Ijumaa ya leo ikukumbushe tu Sabato ni Jumamosi

Ijumaa ya leo ikukumbushe tu Sabato ni Jumamosi

Haa usinielewe vibaya hiyo sikusema ni mwanzo wa sabato, badala nilisema ni moja ya sababu ya wayahudi kuitunza siku ya sabato jumamosi (yaani kama kumbukumbu ya kukombolewa kwao toka misri utumwani). sasa nikakuuliza ni mfuasi wa kristo au wa dini ya kiyahudi bado ? Mpaka unganganie sabato iliokomeshwa na Mungu mwenyewe na kutangazwa kama ilikuwa ni kivuli cha mambo ya kale. '(KIVULI HAKIVALISHWI SUTI JOANNAH)

Kimsingi ziko sababu tatu (3) za
Kwa nini wayahudi walishika na wanaishika sabato.

Wayahudi huishika sabato kwa sababu tatu kama ndiyo msingi wa amri ya kupumzika:


Sababu ya kwanza ishaelezea huko juu.

Sababu ya pili ni kukumbuka siku alipopumzika Mungu baada ya kumaliza kazi ya uumbaji; kama tusomavyo katika kitabu cha Kutoka 20:9-11 “Siku sita fanya kazi lakini siku ya saba ni sabato ya Bwana-usifanye kazi yoyote, maana kwa siku sita bwana alifanya mbingu na nchi, akastarehe siku ya saba.” Vile vile unaweza kusoma kitabu cha Mwanzo 2:3.

Sababu ya tatu na mwisho ni kwamba sabato ni alama ya kwamba Mungu aliliteua taifa la Israeli kuwa mali yake. Kama tunavyosoma katika kitabu cha Kutoka 13:13 “Hakika mtazishika sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote, ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi.”

JITAIDI USIELEWE MAMBO NUSUNUSU.
Mimi Ni mfuasi wa Mungu ndio maana natetea kuhusu kufuata amri zake na kuzitunza, Hakuna sehemu Mungu amebatilisha Sabato ...Hakuna amendment ya amri kumi Hakuna!Amri zitabaki kuwa kumi na amri mpya iliyotolewa katika agano jipya Ni UPENDO basi.
 

Je, Mungu alijua kuwa kuna taasisi inayompinga ambayo ingejaribu kufanya badiliko hilo?​

“Naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.” Dan. 7:25.

Taasisi hii ingediriki kubadili majira (muda) aliyopanga Mungu pamoja na Sheria zake. Zingatia kuwa “atanena maneno kinyume chake Aliye juu.”
1649977239264.png

1649977262992.png

1649977292435.png
 
Daah yaani hapa kailezea fresh Ila watabisha...Unajua watu Ni wavivu kutafuta ukweli Ila Kuna vitu vingi Sana tunafanya ambavyo tunaenda ndivyo sivyo....@ Beyond the infinity
KUSOMA VITABU KUNAFAIDA KUBWA SANA....
ONA HII
👇
👇
👇
..HII NI KATEKISIMU YA WAKATOLIKI WAMEJIELEZA WAZI

SHIDA YA WAKATOLIKI NI KWAMBA HAWASOMI HATA VITABU VYAO NDIYO MAANA WANADANGANYWA KIRAHISI..
View attachment 2188967
 
Mpaka unganganie sabato iliokomeshwa na Mungu mwenyewe na kutangazwa kama ilikuwa ni kivuli cha mambo ya kale. '(KIVULI HAKIVALISHWI SUTI JOANNAH)
tuangalie kama kweli Paulo alibadilisha sabato. Je ni kweli kwamba Paulo aliibadilisha sabato? Au yeye Paulo hakutunza sabato? Kwani desturi yake ilikuaje?

“Na Paulo kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu.” Matendo 17:2

Wengine bado watasema, “hamna alikutana na Wayahudi pekee siku ya sabato, lakini Wayunani alikutana nao Jumapili.”
Je ni kweli kwamba Paulo hakukutana na watu wa mataifa siku ya sabato? Au Je alikutana nao siku ya Jumapili?

“(Paulo) Akatoa hoja zake katatika sinagogi kila sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani.” Matendo 18:4

Wayahudi walipomshitaki Paulo, wakidai amevunja sheria. Je Paulo mwenyewe alisemaje? Aliposingiwa kuwa amevunja sheria Paulo Alisema.

