Ijumaa ya leo ikukumbushe tu Sabato ni Jumamosi

Ijumaa ya leo ikukumbushe tu Sabato ni Jumamosi

Naelewa vizuri kabisa.
Lakini nafikiri itakuwa hukunipata pale juu kabisa maelezo ya mwanzoni kabisa kabla sijaelezea vifungu vya MABADILIKO YA SABATO YALIOTABIRIWA NA KUFANYWA NA MUNGU MWENYE KUPITIA YESU KRISTU.

Sijakataa uwepo wa sabato hiyo ya mwanzo kabla ya ufufuko wa Yesu unayoizubgumzia wewe, mbali na hilo fungu ulilonipatia. Zaidi imefafanuliwa na kuelezewa katika mafungu yafuatayo ya Biblia na hasa agano la kale kuna maagizo, maelekezo na amri nyingi tu kuhusu kuiishi na kuifuata sabato (sabato ya kiyahudi). mfano waweza kurejea mafungu yafuatayo: isaya 56:2, isaya 58:13-14, kutoka 20:8-11, kumb 5:11-15, yeremia 17:19-27, Eze 20:20-24, Mwanzo 2:3, Kutoka 13:13, Kut. 16:23, Kut. 16:29, Kut. 35:3, Hes. 15:32 hayo mafungu yote hapo juu ni maagizo ya Mungu kwa wayahudi(taifa teule) kuhusu kuiishi na kuifuata sabato
Nimeipenda Sana hiyo mistari ya reference,na ninafurahi maana hapa naongea na muabudu jumapili mwenzangu,je tunakubali kwamba tunaenda kinyume na maandiko?

Hivyo vifungu vyote ulivyonipa kwamba vinatabiri mabadiliko ya sabato nimevisoma vyote Ila kiukweli havina uhusiano na mabadiliko ya sabato...Sabato Ni amri ya Mungu tunawezaje kuibalisha kienyeji namna hii hebu tujitafakari kwa kina
 
Sawa msabato, sisi tunamfuata Bwana wa sabato wewe fuata siku ya Jumamosi.
Simple tuu.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Yesu alijitangaza mwenyewe kuwa Bwana wa siku ya Sabato, na bado siyo sahihi kwa hiyo kuhitimisha kwamba Yesu ni siku ya Sabato mwenyewe!
Malkia wa Uingereza siyo Uingereza mwenyewe, lakini tu mkuu juu yake. Katika namna hiyo hiyo, Yesu siyo siku ya Sabato mwenyewe, lakini Mkuu au Bwana juu yake. Kwa hiyo kadiri ambavyo tunapata pumziko letu kwa Yesu, hatutakiwi pia kukataa kupumzika kutoka katika mahangaiko yetu katika siku yake ya Sabato ya kila juma. Na kutokana na kwamba Yesu bado angali leo ni Bwana wa wafuasi wake wote, basi bado kuna siku ya Sabato ambayo yeye ni Bwana wake na ambayo wafuasi wake wote wanatakiwa kuwa wanaitunza leo! Na ni siku ipi ya juma iliyo hii siku ya Sabato ya Mungu katika kipindi cha Agano Jipya?

“Kwa maana [Mungu] ameinena siku ya saba mahali fulani hivi, Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote....Basi, imesalia raha (ya kutunza Sabato) kwa watu wa Mungu. (KUMBUKA: neno hili kwa ajili ya “pumziko” katika Kiyunani ni “sabbatismos” na hutafsiriwa kiuhalisia utunzaji wa Sabato – angalia Strong’’s Exhaustive Concordance, neno la Kiyunani #4520.) Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake. Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu yeyote asije akaanguka kwa mfano uo huo wa kuasi.” Waebrania 4:4, 9-11.
 
Origin ya sabato Kwa Mujibu wa Yesu aliyemuumba mwanadamu Ni siku mwanadamu anaumbwa kesho yake.

'Sabato ilifanyika kwa ajili ya Mwanadamu.

Ingekuwa vinginevyo wiki ingeishia ijumaa tu.
Hii Ni kweli kabisa..na huu ndio ulikuwa mwanzo wa Sabato,Sasa mdau anasema mwanzo wa Sabato Ni ukombozi kutoka utumwani Misri
 
Nimeipenda Sana hiyo mistari ya reference,na ninafurahi maana hapa naongea na muabudu jumapili mwenzangu,je tunakubali kwamba tunaenda kinyume na maandiko?

