Tetesi: Ijue siri ya muhitimu wa UDSM kujiua.

Tetesi: Ijue siri ya muhitimu wa UDSM kujiua.

mwanafyale

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2010
Posts
1,641
Reaction score
538
UPDATES: Kijana Aliyejiua Mwanza Alikuwa na Pesa, Alizidiwa na Stress*

Na Blogu ya Jamii, Mwanza

Saa chache baada ya kijana aliyejiua Mwanza, marafiki wa karibu wameshangazwa na polisi Mwanza kushindwa kufuatilia ukweli wa sababu za kijana aliyejiua katika jengo la Rock City Mall na kutaja tu masuala ya ajira.

Sasa ukweli kamili umeanza kujitokeza baada ya marafiki wa karibu kumueleza marehemu kama mtu ambaye chuoni hakuwa na mambo ya mabinti.

"Ila mwaka wa mwisho akawa na mpenzi, akazama sana katika mapenzi," ameeleza rafiki yake mmoja akihofia kutaja jina asihusishwe na masuala ya upelelezi.

Kama miezi miwili iliyopita inaelezwa baada ya marehemu kupata dili flani kikazi na kusafiri kwa muda, aliporejea alipata sms kutoka kwa mpenzi wake kuwa ameshaolewa na wasijuane tena.

"Kusema ajira ni kuzuga tu, jamaa alichanganyikiwa na hilo penzi lake la kwanza na tangu aambiwe kaachwa kila kazi anayofanya akipata hela analewa sana sana.Tulimuonya hakuelewa," aliongeza rafiki huyo akishauri ni vyema kwa sasa taasisi mbalimbali zikaweka vitengo vya ushauri wa mahusiano, vijana wengi mahusiano yanawamaliza.

"Pale alipolazwa polisi akionekana mlevi tu kwanza alikuwa na hela anakazi zake mwenyewe alikuwa anapata kuendesha maisha yake, kwa hiyo issue sio ajira, lakini polisi wangekuwa na washauri wa kisaikolojia huyu kijana wangemsikiliza na kumweka kwenye tiba maalum na kumwokoa na yaliyokuja kumkuta, jamii pana ina wajibu wa kufanya," aliongeza mmoja wa marafiki zake wakiwa na huzuni eneo la Furahisha.

__Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe_
 
Mki ambiwa msi wabane bane watoto wenu ndo ivi sa mapenzi wana yajulia ukubwani
udakutz_-20181218-0001.jpeg
 
Najua umeandika hivi kwanini, aliyekutuma mwambie umetukuta tuna akili, ila jua maisha ni magumu
Wanakumbuka jamaa aliyejichoma moto mbele ya ofisi za serikali kuu Tunisia na kilichofuatia nchi nzima baada yake.
Wajanja sana matukio ya namna hii yana nguvu sana hizo damu huwa zinafungua nguvu za ziada za mapambano ya kudai haki.
 
Tatizo ajira acha kutulisha maneno
Kwa wabongo IQ zetu ziko ICU! Kwa hiyo mnaona kisa cha kujiua kikiwa ni ukosefu wa ajira kama mnavyotaka ndiyo nini kitatokea? Pengine mngejikusanya kama elfu tatu hivi mjiue ndiyo ingejulikana kweli mna shida ya ajira.
 
Mm nilijiuliza hela ya kulewa alikuwa anatoa wapi yani huna ajira unapataje nguvu za kulewa kweli kama mapenzi hapo yaweza kuwa kweli.
 
Mimi siungi mkono kuwa amejiua sababu ya maisha magumu, pia sikuungi mkono wewe unaposema wabongo uwezo watu wa kufikiri ni mdogo, wewe husikiagi mtu ameacha ujumbe kuwa kajiua sababu ya kitu fulani? Au wewe ulitaka wote waliojiua sababu ya mapenzi nao wangekutana thelathini na kujiua pamoja ndo uamini, maisha ni magumu kwa mtu na mtu,kwani huko nyuma hatukuwa na watu waliojiua sababu ya maisha?tatizo langu kwako pale unapohoji uwezo wa kufikiri wa mtu
Kwa wabongo IQ zetu ziko ICU! Kwa hiyo mnaona kisa cha kujiua kikiwa ni ukosefu wa ajira kama mnavyotaka ndiyo nini kitatokea? Pengine mngejikusanya kama elfu tatu hivi mjiue ndiyo ingejulikana kweli mna shida ya ajira.
 
Mm nilijiuliza hela ya kulewa alikuwa anatoa wapi yani huna ajira unapataje nguvu za kulewa kweli kama mapenzi hapo yaweza kuwa kweli.
Unajua gongo ya buku unakunywa mpaka unajinyea?
 
UPDATES: Kijana Aliyejiua Mwanza Alikuwa na Pesa, Alizidiwa na Stress*

Na Blogu ya Jamii, Mwanza

Saa chache baada ya kijana aliyejiua Mwanza, marafiki wa karibu wameshangazwa na polisi Mwanza kushindwa kufuatilia ukweli wa sababu za kijana aliyejiua katika jengo la Rock City Mall na kutaja tu masuala ya ajira.

Sasa ukweli kamili umeanza kujitokeza baada ya marafiki wa karibu kumueleza marehemu kama mtu ambaye chuoni hakuwa na mambo ya mabinti.

"Ila mwaka wa mwisho akawa na mpenzi, akazama sana katika mapenzi," ameeleza rafiki yake mmoja akihofia kutaja jina asihusishwe na masuala ya upelelezi.

Kama miezi miwili iliyopita inaelezwa baada ya marehemu kupata dili flani kikazi na kusafiri kwa muda, aliporejea alipata sms kutoka kwa mpenzi wake kuwa ameshaolewa na wasijuane tena.

"Kusema ajira ni kuzuga tu, jamaa alichanganyikiwa na hilo penzi lake la kwanza na tangu aambiwe kaachwa kila kazi anayofanya akipata hela analewa sana sana.Tulimuonya hakuelewa," aliongeza rafiki huyo akishauri ni vyema kwa sasa taasisi mbalimbali zikaweka vitengo vya ushauri wa mahusiano, vijana wengi mahusiano yanawamaliza.

"Pale alipolazwa polisi akionekana mlevi tu kwanza alikuwa na hela anakazi zake mwenyewe alikuwa anapata kuendesha maisha yake, kwa hiyo issue sio ajira, lakini polisi wangekuwa na washauri wa kisaikolojia huyu kijana wangemsikiliza na kumweka kwenye tiba maalum na kumwokoa na yaliyokuja kumkuta, jamii pana ina wajibu wa kufanya," aliongeza mmoja wa marafiki zake wakiwa na huzuni eneo la Furahisha.

__Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe_
Uwa nikitazama crime and Investigation uwa nina conclude TZ kuna kesi nyingi polisi uwa wana conclude kuwa watu wamejiua au kufa kwa bahati mbaya wakati wameuawa. Narudia tena kuna kesi nyingi watu uwa wana get away with murder
 
Back
Top Bottom