Ikiwezekana, Bunge lianze na mswada wa dharura kujadili Katiba Mpya; hii Katiba ya sasa kitendo cha Makamu kutambuliwa kuwa mrithi ni hatari

Hicho kipengele cha katiba ni kama kimewatenga wananchi ambao kimsingi ndio wenye jukumu la kuwaweka viongozi.

Halafu mbaya zaidi huyo Rais anayekuja anakuwa na mamlaka ya kuunda upya Baraza lake la mawaziri, na kuwateua wote, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wapya kama akipenda kufanya hivyo.
 
Hoja nzuri ila pia haizuii hilo ulilofikiria kutokea... so long rais ndio anachagua VP wake it's okay
 
Rais wa marekan afe never ever
 
Hivi ile katiba ya warioba ilipendekeza hivi hivi au?
 
Ni imani yangu kuwa like chumba cha miswaada ya hati za dharura kimeshapangishwa na mpangaji ameamua kukinunua kabisa,hivyo sitarajii miswada ya kutetea maslahi ya wachache kwa hati ya dharura.
 
Mimi nadhani hiyo sheria ipo sawa, ila kwa maoni yangu ningependa mtiririko wa kuwa rais kama rais akifariki au kushindwa majukumu yake yawe hivi
1. Rais
2. Makamu wa Rais
3. Mkuu wa majeshi
4. Waziri mkuu
5. Jaji mkuu
 
Mama Samia anatosha kama unateseka nakushauri ungehama nchi kwa miaka 9,
Naam, akimaliza muhula huu atagombea tena na kuendelea kusongesha gurudumu.
 
Hata mtu aliye nje ya mfumo wa utawala anaweza kumdhuru Rais aliye madarakani ama kwa nia ya moja kwa moja au kupitia wasaidizi wa Rais.

Nia yako ni kwamba pindi nafasi ya Urais inapokuwa wazi kwa sababu zozote ikiwemo kifo unataka uchaguzi mpya uitishwe.

Sio kweli kwamba hilo wazo lako halikuwemo kwenye moja ya uwezekano wa kuwekwa kwenye katiba lakini hatimaye kifungu kilicho salama zaidi ndicho kilichowekwa kuepusha mambo mengi oambayo yangesababisha matumizi ya gharama, vurugu, kukosa utulivu.

Sijui umewaza nini mpaka kufuikia hatua ya kutoa pendekezo hilo finye ambalo halijafikiria hasara na faida kisha ukaziweka kwenye mizania.

Wanasiasa ndio mnamatamanio ya kutaka uchaguzi ufanyike ili mpate manufaa yenu binafsi na sio wananchi. Una wasiwasi gani makamu wa Rais kuchukua nafasi hiyo ya juu kabisa ya utawala wa nchi?
 
Mimi nadhani hiyo sheria ipo sawa, ila kwa maoni yangu ningependa mtiririko wa kuwa rais kama rais akifariki au kushindwa majukumu yake yawe hivi
1. Rais
2. Makamu wa Rais
3. Mkuu wa majeshi
4. Waziri mkuu
5. Jaji mkuu
Mtiririko uliouweka ndio uliowekwa kwenye katiba ya Tanzania na ndivyo ulivyotekelezwa
 
Itakua kambi yake haina nafasi kwenye kumtoa VP mkuu..
 
Unateseka Samia kuwa Rais?
Kama huteseki why pendekezo hilo umelileta leo?
Nimeona kifungu hiki kitatuletea shida huko mbele. sinshida na mama samia kuwa Rais, lakini hata yeye anaweza athirika.

Pia tutawapa wanachi nafasi ya kuchagua mtu wanayempenda.
 
Mkuu wa majeshi na Waziri mkuu hawapo kwenye hy ishu
Ni kweli hao hawapo, ila kupendekeza mkuu wa majeshi kuwa miongoni kati ya watu ambao wanaweza kushika nafasi ya Urais endapo yule aliyeko madarakani atakuwa hayupo kwa sababu zozote ikiwemo kifo sio sahihi maana ya yeye anaweza kushikwa na tamaa ya madaraka akaamua kumfitini aliyeko madarakani kwa njia za siri au kufanya uasi.

Kwa hiyo Makamu wa Risi na Jaji mkuu ni sahihi kutokana na kuwa tayari wanafanya majukumu ya kitaifa; kasoro moja ni kwa Jaji mkuu kumtumia kuongoza/kutawala nchi kwenye mambo ya kisiasa.
 
Ni wakati Sasa wa kuwashirikisha 'INTERPOL' kuondoa utata wa USHIRIKI WA WASIOJULIKANA KWA SIASA ZA BONGO, ... tuanzie kwa Lissu, Ben Saanane, Azory ......! ... MAANA HAKUNA TENA NAMNA!
πŸ‘ŠπŸ˜…βœŒοΈπŸ’₯
 
Ni wakati Sasa wa kuwashirikisha 'INTERPOL' kuondoa utata wa USHIRIKI WA WASIOJULIKANA KWA SIASA ZA BONGO, ... tuanzie kwa Lissu, Ben Saanane, Azory ......!
πŸ‘ŠπŸ˜…βœŒοΈπŸ’₯
Ndoto za alicha hizo......sura, maneno na taswira ya kike unayoifikiri kuingilika kwa nia ya kugeuza kilichokuwa kinafanyika usikitarajie la sivyo atapoteza uungaji mkono hivyo ataanza kujuta. Hakuna kitakachobadilika

1. Mshahara kuongezeka ulishapangwa na hayati akishirikiana na makamu, waziri mkuu hivyo kitakachotokea ni kile kilicho kubaliwa tu na kwa mjibu wa Ilani yao. Hakuna matakwa ya mtu kuridhisha kundi fulani linafikiri liliumizwa maana yeye alikuwa sehemu ya kile kichotekelzwa na kitakachotekelezwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…