Ikiwezekana, Bunge lianze na mswada wa dharura kujadili Katiba Mpya; hii Katiba ya sasa kitendo cha Makamu kutambuliwa kuwa mrithi ni hatari

Hili jambo ni la msingi sana maana katiba imewacha sana nafasi ya mambo ya hovyo kufanyika
Huu ni mwanya. unaweza tumika vibaya. Zaidi ya hapo wanchi hawapati nafasi ya kumchagua. Pia, wakati mwingine Nafasi ya makamu wa Rais anapewa tu mtu ili kujaz nafasi, bila kuwaz kwanba anaweza kuwa raisi siku moja.
 
Mimi nadhani hiyo sheria ipo sawa, ila kwa maoni yangu ningependa mtiririko wa kuwa rais kama rais akifariki au kushindwa majukumu yake yawe hivi
1. Rais
2. Makamu wa Rais
3. Mkuu wa majeshi
4. Waziri mkuu
5. Jaji mkuu
Mkuu wa Majeshi ??? Hapana
 
Mnawaza madaraka tu, mngekuwa mnaongoza nyinyi ungekubali?
 
Huu ni mwanya. unaweza tumika vibaya. Zaidi ya hapo wanchi hawapati nafasi ya kumchagua. Pia, wakati mwingine Nafasi ya makamu wa Rais anapewa tu mtu ili kujaz nafasi, bila kuwaz kwanba anaweza kuwa raisi siku moja.
Sio kweli kwamba makamu wa Rais anapewa ila ni haki yake kwa sababu wakati wanajinadi wote kwa pamoja walizunguka nchi nzima kuomba kura ingawa kwa JPM kura nyingi zilitokana na utendaji wake binafsi lakini katika uhalisia wote wanastahili sifa hizo ndio maana kila mgombea Urais anatakiwa kuteula mgombea mwenza makini na sio ilimradi aonekane ametimiza matakwa ya sheria.
 
Mkuu hata mimi nimeshangazwa sana na hili, angetakiwa akaimu hiyo nafasi kwa miezi mitatu na kuitisha uchaguzi upya. Au laa, kama umebaki chini ya mwaka mmoja ndo aendelee hadi muda wa uchaguzi mwingine utakapowadia.

Miaka minne ni mingi sana kwa rais ambaye hajachaguliwa na wananchi.....ndo maana sasa tunashuhudia minyukano ya kugombania nafasi ya umakamu...
 
Umenena vyema. Makamu wa rais huwa ni mgombea mwenza. Asante kwa kukumbusha umma.
 
Una uhakika?
 
Kuna umuhimu wa hicho kipengere cha katiba kibadirishwe. Ikitokea kama hivi vizuri ukaitishwa uchaguzi ndani siku kadhaa
 
kusema kweli Wagobea wenza wengi wana sifa lakini hziwezi kufikia za wagombea wenyewe. halafu kwa upande mwingine makamu anaweza kupata tamaa. Pia ingeondoa kugombania nafasi hiyo kama ilivyo sasa ndani ya CCM
 
Ahahahahaha kilianguka jana
 
Nakubaliana na wewe 100% Makamubawe rais mwa miezi 6 baada ya hapo ufanyike uchaguzi
 
Mkuu unaelewa maana ya mgombea mwenza? Nafasi wameigombania kwa pamoja, kwahiyo ni kama yao wote. Labda angalizo litolewe kwa vyama kuwa wa hakikishe both candidates are of equal capacity\potentials, otherwise it is too early to forecast and judge.
 
Tukia weye dawa iwaingie timu chato!! Hii nchi si yenu, marehemu aliwajazaujinga saana sasa Mungu kaingilia kati hamtoboi.
 
Uchaguzi ili kuwe nini? Uchaguzi huo utakuwa uchaguzi wa raisi tu au uchaguzi mkuu ikiwa ni pamoja na wabunge. Sababu zako za kutaka uchaguzi mpya ni zipi. Au unadhania utapata nafasi ya kuukwaa uraisi. Mtu mwenyewe wa kuwa raisi ni nani? Yule mkimbizi mwenye uraia pacha amba ni illegal TZ! Ngonja Mama Suluhu atawale. Baada ya hapo atagombea na kushinda, na tapewa mingine mitano.

Ambalo sijui ni kama muda wa sasa unahesabika kaktika ukomo wa kuogombea! Hebu wajuvi wa katiba watusaidie, katiba inasemaje. Je anaweza akapiga miaka 14?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…