“Ila neno hili naungama kwako ya kwamba kwa Njia ile ambayo waiita uzushi, ndivyo ninavyomwabudu Mungu wa baba zetu, nikiyaamini yote yanayopatana na torati na yaliyoandikwa katika vyuo vya manabii.” Matendo 24:14

Kwa hiyo Paulo aliiamini torati na manabii, na tofauti kati yake na Wayahudi ilikuwa ni imani ya Yesu, na siyo sheria au torati. Kwa hakika Paulo mwenyewe alipojitetea juu ya shitaka la kuvunja shelia alisema.

“…Mimi sikukosa neno juu ya sheria ya Wayahudi…sikuwakosa Wayahudi neno, kama wewe ujuavyo sana.” Matendo 25:8, 10

Hata walipomfikisha Rumi, Paulo aliendelea kusema wazi kuwa hajakosa katika sheria yoyote ile, alisema.

“…Ndugu zangu, ingawa sikufanya neno kinyume cha watu wetu wala neno lililopingamana na desturi za baba zetu, nalitiwa katika mikono ya Warumi, hali nimefungwa, tokea Yerusalemu.” Matendo 28:17
 
Mbali na yote, nashukurigi sama mola we Catholics hatujawahigi kutikiswa na lolote[emoji23][emoji23] sisi amani tunazo. Ila wap wanateseka juu yetu. Haya kazi iendelew

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
“Swali-Siku ya Sabato ni ipi?

Jibu-Jumamosi ni siku ya Sabato.

Swali-Kwanini tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi?

Jibu-Tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi kwa sababu kanisa la katoliki, katika balaza la Laodikia (364 B.K.), liliihamisha kutoka Jumamosi kwenda Jumapili.

Swali-Kwanini kanisa la katoliki liliweka Jumapili badala ya Jumamosi?

Jibu-Kanisa liliweka Jumapili badala ya Jumamosi, kwa sababu Kristo alifufuka kutoka kwa wafu

Jumapili, na Roho Mtakatifu aliwashukia Mitume Jumapili.

Swali-Kwa mamlaka gani kanisa liliweka Jumapili badala ya Jumamosi?

Jibu-Kanisa liliweka Jumapili badala ya Jumamosi kwa ukamilifu wa ule uwezo wa Uungu ambao Yesu Kristo aliutoa kwake.” –

The Convert Catechism of Catholic Doctrine, Peter Geiermann, C.SS.R., (1946), p 50
 
  • Thanks
Reactions: Ilu
“Swali-Siku ya Sabato ni ipi?

Jibu-Jumamosi ni siku ya Sabato.

Swali-Kwanini tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi?

Jibu-Tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi kwa sababu kanisa la katoliki, katika balaza la Laodikia (364 B.K.), liliihamisha kutoka Jumamosi kwenda Jumapili.

Swali-Kwanini kanisa la katoliki liliweka Jumapili badala ya Jumamosi?

Jibu-Kanisa liliweka Jumapili badala ya Jumamosi, kwa sababu Kristo alifufuka kutoka kwa wafu

Jumapili, na Roho Mtakatifu aliwashukia Mitume Jumapili.

Swali-Kwa mamlaka gani kanisa liliweka Jumapili badala ya Jumamosi?

Jibu-Kanisa liliweka Jumapili badala ya Jumamosi kwa ukamilifu wa ule uwezo wa Uungu ambao Yesu Kristo aliutoa kwake.” –

The Convert Catechism of Catholic Doctrine, Peter Geiermann, C.SS.R., (1946), p 50
Shukraaan kwa kuwajibu mkuu. Mimi wala siwezi tumia nguvu zangu kuwaelezea yote haya. Tupewe tuzo ya civilization katika dini. Sisi hatujawahi kaa tukiwafikiria ila wao daima wanatuwazia sisi. Sijawahi jiumiza juu yao

