Ijumaa Kuu na katazo la kula nyama

Naombeni anaelijua andiko linalokataza wakristo Kula nyama siku ya Ijumaa kuu. Najua ni suala la kiimani,lakini msingi wa Imani ya kikristo,ni Biblia,hivyo tujuzane hilo andiko liko kitabu gani ndani ya Biblia

 
hapo haijakaa sawa, KUHENZI ! Bora wangesema tufunge tusile kabisa siku hiyo. Mi nala tena kitimoto plus
haina shida hiyo sio amri ya mungu ni amri ya kanisa tu! haina kuasi! ni kama sheria za nchi tu tunajiwekea wenyewe
 
Unachekesha sana we mtu. Unamaanisha kama unamsiba usile chakula kuzuri. Kuna watu leo hata mida hii wanakunywa mipombe lakini eti nyama hawali
Hupaswi kula vinono siku ya leo.Mwiko kabisa.Hao wanaobugia "mipombe" leo nao ni wahuni kabisa.
 
Ijumaa kuu sio katazo la kutokula nyama tu ata kufanya mapenzi au tendo la ndoa hairuhusiwi.
 
Hivi itakuwaje siku ukikutana na Yesu,halafu akakwambia mimi sikusulubishwa bali Mungu aliniepusha na mateso nikapalizwa mbinguni?
 
Naombeni anaelijua andiko linalokataza wakristo kula nyama siku ya Ijumaa kuu.

Najua ni suala la kiimani, lakini msingi wa Imani ya kikristo ni Biblia, hivyo tujuzane hilo andiko liko kitabu gani ndani ya Biblia.
Issue ya kutokula nyama ni upagani tu wala sio Ukristo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…