Hivyo vifungu vyote ulivyonipa kwamba vinatabiri mabadiliko ya sabato nimevisoma vyote Ila kiukweli havina uhusiano na mabadiliko ya sabato...Sabato Ni amri ya Mungu tunawezaje kuibalisha kienyeji namna hii hebu tujitafakari kwa kina
Haa eti muabudu jumapili.

Mabadiliko ya yalifanywa na Mungu mwenyewe sio mimi wala mtu fulani. Ni Mungu mwenyewe ndiye aliye ibadili. (Ushahidi na maelezo yake nimekupatia mbona)
 
Wakristo wa Mwanzo walikutana Siku ya Kwanza kwa ajili ya kuumega mkate; "Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.” (Mdo.20:7).
Wakati wa kipindi fulani Kanisa la Mitume huko Yerusalemu lilimega mkate kila siku (angalia Mdo 2:42-46). Kama kipindi kimoja cha kumega mkate kule Troa siku ya kwanza kilifanyiza Sabato, tendo kama hilo la Kanisa la Mitume lisingeendelezwa katika kumega mkate siku zingine [na] kuwa linatosha kuzifanya siku hizi Sabato pia?
Kwa nini kujaribu kupokea kielelezo ambamo mkutano wa jioni ulifanyika Jumapili, na kisha kujaribu pasipo mafanikio kuthibitisha kwamba Sabato imebadilishwa, wakati ukiacha kuangalia ukweli kwamba mtume huyu huyu Paulo alihubiri kila siku ya saba ya Sabato, siyo tu kwa Wayahudi, bali pia kwa Wamataifa? (Angalia Mdo 13:14, 42, 44, 16:13, 17:2, 18:4.)
 
Wakristo wa Mwano walipumzika Siku ya Kwanza; "Siku ya Kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake: ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja.” (1Kor.16:2); labda kama huamini hilo andiko au wewe sio mkristo unaweza kupinga.
Paulo, hata hivyo, hasemi: “Wekeni matoleo yenu katika hazina ya Kanisa katika siku ya kwanza ya juma,” lakini anasema: “Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake.”
Mtume [Paulo] alimwambia kila mmoja wa ndugu wa Korintho kuweka nyumbani kiasi fulani cha mapato yake ya kila juma katika siku ya kwanza au mwanzo wa juma kabla hawajawa na nafasi ya kukitumia chote. Katika kufuata ushauri wa Paulo, wangekuwa wanamweka Mungu na kazi yake kwanza katika mambo yao ya kifedha, badala ya kumweka mwisho wa juma baada ya fedha yao yote kuwa imetumika.
Swali zima linageuka kwenye maana ya maelezo, “kwa njia yake.” Tafsiri za Kilatini, Vulgate na ile ya Castellio hutoa maana ya kirai, “apud se,” – “pamoja na nafsi yake, nyumbani.” Tafsiri kama hiyo hiyo imetolewa katika tafsiri kadhaa au nyingine.
Fungu, kwa hiyo, halithibitishi kwamba Kanisa la Korintho lilikuwa limekutanika kwa ajili ya ibada ya wote siku ya Jumapili; lakini, kinyume chake, linathibitisha kwamba kila mmoja anapaswa kuwa nyumbani kwake mwenyewe ambapo angeangalia mambo yake mwenyewe ya kidunia na kuweka mwenyewe katika ghala mwanzoni mwa kila juma kadiri Mungu alivyokuwa amemfanikisha. Kama kila mmoja angekuwa amefanya hivyo, wakati ambapo mtume angekuja, malimbikizo yao yangekuwa tayari na kila mmoja angeweza kumletea kile ambacho walikuwa wamekusanya.
 
Kanisa liliundwa rasmi Siku ya Kwanza almaarufu kama Pentekoste; Mdo 2:1-6; "Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi."; pengine ungetamani andiko hili lisiwepo ila ndio hivyo tena.
Tukikubali kwamba siku ya Pentekoste ilitokea siku ya kwanza ya juma, inabaki [hatimaye] kuthibitishwa kwamba siku hii ilikuja kuwa Sabato. Ilikuwa ni sikukuu ya Pentekoste, na siyo siku ya kwanza ya juma, ambayo Mungu alipanga kuiheshimu.