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: Ilu
Hivyo Yesu mwenyewe alikuwa anasali siku gani? Hakuna hata sehemu moja kwenye biblia inayosema yesu aliingia hekaluni kuabudu siku ya kwanza ya juma (jumapili) bali biblia inasema Yesu aliingia hekaluni kusali siku ya sabato (jumamosi) kama ilivyokuwa desturi yake na desturi ya wayahudi (Yesu ni myahudi kwa kuzaliwa). Nitaftutie andiko lolote kwenye biblia ambapo Yesu au Mungu alihalalisha siku ya ya jumapili (siku ya kwanza ya juma) kuwa ndio siku ya kumuabudi Mungu wa mbinguni. MITUME WOTE NA WAKRISTO WA KWANZA WALIKUWA WASABATO (walisali siku ya sabato kama ilivyoamriwa kwenye torati ya Musa aliyopewa na Mungu mwenyewe ikiwa imeandikwa kwenye mbao za Mawe). Hakuna wakatyi wowote ambapo Mungu wa mbinguni alibadilisha siku ya kumuabudu.
Wewe jamaa kuwa mwelewa basi,Yesu kabla ya ufufuko wake alisali siku ya sabato km Myahudi mwingine yeyote, ilikuwa ni desturi yao, kulikuwa hakuna Kanisa la Jumapili,Lkn kwa kufufuka kwake siku ya kwanza ya juma yaani Jumapili ndio inatufanya tusherehekee siku hiyo Ufufuko wake hivyo kila Jumapili ni Pasaka ndogo, Ufufuko wa Yesu Kristo ni kitu kikubwa sana kuliko hiyo sabato mnayoing'ang'ania.Hata hivyo Yesu hakuwa Msabato km ninyi bali alifuata taratibu za dini ya Kiyahudi,ili kutimiza taratibu za Agano la kale na ili kuwapata watu ambao aliwahubiria Neno la MUNGU.Hivyo sasa hivi hatuishi kadiri ya Agano la kale Bali kadiri ya Agano jipya maana Agano jipya ni Kuu kuliko Agano la kale, rejea Waebrania 8:8-13.
 
kwahio siku ya sabato hutakiwi kufanya kazi yoyote?
Yesu aliwashushua hao wanaojidai sabato ndiyo msingi, akamponya mgonjwa. Hiyo yote kuwakomesha kuwaonyesha, kwenye Hilo Mungu yupo flexible, haiwezekani mnyama atumbukie kwenye shimo, usimuokoe kisa sabato, au usiwanyweshe maji kisa Sabato,

Huu ufarisayo na usadukayo upo mpaka kizazi cha dot com.

Wasabato wanawake wasisuke, waafrika hao, kina wazungu minywele hiyo, yaani Mie nawakubali wazee wa Mila. Hizi dini zilizokuja na merikebu, baguzi na zinanyanyasa na kunyanyapaa Sana!

Dini zihubiri upendo, Amani na matumaini n.k
 
1: Kwa sababu Paulo alikuwa anaongea na watu wa kanisani wanaojua maandiko. Hizo tofauti kati ya siku na siku ni siku ambazo hazinauhusiano na Mungu alivyoelekeza. Maana hapo nazungumzia mtu hivyo hizo tofauti ni nje ya maagizo ya Mungu. Ndio maana na Mimi nimemwambia siku ya jumatano huwa nasalikama mtu na sihukumu anayesali jumanne, au pia tunasali jumapili asubuhi. Hizo zote hazina uhusiano na agizo la Mungu la sabato.

2: Ukisikia kitu kwenye Biblia kinaitwa kivuli. Tambua kimeanza baada ya dhambi kuingia duniani. Mfano mfumo wa kafara, na sabato nyingi vivuli duniani.

Hapa tunajadili sabato ya week ambayo IPO kabla ya wayahudi kwa kauli ya Yesu kuwa ilianzishwa kwa ajili ya mwanadamu. Hivyo andiko hilo halihusiani na agizo la sabato ya wiki maana sio kivuli cha yajayo Bali ni ukumbusho wa yaliyopita.

Mkuu vipi kuhusu sheria ya kutokula nguruwe nayo ni kivuli cha mambo yajayo?
 
Yesu aliwashushua hao wanaojidai sabato ndiyo msingi, akamponya mgonjwa. Hiyo yote kuwakomesha kuwaonyesha, kwenye Hilo Mungu yupo flexible, haiwezekani mnyama atumbukie kwenye shimo, usimuokoe kisa sabato, au usiwanyweshe maji kisa Sabato,

Huu ufarisayo na usadukayo upo mpaka kizazi cha dot com.

Wasabato wanawake wasisuke, waafrika hao, kina wazungu minywele hiyo, yaani Mie nawakubali wazee wa Mila. Hizi dini zilizokuja na merikebu, baguzi na zinanyanyasa na kunyanyapaa Sana!

