Naunga mkono hoja yako kejuu! Tatizo chadema ukikosoa wanakuita Lumumba .
Jn baada yakuona kilichotokea mbagara, nilihoji swala la uzinduzi wa ilani yao.
Lakini nilihoji kuhusiana na nini chakusema mgombea wao TL awapo ktk kampeni maana niliona anaendeleza wimbo wa kupigwa risasi ambao kwa masikio yawengi umechosha.
Naona leo mbowe imebidi amwambie pale pale tena live kwamba ajikite kwenye ilani yao ya uchaguzi.
Tatizo ndani ya chadema kuna makundi! Nakama umesikia salam za E.bulaya na za mdee utagundua kuwa kila mtu anajimwambafai kivyake.
E.bulaya anasema kwake hawakuthubutu.
Mdee anasema jimboni kwake hawakujaribu.
Sasa unajihoji hivi ndani ya chadema kuna umoja??
Kifupi kwa picha hii iliyoanza mapema, hata week haijaisha, baada ya 2weeks cyo ajabu ndo mtakuwa mnakutana wenyewe.
Harafu tundu lissu alikosea kuanza kutembea nakufanya mikutano nchi nzima.
Saivi TL ni marudio ya picha. Cyo picha harisi tena.