Ikulu imefanikiwa kudhibiti kabisa uvujaji wa taarifa zote nyeti na za siri

Ikulu imefanikiwa kudhibiti kabisa uvujaji wa taarifa zote nyeti na za siri

Zilikua ni habari za uwongo Ili wapate 'tundu'lao
Mdomo huumba.

Mwanzoni mwa mwaka huu kijana mmoja alipiga simu kwa Supervior wake wa idara kumjulisha kuwa "hataingia kazini kwa sababu amepata ajali ya bodaboda"
Na haikuwa kweli alitengeneza sababu ya uongo ili tu asiende kazini,
Baada ya miezi kadhaa kupita usiku wa July 9 akiwa anatoka kazini kwa usafiri wa bodaboda wakiwa wamepakiwa mtungo walipata ajali na alifariki yeye peke yake.

Mdomo huumba.
 
Mdomo huumba.

Mwanzoni mwa mwaka huu kijana mmoja alipiga simu kwa Supervior wake wa idara kumjulisha kuwa "hataingia kazini kwa sababu amepata ajali ya bodaboda"
Na haikuwa kweli alitengeneza sababu ya uongo ili tu asiende kazini,
Baada ya miezi kadhaa kupita usiku wa July 9 akiwa anatoka kazini kwa usafiri wa bodaboda wakiwa wamepakiwa mtungo walipata ajali na alifariki yeye peke yake.

Mdomo huumba.
Mdomo hauumbi,kazi ya ukachero ina mengi
 
Ndugu zangu Watanzania,

Napenda niwaambieni ya kuwa Ikulu ni jumba moja kubwa sana lenye kila aina ya watu,idara na viongozi mbalimbali nyeti ambao wengine inawezekana kabisa hawajawahi kuonekana wala kuonyesha sura zao katika macho ya watanzania au kunaswa na Camera ya aina yoyote ile.

Ikulu ni mahali ambapo ndipo Makazi Rasmi ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama.ndipo akaapo Raia nambari Moja ambaye yeye ndiye kila mtanzania humuangalia yeye na mahali ambapo taarifa zote za siri na nyeti hufikia na kutua hapo na kuchakatwa kila uchao kutoka ndani na nje ya Nchi.

Ni mahali ambapo maamuzi yote makubwa huanzia na kutolewa hapo,ni mahali ambapo macho ya vyombo vyote vya ulinzi na idara zake zote huelekeza macho yake.ni mahali ambapo ndio hutoa taswira ya Nchi na muelekeo wake, ni mahali ambapo ndio msingi wa kila kitu tukionacho hapa Nchini, ni mahali ambapo teuzi zote nyeti na kwa watu wote huchakatwa hapo na kutikisa vichwa ili hatimaye yasifanyike makosa ya kiufundi.

Ni mahali penye kioo chenye kuonyesha Tanzania yote na kujua kila kitu kinachoendelea mahali popote pale Tanzania,ni mahali ambapo hata ukizungumza jambo lolote lile bar litafika na kuonekana katika kioo cha Ikulu. Ni mahali penye mlolongo mrefu sana na wa kila aina ya watu na vyeo na majukumu yao na idara zao katika kukamilisha muundo mzima wa ikulu na taasisi ya Urais.

Hivyo basi Ukiona Jengo kama lile na taasisi ya Urais yenye watu mbalimbali na wa kila aina kutoka makabila mbalimbali. wanafanikiwa kudhibiti kabisa uvujaji wa siri na taarifa nyeti kwenda kwa watu ,.basi ujuwe mahali hapo ni salama sana.

Ukiona Rais wa Nchi tena anayependwa na wananchi wake na kuulizwa na watu hata asipoonekana hadharani kwa siku moja kama ilivyo kwa Rais Samia.lakini taarifa zake za wapi alipo zaidi ya wiki moja pasipo kuonekana hadharani kuwa siri.basi Ujuwe kuwa Rais ni salama sana na anawatu makini sana waliomzunguka na wenye kuzingatia viapo vyao kikamilifu.

Hii Maana yake ni kuwa Rais amezungukwa na watu sahihi,makini,wenye kuzingatia viapo vyao, waadilifu,waaminifu wa kiwango cha juu, wazalendo na waliotayari kufia viapo vyao pasipo kukiuka na kusaliti viapo vyao. Hii Maana yake ni kuwa Rais wetu yupo salama wakati wote na katika mzunguko wa watu waaminifu na wenye upendo wa dhati kabisa kwake na Taifa letu.