Siku ya Pentekoste imetajwa kwa pekee, lakini siku ya juma ambapo ilitokea inapitwa kwa ukimya. Haukuwa mpango wa Mbingu kuiheshimu siku ya kwanza ya juma, lakini kuweka alama [ya kitu] halisi cha sikukuu ya Pentekoste.
Kuchinjwa kwa mwanakondoo wa pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza ilikuwa imekutana na kitu halisi katika kifo cha Mwana-kondoo wa Mungu siku hiyo (angalia Kutoka 12; Yohana 19; 1 Wakorintho 5:7). Matoleo ya malimbuko ya kwanza siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza yaliendana na kitu chake halisi katika ufufuo wa Bwana wetu siku hiyo, malimbuko ya kwanza ya wale waliolala (angalia Walawi 23; 1 Wakorintho 15:20-23; Mdo 1:1-2).

Na kumwagwa kwa Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste kulitimiza kivuli cha sikukuu ya Pentekoste. Haikuwa siku ambamo matukio haya yalitokea ambayo yalikuwa ni ya muhimu, lakini kwamba taratibu hizi za mfano za zamani na huduma zilikuwa zinafikia utimilizo wake katika kivuli.
Mungu hakusema lolote katika sehemu hii kuheshimu siku ambamo matukio haya yalitokea, na hivyo hakuna uthibitisho uliopo kuhusiana na badiliko katika wakati wa Sabato ya Mungu. “Usiongeze neno katika maneno yake; Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.” Mithali 30:6.
 
Sasa mzee hapo si walikuwa hawajui km Yesu atafufuka!!!,Lkn baada ya kujua kuwa Yesu alifufuka siku ya Jumapili,Mitume walianza kukutanika kwaajili ya Ibada siku ya Jumapili km ilivyo Leo rejea 1Kor.16:1-2.
Hivyo Yesu mwenyewe alikuwa anasali siku gani? Hakuna hata sehemu moja kwenye biblia inayosema yesu aliingia hekaluni kuabudu siku ya kwanza ya juma (jumapili) bali biblia inasema Yesu aliingia hekaluni kusali siku ya sabato (jumamosi) kama ilivyokuwa desturi yake na desturi ya wayahudi (Yesu ni myahudi kwa kuzaliwa). Nitaftutie andiko lolote kwenye biblia ambapo Yesu au Mungu alihalalisha siku ya ya jumapili (siku ya kwanza ya juma) kuwa ndio siku ya kumuabudi Mungu wa mbinguni. MITUME WOTE NA WAKRISTO WA KWANZA WALIKUWA WASABATO (walisali siku ya sabato kama ilivyoamriwa kwenye torati ya Musa aliyopewa na Mungu mwenyewe ikiwa imeandikwa kwenye mbao za Mawe). Hakuna wakatyi wowote ambapo Mungu wa mbinguni alibadilisha siku ya kumuabudu.
 
Yesu Kristo alifufuka Siku ya Kwanza ya Juma (Mt.28:1). Ufufuko wa Yesu ndio wokovu wenyewe; labda kama huamini katika wokovu.
Mungu kamwe hakuwataka watu kutunza siku yoyote kama ukumbusho wa ukombozi. Lakini alituamuru kutunza kitakatifu Sabato ya siku ya saba kama ukumbusho wa uumbaji wake na hivyo kumtambua Mungu kama Mwumbaji wetu.

Hata hivyo kama, ingekuwa wajibu kutunza siku moja ya juma kutokana na sababu hii, zaidi kwa uhakika siku ya kusulibishwa ina madai yenye uzito. Haisemwi kwamba tuna ukombozi kupitia katika ufufuo wa Kristo, lakini inasemwa kwamba tuna ukombozi kwa njia ya kumwagwa kwa damu yake [Kristo] (angalia Ufunuo 5:9; Waefeso 1:7; Wakolosai 1:14; Waebrania 9:12, 15). Maajabu ya tendo la Yehova katika kumtoa Mwanawe mpendwa na wa pekee kufa kwa ajili ya jamii ya waasi ilikuwa ni miwani ya ukombozi wa upendo ambao juu yake ulimwengu ulitakiwa kuangalia kwa mshangao katika kipindi chote cha milele. Nani angeshangaa kwamba jua lilikuwa limefunikwa katika giza na kwamba [vitu vyote vya] asili vilitetemeka kwa mwonekano! Ijumaa, siku ya mateso, kwa hiyo, ina madai makubwa zaidi kuliko siku ya ufufuo; lakini Mungu hajatoa amri ya kutunza mojawapo.
 
