Ijue siri na sababu za malalamiko ya Teuzi kwa hoja za Udini katika Awamu hii ya Sita

Ijue siri na sababu za malalamiko ya Teuzi kwa hoja za Udini katika Awamu hii ya Sita

Vitu vingine sio hata vya kulalamika

Sasa kweli ishu ya mtu kutosalimia Bwana Yesu asifiwe ndio itafsiriwe kuwa ni mdini?

Punguzeni lawama ambazo hazina msingi.
 
Siyo TEC imeleta udini kwa kubaniwa njia zao za wizi.


Na bado pesa zinazotoka serikalini, zitafinywa tu hivi karibuni.
Wenzako wanajua siri ya kufanya kazi na TEC na kufanyia kazi hoja zao ili kuleta maendeleo kwa wananchi we unafikiria yasiyofikirika.
Screenshot_20230827-130719.png
 
Wenzako wanajua siri ya kufanya kazi na TEC na kufanyia kazi hoja zao ili kuleta maendeleo kwa wananchi we unafikiria yasiyofikirika.View attachment 2730501
Huyo ni Rais mwana diplomasia.

Usicheze na Kikwete, ni Rais pekee duniani aliyeweza kuwakutanisha Marais wote wa USA nje ya USA kwa wakati mmoja.


Aliwakutanisha hapa George Bush, Clinton, Obama na Jimmy carter.

Haijawahi kutokea duniani.
 
Wahenga walisema,Mdharau mwiba umchoma,ilianza mzaa mzaa akakaa kimya,marehemu akatukanwa nchi nzima akakaa kimya,Pengine ilikuwa turufu yake Mwenyekiti,licha ya kwamba yapaswa kuheshimu "privacy" ya familia iliyopatwa na msiba,na pia kutetea heshima ya nchi kwa Marehemu aliyewahi kuwa Kiongozi wa nchi,

Mambo yakahania kwenye dini,akakataa kusalimia Wakristo kwa salamu ya Bwana Yesu asifiwe,au tumsifi Yesu kristo,mtangulizi wake haikuwa shida kwake alisalimia Assalamualaikum,Bwana Yesu asifiwe,Tumsifu Yesu Kristy,akaongezea na salamu za kabila zaidi ya ishirini alianza na amsindile,Subhai takwenya,na makabila mengine thelathini,

Athari yake tumeanza kuiona sasa udini umeingia,mkataba mbovu wa bandari unatetewa na Waislamu na kupingwa na Wakristu,hii ni "nightmare" ambayo hatutaki itokee katika maisha ya Watanzania,lakini yupo aliyekaa kimya matokeo yake bomu linalipuka,

Nini kifanyike,aingie kanisani na kusali nao hao aliokataa kuwasalimia Bwana Yesu asifiwe na Tumsifu Yesu kristo,aingie msikiti asali nao hao na kuwasalimia assalamualaikum,halafu aende bungeni akasalimie Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dini ya kweli ni pesa, hizo imani zenu hazina maana yoyote kwenye dunia hii. Umeharibu kabisa kwa kumtaja dhalimu kwenye huo uzi wako wa vitisho vya kidini.
 
Wakristo ni wadini sana, na kila inchi wanayoona wanaenda kushindwa basi huanzishwa fujo, yaani wako radhi inchi isitawalike kwa kuwa tu wao sio viongozi,

tena hili la kuwa mama wa kiislamu ndio amekuwa rais wa kwanza mwanamke tanzania kwa kweli wameumia sana

Nadhani hawapo sahihi
Mama wa kiislam kuwa rais ni sahihi mbele ya allah?au quran imechakachuliwa siku hizi,au ndo unafiki kwanza ndio imekuwa jihad?
 
Huyo ni Rais mwana diplomasia.

Usicheze na Kikwete, ni Rais pekee duniani aliyeweza kuwakutanisha Marais wote wa USA nje ya USA kwa wakati mmoja.


Aliwakutanisha hapa George Bush, Clinton, Obama na Jimmy carter.

Haijawahi kutokea duniani.
Sifa za kijinga, tulifaidika na nini kwa kukutanishwa huko?
 
