakuna nchi iliyoingia katika kudai uhuru wake ikawa waliokuwa mstari wa mbele kudai uhuru ni watu kutoka jamii iliyokuwa haina uongozi katika wingi wa wananchi ndani ya harakati hizo.

Tafuta dunia nzima hili hutolipata."
Nilipomaliza kujibu ukumbi mzima ulikuwa kimya kabisa.

Mkuu wa African History Northwestern University, Jonathon Glassman alinifata na kuniomba hapo hapo twende chuoni kwake tukafanye mjadala kama huu.

Nilikubali mwaliko na nikazungumza Northwestern University katika Ukumbi wa Eduardo Mondlane.

View attachment 2534353
Northwestern University, Evanston Chicago​
Big up mzee wangu, hakika kila jema litalipwa na utalikuta kwenye mizani yako, naomba kama umeweka au bado basi uweke hizi habari na nyingine kwa ajili ya vizazi vijavyo, hawa jamaa wanadanganya sana vizazi vyetu

Kama tayari nielekeze jinsi ya kupata nami nisupply au nihifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo
 
Big up mzee wangu, hakika kila jema litalipwa na utalikuta kwenye mizani yako, naomba kama umeweka au bado basi uweke hizi habari na nyingine kwa ajili ya vizazi vijavyo, hawa jamaa wanadanganya sana vizazi vyetu

Kama tayari nielekeze jinsi ya kupata nami nisupply au nihifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo
Pye...
Kipo kitabu cha maisha ya Abdul Sykes nimeeleza yote unayosoma hapa.
 
Kwa jinsi nilivyokusoma na kukuelewa ndugu Mohamed, inaonekana harakati za kupigania uhuru wa tanganyika kwa mujibu wa waisilamu ilikuwa ni uhuru kwa ajili ya uisilamu, bahati mbaya iliyotokea ni kwamba Nyerere aliushtukia huu mchezo hivyo akautengenezea dawa ila akaifucha akasubiri uhuru upatikane ndipo akaiachia.

Nashukuru kwa elimu hii sikuwahi KUFIKIRIA hivyo.
Na kwa hali ilivyo nadhani mna haja ya kukubali yaishe kwamba Nyerere aliwadhibiti sana kwa namna ambavyo ni ngumu sana kunasuka kama jamii ya kiisilamu.

Ukifanya sensa ya vyuo vikuu vinavyomilikiwa na kanisa hapa nchini ukalinganisha na idadi ya vyuo vikuu vinavyomilikiwa na waisilamu utagundua kuna pengo kubwa sana, maana hadi sasa chuo kikuu cha waisilamu kinachofahamika sana ni mum.

Kwa mantiki hiyo ningeomba acheni kufikiri wakristo wanapendelewa fikirini kwamba waisilamu hawajaandaliwa. Waombeni wafadhili wenu wajenge vyuo vikuu Kila mkoa pia waweke hela ya kufadhili watoto wa kiisilamu wasome bure ikibidi wapewe na ruzuku juu. Ili kuwapiku wakristo Kwa idadi ya wasomi.

Jambo lingine ni namna unavyomuongelea nyerere, yaani unamzungumzia kana kwamba ni kamtu tu ambako waisilamu walikaokota wakakaweka pale Kwa huruma zao. Ukweli ni kwamba waongoza harakati za kupigania uhuru walipokutana na Nyerere waliona hawana sifa hata nusu za kumkaribia hivyo ikabidi wasalimishe harakati zote kwake.
Na kuonyesha kwamba aliwazidi parefu ni namna alivyowageuka na kuwabana vilivyo, na ndiyo maana nakumbuka miaka ya nyuma kulikuwa na makongamano ya kupinga mfumo kristo Tanzania yakiratibiwa na mum redio na tv Iman na wanazuoni wa kiisilamu walikuwa wakifikia kumtaja Nyerere basi utasikia wanasoma dua ya kumlaani.
The...
Umeandika kinyume cha ukweli.

Historia yote kwa ukweli na ukamilifu wake iko katika kitabu cha Abdul Sykes (1989).

Kuhusu mengine uliyotaja kuhusu Nyerere kuwadhibiti Waislam soma Bergen (1981), Sivalon (1992) na Njozi (2002).

Utajifunza mengi.
 
Ni rahisi sana adui wa Tanzania kupitia hapo trust me.
 