Mabadiliko ya yalifanywa na Mungu mwenyewe sio mimi wala mtu fulani. Ni Mungu mwenyewe ndiye aliye ibadili. (Ushahidi na maelezo yake nimekupatia mbona)
“Kanisa Katoliki kwa zaidi ya miaka elfu moja kabla ya kuwepo Mprotestanti, kwa mamlaka ya utume wake wa Ki-Mungu, lilibadilisha siku kutoka Jumamosi kwenda Jumapili….Ulimwengu wa Kiprotestanti wakati wa kuzaliwa kwake ulikuta Sabato ya Kikristo ikiwa imeshika mizizi kwa nguvu kiasi cha kushindwa kwenda kinyume na uwepo wake; iliwekwa kwa hiyo chini ya [vitu] muhimu vya kukubalika pasipo upinzani katika mpangilio, hivyo ikimaanisha haki ya Kanisa (Katoliki) kubadilisha siku, kwa zaidi ya miaka mia tatu. Sabato ya Kikristo kwa hiyo mpaka siku ya leo, inakubaliwa na kizazi cha Kanisa Katoliki kama mwenza wa Roho Mtakatifu, bila neno la upinzani kutoka katika ulimwengu wa Kiprotestanti.” James Cardinal Gibbons katika Catholic Mirror, Septemba 23, 1893.

“Swali – Sabato ni siku ipi?
“Jubu – Jumamosi ni siku ya Sabato.
“Swali – Kwa nini huwa tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi?
“Jibu – Tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi kwa sababu Kanisa Katoliki…lilihamisha uzito [wa utakatifu] kutoka Jumamosi kwenda Jumapili.” Peter Geiermann, C.S.S.R., The Convert’’s Catechism of Catholic Doctrine, ukr.. 50, Toleo la 3, 1957.
1649974804612.png
 
Mabadiliko ya yalifanywa na Mungu mwenyewe sio mimi wala mtu fulani. Ni Mungu mwenyewe ndiye aliye ibadili. (Ushahidi na maelezo yake nimekupatia mbona)
“Wao [Waprotestanti] huona ni wajibu wao kuitunza Jumapili kitakatifu. Kwa nini? Kwa sababu Kanisa Katoliki huwaambia kufanya hivyo. Hawana sababu nyingine [zaidi]....Utunzaji wa Jumapili hivyo basi huja kuwa sheria ya kikanisa tofauti kabisa kutoka katika sheria ya Mungu ya kutunza Sabato....Mwanzilishi wa sheria ya Jumapili...ni Kanisa Katoliki.” Ecclesiastical Review, Februari, 1914.

“Jumapili...ni uumbaji kabisa wa Kanisa katoliki.” American Catholic Quarterly Review, Januari, 1883.

“Jumapili...ni sheria ya kanisa Katoliki pekee...” American Sentinel (Catholic), Juni, 1893.

““Jumapili ni pando la Kikatoliki na madai yake kuitunza yanaweza kutetewa tu kwa njia ya kanuni za Kikatoliki....Kutoka mwanzo hadi mwisho wa Maandiko hakuna hata fungu moja ambalo linahalalisha kubadilishwa kwa ibada ya hadhara ya kila juma kutoka siku ya mwisho ya juma kwenda siku ya kwanza.” Catholic Press, Sydney, Australia, August, 1990.
 
Wakolosai 2:16-17
"Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo"

