Ikiwa watalipwa vyeti feki, nimekusudia kuishitaki Serikali

cheti kina badirishwa jina?!!ninachopingana nacho ni kuniambia eti kwa kutumia cheti cha kidato cha nne,cha mtu nikajiendeleza hadi nikawa DR.bingwa bado nitaonekana kuwa cwezi kuwa dr.mzuri,au kuwa injinia mzuri?!
Hilo ndilo jibu nililokua nalitaka sasa wewe huoni hata aibu upo kazini unaitwa jina ambalo silo lako??

Kama wewe ungekua una akili sana ya kufika hadi PHD kwanini usingekazana ufaulu kidato cha nne na kusoma kwa jina lako???

Wizi ni Wizi tu, ilifaa mtupwe jela muda huu
 
Yaani mkuu sijui watu wanatumia akili gani kutetea Wizi huu wa wazi kabisa.......ni kwasababu tu tunaishi kwenye nchi ya kipuuzi....lakini nchi zingine walitakiwa wawe jela.....lakini nchi hii matapeli wanatetewa na kulipwa matunda ya utapeli wao.......inashangaza sana.....
 
Kwan michango imetokana na nini? Si na mshahara
 
Yaani nchi haina Maji afu mtu na kiherere chake tu ana lipa walio foji vyeti? Wahujumu Ajira? Mafisadi?
Chukua hizo hela jenga miradi ya Maji hao wezi watatumia hayo MAJI pia.
 
Kama umekili kweli ulinunuwa cheti cha mtu cha elimu ya kidato cha nne,pia huwezi shindwa nunua cheti Cha Mtu Cha taaluma!! Kugushi ni kugushi tu no excuses,hiyo ni Jinai tayari!! Bora hata unge re siti ningekuona una akili kidogo!!
kwa hiyo mimi leo ni nimeishia kidato cha sita,tena kwa mchepuo wa HGL,naweza vipi kununua cheti cha taaluma cha mtu aliyemaliza shahads ya sheria/udaktari na nikakifanyia kazi kwa ufanisi ,nikaonekana mwanasheria mzuri au daktari bingwa?
 
Hiyo ndo jinai yenyewe
 
Pambana. Unaweza kushinda, hii ni nchi huru
Kwa mfano endapo atashinda kesi, unadhani hukumu ya mahakama itakuwa ni nini? Kwasababu waliolipwa hawataweza kuambiwa wazirudishe maana watakuwa tayari wameshazitafuna. Hukumu si itakuwa ni, "serikali irudishe hizo fedha serikalini". Je hapa si ni sawa na kuhamisha fedha zako kutoka mfuko mmoja na kuziweka mfuko mwingine?
 
Reactions: Tsh
Yaani hata sijaelewa kabisa Hawa watu wanatakiwa wafunguliwe mashtaka...

...
mashitaka gani?ni nani mwenye kosa kati ya serikali na hao vyeti feki.pia tunatakiwa kuwa makini kwa jambo hili nadhani wengi hawajaelewa kiini cha vyeti feki.sijajua wengi wanalitafsiri kwa namna ipi hili jambo.huenda jambo hili linahitaji mjadala mpana ili kuwa na ile kitu inayoitwa common understanding.mfano mm nilimaliza darasa la saba na jamaa mmoja ambaye hakufaulu kwenda kidato cha kwanza enzi hizo tulikuwa tunasema hakuchagulakini akajiunga na chuo cha RMA kwa maana ya rural medical assistant.alivyomaliza aliajiriwa na baada ya miaka mitatu akaenda kusoma CO yaani clinical officer na hatimaye AMO.assistant medical officer.Serikali ilitoa mwongozo baadaye kuwa pia walipaswa kujiendeleza kwa maana ya kuwa na elimu ya sekondari.akafoji cheti cha kidato cha nne na akaondolewa kwenye ajira.je mtu huyo hakuwa competent kama watu wengi humu wanavyojiaminisha?ukiangalia wengi walikumbwa ktk mtego huu kwa ajili ya cheti cha kidato cha nne tu.tujadili.
 
kwa hiyo mimi leo ni nimeishia kidato cha sita,tena kwa mchepuo wa HGL,naweza vipi kununua cheti cha taaluma cha mtu aliyemaliza shahads ya sheria/udaktari na nikakifanyia kazi kwa ufanisi ,nikaonekana mwanasheria mzuri au daktari bingwa?
Why do you have to cheat the process bro!!??
 