Dini zihubiri upendo, Amani na matumaini n.k
utumwa upo kila mahali mkuu ni mtu mwenyewe ndio mwenye maamuzi ya kujinasua, mbali na hizi dini zilizokuja kwa meli hata imani za mababu zinamambo flani ya ki-utumwa pia.

unachukua mazuri yanayokufaa (kmf. mafundisho ya namna bora ya kuishi na jamii) unawaachia mabaya (kmf. masharti yasiyo na msingi wowote)
 
utumwa upo kila mahali mkuu ni mtu mwenyewe ndio mwenye maamuzi ya kujinasua, mbali na hizi deni zilizokuja kwa meli hata imani za mababu zinamambo flani ya ki-utumwa pia.

unachukua mazuri yanayokufaa (kmf. mafundisho ya namna bora ya kuishi na jamii) unawaachia mabaya (kmf. masharti yasiyo na msingi wowote)
Kweli kabisaaaah!
Nilikuwa na boss Polish, mzungu, kipindi Fulani hakuwa na dini wala dhehebu, Ila alikuwa na wema uliopitiliza, hajui biblia, kurani wala Buddha Ila alikuwa mwema Sana.
Hakasiriki, anaongea facts, Hana unafiki sijui fitina za kumsema mtu pembeni hadhulumu, alikuwa mtu wa haki na msaada Kwa wote alioweza kuwafikia.

Sijui huko aliko Ka mzima au alishatangulia mbeleni. Mungu hawezi kuacha mtu kama Yule kumuingiza katika ufalme wake.
 
Wala msiache kukusanyika kama ilivyodesturi ya watakatifu.

Asiyefanya kazi na asile

Siku sita Fanya kazi lakini siku ya saba ni SABATO ya Bwana Mungu wako.

Ambao wanapuuza agizo la sabato ndio wako kwenye kifungo.
Maana suala la kumuabudu Mungu linajulikana. Na kwa hekima zake akatenga siku nzima ukae ukitafakari ukuu wake.

Kupinga agizo hili la kifalme ni kumuonyesha dharau Mungu na kuyilia shaka uwezo wake na maamuzi take
Ukianza fikiri kwa akili yako ukaacha kufikiri kwa mapokeo uliyopokea urudi usome tena ulichoandika alafu ujiulize huyo Mungu wako anataka umuabudu jumamosi TU au anahitaji Kila siku na Kila wakati umuabudu,
 
Hivyo Yesu mwenyewe alikuwa anasali siku gani? Hakuna hata sehemu moja kwenye biblia inayosema yesu aliingia hekaluni kuabudu siku ya kwanza ya juma (jumapili) bali biblia inasema Yesu aliingia hekaluni kusali siku ya sabato (jumamosi) kama ilivyokuwa desturi yake na desturi ya wayahudi (Yesu ni myahudi kwa kuzaliwa). Nitaftutie andiko lolote kwenye biblia ambapo Yesu au Mungu alihalalisha siku ya ya jumapili (siku ya kwanza ya juma) kuwa ndio siku ya kumuabudi Mungu wa mbinguni. MITUME WOTE NA WAKRISTO WA KWANZA WALIKUWA WASABATO (walisali siku ya sabato kama ilivyoamriwa kwenye torati ya Musa aliyopewa na Mungu mwenyewe ikiwa imeandikwa kwenye mbao za Mawe). Hakuna wakatyi wowote ambapo Mungu wa mbinguni alibadilisha siku ya kumuabudu.
Kasome Matendo ya mitume 20:7 alafu urudi tena tuendelee kuelimishana
 
Inasitaajabisha mno,hadi baada ya miaka 300 baada ya UFUFUKO WA YESU hakuna MKRISTO yeyote aliyewahi kukanyaga KANISANI SIKU YA JUMAPILI.

IKIWA KWA KINYWA CHA YESU MWENYEWE ANAWAAMBIA

"WATU WANGU SABATO ILIFANYIKA KWA AJILI YA WANADAMU" - MARKO 2 : 21.

WAO WANASEMA HAPANA,SABATO NI KWA AJILI YA WAYAHUDI ILA JUMAPILI KWA AJILI YA WAKRISTO,UKIWAULIZA ANDIKO HAWANA HATA MOJA,WAULIZE HAYO MMEYATOA WAPI,HAWAJUI.
UKIIONA RAIA HUMU INAPINGA JUU SABATO

UKIONA DALILI HIZO TAMBUA TU HUONGEI NA BINADAMU UNAONGEA NA NYANI. (KWA MUJIBU WA QURAN).




QURAN AL A'RAAF 7 : 163 - 166.