Na sijawah kuona katika kusoma soma kwangu biographies mbalimbali iwe kwamba mtu anapinga maisha ya muhusika kwa mchango wake katika jamii.mleta hoja anabisha kuwa Rajab Kirama hakuyafanya hayo? Anabishia maisha binafs ya mtu na harakat zake? Nadhan kuna historia nying za watu wa kaskazini na ya Rajabu Kirama nayo mojawapo.sio kwamba mwandish amesema eti hakuna historia ya wachaga isipokuwa ya Rajab Kirama,ila na Ya Kirama katika harakat mbalimbal imo tena kwa ushahid wa nyaraka
Sheikh huyu mimi cjaanza nae huku
 
Tangu Rais Samia aingie madarakani amefanya teuzi nyingi tu na katika teuzi hizo wapo watu wamekaa standby kuangalia majina ya Kizungu (isomeke Kikristo) na Kiarabu (isomeke Kiislamu) ili waone kuwa watu wanaoendana nao kiimani "wameula" zaidi au la!

Nataka nieleze sababu za hivyo:

1. Mosi, kuna sense of entitlement.
Kwa miaka mingi sana nchini tangu Uhuru mpaka leo hii, nafasi za Utumishi wa Umma na Serikali zimekaliwa zaidi na Wakiristo kuliko Waislamu. Teuzi nyingi kuanzia Nyerere hadi leo hii Rais Samia, teuzi nyingi zinakwenda kwa Wakiristo.

Hali hii imelalamikiwa sana na Waislamu kwa miaka mingi, kuwa, hili jambo lina ukakasi. Iweje teuzi ziende kwa watu wa mrengo mmoja tu kila wakati wakati nchi hii ni yetu sote, na watu wenye vigezo wapo pande zote? Majibu ambayo watu hawa wamekuwa wakipata ni kejeli, kuwa nyie hamjasoma, kuwa nyie mnaendekeza elimu ahera, lakini hoja yao hiyo siku hizi imekuwa proven wrong.

Hata ikafikia hatua hadi Sheikh Khalifa kutoa orodha ya Waislamu wasomi mamia kwa mamia ili kufuta propaganda kuwa waislamu wenye vigezo vya kutosha kuhudumu katika teuzi mbalimbali hawapo, lakini licha ya hivyo hoja hiyo imekuwa ikifumbiwa macho. Sasa leo, Samia licha ya bado kuendelea kuteua Wakiristo wengi zaidi kuliko waislamu lakini angalau kidooogo waislamu nao wanaonekanaonekana kwa mbali.

Hili limeshtua wale waliozoea kuona teuzi za mrengo mmoja, wanahaha, wamepandwa na ghadhabu, wanataka waendelee kuteuliwa watu wa imani yao kwa wingi uleule (over representation) kama zamani.

2. Sababu ya pili ni kuwa, Siyo kweli kuwa baadhi ya hawa wanaolalamikia udini katika teuzi hawajui kuwa Samia bado anateua Wakiristo wengi zaidi kuliko Waislamu.

Bali wanataka kumblackmail ili asije akazoea kuteuateua Waislamu. Wanampa meseji kuwa, ukijaribu kubadili status quo katika nchi hii na kuwapa nafasi watu wa imani nyingine katika Utumishi wa Serikali kwa wingi kama sisi basi tutakusagia kunguni kwa watu wa imani yetu ili upate wakati mgumu kisiasa.

Kwa hiyo hizi kelele kimsingi ni fitina ya kumchonganisha Rais na Wakiristo ili Rais aogope kuwapa Waislamu nafasi na kwa hiyo Status quo ya Wakiristo kuendelea kudominate Utumishi wa Umma na Serikali, uendelee kama ilivyokuwa tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza hadi leo.

3. Sababu ya tatu ni chuki tu, na ufia dini.

Islamophobia is real, kuna watu wanaamini kuwa, kwa kuwabagua watu wa dini nyingine na kuwapendelea watu wa dini yao ni kumfanyia Mungu Ibada!

Wapo watu makazini wakiona kuna wafanyakazi wanavaa hijabu, muda wa swala umefika wanaenda kuswali, au Salamu ya "Assalam Aleikum" imekuwa nyingi katika korido za ofisi wanaanza kuchukia, wanajenga hila mioyoni mwao na kibaya zaidi kuna baadhi wanakwenda mbali hadi ku collude na like minded people ili kuwaletea fitina wenzao n.k.

Enzi hizo wakati nasoma katika chuo kikuu kimoja hapa nchini, wanafunzi Waislamu waliomba chumba kimoja kilicho idle ili wafanye ibada wakazunguushwa mno, wengine wakawa wanapewa vitisho vya siri kuwa wawe makini na ajenda yao hiyo kwamba wachague chuo au dini (yaani ni kitisho cha kupigwa fitina hadi wafukuzwe chuo).