Asiyependa hizi mistari achukue Biblia yake azichane azitupe chooni!
Sabato ya siku ya saba ilitolewa kwa watu wa Mungu wakati wa uumbaji. Hii ina maana kwamba Sabato ilikuwepo kabla dhambi haijaingia ulimwenguni, na hivyo basi kabla ya sheria za kafara na maagizo kuwa zimewekwa. Hivyo, Sabato ya kila juma ya Mungu isingekuwa sehemu ya sheria za maagizo, na isingekuwa imegongomelewa msalabani samabamba na sheria za maagizo.
Kutokana na kwamba wengi wana shida kutofautisha baina ya sheria za maagizo zilizoandikwa na Musa, na Sheria takatifu ya amri 10 iliyonenwa na Mungu, hebu na tuchunguze tofauti za wazi baina ya hizi mbili.
Sheria za maagizo zinahesabiwa kama “sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili” (Waebrania 7:16); na Sheria takatifu ya Mungu, imesemwa, “Twajua ya kuwa torati asili yake ni rohoni.” Warumi 7:14. Moja ni sheria ambayo “hapana budi sheria nayo ibadilike.” Waebrania 7:12. Sheria takatifu ni sheria ambayo Kristo husema, “Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.” Mathayo 5:18.
Sheria ya maagizo ilikuwa ni “kivuli cha mema yatakayokuwa” (Waebrania 10:1), na iliwekwa tu “hata wakati wa matengenezo mapya.” Waebrania 9:10. Lakini nyingine ilikuwa ni sheria takatifu, ambayo inasemwa na Yohana, “Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi [wa sheria].” 1 Yohana 3:4. Moja ni nira isiyoweza kubebwa (angalia Mdo 15:10); nyingine ni ile “sheria ya uhuru” ambayo kwayo tutahukumiwa (angalia Yakobo 2:8-12).
Sheria ya maagizo ni ile ambayo Kristo “aliiondoa katika mwili wake” (angalia Waefeso 2:15); sheria takatifu ni ile ambayo hakuja kuiondoa (angalia Mathayo 5:17). Moja inahesabiwa kama “hati ya kutushitaki kwa hukumu” “iliyokuwa na uadui kwetu,” ambayo iligongomelewa msalabani na kuondolewa kwa kifo cha Kristo (angalia Wakolosai 2:14); nyingine ni ile Sheria ambayo alikuja kutimiliza na kuitukuza (angalia Isaya 42:21) na ambayo Yakobo hueleza kama “sheria ya kifalme” ambayo ni dhambi kuiasi (angalia Yakobo 2:8-12). Moja ilikuwa ni sheria ya muda ambayo ilibatilishwa “kwa sababu ya udhaifu wake, na kutokufaa kwake” (Waebrania 7:18); nyingine ni Sheria isiyobadilika ya milele ambayo haiwezi kutanguliwa: “Basi, je twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? Hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.” Warumi 3:31.
Sheria ya maagizo ni sheria ambayo ilikuwa ni ukuta wa katikati wa kiambaza baina ya Wayahudi na Mataifa (angalia Waefeso 2:14); nyingine ni Sheria ile, kazi ya hiyo hata mataifa wanasemwa kuwa imeandikwa katika mioyo yao (angalia Warumi 2:14-15). Moja ni sheria ya amri iliyo katika maagizo (angalia Waefeso 2:15); Sheria takatifu ni amri za Mungu, ambazo ni wajibu wa jamii ya wanadamu kuzitunza (angalia Mhubiri 12:13).

Hii Sheria kuu takatifu ya amri 10 inaletwa mbele na ujumbe wa malaika wa tatu (angalia Ufunuo 14:9-12). Hii ni Sheria ambayo masalio wa mbegu ya mwanamke walikuwa wanatunza wakati joka alipofanya vita juu yao (angalia Ufunuo 12:17). Sheria hii takatifu itawahakikishia, wale wote wanaoitunza, haki kuingia mbinguni na kula mti wa uzima (angalia Ufunuo 22:14).

Hakika, sheria hizi mbili hazitakiwi kuchanganywa. Sheria takatifu ilitimilizwa, kutukuzwa, kuadhimishwa, na ni takatifu, ya haki, ya kiroho, njema, na ya kifalme; wakati nyingine ni ya mwilini, kivuli, mzigo, na iliondolewa, kuvunjwa, kufutwa, kugongomelewa msalabani, kubadilishwa, na kubatilishwa kwa sababu ya udhaifu wake na kutofaa kwake.
 
Kama Ww Ni mkristo kuifuata Sabato ni Makosa. Maana Bwana Aliipinga
WALE AMBAO HAMSOMI HATA KATEKISIMU YENU WAKATOLIKI KILA KITU TUKIWAAMBIA MTASEMA TUNAWAKASHIFU....
SASA SOMA HIYOOOOO.....IBADA YA JUMAPILI NI MPANGO WA MWANADAMU NA SIYO MPANGO WA MUNGU.....

KATEKISIMU UK 74

1649975213603.png
 
Nimeipenda Sana hiyo mistari ya reference,na ninafurahi maana hapa naongea na muabudu jumapili mwenzangu,je tunakubali kwamba tunaenda kinyume na maandiko?