Wahenga walisema,Mdharau mwiba umchoma,ilianza mzaa mzaa akakaa kimya,marehemu akatukanwa nchi nzima akakaa kimya,Pengine ilikuwa turufu yake Mwenyekiti,licha ya kwamba yapaswa kuheshimu "privacy" ya familia iliyopatwa na msiba,na pia kutetea heshima ya nchi kwa Marehemu aliyewahi kuwa Kiongozi wa nchi,

Mambo yakahania kwenye dini,akakataa kusalimia Wakristo kwa salamu ya Bwana Yesu asifiwe,au tumsifi Yesu kristo,mtangulizi wake haikuwa shida kwake alisalimia Assalamualaikum,Bwana Yesu asifiwe,Tumsifu Yesu Kristy,akaongezea na salamu za kabila zaidi ya ishirini alianza na amsindile,Subhai takwenya,na makabila mengine thelathini,

Athari yake tumeanza kuiona sasa udini umeingia,mkataba mbovu wa bandari unatetewa na Waislamu na kupingwa na Wakristu,hii ni "nightmare" ambayo hatutaki itokee katika maisha ya Watanzania,lakini yupo aliyekaa kimya matokeo yake bomu linalipuka,

Nini kifanyike,aingie kanisani na kusali nao hao aliokataa kuwasalimia Bwana Yesu asifiwe na Tumsifu Yesu kristo,aingie msikiti asali nao hao na kuwasalimia assalamualaikum,halafu aende bungeni akasalimie Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika sakata hili la bandari, udini kaupalilia mwenyewe pamoja na Serikali yake na chama hasa baada ya kukosa hoja za kujibu sintofahamu kwenye mkataba husika. Wamekuwa ni watu wa kurukaruka na kuokoteza vihoja visivyo na msingi. Wanatumia watu wasiyo na uwezo wa kuchanganua mambo kueneza chuki. Hoja zilizotolewa na TEC hazijibiwi hisipokuwa wanawatumia upande wa pili kuwashambulia tena si kwa kujibu hoja zao bali kulalamika, utadhani tangu nchi iwepo Marais wamekuwa wakitokea kwa wakiristo na huko kwingine hakujawai kutoa Rais. Ni kuhishiwa hoja ndiko kunapalilia udini. Mwanzoni mwa sakata ulianza kuchomoza Uzanzibar na ubara, lakini Sasa hivi naona udini umekolea. Najiuliza, hivi hawa Waarabu wanakuja kueneza dini, kugawa tende na nyama za ngamia au wanakuja kuwekeza? Kama siyo kwann upande wa pili unashupalia sana udini?
 
Huyo ni Rais mwana diplomasia.

Usicheze na Kikwete, ni Rais pekee duniani aliyeweza kuwakutanisha Marais wote wa USA nje ya USA kwa wakati mmoja.


Aliwakutanisha hapa George Bush, Clinton, Obama na Jimmy carter.

Haijawahi kutokea duniani.
Alikuwa kuwadi wa mafisadi wa kimataifa! Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Mbuga zetu walikuwa wananadi tu. Sijui ni kwani ni wakija wa aina hii wao ni kunadi maliasili tu!! Mwinyi Baba yake samia ndio mwanzilishi wa mauzo ya Loliondo! They too soft and, incompetent to be heads of states>
 
Wakuu inasemekana safari unapangwa kwenda Vatican kukutana na Baba mtakatifu Pope Francis


Je kwanini ziara hii inapangwa wakati huu?


Je ziara inalenga kuwaonyesha wawakilishi wa kiroho wa pope Tanzania si kitu?
Pope anawasilkiliza Ma Askofu wake na sio Rais wenu

Rais anapita ila MAASKOFU wapo
 
Wahenga walisema,Mdharau mwiba umchoma,ilianza mzaa mzaa akakaa kimya,marehemu akatukanwa nchi nzima akakaa kimya,Pengine ilikuwa turufu yake Mwenyekiti,licha ya kwamba yapaswa kuheshimu "privacy" ya familia iliyopatwa na msiba,na pia kutetea heshima ya nchi kwa Marehemu aliyewahi kuwa Kiongozi wa nchi,