Hii maana yake ni kuwa Rais wetu anakubalika sana katika idara zote na kwa watu wote , anapendwa sana na amekidhi matarajio ya watu na ndio maana ya kuaminika na watu kuwa wazalendo.Maana kama ingekuwa tofauti ungekuwa ukiona uvujaji wa taarifa juu ya wapi aliko Rais. Watu wenye chuki binafsi au kutumiwa na watu wangevujisha siri.

Lakini sote ni mashuhuda tuliona namna ambavyo taarifa zilibakia kuwa siri mpaka RAIS wetu mpendwa alipotokea hadharani kikomandoo na kuifanya Nchi yote kulipuka kwa shangwe, nderemo,vifijo na kutamalaki kwa tabasamu, furaha na vicheko vya furaha katika nyuso za Watanzania.

Huku wale wapiga Ramli na mashetani wakubwa wafanyao kazi ya uwakala wa shetani wakishikwa na aibu kuu na kubakia Kama mahayawani tu yasiyojitambua. Umbea, uzushi na uongo wao ukafa kifo cha aibu na fedheha kubwa sana.

Rais wetu kipenzi akatokeza akiwa mwingi wa tabasamu, kikakavu, kishupavu, kihodari Utafikiri wale makomandoo waliokwenda mpaka pakstani kupambana na Osama bin laden na kummaliza kikomandoo ndani ya dakika chache sana.

Napenda kusema kuwa wale Wenye chuki binafsi na Rais Samia watakufa kwa presha mwaka huu.Huyu Mama ni chaguo la Mungu mwenyewe na ni mpango wake Mungu mwenyewe kufika hapo alipo fika. Rais Samia ataishi zaidi ya karne Moja hapa Duniani kwa Uweza wa Mwenyezi Mungu mwenyewe huku akiwa mwenye afya njema na nguvu kimwili na kiakili.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kwa hili naungana na wewe kabisa...Safari hii wamelamba hola...Ahsanteni sana askari in and un combat...Mmetisha!
 
Kwani ikulu ni Mali ya mtu binafsi hadi wafanye mambo Kwa Siri?kwani nchi ni ya mtu binafsi Hadi wananchi ambao ndiyo wenye Nchi wafichwe yanayofanywa na viongozi?Ikulu inayoficha taarifa ili wananchi ambao ndiyo wenye Nchi, ujue hiyo Nchi inaongozwa na wahuni na hawafai kabisa kupewa ofisi za umma
Acha hasira, kaanze upya😂
 
Huyu mama mtamuua kwa stress, sijaona comment nzuri humu.
 
Tanzania 🇹🇿

Nchi ambayo raia wake hawana msimamo.

Nchi ambayo viongozi wa dini pia ni chawa.

Nchi ambayo uzalendo ni kwa masikini tu.

Nchi ambayo elimu yake haina maana au impact kwa maendeleo.

Nchi ambayo wanasiasa ni tajiri kuliko wafanya biashara.

Nchi ambayo michezo wa timu mbili za mpira ni gumzo la nchi nzima nk nk.
Nchi ambayo sera yake kila siku ni matukio ya kuwadistract watu wake.
 
downloadfile-1.jpg
 
Kama Taharifa za nchi kama China zinavuja sembuse TZ..

Wamkamate kwanza kigogo ndio nitaamini Tuna ulinzi wa kutosha..

Acheni BLAH! BLAH!
 
Ndugu zangu Watanzania,

Napenda niwaambieni ya kuwa Ikulu ni jumba moja kubwa sana lenye kila aina ya watu,idara na viongozi mbalimbali nyeti ambao wengine inawezekana kabisa hawajawahi kuonekana wala kuonyesha sura zao katika macho ya watanzania au kunaswa na Camera ya aina yoyote ile.

Ikulu ni mahali ambapo ndipo Makazi Rasmi ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama.ndipo akaapo Raia nambari Moja ambaye yeye ndiye kila mtanzania humuangalia yeye na mahali ambapo taarifa zote za siri na nyeti hufikia na kutua hapo na kuchakatwa kila uchao kutoka ndani na nje ya Nchi.