Hivyo vifungu vyote ulivyonipa kwamba vinatabiri mabadiliko ya sabato nimevisoma vyote Ila kiukweli havina uhusiano na mabadiliko ya sabato...Sabato Ni amri ya Mungu tunawezaje kuibalisha kienyeji namna hii hebu tujitafakari kwa kina
KUSOMA VITABU KUNAFAIDA KUBWA SANA....
ONA HII
👇
👇
👇
..HII NI KATEKISIMU YA WAKATOLIKI WAMEJIELEZA WAZI

SHIDA YA WAKATOLIKI NI KWAMBA HAWASOMI HATA VITABU VYAO NDIYO MAANA WANADANGANYWA KIRAHISI..
1649975387564.png
 
Sabato ya siku ya saba ilitolewa kwa watu wa Mungu wakati wa uumbaji. Hii ina maana kwamba Sabato ilikuwepo kabla dhambi haijaingia ulimwenguni, na hivyo basi kabla ya sheria za kafara na maagizo kuwa zimewekwa. Hivyo, Sabato ya kila juma ya Mungu isingekuwa sehemu ya sheria za maagizo, na isingekuwa imegongomelewa msalabani samabamba na sheria za maagizo.
Kutokana na kwamba wengi wana shida kutofautisha baina ya sheria za maagizo zilizoandikwa na Musa, na Sheria takatifu ya amri 10 iliyonenwa na Mungu, hebu na tuchunguze tofauti za wazi baina ya hizi mbili.
Sheria za maagizo zinahesabiwa kama “sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili” (Waebrania 7:16); na Sheria takatifu ya Mungu, imesemwa, “Twajua ya kuwa torati asili yake ni rohoni.” Warumi 7:14. Moja ni sheria ambayo “hapana budi sheria nayo ibadilike.” Waebrania 7:12. Sheria takatifu ni sheria ambayo Kristo husema, “Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.” Mathayo 5:18.
Sheria ya maagizo ilikuwa ni “kivuli cha mema yatakayokuwa” (Waebrania 10:1), na iliwekwa tu “hata wakati wa matengenezo mapya.” Waebrania 9:10. Lakini nyingine ilikuwa ni sheria takatifu, ambayo inasemwa na Yohana, “Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi [wa sheria].” 1 Yohana 3:4. Moja ni nira isiyoweza kubebwa (angalia Mdo 15:10); nyingine ni ile “sheria ya uhuru” ambayo kwayo tutahukumiwa (angalia Yakobo 2:8-12).
Sheria ya maagizo ni ile ambayo Kristo “aliiondoa katika mwili wake” (angalia Waefeso 2:15); sheria takatifu ni ile ambayo hakuja kuiondoa (angalia Mathayo 5:17). Moja inahesabiwa kama “hati ya kutushitaki kwa hukumu” “iliyokuwa na uadui kwetu,” ambayo iligongomelewa msalabani na kuondolewa kwa kifo cha Kristo (angalia Wakolosai 2:14); nyingine ni ile Sheria ambayo alikuja kutimiliza na kuitukuza (angalia Isaya 42:21) na ambayo Yakobo hueleza kama “sheria ya kifalme” ambayo ni dhambi kuiasi (angalia Yakobo 2:8-12). Moja ilikuwa ni sheria ya muda ambayo ilibatilishwa “kwa sababu ya udhaifu wake, na kutokufaa kwake” (Waebrania 7:18); nyingine ni Sheria isiyobadilika ya milele ambayo haiwezi kutanguliwa: “Basi, je twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? Hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.” Warumi 3:31.
Sheria ya maagizo ni sheria ambayo ilikuwa ni ukuta wa katikati wa kiambaza baina ya Wayahudi na Mataifa (angalia Waefeso 2:14); nyingine ni Sheria ile, kazi ya hiyo hata mataifa wanasemwa kuwa imeandikwa katika mioyo yao (angalia Warumi 2:14-15). Moja ni sheria ya amri iliyo katika maagizo (angalia Waefeso 2:15); Sheria takatifu ni amri za Mungu, ambazo ni wajibu wa jamii ya wanadamu kuzitunza (angalia Mhubiri 12:13).

Hii Sheria kuu takatifu ya amri 10 inaletwa mbele na ujumbe wa malaika wa tatu (angalia Ufunuo 14:9-12). Hii ni Sheria ambayo masalio wa mbegu ya mwanamke walikuwa wanatunza wakati joka alipofanya vita juu yao (angalia Ufunuo 12:17). Sheria hii takatifu itawahakikishia, wale wote wanaoitunza, haki kuingia mbinguni na kula mti wa uzima (angalia Ufunuo 22:14).