163. Na waulize khabari za mji ulio kuwa kando ya bahari, wakiivunja amri ya Sabato (Jumaamosi ya mapumziko). Samaki walikuwa wakiwajia juu juu siku ya mapumziko yao, na siku zisio kuwa za kupumzika (Sabato) hawakuwa wakiwajia. Kwa namna hiyo tuliwajaribu kwa sababu walikuwa wakifanya upotovu.

164. Na kikundi kati yao walisema: Kwa nini mnawawaidhi watu ambao tangu hapo Mwenyezi Mungu atawateketeza au atawaadhibu adhabu kali? Wakasema: Ili uwe ni udhuru kwa Mola Mlezi wenu, na huenda nao wakamchamngu.

165. Basi walipo yasahau waliyo kumbushwa, tuliwaokoa walio kuwa wakikataza maovu, na tukawatesa walio dhulumu kwa adhabu mbaya kwa vile walivyo kuwa wakifanya upotovu.

166. Walipo jifakharisha katika waliyo kanywa tuliwaambia: Kuweni manyani wa kudharauliwa
We mkuu nimesoma comments zako nyingi humu
nina uhakika tukikaa tukijadiliana kwa kina unaweza ukasilimu kabisaaa
 
Ukianza fikiri kwa akili yako ukaacha kufikiri kwa mapokeo uliyopokea urudi usome tena ulichoandika alafu ujiulize huyo Mungu wako anataka umuabudu jumamosi TU au anahitaji Kila siku na Kila wakati umuabudu,
Kuna miss nyingi sana kwenye ufikiri juu ulioutoa.

Mungu ni Mungu WA mahusiano. Ndio maana licha ya siku zote sita kuwa na wewe anajua utakuwa na kazi za kufanya. Alafu wewe ni kiumbe cha mahusiano huwezi kuwa peke yako tu. Akaweka mfumo bora kabisa baada ya yote MWANADAMUaache yote akusanyike na wenzake kufurahia Mungu wake huku akigusa maisha ya wenzake wanaopitia nyakati ngumu.


Mungu amenyooka, naona unataka kumpindisha
 
Yesu alifufuka Siku ya kwanza ya Juma.
Leo Ijumaa ndicho kile kinachoitwa Siku Maandalio ya Juma au Siku ya sita.

Jumapili ni Siku ya kwanza ya Juma. Na Sabato kesho ni Jumamosi.

Mambo ya kutafakari.

1: Ni dharau na ukosefu wa adabu kwa Mungu mfalme kuiita Jumapili au ijumaa Sabato. Ni kuhariri sentensi za Mungu.

2: Inatukumbusha Dunia iliumbwa Siku sita za wiki. Hii ya Saba ya Sabato ilikuwa in ofa kwa mwanadamu. Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu. Isingekuwa Sabato wiki ingebaki na Siku sita tu.

3: SABATO imetajwa Mara ya kwanza katika maandiko kabla ya dhambi. Hivyo wazo LA Sabato Galina uhusiano na vivuli vya maagizo ya jangwani.

4: Yesu sio Sabato, wala Sabato sio Yesu. Yesu ni mmiliki au Bwana wa hiyo Sabato. Sabato sio Siku ya wayahudi ni ya Yesu na wanaomfuata.

5: Kukusanyika kwa ibada baada ya Siku sita za kazi kwa Siku isiyo Sabato ya Jumamosi ni kumkosoa na kumdharau Mungu na maagizo yake.

6: Sabato sio kwa ajili ya wakristo. Ni mwanadamu wote. Kama ni mwanadamu na ulikuwa hujui hujachelewa. Nakukumbusha. Ikumbuke Siku ya Sabato.

7: Mungu hakuumba weekend. Alitutengenezea Siku sita za kazi na ya saba ya sabato sio Siku mbili zinazoitwa weekend. Hii taarifa ni muhimu kwako.


Niwatakie ijumaa njema.

Maelekezo ya Mungu hayataki mjadala mrefu yanataka utekelezaji. Huwezi kuhoji kauli za mfalme asiyekosea.
Haya Bwana leo tumeiona Sabato na Tumeabudu.
 
Wasabato buana mna kazi kweli kweli… sabato sio tiketi ya kuona ufalme wa Mungu abiii!
Ni matendo yako duniani ndio yatakuwezesha kuuona ufalme wa Mungu au tuseme kwenda mbinguni. Aliye na dini asiye na dini Imani ndio kila kitu… Kwa Mungu siku zote ni sawa aliaagiza tutenge siku moja tu ya kumwabudu…. so iwe Jumamosi Jumapili Ijumaa zote ni siku za Bwana msitengeneze utengano…
 
Back
Top Bottom