Lakini at the same time, kila siku jioni na siku za Jumamosi na Jumapili madarasa ya chuo hichohicho Wakiristo wameruhusiwa kuyatumia kusali na kuabudu. Umeona aina hii ya chuki, choyo na roho mbaya?

Ushauri wangu:
1. Watanzania tuachane na habari za kutaka upendeleo katika ajira na teuzi. Hii nchi ni yetu sote. Si vizuri kunung'unika watu wa imani nyingine pia wakipata fursa za kuhudumu katika nchi.

2. Lakini kama tunaona upendeleo wa dhahiri katika teuzi, hapo kweli tuseme na tupige kelele. Kuna wakati nchi hii Rais mmoja aliunda Baraza la Mawaziri la watu zaidi ya 20 akaweka Waislamu watatu. Sasa katika situation kama hiyo kweli hapo jamii nzima haipaswi kukaa kimya.

Hivyo hivyo leo hii Samia akiunda Baraza la Mawaziri akaweka Wakiristo watatu tu hata mimi sitokaa kimya. Tusiwe na double standard, kwamba teuzi zikifavour watu wetu tunanyuti, ila wengine wakianza kuchomoza basi tunakuja hapa JF kuanzisha nyuzi lukuki za udini. Hiyo siyo fair.

3. Tuzidi kuimarisha, Umoja, Amani na Mshikamano. Nchi hii Wakiristo are here to stay, Waislamu are here to stay. Yesu hakuoni mfuasi wake bora kwa kuwa mbaguzi na wala Mtume Muhammad hakuoni mfuasi wake bora kwa kuvunja amana za watu wote. Tupendeane mazuri.

Nawasilisha.
Hili bandiko lako mtu akilisoma akiwa na free mind atakuelewa sana. Ila sasa mtu akisoma huku tayari yuko katika kundi au fikra mojawapo ya ulizotaja basi atakupinga.

Yaani ili mama awaridhishe hao basi aendelee na utaratibu ule ule wa kuweka watatu katika 20 ndio kwao wataona sawa.
 
Kwa nyie waislamu sawa Lakin kwa wachagga wala hajulikani.
Kitali,
Nitakueleza kitu.

Kwa miaka mingi sana watu waliamini kuwa historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ni historia ya Julius Nyerere.

Nilipoandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes ndipo ilipojulikana kuwa baba yake Abdul, Mzee Kleist ndiye muasisi wa African Association 1929 na Abdul Sykes kadi yake ya TANU ni No. 3 na No. 2 ni ya mdogo wake Ally na ndiye aliyesanifu kadi na kuchapa kadi 1000 kutoka mfukoni kwake.

Ally Sykes ndiye aliyemwandikia Nyerere kadi yake No. 1 kama Territorial President.

Wakajua na mengine mengi mfano kuwa mipango yote ya safari ya Nyerere UNO 1955 ilifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu ndipo kilipokuwa kituo kikuu cha mikakati.

Mkusanyaji wa fedha za safari hiyo alikuwa Iddi Faiz Mafungo kadi yake ya TANU No. 24 na ndiye alikuwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) chama alichounda Kleist Sykes 1933 na Mweka Hazina wa TANU 1954.

Kwa nini historia hii haikuwa sehemu ya historia ya Nyerere na TANU?

Sababu ni kuwa Nyerere alikuwa kimya, wanahistoria pia walikuwa kimya na TANU yenyewe ilikuwa kimya.

Leo hawa wote niliowataja ni sehemu ya historia ya Tanganyika.

Rajabu Ibrahim Kirama leo ni sehemu ya historia ya Wachagga.

Shule na msikiti aliojenga Machame vyote vipo hadi leo na kizazi cha Waislam Kilimanjaro kinamfahamu na kila mwaka wanasoma khitma kubwa kumkumbuka.
 
62% hiyo umeitoa wapi?? Lini uliwahi kuulizwa dini yako? Nani alifanya sensa ya kujua Idadi ya Waislam Na Wakristo?
Wikipedia ni tovuti na hata wewe unaweza kuibadili tu.
Wikipedia ni tovuti reliable, hili liwekwe hivyo ukiweza kuwapinga kwa facts hakuna tatizo ila huwezi kuwapinga kwa blah blahs au kwa sababu za kiushabiki.
Weka facts zako ili uwakosoe kwani kuna tovuti haziwezi kuharibu credibility wanayokuwa wemeijenga kwa gharama,muda na maarifa.
 
Back
Top Bottom