Hakika, sheria hizi mbili hazitakiwi kuchanganywa. Sheria takatifu ilitimilizwa, kutukuzwa, kuadhimishwa, na ni takatifu, ya haki, ya kiroho, njema, na ya kifalme; wakati nyingine ni ya mwilini, kivuli, mzigo, na iliondolewa, kuvunjwa, kufutwa, kugongomelewa msalabani, kubadilishwa, na kubatilishwa kwa sababu ya udhaifu wake na kutofaa kwake.
Umesoma ili kuelewa hizo mistari? Au umesoma ili kujibu? Hiyo ni mistari iko kwenye Biblia yako na inasema wazi kuwa

"Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo"

Umeelewa inachosema? Wakristo hapa tunaambiwa mtu yeyote. Yeyote maana yake ni yeyote, asituhukumu sisi kwa sababu ya sikukuu au sabato. Imeeleweka hapo? Yaani huwezi kumhukumu Mkristo kwa sababu ya Sabato.

Kama hulitaki hili kazichane mistari hii kwenye Biblia yako. Maelezo marefu hayabadilishi maagizo simple na straightforward kama haya!
 
Hii Ni kweli kabisa..na huu ndio ulikuwa mwanzo wa Sabato,Sasa mdau anasema mwanzo wa Sabato Ni ukombozi kutoka utumwani Misri
Haa usinielewe vibaya hiyo sikusema ni mwanzo wa sabato, badala nilisema ni moja ya sababu ya wayahudi kuitunza siku ya sabato jumamosi (yaani kama kumbukumbu ya kukombolewa kwao toka misri utumwani). sasa nikakuuliza ni mfuasi wa kristo au wa dini ya kiyahudi bado ? Mpaka unganganie sabato iliokomeshwa na Mungu mwenyewe na kutangazwa kama ilikuwa ni kivuli cha mambo ya kale. '(KIVULI HAKIVALISHWI SUTI JOANNAH)

Kimsingi ziko sababu tatu (3) za
Kwa nini wayahudi walishika na wanaishika sabato.

Wayahudi huishika sabato kwa sababu tatu kama ndiyo msingi wa amri ya kupumzika:


Sababu ya kwanza ishaelezea huko juu.

Sababu ya pili ni kukumbuka siku alipopumzika Mungu baada ya kumaliza kazi ya uumbaji; kama tusomavyo katika kitabu cha Kutoka 20:9-11 “Siku sita fanya kazi lakini siku ya saba ni sabato ya Bwana-usifanye kazi yoyote, maana kwa siku sita bwana alifanya mbingu na nchi, akastarehe siku ya saba.” Vile vile unaweza kusoma kitabu cha Mwanzo 2:3.

Sababu ya tatu na mwisho ni kwamba sabato ni alama ya kwamba Mungu aliliteua taifa la Israeli kuwa mali yake. Kama tunavyosoma katika kitabu cha Kutoka 13:13 “Hakika mtazishika sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote, ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi.”

JITAIDI USIELEWE MAMBO NUSUNUSU.
 
Mbali na yote, nashukurigi sama mola we Catholics hatujawahigi kutikiswa na lolote[emoji23][emoji23] sisi amani tunazo. Ila wap wanateseka juu yetu. Haya kazi iendelew

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
KWANINI TUNASALI JUMAPILI WA KATOLIKI HUKU MADHEHEBU YA KIPENTEKOSTE YAANI WALOKOLE WAKITUFUATA BILA KUJUA KUWA SISI NDIO WANZILISHI WA IBADA YA JUMAPILI?*
JIBU

TULIONELEA KANISA KATOLIKI KUBADILI SABATO YA BWANA KUTOKA SIKU YA SABA (YAANI JUMAMOSI ) KWENDA SIKU YA KWANZA YA JUMA (YAANI JUMAPILI )

Nanukuu kitabu cha
BUSTANI YA KATEKISTA CHA PADRE RAPHAEL ROGEAU W.F.
PUBLISHING-benedictine publications ndanda-peramiho ukurasa wa 74

Swali: KWA NINI TUNASALI SIKU YA JUMAPILI SIO SABATO?
Jibu: Kihistoria tunaelewa kwamba wakristo wa kwanza waliendelea kuadhimisha siku ya Bwana Jumamosi, walivyozoea wayahudi; hasa wakristo waliotoka dini ya kiyahudi......
Wale ambao walikuwa wanatoka upagani, hawakujisikia kuwa wanabanwa na sheria zile.........
Sababu nyingine ya kusali Jumapili ni hii; wafuasi wa Yesu walitaka kujitofautisha na waamini wa dini ya kiyahudi walioadhimisha ibada siku ya Jumamosi......
Polepole wakristo wakaanza kuzoea kukutana, kusali, kusoma masomo yao na kumega mkate siku ya kwanza.....

