Tetesi: Ikulu ya Marekani yatangaza dawa dhidi ya Corona, shukrani sana wazungu, mbarikiwe

Virus anakaa kwenye damu, sasa kujifukiza na mvuke kuna tibu vipi au kuua vipi yule virus? Ule mvuke unaenda kuchemsha damu au?
Binafsi siamini katika hilo kwa maana wengi wamepona pasipo hata dawa, Tatizo tiba za huku Africa ni kama watu wana tapa tapa na kubahatisha kama michezo ya Casino, mtu anakwambia jifukize 100°C mvuke, hivi hii imekaaje?
At least wazungu dawa zao wanaelezea kitaalamu na kisayansi, hapa jamani tusichukie, kama tunatumia mitishamba basi wafanye tafiti za kisayansi kujua huyo kirusi yuko vipi na jinsi gani ya kumkabili,wazungu ndio waligundua yule virus kwa sehemu kubwa ni mafuta wakitumia vyombo vya kisasa kama microscope za umeme, mwafrika kuona hivyo akaona amalizie kwa kufukiza eti kisa ni futa, we unaweza kuua virus yupo damuni kwa mvuke?
Dawa hata ile ya Madagascar inapaswa waelezee kitaalamu, waelezee ina vyofanya kazi mwanzo mwisho, waelezee inawezaje kumkabili yule mdudu? Tukifanya hivi hakika hata mzungu atajiona mjinga,hata wakitu beza kuna mataifa mengi watavutiwa na utaalamu kama huo,jamani tuishi kwa nyakati, tusikasirike kuambiwa ukweli, hata ukinunua mseto ya malaria utakuta ndani karatasi ina maelezo ya kitaalamu mwanzo mwisho,mpaka effects za dawa,vyakula vipi usile n.k, wazungu wapo specific sana tuchukueni mazuri yao na tujifunze, dawa nyingi za Africa tunapona kwa imani tu kama sio kubahatisha.TUBADILIKE.
 
Fauci nae ameshakuwa politician tu sasa hii pandemic ka grab attention ya kutosha haswa alivyo mlipua trump
 
Alafu hii habari mbona inatembea sana kwenye source za Africa US. Hata hakuna
Ndio mujijue kama waafrica mnawapenda wazungu mpaka mnawazushia habari ambazo hata wenyewe hawana

Sent using My COVID-19
 
Huu udaku umeutoa wapi wewe mkikuyu[emoji23][emoji23][emoji23] Kama dawa waache watibiane wenyewe kwanza huko maana wanafariki kama kuku wamdondo

Mungu awafanyie wepesi wapone ila kwaleo umetudanganya wewe mkikuyu

Sent using My COVID-19
 
Huu udaku umeutoa wapi wewe mkikuyu[emoji23][emoji23][emoji23]Kama dawa waache watibiane wenyewe kwanza huko maana wanafariki kama kuku wamdondo

Mungu awafanyie wepesi wapone ila kwaleo umetudanganya wewe mkikuyu

Sent using My COVID-19
Muajemi ndio umeamka nini? Maana huu sijakuona kwenye siti za mbele.
 
Huu uzi mbona wenye akili wachache ndo wameuelewa. Hata mleta mada mwenyewe kauleta kishabiki. Dawa hakuna.
 
Ndio mujijue kama waafrica mnawapenda wazungu mpaka mnawazushia habari ambazo hata wenyewe hawana

Sent using My COVID-19
Ni kweli Anthony kazungumza hivyo lakini hiyo habari hata hai-trend kwenye source zao even H.E Trump hajasema lolote.
 
Huu uzi mbona wenye akili wachache ndo wameuelewa. Hata mleta mada mwenyewe kauleta kishabiki. Dawa hakuna.
Wewe ndiye unapigwa chenga na mambo ya kiutaalam kama haya, au labda lugha inakupiga chenga, ni kweli hamna dawa ya kuponya Corona, actually hamna dawa ya kuponya kirusi chochote dunia hii hata mafua, dawa iliyopo ni ya kupunguza makali yake mpaka siku kitakufa chenyewe. Mutations za virusi hufanya ngumu kutengeneza dawa ya kuponya, na ndio maana hata UKIMWI mpaka leo hamna dawa ya kuponya, ila ipo ya kupunguza uwezo wake.

Hii Corona haidumu kwa mwili kwa muda mrefu, hivyo ukiwa na uwezo wa kubaki hai mpaka wakati inajifia, basi unapona, na ndio maana zipo dawa za kusaidia kwenye hiyo process.
 
"Ikulu ya Marekani yatangaza dawa dhidi ya corona" ndo heading yako.
Kwenye content kuna point ya msingi umeambiwa "...experimental drug" sasa wewe tiyari ushaanza kushangilia na kuiita dawa ya kutibu.
Experimental drugs za UKIMWI zilishafanyika mara nyingi na mpaka leo ugonjwa upo. Experimental drug haiwezi tolewa kwa watu waitumie, hiyo itakaa kwa watu wachache waliojitolea na wawe monitored. Dawa hujajua side effects zake na effectiveness yake unaitoaje kwa watu.
Ndo maana nakwambia umeikuza taarifa.
 
Muajemi ndio umeamka nini? Maana huu sijakuona kwenye siti za mbele.
Dawa ya Virus Uliwahi Kuiona Wapi [emoji23][emoji23][emoji23]


Au unaongelea Ant Virus Ya Window[emoji12][emoji14][emoji12]

Sent using My COVID-19
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Kama unajua nakuelewa nakufahamu yakwamba hakuna dawa yakorona futa huu udaku wako ulio andika au wewe umeandika Ikulu Yamarekani Imetangaza Nini [emoji3][emoji23][emoji16]?!

Wamarekani Wakismayo na Mombasa Mnataabu Sana Asee [emoji23][emoji23][emoji23][emoji3][emoji23]

Sent using My COVID-19
 

Ikulu ya Marekani imetangaza dawa dhidi ya Corona, kwa kifupi dawa waliotangaza ni ya kupambana na Corona, sio Malaria au kitu kingine.
Pili, jua tofauti kati ya kutibu na kuponya, sijasema wametangaza dawa ya kuponya Corona.
Wametangaza imefaulu majaribio na kuonyesha uwezo mkubwa dhidi ya Crona.
Taasisi ya U.S. Food and Drug Administration imeombwa itoe ruhusa ya matumizi yake kwa dharula.
 
Mbona ya nchini Madagasca waliikataa eti kwa kuwa bado muda ni mapema sana? Sisi tutatumia ya Waafrika wenzetu ambao walishaitangaza mapema!
 
Vipi na yule Mwingereza waliyemchoma dawa ya majaribio ya chanjo akafa imekuaje mpambe wa wazungu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…