Ikulu yawajibu Maaskofu wa Pentekoste kuhusu Wajumbe wa Bunge la Katiba

Ikulu yawajibu Maaskofu wa Pentekoste kuhusu Wajumbe wa Bunge la Katiba

Kwani msimamo wao ni wa kutambua serikali tatu au mbili? Kama wanapendelea serikali tatu ndo maana wameachwa na ikulu yetu tukufu! Ccm kwanza,taifa baadae!
 
Sijawahi kusikia tamko lolote lenye chembe ya ukweli kutoka Ikulu ya Magogoni...
 
Ikulu imetoa taarifa ndefu kuhusu madai ya maaskofu wa pentekoste (PCT) kuwa wametengwa kwa mjumbe wao kutokuchaguliwa katika bunge la katiba licha ya kupeleka majina kwa rais.

Kwa ufupi ikulu imesema baada ya uchunguzi imegundua kuwa maaskofu wa pentekoste hawakuwasilisha majina kwa njia ya kawaida, kujiteua ama kwa kuchelewa kwani database ya ikulu haijaonyesha ripoti ya maaskofu hao kutuma majina kwao.

Aidha ikulu imesema mjumbe mmoja alieteuliwa kwenye taasiai za dini Bi Edna Adam ametoka kanisa la EAGT ambao ni miongoni kwa wanachama wa baraza la maaakofu wa Pentekoste licha ya kwamba jina lake liliwasilishwa na taasisi nyingine ya dini na sio Baraza hilo la Maaskofu wa Pentekoste. Hivyo ikulu imewaomba maaskofu hao kumtumia mjumbe huyo kama mwakilishi wao na kuwa watawakilishwa kikamilifu.

Nitaiweka statement yote later licha ya kwamba ni ndefu sanaaa.
Lakini sisi tulitaka kakobe buana.
 
Hata Mtikila ni Pentecoste si wangle sema ndio mwakilishi wao? Kingunge anawasilisha wachawi, JK angeweka waliookoka si majini ya Kingunge yangekosa nguvu...

Na ulinzi wa majini maimuna yanamlinda kikwete yangekula kona mweee, mola akulaze unapostahili ewe shehe yahaya
 
Serikali dhaifu na ya kijanja haikosi neno la kusema hata kama imekosea itajitutumua ili kuzidi kuwahadaa Wananchi kwa kujionyesha mbele ya Vyombo vya Habari kuwa wao wako sahihi.
 
Simple like that??? Jk anafanya urais uonekane hata darasa la saba anaweza kuongoza,kama majibu yenyewe niya rejareja hivi. Hivi ikulu mnajidanganya kuwa wapentekoste ni kikundi kidogo siyo!!!!
 
Serikali dhaifu na ya kijanja haikosi neno la kusema hata kama imekosea itajitutumua ili kuzidi kuwahadaa Wananchi kwa kujionyesha mbele ya Vyombo vya Habari kuwa wao wako sahihi.
 
poleni maaskofu, hata hivyo wajumbe hawaendi kuandika biblia mpya isuiwaume sana ya kaizer mwachieni kaizer, au ninyinyi ni maaskofu maslahi???
 
poleni maaskofu, hata hivyo wajumbe hawaendi kuandika biblia mpya isuiwaume sana ya kaizer mwachieni kaizer, au ninyinyi ni maaskofu maslahi???

Acha siasa za ujamaa hapa. Katiba ni ya Watanzania wote, siyo ya Kaisari. Maaskofu hao nao wana haki ya kuwakilishwa. Period.
 
Wimbo wa "Serikali haina dini" ni ulaghai. Inazidi kuwa dhahiri sasa kwamba Serikali ya Tanzania ina "dini zake"!
 
"Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa, shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa, lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu." (MATENDO 5:38-39).
 
Nchi ya ajabu sana hii, najiuliza hivi ingekuwa ni Sunni ama Shia ndo wameandika kulalamika kama hawa maaskofu ikulu ingejibu? kwanini hawa maaskofu ndo wanajiona wao ni makundi maalum wanataka nafasi maalum?
 
mbona mnalala sana mlikuwa wapi siku zote?

Hili nalo neno,maaskofu wa kipentekosti wengi wao humsifu sana kikwete,kasoro Gwajima na kakobe.Huwenda Mungu anawakumbusha wajibu wenu wa kukemea watawala waovu.
 
Sijafuatilia sana na madai ya maaskofu, ila ku-comment tu kuhusiana na majibu ya ikulu... Hivi mtu atakuwakilisha vipi wakati haukumtuma akuwakilishe..? Huyu atakuwakilisha wewe au atawakilisha waliomtuma na waliompendekeza akuwakilishe...!.?
 
Back
Top Bottom