Ndivyo, tarehe 03/03/321, mfalme Konstantino alivyotangaza rasmi kwamba Jumapili iwe SIKU YA BWANA, wakristo wapumzike na kusali. Hayo ndiyo mapokeo ya Makanisa mengi ya JUMAPILI


SWALI KATI YA MFALME KONSTANTINO NA MUNGU YUPI TUMFUATE JE KUNA AYA KUNA AYA NDANI YA BIBLIA KUWA SABATO TAKATIFU NI JUMAPILI? WAPI MANABII NA WALIFUATA MITUME WALIMFUATA KONSTANTINO BADALA YA MWENYEZI MUNGU?
MUNGU ALIIBARIKI,ALIITAKASA,NA ALISTAREHE SIKU YA SABA AMABAYO NDIYO SABATO TAKATIFU YAKE NA SI SIKU YA KWANZA YA JUMA
NA KUITAKASA ,
1649976485499.png

1649976510308.png
 
Haa usinielewe vibaya hiyo sikusema ni mwanzo wa sabato, badala nilisema ni moja ya sababu ya wayahudi kuitunza siku ya sabato jumamosi (yaani kama kumbukumbu ya kukombolewa kwao toka misri utumwani). sasa nikakuuliza ni mfuasi wa kristo au wa dini ya kiyahudi bado ? Mpaka unganganie sabato iliokomeshwa na Mungu mwenyewe na kutangazwa kama ilikuwa ni kivuli cha mambo ya kale. '(KIVULI HAKIVALISHWI SUTI JOANNAH)
Je Mitume walibadilisha Sabato? Au Je baada ya Yesu kupaa mbinguni Mitume walifanya nini katika Sabato iliyofuata kabla ya Pentekoste?

Baada ya Yesu kupaa mbinguni wanafunzi wake walirudi Yerusalemu kutoka mlima wa mizeituni, vile vile kama Yesu alivyowaamuru kwamba wasitoke Yerusalemu mpaka atakapowaletea Msaidizi (Roho Mtakatifu). Hivyo sabato iliwakuta wamefika Yerusalemu.

“Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.” Matendo 1:12

Walipofika Yerusalemu, yapata watu mia na ishirini walipanda orofani, walipokuwa wakikaa kina Petro kwa ajili ya kusali, siku hiyo ilikuwa ni siku ya sabato, na Biblia inasema.

“Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.” Matendo 1:14

Katika siku hiyo hiyo ya sabato mtume Petro alisimama akahubiri Injili ya Yesu mbele ya wale watu 120 (angalia Mdo 1:15-20), tena sabato hiyo hiyo walipiga kura na kumchagua Mathiya mahali pa Yuda Iskariote (angalia Mdo 1:21-26). Lakini kesho yake, siku iliyofuata ndiyo ilikuwa Jumapili, siku ya Pentekoste, na Biblia inasema.

“Hata ilipotimia siku ya pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.” Matendo 2:1

Kwa hiyo mpaka hapo unaweza kuona kuwa japokuwa walihubiri neno la Mungu siku ya Pentekoste (Jumapili), lakini hawakuvunja sabato ya Jumamosi. Hivyo kila mchungaji anayetumia siku ya Pentekoste kudanganya watu kwamba sabato ilibadilishwa, ni muongo na anamfanya shetani kuwa baba yake kwa kusema uongo na kuwakosesha watu wa Mungu, wachungaji kama hao Yesu anawauliza.

Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu. Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika KWELI, kwa kuwa hamna hiyo KWELI ndani yake. Asemapo UONGO, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni MWONGO, na baba wa huo.” Yohana 8:43, 44.
 
Wayahudi huishika sabato kwa sababu tatu kama ndiyo msingi wa amri ya kupumzika:

Sabato iliwahusu Wayahudi peke yao?TUSIDANGANYANE​

“Na walipokuwa wakitoka, wakawasihi waambiwe maneno haya Sabato ya pili.” “Hata Sabato ya pili, watu wengi, karibu mji wote, wakakusanyika walisikie Neno la Mungu.” Mdo. 13:42,44. “Akatoa hoja zake katika sinagogi kila Sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani.” Mdo. 18:4.
 
Back
Top Bottom