Ikiwa ni upumbavu kusema Tanzania kuna COVID-19 bila kuwa na takwimu, basi iwe pia ni upumbavu kusema Tanzania hakuna COVID-19 bila takwimu

Ikiwa ni upumbavu kusema Tanzania kuna COVID-19 bila kuwa na takwimu, basi iwe pia ni upumbavu kusema Tanzania hakuna COVID-19 bila takwimu

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Sio nia yangu kupingana na serikali yangu, lakini acha ukweli uwe ukweli. NIlishasema humu JF kwamba, kama viongozi wetu wanataka tuamini kwamba hatuna tatizo la COVID-19 nchini na hata kuutangazia ulimwengu kwamba hapa kwetu Tanzania tuko salama kabisa, basi angalau kwa wiki mbili mfululizo tupime watu angalau 50 kwa siku pale Kariakoo sokoni, Manzese, Temeke na Kinondoni. Tukiona hawa watu 200 tutakaowapima kila siku, hata kama ni juu kidogo ya 50% hawana COVID-19 basi tuutangazie ulimwengu kwamba hatuna COVID-19.

Lakini serikali yetu haitaki kufanya hili. Swali ni kwa nini?

Japo hatutaki kufanya hivyo, watu wakijitokeza, kama ubalaozi wa Marekani, na kutangaza hadharani kwamba raia wake wanapokuja Tanzania wajihadhari na maambukizi ya COVID-19, au Kenya kusema wataweka vizuizi dhidi ya abiria kutoka Tanzania, tunaanza kuwapigia kelele - ooh mabeberu nyie, hamuitakii mema nchi yetu nk. Hivi tuna akili sawasawa sisi? Uwezo wetu wa kufikiri ndio unaishia hapo, kupiga kelele mabeberu?

Yapaswa iwe wazi sana kwetu kwamba ikiwa ni upumbavu kusema Tanzania kuna COVID-19 bila kuwa na takwimu za kuthibitisha hilo, basi iwe pia ni upumbavu kusema Tanzania hakuna COVID-19 bila kuwa takwimu za kuthibitisha hilo!
 
1596789771360.png
 
Aisee takwimu inakuwaje kwenye kitu akuna.

Yaani sifugi kuku alafu nikupe takwimu za kuku.
Hizo ndio arguments unataka Magufuli apeleke WHO? Naona hujui mambo ya takwimu katika mambo ya magonjwa ya kuambukiza. Takwimu za Covid-19 maana yake sio kuhesabu wagonjwa! Shule utajirir bila shaka.
 
Hizi story za corona zimechosha leteni zingine
 
Na MIMI nasema Hakuna korona Tanzania,,,mnang'ang'ana na hilo liugonjwa la kichina mtafikiri mnalipwa,,
Kwa sababu si wote tunachagua kwa makusudi kuwa wapumbavu. Kama huna Corona, kwa nini unakataa kufanya testing chache kwa muda mfupi kuthibitisha huna Corona? Unaogopa nini?

NIkuulize swali. Mtu mtanashati, anaonekana ana afya nzuri, amependeza na kuvutia sana, anakuja kwako na kusema anakupenda yuko tayari kufanya mapenzi na wewe. Unamwambia ungependa kufanya mapenzi lakini unaogopa ukimwi. Anakuambia hunioni nilivyo, kwani naonekana kama nina ukimwi mimi? Unaona dalili yeyote kuwa ninao?

Anasisitiza hana kabisa ukimwi. Lakini na wewe unasisitiza kuwa ni vema apime ili kuthibitisha hilo, kwa sababu sio tatizo kama anajua ana uhakika hana ukimwi. Anaanza kukuita bebebru kwa kuwa anakuambia hana ukimwi na wewe humwamini. Anakuambia unamwonea wivu na kumzushia uongo kuwa ana ukimwi ili hata watu wengine wakatae kufanya nae mapenzi.

Nani kati yenu ni mwendawazimu? JIbu lako litakuambia jambo kuhusu post yako.
 
Ivi mijadala ya Corona inaendelea tu?
Lissu kahojiwa kuhusu Corona Tanzania na chombo cha habari Kenya akalianzisha tena.

Lakini tutaachaje kuendelea kuongea Corona wakati habari kuu iliyopo kati ya Kenya na Tanzania wiki hii ni kupigana marufuku kupeleka ndege?
 
Hivi kwani mnautamani huo ugonjwa? Bila kuusema hampumui? Kitu chenyewe kibaya lakini mnavyokipenda kukitaja taja chanini jamani? Si muache shetani apite aende zake?
 
Kwa sababu si wote tunachagua kwa makusudi kuwa wapumbavu. Kama huna Corona, kwa nini unakataa kufanya testing chache kwa muda mfupi kuthibitisha huna Corona? Unaogopa nini?

NIkuulize swali. Mtu mtanashati, anaonekana ana afya nzuri, amependeza na kuvutia sana, anakuja kwako na kusema anakupenda yuko tayari kufanya mapenzi na wewe. Unamwambia ungependa kufanya mapenzi lakini unaogopa ukimwi. Anakuambia hunioni nilivyo, kwani naonekana kama nina ukimwi mimi?...
Njia rahisi ya ww kuiprove wrong serekali ni kwenda kujipimisha ww na familia yako then ukiona hauna corona juwa watanzania wote hatuna corona maana kila siku unafanya interaction na watu tofauti tofauti nadhani hiyo itakusaidia kuujuwa ukweli
 
Kwa sababu si wote tunachagua kwa makusudi kuwa wapumbavu. Kama huna Corona, kwa nini unakataa kufanya testing chache kwa muda mfupi kuthibitisha huna Corona? Unaogopa nini?...

Kama hana ukimwi??...Nani mwendawazimu
 
Njia rahisi ya ww kuiprove wrong serekali ni kwenda kujipimisha ww na familia yako then ukiona hauna corona juwa watanzania wote hatuna corona maana kila siku unafanya interaction na watu tofauti tofauti nadhani hiyo itakusaidia kuujuwa ukweli
Yaani wewe masuala ya takwimu yamekupitia mbali mno! Ni vema ukae kimya tu, maana unaonyesha sifa yako fulani hapa ambayo sio nzuri watu waijue!
 
Njia rahisi ya ww kuiprove wrong serekali ni kwenda kujipimisha ww na familia yako then ukiona hauna corona juwa watanzania wote hatuna corona maana kila siku unafanya interaction na watu tofauti tofauti nadhani hiyo itakusaidia kuujuwa ukweli
Ndiyo mtu akiona hakuna takwimu abebe familia yake iwe mfano wakapime ili tujue corona ipo au laa, ugonjwa wenyewe mbaya jamani kutwa midomoni si mkapime mlete majibu hapa! Magonjwa yaliyokwisha beba ndugu zetu basi acheni tupumzike kulia! Maisha yenyewe magumu hivi!
 
Back
Top Bottom