ILBORU SEC SCHOOL chini ya jeshi la polisi kuanzia muda huu!


daahh inasikitisha sana kuondoka shule hasa kipindi hiki
 
Sisi watanzania tunapenda kupewa sifa na kujisifia unaweza kuwa umefaulu vizuri kumbe ni kwa kukariri au kuibia, usomi ni pamoja na kuwa na staha, heshima, na kuthamini wengine sasa nyie wasomi wa siku hizi ni kujisifia tuuu, amkeni.
 
daahh inasikitisha sana kuondoka shule hasa kipindi hiki



Mkuu nakwambia yani ni janga fluu ila haya yote yanajiri kwa sababu ya uongozi legelege ya Serikali iliyoko madarakani na hata haya yote wanajua vyanzo.
 
Molembe hebu funguka vizuri maana labda una kitu unataka kusema ila unasita Molembe..........funguka tu hapa jukwaani tunaelimishana muda mwingine. Karibu Molembe
 
Last edited by a moderator:
Habari zilizonifikia toka kwa mmoja wa wanafunzi wa shule tajwa hapo juu ni kwamba mkutano umeendelea tangu juzi na mpaka waziri wa elimu na kutaka bodi ya shule iwarudishe wanafunzi wote shuleni mara moja.
Hata leo mkutano huo umeendelea na yote yaliyojiri nitawajuza kwani nafanya mpango wa kukutana na mdau mmoja ambaye ni mmoja kati ya wanabodi wa shule anipe michapo yanayoendelea mpaka leo wanafunzi hawako shuleni.

Ntarudi...............!
 

Kwani hujui chanzo? Mbona kipo wazi kuwa baadhi ya wanafunzi walipandisha BENDERA YA CHADEMA shuleni. Na walipotaka wataje, hakuna aliyethubutu hata kwa kutishwa. Ndipo watu wa kazi walipoitwa kuiwasimamia wanafunzi kuondoka.
 
huo mgomo tuu! Nakumbka ndanda tulipewa masaa matatu tuu kila mtu asepe daah we achaa.! Polen wana najua hapo wengine wana elfu 10 tuu na home mbali nje ya mkoa

HAHAHAHA kumbe umesomea ndanda? ,serikali itatue kero za shule zake bila kuathiri taaluma
 
Kwani hujui chanzo? Mbona kipo wazi kuwa baadhi ya wanafunzi walipandisha BENDERA YA CHADEMA shuleni. Na walipotaka wataje, hakuna aliyethubutu hata kwa kutishwa. Ndipo watu wa kazi walipoitwa kuiwasimamia wanafunzi kuondoka.


Updates.........!

Pamoja na kuwaondosha wanafunzi shuleni kuanzia form one hadi six hatimaye walikuja kuwarudisha form two kwa ajili ya mtihani wa national ambao umemalizika mwishoni mwa wiki hii na hata hivyo baada ya mtihani habari nilizonyaka ni kwamba watoto wote warudi makwao na ifikapo tar 28/10/2013 wafike hapo shuleni na wazazi wao.
Na hata hivyo waje na barua ya watendaji wa vijiji wanavyotoka. Sasa sijui ni nini hawa walimu na uongozi wote wa juu wanataka. Na ukizingatia form four ndio hao kwenye mtihani siku si nyingi.

Kwa kweli Mi idara ya elimu na serikali yake yote tawala inatupa maswali yasiyo na majibu hata kidogo.

Haya maneno ya Mbunge wangu G. Lema inanipaga Amani sana.

Ukiona giza linatanda sana, ujue karibia kunakucha!
 
yaani huyo mkuu alitususpend kwa miez saba kosa la cm form five huna shule six unakuja ck ya necta.sio sili huyo mkuu atawaumiza na kushusha taaluma ya shule.nilisikia kahamia hapo akitokea tosamaganga.kuwen makini mtaumia nyie.nawaonea huruma wadogo zangu.c mbali sana yalinikuta hapo tosa tar 27mwez wa 8 mwaka 2012.
 
kifumbiko nakwambia hiyo tarehe tajwa hakika nitaenda pale shuleni kama mzazi wa mtoto na nitakuja na maneno ya huko.
 