Mambo yakahania kwenye dini,akakataa kusalimia Wakristo kwa salamu ya Bwana Yesu asifiwe,au tumsifi Yesu kristo,mtangulizi wake haikuwa shida kwake alisalimia Assalamualaikum,Bwana Yesu asifiwe,Tumsifu Yesu Kristy,akaongezea na salamu za kabila zaidi ya ishirini alianza na amsindile,Subhai takwenya,na makabila mengine thelathini,

Athari yake tumeanza kuiona sasa udini umeingia,mkataba mbovu wa bandari unatetewa na Waislamu na kupingwa na Wakristu,hii ni "nightmare" ambayo hatutaki itokee katika maisha ya Watanzania,lakini yupo aliyekaa kimya matokeo yake bomu linalipuka,

Nini kifanyike,aingie kanisani na kusali nao hao aliokataa kuwasalimia Bwana Yesu asifiwe na Tumsifu Yesu kristo,aingie msikiti asali nao hao na kuwasalimia assalamualaikum,halafu aende bungeni akasalimie Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ni mpumbavu na upumbavu wake akili zake nyepesi sana
 
La udini Rais wetu amelikorogaje,,wapi, kivipi
Ngoja nikujibu hivi, na siyo vile unavyotegemea wewe.
Hata kama hakulenga/hakutegemea matendo yake katika jambo hili la Bandari kugeuka na kuwagawa waTanzania katika makundi; baadhi wakifuata tu kundi la udini wao kwa vile rais ni wa dini yao, au huko tunakotafuta kushirikiana nako wanatambuliwa na baadhi ya watu kuwa ni wa dini fulani, ni wazi sasa ni lazima atambue kuwa udini ni sehemu ya matokeo ya matendo yake hayo, kwa hiyo ni wajibu wake, tena mkubwa sana kulishughulikia hilo kama tatizo lililojitokeza sasa.
Yeye ananyamaza, kama haoni lolote! Hapo wewe hulioni tatizo hilo? Au tuseme sasa anasubiri mpambano wa haya makundi ya dini ndiyo yamwondolee tatizo la msingi alilo liasisi yeye?
Tuanze kuchinjana, atakayebaki kasimama, ndiye atakayekuwa upande wa rais, iwe kuendelea na mkataba wa bandari, au kuukata huo mkataba?

Wewe hapo ulipo huoni kuwa jambo alilolianzisha rais limekuwa ndicho kichocheo kikubwa sasa kwa mfarakano wa waTanzania? Wewe hilo hulioni kabisa?

Na kwa bahati mbaya sana, huyu siyo rais mwenye uwezo wa kuwaunganisha wananchi, kwa hiyo tutegemee mfarakanyo huu kuzidi kuongezeka wakati wote yeye akiwa madarakani.
 
Sijui Hayati Rais Magufuli alilala wapi alipotembelea Morogoro kufungua soko la kingalu,ila Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipotembelea Morogoro na Mkoa wowote alilala Uaskofuni wa Kanisa Katoliki la Roma.
Tabora Magufuli aliwahi kulala jimboni
 
Huyo ni Rais mwana diplomasia.

Usicheze na Kikwete, ni Rais pekee duniani aliyeweza kuwakutanisha Marais wote wa USA nje ya USA kwa wakati mmoja.


Aliwakutanisha hapa George Bush, Clinton, Obama na Jimmy carter.

Haijawahi kutokea duniani.
Maajabu ya nchi yetu ni kama haya. Mtu huyo huyo mmoja, mwenye kichwa kilekle kimoja anachotumia kufikiri na kutafakari mambo mbalimbali, ambayo mara zote yanapingana yenyewe.
 
Huyo ni Rais mwana diplomasia.

Usicheze na Kikwete, ni Rais pekee duniani aliyeweza kuwakutanisha Marais wote wa USA nje ya USA kwa wakati mmoja.


Aliwakutanisha hapa George Bush, Clinton, Obama na Jimmy carter.

Haijawahi kutokea duniani.
Hata sijui nachekea nini ila nimejikuta nacheka tu[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Bwana Yesu asifiwe ni zaidi ya salamu, hili jina saa nyingine likitajwa na mtu asiye na mamlaka nalo huleta uharibifu kwenye ulimwengu wa kiroho. Kuepukana na hii kadhia ni bora kutokulitaja tu.
 
Back
Top Bottom