Ni mahali ambapo maamuzi yote makubwa huanzia na kutolewa hapo,ni mahali ambapo macho ya vyombo vyote vya ulinzi na idara zake zote huelekeza macho yake.ni mahali ambapo ndio hutoa taswira ya Nchi na muelekeo wake, ni mahali ambapo ndio msingi wa kila kitu tukionacho hapa Nchini, ni mahali ambapo teuzi zote nyeti na kwa watu wote huchakatwa hapo na kutikisa vichwa ili hatimaye yasifanyike makosa ya kiufundi.

Ni mahali penye kioo chenye kuonyesha Tanzania yote na kujua kila kitu kinachoendelea mahali popote pale Tanzania,ni mahali ambapo hata ukizungumza jambo lolote lile bar litafika na kuonekana katika kioo cha Ikulu. Ni mahali penye mlolongo mrefu sana na wa kila aina ya watu na vyeo na majukumu yao na idara zao katika kukamilisha muundo mzima wa ikulu na taasisi ya Urais.

Hivyo basi Ukiona Jengo kama lile na taasisi ya Urais yenye watu mbalimbali na wa kila aina kutoka makabila mbalimbali. wanafanikiwa kudhibiti kabisa uvujaji wa siri na taarifa nyeti kwenda kwa watu ,.basi ujuwe mahali hapo ni salama sana.

Ukiona Rais wa Nchi tena anayependwa na wananchi wake na kuulizwa na watu hata asipoonekana hadharani kwa siku moja kama ilivyo kwa Rais Samia.lakini taarifa zake za wapi alipo zaidi ya wiki moja pasipo kuonekana hadharani kuwa siri.basi Ujuwe kuwa Rais ni salama sana na anawatu makini sana waliomzunguka na wenye kuzingatia viapo vyao kikamilifu.

Hii Maana yake ni kuwa Rais amezungukwa na watu sahihi,makini,wenye kuzingatia viapo vyao, waadilifu,waaminifu wa kiwango cha juu, wazalendo na waliotayari kufia viapo vyao pasipo kukiuka na kusaliti viapo vyao. Hii Maana yake ni kuwa Rais wetu yupo salama wakati wote na katika mzunguko wa watu waaminifu na wenye upendo wa dhati kabisa kwake na Taifa letu.

Hii maana yake ni kuwa Rais wetu anakubalika sana katika idara zote na kwa watu wote , anapendwa sana na amekidhi matarajio ya watu na ndio maana ya kuaminika na watu kuwa wazalendo.Maana kama ingekuwa tofauti ungekuwa ukiona uvujaji wa taarifa juu ya wapi aliko Rais. Watu wenye chuki binafsi au kutumiwa na watu wangevujisha siri.

Lakini sote ni mashuhuda tuliona namna ambavyo taarifa zilibakia kuwa siri mpaka RAIS wetu mpendwa alipotokea hadharani kikomandoo na kuifanya Nchi yote kulipuka kwa shangwe, nderemo,vifijo na kutamalaki kwa tabasamu, furaha na vicheko vya furaha katika nyuso za Watanzania.

Huku wale wapiga Ramli na mashetani wakubwa wafanyao kazi ya uwakala wa shetani wakishikwa na aibu kuu na kubakia Kama mahayawani tu yasiyojitambua. Umbea, uzushi na uongo wao ukafa kifo cha aibu na fedheha kubwa sana.

Rais wetu kipenzi akatokeza akiwa mwingi wa tabasamu, kikakavu, kishupavu, kihodari Utafikiri wale makomandoo waliokwenda mpaka pakstani kupambana na Osama bin laden na kummaliza kikomandoo ndani ya dakika chache sana.

Napenda kusema kuwa wale Wenye chuki binafsi na Rais Samia watakufa kwa presha mwaka huu.Huyu Mama ni chaguo la Mungu mwenyewe na ni mpango wake Mungu mwenyewe kufika hapo alipo fika. Rais Samia ataishi zaidi ya karne Moja hapa Duniani kwa Uweza wa Mwenyezi Mungu mwenyewe huku akiwa mwenye afya njema na nguvu kimwili na kiakili.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.

Kweli sisi ni special specie wandugu, yani chawa bila aibu unakuja kujivunia kabisa wanasiasa na waajiriwa wa wananchi kufichwa taarifa? Watu wanataka uwazi na hata hao unaowasifia wanajisifia wana uwazi japo ni uongo. Aisee...

Nisijekufuru nchi ya baba na mama yangu ilipofikia nijinyamazie tu sasa
 
Back
Top Bottom