Last edited by a moderator:
Leo ni tar 28/10/2013

HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA
SHULE YA SEKONDARI ILBORU
UTARATIBU WA KUFUATWA ILI MWANAFUNZI AWEZE KUPOKELEWA SHULENI BAADA YA SHULE KUFUNGWA (17.09.2013)

A) Sambamba na sheri,kanuni na taratibu za shule mwanafunzi anatakiwa kukubali kuwa;
1. Hatapatikana nje ya shule bila kibali cha Mkuu wa Shule ikiwa ni pamoja na kutokuonekana katika nyumba za watumishi bila kibali cha Mkuu wa shule.
2. Usafi shuleni ni jukumu la kila mwanafunzi tangu kidato cha 1-6,na badiliko lolote litatokana na uamuzi wa Mkuu wa shule.
3. Mfanyakazi yeyote wa shule bila kujali jinsia ataingia Bwenini bila kizuizi cha mwanafunzi yeyote.
4. Mwanafunzi atapangiwa na mwalimu husika darasa na bweni na kuwajibika kutii sheria na kanuni zilizopo shuleni kama ilivyoambatanishwa.(Kiambatisho cha 2)
5. Hakuna Mwanafunzi atakayeruhusiwa kumiliki chumba ama ofisi shuleni.
6. Ni marufuku mwanafunzi kufanya marekebisho yoyote ya miundombinu ya shule.
7. Katika ukaguzi wowote shuleni mwanafunzi yoyote yuko chini ya mamlaka akaguliwe na mtumishi yeyote wa shule.
8. Mwanafunzi akubali kula chakula kitolewacho shuleni kulingana na uwezo na maelekezo ya serikali.
9. Sare ya shule inayotakiwa kwa mwanafunzi anayetakiwa kurejea shuleni izingatie vipimo na isibanwe wala kuongezwa mtindo tofauti na maagizo ya masharti ya kujiunga na shule. (suruali upana chini iwe kati ya inchi 17-18)
10. Kila mwanafunzi awajibike binafsi kutoshiriki kikao ama mkutano wowote au matangazo yasiyo na kibali cha mkuu wa shule.
11. Ni marufuku mwanafunzi kutohudhuria darasani,kutokufanya ama kugomea mtihani ama masomo.
12. Hairuhusiwi mwanafunzi kubaki shuleni wakati wa likizo au amri ya kuondoka shuleni.
13. Mwanafunzi haruhusiwi kujadili au kuhoji maamuzi halali iliyofikiwa na vikao vya wafanyakazi,uongozi wa shule ama bodi ya shule.
14. Ni marufuku mwanafunzi kumkataa mwalimu,kukataa kufanya kazi darasani.
15. Ni makosa makubwa kuchelewa kurudi shuleni kutoka likizo.
16. Mwanafunzi atapokewa akiwa amelipa ada na michango yote ya shule. Pamoja na wale wanaolipiwa na Halimashauri

17. Makosa yafuatayo adhabu yake ni kufukuzwa shule.
1; Wizi 2;Uasherati,ubakaji,ushoga 3;Ulevi na matumizi ya dawa za kulevya 4;Uvutaji wa bangi 5; Makosa ya jinai 6; Kupigana au kupiga 7; Kuharibu kwa makusudi mali ya umma. 8; kudharau bendera ya Taifa 9; Kuoa 10;Kusababisha mimba ndani na nje ya shule 11; Kushiriki kutoa mimba 12;Kugoma kuchochea na kuongoza ama kuvuruga amani na usalama wa shule 13; Kukataa adhabu 14; Kukamatwa na simu shuleni.

Hayo ndio masharti bodi ya shule kongwe ya Ilboru imeweka kwa wanafunzi wao.
Wanafunzi wote wamerejea shuleni na vipengele hivyo leo.

Nitarudi!

Copy kwa kifumbiko lane
 
Last edited by a moderator:
Nipo ndani ya Ilboru sec school na kufika kwangu hapa ni maamuzi ya kibinafsi kabisa..........wanafunzi ni wengi sana wanarudi shuleni baada ya kuwa nje ya shule tangu tarehe tajwa hapo juu. Ni wa kuanzia form 1,3,4,5 na 6 ndiyo wamerejea..............naona wote wanaorejea ni lazima wafanyiwe ukaguzi kwa chochote walichokuja nayo baada ya hali hii kurejea hapa shuleni. Nawaona walimu wanawajibika kwa jinsi yoyote wawezavyo.

Natamani niseme nao ila hawanipi nafasi......na hapa namwona dogo mmoja amekataa katu katu kukaguliwa na mkononi ameshikilia kitu kama kahirizi na naona kama anarudishwa kwao baada ya kukataa ukaguzi ule. Najaribu kama nitapata jina lake kamili na baada ya hapa nitarudi.

Majanga ni mengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…