ngoja tukuambie Kuna vyeti fake walikuwa wazuri mno kuliko hata waliokuwa na vyeti vyenye majina Yao halisi.cha pili siyo kwamba wanalipwa mafao wanalipwa/wanarejeshewa michango waliochangia kwenye mifuko ya jamii.yaani wanarudishiwa 5%.si unajua mtimishi huchangia 5% na mwajiri humuongezea 15% na hivyo Kila mwezi huwekewa 20% ya mshahara wake kwenye mfuko wa jamii(psssf)maana yake kama alikuwa amechangia 20,000,000/=atalipwa 5% yaani 1,000,000/= tu,hapo kama ingekuwa ni mafao ni ndefu.
 
mwigulu nchemba alisoma Ilboru mm nilikuwa naye ijapo nilimtangulia kwa mbali sana na labda tujadili ukitumia majina ambayo siyo yako lkn ni wewe ndo uliyesoma au kaa darasani ni kosa.huenda alirudia shule akaamua kubadili majina na kwa enzi hizo ilikuwa ni kawaida.hapo kosa liko wapi?
 
Unaishitaki kwa nani ?

Huku ni kama kujipiga kofi mwenyewe !!!!

Labfa utengeneze mchongo ili wakubali Serikali ishindwe ili fidia fulani ilipwe ili wenyewe wajilipe tena kwa Tozo zetu mara baada ya kuunda TUME kuona ni wapi palikosewa..., By the way watakaolipwa huenda kukawa na hewa asilimia kadhaa....

Yaani vyeti feki hewa...., Yaani hizi nguvu na akili zinazotumika kunyonya vijisenti vyetu zingetumika kufikiri jinsi ya kuongeza Keki ya Taifa wala tusingekuwa tunagombania haya makombo
 
Unaandika kwa hisia zako zisizo na ushahidi na kwa kulishwa maneno tu ya watawala waovu..

Una ushahidi hata mtu mmoja unayedai "amesababisha hasara au kifo cha mtu yeyote" kwa sababu ya hiki inachosema "walikuwa na elimu ndogo..?"

Ukitoa ushahidi hapo, mimi pia nitakupa ushahidi wa "wenye elimu kubwa - stashahada, shahada, masters, PhD nk" lakini wenye ufanisi zero kazini kiasi cha kusabisha hasara kwa taifa na pengine vifo kwa watu wengi...!

KWA HIYO SASA;

Kesi yako hiyo ukifanikiwa kuifungua, basi juwa na hakika ya jambo moja kuwa, utashindwa asubuhi na mapema kabla jogoo hajawika...!!

Kazi haifanywi na makaratasi yaitwayo "vyeti". Kazi hufanywa na mtu na matokeo kuonekana...

Kwa mantiki hiyo, watu hawa walikuwepo physically kila mtu akiwaona wakifanya kazi zao vyema na taifa kunufaika na kazi ya mikono yao. Hawakuwa "watu hewa..."

Kwa hiyo hawajaiba popote, hawajamwibia mtu yeyote. Kilicholipwa ni stahili yao..

Na ofcoz kama ni mashitaka, basi ni serikali ndiyo inayopaswa kufunguliwa mashitaka kwa kunyima/kunyang'anya watu haki zao na kuwadhalilisha na wengine kuugua magonjwa ya shinikizo la damu kiasi cha wengi wao kupoteza maisha na familia zao kuvurugika/kusambaratika..

Watu ambao serikali yenyewe iliwapa ajira hizo kwa kupitia michakato halali ya kuajiri na ile ya malipo. Iweje ghafla serikali hiyohiyo iwaone watu hao hao hawana sifa na ni wezi...??

No way..! Yenye makosa makubwa hapa ni serikali...

Iwarudishe watu kazini na iwalipe haki zao zote na pia ilipe gharama za usumbufu iliyowapatia...!
 
Zinatumika njia hata zile haramu alimradi tu malengo ya kisiasa yatimie.
 

Unapoteza muda kaka
 
Mkuu, inasemekana kuna mtu aliwahi koswa koswa na radi akamshtaki MUNGU na kesi ilifunguliwa, huyu kesi yake mbona itasikilizwa tu. Kuna mambo hutakiwa kutumia nguvu kueleweshana, unamuacha mtu atimize nia.
 
Hivi mahakama ikiona hawa vyeti feki hawana hatia serikali ndiyo yenye makosa warudishwe kazini utasaidia serikali kuwalipa malimbikizo yao ya mshahara?

Lakini mwenye roho mbaya hakosi sababu. Ndiyo maana Nyerere aliwafungia vijijini watu walikuwa na kimbelembele. Mapovu yanakutoka utafikiri ni pesa zako. Unaelimishwa lakini una kichwa kigumu Kama mfupa wa goti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…